Thursday, February 28, 2013

Mkondo wa lala samala nchini Kenya

Kinyang'anyiro, cha uchaguzi utakaofanyika Jumatatu kinaingia mkondo wa lala salama hii leo, na Ijumaa huku wagombea wakienda kwenye majimbo kuwaomba watu kura.
Kura za maoni zinaonyesha ushindani mkali kati ya mgombea Uhuru Kenyatta wa Jubilee na Raila odinga wa CORD.
Mshindani anayewafuata ni Musalia Mudavadi wa muungano wa Amani na anashikilia nafasi ya tatu nyuma ya wawili hao kulingana na kura za maoni.
Kwa mgombea kushinda uchaguzi lazima apate zaidi ya asilimia hamsini na takriban asilimia 25 ya kura katika nusu ya majimbo 47.
Miungano ambayo inaongoza kwenye kura zamani inatumia mbinu mbali mbali kuwashawishi wapiga kura kujitokeza siku ya kupiga kura.
Muungano wa Cord wake, Raila Ofinga, ulisema kuwa unawataka watu 330,000 kuwaombea kura kwa wapiga kura kote nchini.
Bwana Kenyatta amekuwa akiwashawishi wapiga kura kupiga kura mapema kabla ya kuelekea kazini na makwao wakati mgombea mwenza wake William Ruto,amewataka vijana kuhakikisha kuwa marafiki zao na jamaa zao wameweza kupiga kura.
Jimbo la Rift Valley, moja ya majimbo makubwa, ina kauti 14 ikiwa na wapiga kura milioni 3,373,853. Eneo hilo linatazamiwa kama ngome ya William Ruto.
Utafiti wa mwisho uliofanywa kuhusu maoni ya watu kuwahusu wagombea wakuu, ulionyesha kuwa Kenyatta angemshinda Raila asilimia 60 kwa asilimia 23.
Pande hizo mbili hata hivyo zina matumaini ya kuibuka mshindi.
Kwa upande wake, Muungano wa Jubilee wake Kenyatta umeelezea matumaini makubwa, ukitaka kushinda kiwango kikubwa cha kura.
Mkoa wa kati ndio wa pili wenye idadi kubwa zaidi ya wapiga kura na eneo hilo ni ngome ya Uhuru Kenyatta.
Kura zote za maoni, zinawaweka zinaonyesha kuwa Kenyatta anaweza kushinda asilimia tisini ya kura katika eneo hilo.

Kamanda Mbowe ndani ya Mbeya maandalizi ya uzinduzi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

MWENYEKITI wa Taifa, Freeman Mbowe leo ameingia Jijini Mbeya, kwa ajili ya vikao vya ndani kwa ajili ya maandalizi ya uzinduzi wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Ruvuma, Njombe, Iringa na Mbeya) utakaofanyika kesho kwenye Viwanja vya Dkt. Slaa (zamani Mama John), ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya ndani na hadhara kutekeleza maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA, kuielezea dhana ya uendeshaji wa chama kupitia kanda ambayo lengo lake kuu ni kushusha mamlaka ya uendeshaji wa chama katika ngazi ya chini, simply decentralization of powers from the centre.

Papa wawili katika mgongano wa kimadaraka

 
YAMETIMIA. Safari ya miaka saba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI inakamilika leo pale atakapong’atuka rasmi katika uongozi wa Kanisa Katoliki, ifikapo saa 2:00 usiku kwa saa za Italia (saa 4:00 usiku kwa saa za Tanzania).

Kwa siku mbili, Papa amekuwa na shughuli nyingi katika makao yake, Gandolfo Castel, Vatican akijiandaa kimwili kuondoka, akiweka sawa nyaraka zake binafsi na zile za kanisa ambazo zitawekwa katika kumbukumbu.

Kwa upande mwingine Vatican, nchi ambayo ipo ndani ya Jiji la Rome iliyozungukwa na ukuta, ikiwa na ukubwa wa hekta 44 na wakazi 832 pekee, imekuwa katika hekaheka nyingi.
Jana, waumini zaidi ya 50,000 na wengine wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wakiwamo makardinali, maaskofu, mapadri na walei walialikwa kwa shughuli rasmi ya kumuaga kiongozi huyo.

