Sunday, October 21, 2012

Mkenya victor Wanyama ang'aa Scotland


Victor Wanyama
                                                 Victor Wanyama
Mkenya, Victor Wanyama amefunga mabao mawili kwa kuisadia klabu yake ya Celtic kuinyeshea klabu ya St. Mirren kwa mabao 5-0, na kuendeleza uongozi wao katika ligi kuu ya premier nchini Scotland.
Ushindi huo umeipa Celtic matumaini makubwa huku ikijiandaa kwa michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa barani ulaya dhidi ya Barcelona.
Hata hivyo, St Mirren ilipoteza nafasi nyingi za kufunga wakati wa mechi hiyo. Garry Hooper aliifungia celtic bao lake la kwanza kunako dakika ya kumi na tano kabla ya Efe Ambrose kufungwa bao la pili.
Wanyama naye akafunga bao la tatu kunako dakika ya 32 na dakika chache baadaye Wanyama aklafunga bao la pili.
Kocha wa St Mirren Danny Lennon amesema amehuzunishwa sana na matokeo ya mechi hiyo, kwani wachezaji wake hawakucheza kama kawaida yao.
Lakini kocha wa Celtic, Neil Lennon amesema mechi hiyo imekuwa fursa nzuri kwa wachezaji wake kujiandaa kwa mechi yao ya wiki ijayo dhidi ya Barcelona

No comments:

Post a Comment