Thursday, September 5, 2013

ndugu wanavujno na viunga vyake

Ndugu wana VUNJO!


Natangaza rasmi kuwa nitagombea ubunge wa jimbo la VUNJO 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA),

huu ni uamuzi wangu binafsi na wa kidemokrasia kwa kuzingatia misingi ya sheria na katiba ya nchi pamoja na ya chama changu,

ninaamini ninazo hoja za msingi, uwezo na kipaji cha kipekee katika kutimiza azma yangu ya kuwatumikia wana Kilimanjaro na Taifa kwa ujumla.

Ninaamini ya kuwa, yapo mambo ya msingi sana ambayo yanahitaji uwepo wangu wa moja kwa moja katika kuyafanya na kuyasimamia mwenyewe kwani mtu mwingine hawezi kufanya kwa weledi kama nilivyokusudia mimi.

Natambua mengi mema aliyoyafaya na anayoyafanya Mhe MREMA, lakini pia ikumbukwe uwezo wetu wa kufikiri ni tofauti, anayoyafikiri Mhe MREMA AU MWINGINE YOYOTE inaweza isiwe ndivyo ninayofikiri mimi,

*NATAMANI KUONA MATUMAINI MAPYA KATIKA VUNJO NA TAIFA LANGU,

*NATAMANI KUONA FIKRA MPYA NA ZENYE UHAI KATIKA NCHI,

*NATAMANI KIZAZI CHENYE MITAZAMO CHANYA KWA KUMAANISHA,

*NATAMANI KUONA MATOKEO MAPYA NA MATUNDA MEMA KATIKA VIWANGO VYA JUU ZAIDI KWA MAENDELEO YA VUNJO NA TAIFA ZIMA,

NB: CHANGAMOTO HAI NA ZENYE MANUFAA HULETWA NA KIZAZI KINACHOFIKIRI SAWASAWA, mimi ni mmoja wapo.

Natambua ugumu uliopo katika safari hii hasa ikizingatiwa kuwa MheMREMA ana wafuasi wengi, jambo hili ninanipa fursa nzuri ya kujiandaa vyema kama ilivyosemwa "BELIEF CREATES THE ACTUAL FACT" ALBERT EINSTEIN.

wenu
MWANAVUNJO MTIIFU NA JASIRI