Tofauti na kanuni yake, leo Benedict hatavaa viatu vyekundu kama ilivyozoeleka na badala yake amechagua viatu rahisi vya ngozi vilivyobuniwa Mexico. Alipewa viatu hivyo ikiwa ni zawadi wakati wa ziara nchini humo 2012.

Tangu alipotangaza uamuzi wake wa kung’atuka Februari 11, mwaka huu, utata umegubika nafasi yake katika maisha mapya ndani ya Vatican, akiitwa Papa Mstaafu.

Waumini, wataalamu na hata viongozi mbalimbali wa Kikatoliki wameanza kuhoji ni jinsi gani viongozi wawili (Papa) wataishi, huku wote wakivaa mavazi meupe wakiitwa Papa, wakiishi umbali mdogo kati yao, wakiwa na wasaidizi wengi wanaowahudumia.

Vatican
Nje ya Gandolfo Castel, ulinzi umeimarishwa na vibali vya kuingia Vatican vimesitishwa.
Juzi, Vatican ilitangaza kwamba Papa Benedict XVI atajulikana kama ‘Emeritus Pope’, yaani Papa Mstaafu mwenye cheo cha heshima, akiendelea kuitwa, ‘mtakatifu’ na ambaye ataendelea kuvaa nguo nyeupe.

Mavazi na hata jina lake jipya ni masuala ambayo yamezua uvumi mwingi, huku suala la mrithi wake mpya pia likiwa gumzo, kwani tukio kama hilo lilitokea miaka 600 iliyopita.
Ni uamuzi uliolishtua kanisa hilo lenye waumini 1.2 bilioni duniani na wengi wanasema awali, haikushauriwa Papa kustaafu kwani kwa kufanya hivyo kunaacha mizozo na minong’ono ya kuwania madaraka.

Hata hivyo, uongozi wa Vatican umesisitiza kuwa uamuzi huo wa Papa Benedict XVI ni wa kipekee na hakuna mzozo ambao utatokea baina yake na mrithi wake ambaye mchakato wa kumpata unatarajiwa kuanza ndani ya wiki mbili zijazo.

“Kulingana na mabadiliko katika kanisa letu, kuna Papa mmoja. Ni dhahiri kwamba katika hali ya sasa hakutakuwa na tatizo,” anasema Mhariri wa Gazeti la L’Oservatore Romano linalomilikiwa na Vatican, Giovanni Maria Vian.

Hofu iliyopo
Hata hivyo, wakosoaji wa mambo hawakubaliani na hoja hiyo na baadhi ya makardinali walioko Vatican kwa usiri mwingi, wanazungumzia suala hilo wakieleza kwamba litazua tatizo kubwa kwa Papa ajaye, hasa ikiwa mtangulizi wake, Benedict akiwa bado hai.

Mtaalamu wa tauhidi (theolojia), raia wa Uswisi, Hans Kueng ambaye amekuwa mtu wa karibu wa Papa Benedict XVI, ingawa kwa sasa ni mkosoaji wake amesema:
“Kwa sasa, Benedict XVI akiwa bado hai, kuna hatari ya kuwa na Papa kivuli, mwenye mamlaka kamili ambaye kwa chinichini anaweza kumshinikiza mrithi wake kufikia uamuzi.”
Hans Kueng alisema hayo alipozungumza na Gazeti la Der Spiegel la Ujerumani.

Msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi alisema Papa Benedict XVI kwa upande wake aliamua aitwe Papa Mstaafu au ‘kiongozi mstaafu wa Roma.’ Anasema haelewi ni kwa nini ameamua kuacha jina lake la sasa la Askofu wa Rome.

Kwa wiki mbili zilizopita, maofisa mbalimbali wa Vatican wamekuwa wakifikiri kwamba Papa angeanza kuvaa mavazi meusi na kutumia jina la Askofu Mstaafu wa Rome ili kuepuka mkanganyiko na mrithi wake.

Mtanzania apewa uwaziri Rwanda

 
RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).

Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua kuchukua uraia wa Rwanda na wote baba yao ni Mzee Titus Rwamushaija... “Huyu ni kaka yangu wa tumbo moja na kwa kweli tumefurahi sana kwa mafanikio yake sisi kama wanafamilia.”

Naibu Makamu Mkuu - Taaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Profesa Makenya Maboko alisema Profesa Rwakabamba alifanya kazi katika chuo hicho na aliondoka akiwa Mkuu wa Kitivo cha Uhandisi.

“Aliondoka wakati Kagame alipoingia madarakani na alikwenda kuongoza Taasisi ya Teknolojia ya Kigali (KIST) kabla ya kwenda katika Chuo Kikuu cha Kigali,” alisema Profesa Maboko.

Msomi huyo alikwenda Rwanda mwaka 1997, baada ya kuombwa na Rais Kagame ambaye alikwenda UDSM kuwaomba baadhi ya wahadhiri kwenda Kigali kufungua chuo kikuu katika taifa lake baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994.

Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa kwanza wa KIST na kukifanya kuwa miongoni mwa vyuo bora barani Afrika kwa masuala ya teknolojia jambo lililomfurahisha Rais Kagame.

Baada ya mafanikio hayo, Rais Kagame alimteua kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda, Butare ambako pia alijizolea sifa baada ya kusimamia vyema ujenzi wa mabweni kwa wingi na kiongozi huyo alimtunukia uraia wa nchi hiyo kama zawadi.

Hata hivyo, Profesa Rwakabamba atakuwa amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili.
Profesa Rwakabamba alipata elimu ya msingi huko Muleba na akajiunga na Shule ya Sekondari ya Ihungo.

Baada ya hapo, alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds, Uingereza na kupata Shahada ya Uhandisi mwaka 1971 na 1975 alipata Shahada ya Uzamivu katika fani hiyohiyo.

Zaidi ya 1000 wajiunga CHADEMA

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia kikosi kazi chake cha Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), Kanda ya Ziwa, kimefanikiwa kuzoa zaidi ya wanachama wapya 1,000, wengi wakitokea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Wakizungumza na Tanzania Daima jana wilayani hapa, viongozi waandamizi wa M4C Kanda ya Ziwa, Husina Amri Saidi, na Alfonce Mawazo, walisema M4C imedhamiria kujikita zaidi maeneo ya vijijini.

Walisema baadhi ya wananchi hao walipatikana katika mikutano yao iliyofanyika kisiwa cha Bumbile, kata ya Bumbile, jimbo hilo la Muleba Kaskazini ambao ni zaidi ya 200 waliojiunga na CHADEMA.

Mbali na hilo alisema zaidi ya wanachama 100 wa CCM walilazimika kurudisha kadi zao na kujiunga CHADEMA.

“Kwa kweli CHADEMA kupitia M4C tumeweza kuzoa wanachama wengi katika visiwa vya Muleba Kaskazini.

“Kisiwa cha Bumbile, kata ya Bumbile, zaidi ya wananchi 200 wamejiunga na CHADEMA kwa kununua kadi kwa hela zao.

“Lakini, wapo zaidi ya wana CCM 100 wamerudisha kadi za ‘magamba’ kisha kuvaa ‘kombati’,” alisema Husina.

Walisema wakiwa katika visiwa vya Lushonga na Mchangani zaidi ya wananchi 438 walijiunga na CHADEMA.

Akizungumzia harakati za CHADEMA katika kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014 na uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015, Kamanda wa M4C Kanda ya Ziwa, Mawazo, aliwasihi wananchi wote wa Kanda ya Ziwa na Tanzania kwa jumla kutumia nguvu ya umma kuiondoa CCM madarakani kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Mwanafunzi Mbeya anaswa mtandao wizi wa Benki NMB

 
POLISI wilayani Rungwe, mkoani Mbeya, limewanasa watu wanne akiwamo mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne mwaka jana, wilayani Bunda, mkoani Mara, baada ya kukutwa wakiiba fedha Benki ya NMB tawi la Tukuyu kupitia mashine za kutolea fedha (ATM).
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Chrispin Meela alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 2:30 usiku.
Meela aliwataja watuhumiwa  hao kuwa ni mkazi wa mjini Tukuyu,  Mfanyabishara wa Mbozi, mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne mwaka jana wilayani Bunda na mkazi wa Msasani Tukuyu.
Alisema akiwa nyumbani kwake usiku, alipigiwa simu na msamaria mwema na kuambiwa taarifa za kuwapo watu  wakiwa kwenye mashine hizo za kutolea fedha, huku wakiwa wanatoa fedha mfululizo na aliwatilia shaka.
“Jana  usiku saa 2:30 nilipigiwa simu na msamaria mwema na kuniambia kuwa,  kuna watu wapo Benki ya NMB wanatoa fedha ATM tena mfululilo huko wakiwa na kadi nyingi za ATM,” alisema Meela na kuongeza:“Baada ya kuambiwa hivyo nilimpigia simu OCD (Mkuu wa polisi wilaya), akatuma timu ya makachero eneo ta tukio na wakabahatika kuwakuta na kuwatia nguvuni.”
Meela alisema watuhumiwa  walikutwa wakiwa na kadi bandia za ATM 150 za watu tofautitofauti  na kwamba, hadi wanatiwa mbaroni tayari walikuwa na Sh20.5 milioni mkononi. Alisema kadi zote ni za NMB na kwamba, zilikuwa zinaonyesha  wateja wote ni walimu kutoka wilayani Mbozi.
Alisema baada ya watuhumiwa kuhojiwa  walidai ni wafanyabiashara wanajihusisha na kukopesha fedha walimu, hivyo  katika kuzirejea fedha hizo walimu waliwapatia kadi zao ili waende kutoa  benki.
“Kinachotupa hofu  hapa ni kwamba, kadi zote hizi zinaonyesha wateja kutoka wilayani Mbozi, sasa swali kwa nini waje kutolea fedha hizo wilayani kwetu?” alihoji Meela.
Alisema watuhumiwa wote wapo Kituo cha Polisi Tukuyu kwa mahojiano zaidi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani alikiri kupata taarifa hizo, lakini alikataa  kulitolea ufafanuzi kwa sababu  wanaendelea na uchunguzi.

Tuesday, February 26, 2013

Utafiti: Dk Slaa aongoza vinara tisa urais 2015

 
WAKATI baadhi ya wanasiasa wakiwa wameanza kujiwinda kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Shirika la Utafiti la Synovate limetoa matokeo ya utafiti wake ambao unaonyesha vigogo tisa kuwamo katika mchuano huo.
Utafiti huo umeonyesha kuwa endapo uchaguzi huo ungefanyika sasa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi baada ya kuongoza orodha hiyo akipata asilimia 17.

Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kila mmoja akipata asilimia tisa.

Hata hivyo, licha ya kuongoza, Dk Slaa ameporomoka kwa asilimia 25 ikilinganishwa na matokeo ya utafiti kama huo uliofanywa na taasisi hiyo mwaka 2011 ambapo alipata asilimia 42.

Kadhalika, umaarufu wa Pinda ambaye anaongoza miongoni mwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeshuka kwa asilimia tatu kutoka 12 za mwaka juzi, wakati Zitto ameendelea na kiwango kilekile cha asilimia tisa alizopata katika utafiti uliotangulia.
Wengine wanaofuata na asilimia walizopata kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (8), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (7) na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (5).

Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (4) ambaye amefungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (4) na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2).
Ikilinganishwa na utafiti wa 2011, Lipumba ameporomoka kwa asilimia tisa.
Lowassa amepanda kwa asilimia sita, Dk Magufuli asilimia nne, Mbowe na Membe wamepanda kwa asilimia mbili kila mmoja, wakati Sitta amebaki katika kiwango kilekile cha asilimia mbili.

Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi ambao hawana uamuzi wa kuchagua mtu yeyote kati ya hao kwa sasa ni asilimia 18, likiwa ni ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa na utafiti uliotangulia.

CCM yatamba
Katika utafiti huo, CCM kimeonyesha kuwa ni chama ambacho asilimia 52 ya wananchi wangependa kujiunga nacho, kikiwa kimepanda chati kwa asilimia moja kutoka asilimia 51 mwaka jana.

Kwa upande wa Chadema, wananchi ambao wanapenda kujiunga nacho imeshuka kutoka asilimia 35 mwaka 2011 hadi 31 mwaka jana.

Uwezekano mkubwa wa CCM kupanda chati ni kutokana na ukweli kuwa mwaka jana kilikuwa na uchaguzi ulioanzia ngazi ya mashina hadi taifa na kuibua vuguvugu kubwa masikioni mwa wananchi.

Chadema hakikuwa na harakati kubwa za kisiasa ukiacha kampeni ya Movement For Change (M4C), ambayo kwa kiasi haikuwa na pilika kama uchaguzi wa CCM.
Chama kingine ni CUF ambacho kimeporomoka kwa kupata asilimia 10 mwaka 2011 hadi nne mwaka 2012.

Hata hivyo, asilimia ya wananchi kutokutaka kujihusisha na chama chochote imepanda kutoka asilimia mbili mwaka 2011 hadi 12 mwaka 2012.

Rushwa
Katika suala la rushwa nchini, utafiti huo umeonyesha kuwa kati ya watu 10 waliohojiwa, wanne walikuwa na maoni kuwa rushwa imeongezeka kufikia asilimia 41, asilimia 30 walisema iko palepale, asilimia 23 walisema imepungua na asilimia tano hawajui.

John Mnyika kufanya mkutano London 09 March 2013 saa 9 mchana

Monday, February 25, 2013

kumbukumbu ya mwezi huu,Picha: Mapokezi ya wabunge wa CHADEMA jijini Dar na Mkutano wa hadhara


Katika maandamano kuelekea uwanjani Temeke, sehemu ya viongozi na wabunge wa CHADEMA

Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu A. Lissu
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema
Sehemu ya mabango ambayo wananchi walikuwa wameyabeba
Viongozi wa CHADEMA: Katibu Mkuu, Dr. W.Slaa, Mwenyekiti, F. Mbowe na Naibu Katibu Mkuu, Z. Kabwe 
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee
 Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mch. Peter Msigwa 
Shukrani kwa chanzo: http://michuzi-matukio.blogspot.com/2013/02/chadema-waandamana-dar-leo.html#links



Sunday, February 24, 2013

Ndege zisokuwa na rubani zatumika Mali

Marekani inatumia ndege za ujasusi zisokuwa na rubani kuwasaidia wanajeshi wa Ufaransa na Umoja wa Afrika kupigana na wapiganaji wa Kiislamu wa Mali.
Afisa mmoja wa jeshi la Marekani alieleza kuwa ndege hizo, yaani drones, hazitakuwa na silaha na zitaongozwa na wanajeshi kama 100 wa Marekani kutoka nchi jirani, yaani Niger.
Mapigano nchini MaliHatua hiyo inafuatia juhudi za Marekani za kupambana na wapiganaji wenye uhusiano na Al Qaeda kaskazini na magharibi mwa Afrika.
Chad inasema kuwa wanajeshi wake wamekuwa wakipambana vikali na wapiganaji katika eneo la milima kaskazini mwa Mali.
Inaarifiwa kuwa wapiganaji kama 65 na wanajeshi 13 wa Chad wameuwawa.

Makubaliano ya mapatano DRC yatiwa saini


Mpiganaji akitembea Rutshuru, kaskazini ya Goma, jimbo la KIvu Kaskazini
Viongozi wa nchi za Maziwa Makuu wametia saini makubaliano ya kumaliza mapigano katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Umoja wa Mataifa umekuwa mpatanishi katika makubaliano hayo ambayo yamekusudiwa kumaliza vita baina ya wapiganaji na serikali mashariki mwa Congo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, alisema anatumai kuwa makubaliano hayo yanayoitwa "mwongozo wa amani na ushirikiano" yataleta amani na utulivu katika eneo hilo.
Lakini piya alisema unahitaji kushughulikiwa kwa muda.
Na piya kuna swala la vipi utatekelezwa.
Makubaliano hayo yakitarajiwa kutiwa saini mwezi uliopita wakati viongozi wa nchi za Umoja wa Afrika walipokutana mjini Addis Ababa.
Makubaliano yanalenga mapatano ya jumla ya kisiasa.
Piya kuna mazungumzo mengine yanayofanywa nchini Uganda baina ya wapiganaji wa kundi la M23 na wakuu wa serikali ya Congo.
Pande hizo zimekuwa zikizozana juu ya udhibiti wa eneo la Kivu Kaskazini lenye utajiri wa madini.
Haya ndio mapigano ya karibuni kabisa katika mizozo ya Congo iliyoendelea kwa karibu miongo miwili.

Man United yaelekea kushinda ligi kuu



Ligi kuu ya soka nchini England, imeendelea leo kwa michezo kadhaa kupigwa kwenye viwanja mbali mbali.
Ryan Giggs
Huko Loftous Road, Manchester United imeebuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya QPR, huku mshambuliaji Ryan Giggs akifunga bao la pili na kufikisha mabao 999 toka aanze kucheza soka la ushindani na kuifanya timu yake ya Manchester United, kuongeza tofauti ya point 15 na mabingwa watetezi Manchester City.
United ilipata bao lake la mapema kupitia kwa Rafael Da Silva ambaye alifunga kwa shuti kali dakika ya 23 ya kipindi cha kwanza baada ya mlinda mlango wa QPR,Julio Cesar kuokoa kiki la Robin Van Persie.
Rafael ambaye mdogo wake,Fabio yupo QPR kwa mkopo,hii leo alionekana kuwa kwenye kiwango kizuri na kuokoa hatari kadhaa langoni mwa United hasa baada ya kuokoa mpira wa kichwa wa Criss Samba ambao ulikuwa uingie nyavuni.
Licha ya Dan Welbeck na Wayne Rooney kuingia wakitokea benchi,hii leo hawakuweza kupata bao katika ushindi huo ambao unawabakisha United kileleni mwa msimamo wa ligi kuu soka nchini England.
Matokeo haya,yanaendelea kuwabakisha QPR kwenye nafasi ya mwisho ya msimamo wa ligi hiyo yenye upinzani mkubwa duniani.

Man City yailemea Chelsea,yaichapa 2-0,na newcastle yapeta


Wachezaji wa Manchester City
Mabingwa watetezi wa kombe hilo Manchester City wameandikisha ushindi mkubwa dhidi ya mabingwa wa ulaya Chelsea na hivyo kufufua matumaini yao ya kuhifadhi kombe hilo kwa mwaka wa pili, licha ya kukabiliwa na upinzani mkali kutoka wa vinara wa ligi hiyo kwa sasa Manchester United.
Mechi hiyo iliyokuwa na mashambulizi na kila aina ya vivutio baina ya timu hizo zinazomilikiwa na matajiri wawili tofauti,imemalizika kwa ushindi wa Man City wa mabao mawili kwa bila.
Mabao ya kipindi cha pili ya Yaya Toure na Carlos Tevez yalitosha kuizamisha Chelsea, na kufufua matumaini ya Man City, kutetea taji lao ambalo sasa linaonekana kuwa mikononi mwa majirani zao Manchster United wanaoongoza ligi wakiwa na tofauti ya point 12.
Mapema kipindi cha pili, Chelsea, walipata penat baada ya Demba BA, kuangushwa katika eneo la hatari na mlinda mlango wa Man City, Joe Hart, lakini penat iliyopigwa na nahodha wa Chelsea, Frank Lampard, ilipanguliwa Joe Hart na kuamsha mashambulizi zaidi ya Manchester City.
Wachezaji wa Newcastle
Yaya Toure kunako dakika ya 63 alipenyeza shuti la wastani pembeni mwa lango la Chelsea na kuwafanya Manchester City, kuongoza kwa bao moja kabla Chelsea, kufanya juhudi za kutaka kusawazisha lakini wakajikuta wanoangezwa bao la pili maraidadi kabisa lililofungwa na Carlos Tevez ambaye aliingia akitokea benchi,huku likiwa bao lake la kwanza baada ya mechi sita alizocheza bila kuifungia timu yake.
Kwingineko,katika mchezo mwingine wa leo, Newcastle wakiwa nyumbani,walitoka nyuma baada ya kufungwa bao la mapema na kuchomoza na ushindi wa mabao manne kwa mawili dhidi ya Southampton.
Mabao wa Newcastle yamefungwa na Musa Sisoko,Papis Demba Cisse,Yohan Cabaye aliyefungwa kwa mkwaju wa penati huku bao la nne watakatifu au Southampton wakijifunga.
Mabao ya Southampton yalifungwa na Morgan Scheneiderlin dakika tatu tu baada ya mchezo kuanza huku bao la pili likifungwa na Rickie Lambert.

Matokeo ya Kidato cha nne 2012: Mataifa mawili katika nchi moja

Matokeo ya Kidato cha nne 2012: Mataifa mawili katika nchi moja
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Joyce Ndalichako akionyesha karatasi ya majibu ya mmoja wa watahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2012, Dar es Salaam jana. Picha hisani ya Mwananchi
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Joyce Ndalichako akionyesha karatasi ya majibu ya mmoja wa watahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2012, Dar es Salaam jana.
Picha hisani ya Mwananchi
Kila Mtanzania sasa anajadili matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2012 yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi mwanzoni mwa wiki hii. Matokeo hayo yanaonyesha kwamba zaidi ya asilimia 90 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne walipata daraja la nne na daraja la sifuri. Dara la Sifuri limebeba asilimia 60 ya matokeo yote. Taifa limepata mtikisiko mkubwa kuona vijana wake wakiwa wamefeli kwa kiwango hiki.
Hata hivyo hii sio mara ya kwanza kupata matokeo ya namna hii. Ukiangalia matokeo ya kidato cha nne kuanzia mwaka 2009 utaona kuwa kila mwaka wanafunzi wanaofeli wanaongezeka. Mwaka 2011, wanafunzi 302,000 sawa na asilimia 89 ya wahitimu wote wa kidato cha nne walipata daraja la nne na sifuri. Mwaka 2010 wanafunzi 310,000 ambao ni asilimia 90 ya wahitimu walipata madaraja hayo ya chini kabisa na mwaka 2009 jumla ya wanafunzi 195,000 sawa na asilimia 78 ya wahitimu wote walipata madaraja ya sifuri na daraja la nne. Kila mwaka matokeo yakitangazwa kuna kuwa na mjadala wa wiki moja au mbili, wabunge tunapiga kelele kidogo kisha tunasahau kabisa suala hili mpaka matokeo mengine.
Hivi tumewahi kujiuliza hawa vijana wanaoishia kidato cha nne wanakwenda wapi? Wanafanya nini? Hii nguvu kazi kubwa ya Taifa inapotelea wapi?
Ni vema ifahamike kwamba Tanzania ni Taifa la vijana na watoto. Kwa mujibu wa taarifa za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, hivi Tanzania ina jumla ya vijana 38 milioni wa chini ya umri wa miaka 35 , hii ni sawa na idadi ya watu waliokuwepo Tanzania mwaka 2003. Asilimia 78 ya Watanzania wapo chini ya umri wa miaka 35 na nusu ya Watanzania wapo chini ya umri wa miaka 17. Kwa takwimu hizi ni dhahiri kwamba suala moja kubwa kuliko yote linalohusu Watanzania ni Elimu. Suala moja kubwa linaloweza kujenga au kubomoa Taifa hili ni Elimu. Suala moja kubwa linaloweza kuepuka matabaka katika nchi ni Elimu. Tena Elimu Bora, na BURE.
Kuna nadharia inaitwa ‘gawio la idadi ya watu’ na ‘bomu la idadi ya watu’. Nadharia hizi zatumika kuelezea namna mataifa yanaweza kufaidika au kupata hasara kutokana na kuwepo kwa nguvu kazi kubwa ambayo ama inatumika kwa faida ya nchi hiyo kwa kufanya kazi na kuongeza uzalishaji ama inatumika kwa kwa kukaa tu kwenye vijiwe na kupiga soga. Taifa ambalo linaandaa vijana wake kwa maarifa na stadi za kazi huvuna gawio (demograpich dividend). Mataifa yaliyofaidika na hali hii ni kama India, Uchina na Ujapani ambapo nyakati wana vijana wengi sana kuliko wazee vijana hawa walipewa ujuzi mkubwa na stadi za maisha na hivyo kuongeza uzalishaji mali kwa Taifa. Watu ndio mtaji mkuu wa Taifa lolote lile duniani. Taifa ambalo haliandai vijana wake kupata elimu huingia kwenye mgogoro mkubwa maana kundi la vijana wasio na kazi na wasio na maarifa yeyote ni sawa sawa na bomu.
Tanzania tuna chaguzi katika masuala haya mawili, ama tuvune gawio la kuwa na vijana wengi sana kwa kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika Elimu au tusubiri bomu lilipuke. Kwa matokeo haya ya kidato cha nne kwa miaka minne iliyopita, ni dhahiri tumeamua kulipikiwa na bomu.
Tunajua chanzo cha matokeo haya. Watoto hawasomi wala kujifunza shuleni. Hasa watoto wa vijijini ambapo hakuna walimu wala vitabu. Tumejenga mataifa mawili ndani ya nchi moja, Taifa la masikini na wana shule zao, wanapata masifuri kila siku. Taifa la walalaheri wana shule zao na wanapata madaraja ya juu. Hawa ndio watakaoenda vyuoni na wenye elimu wataendelea kutawala. Suluhisho ni moja tu, kuamua kwa dhati kabisa kuwekeza kwenye elimu kwa kuhakikisha kuna walimu wa kutosha, walimu wanalipwa vizuri na kuishi kwenye mazingira mazuri. Iwe na marufuku wenye kufeli ndio wafanye kazi ya ualimu.
Ni lazima kuhakikisha kuwa kunakuwa na vitabu vya kutosha kwenye mashule. Serikali ihakikishe kwamba inaingia makubaliano na wachapishaji wa vitabu wa ndani na kutoa vitabu vinavyojenga Taifa kwa kutoa maarifa ya uhakika kwa watoto. Ieleweke kwamba shughuli ya uchapishaji wa vitabu ni ajira tosha iwapo tutawezesha wachapishaji wa ndani kutoa vitabu vingi zaidi na vyenye ubora.
Matokeo ya mwaka huu ya kidato cha nne yanatuambia jambo moja kubwa sana, kwamba sisi ni Taifa linalokufa. Tuweke siasa pembeni na kahakikisha kwamba kunakuwa na uwajibikaji kwa viongozi kutokana na matokeo ya namna ya hii ya vijana wetu. Tusione tabu kubadilisha mawaziri wa Elimu kila mwaka kwa kuwafukuza kutokana na matokeo ya mitihani ya watoto wetu. Hii itafanya Waziri ajue umuhimu wa elimu anayoisimamia. Tukate mzizi wa fitina, elimu ni suala la uwajibikaji. Makala zijazo tutaona hatua za kuchukua ili kuhakikisha hawa watoto zaidi ya 300,000 waliofeli tunawafanya nini.

Zitto na Demokrasia

Muhimbili, Aga Khan kufanya operesheni ya moyo

HUDUMA za matibabu na upasuaji wa moyo zitaanza kupatikana nchini, kutokana na mipango ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na ile ya Aga Khan.
Hatua hiyo itawawezesha wagonjwa wa moyo nchini kutopelekwa kwa wingi nje ya nchi kama ilivyo sasa. Pia itaokoa mamilioni ya fedha ambazo zimekuwa zikitumika kugharimia tiba hiyo nje ya nchi.
Mkurugenzi wa Huduma za Afya wa Hospitali za Aga Khan Tanzania, Dk Jaffer Dharsee akiwasilisha taarifa kuhusu ongezeko la magonjwa ya moyo nchini katika kongamano la wataalamu wa magonjwa hayo alisema, jitihada kubwa zinafanywa ili kuhakikisha tiba ya moyo inaanza kutolewa nchini.
Alisema Hospitali ya Muhimbili inakusudia kuanza kutoa tiba hiyo katika kipindi cha miezi miwili ijayo baada ya ujenzi wa taasisi yake kukamilika, wakati Hospitali ya Aga Khan itaanza kutoa matibabu hayo mwakani. Kongamano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.
Hatua ya kuwapo kwa tiba za moyo nchini, itawezesha gharama za tiba kupungua kwa asilimia 57.1, ikilinganishwa na gharama za tiba hizo nje ya nchi.
Dk Dharsee alisema hapa nchini gharama za tiba zitakuwa Dola za Marekani 1,500 sawa na Sh2.4 milioni tofauti na Dola 3,500 (Sh5.6 milioni) zinazotumika kumpeleka mgonjwa kwa ajili ya upasuaji nchi za nje kama India.
Alisema gharama hiyo inatokana na kuwapo kwa gharama kubwa zinazohitajika kuandaa maabara hiyo ambayo ina thamani ya Dola 200 milioni (Sh320 bilioni) bila kuingiza gharama za wataalamu wa kuiendesha na kuhudumia wagonjwa.
Muhimbili
Habari ambazo gazeti hili lilizipata zinasema kwamba Taasisi ya Tiba ya Moyo Muhimbili itaanza kazi zake rasmi katika muda wa miezi miwili kuanzia sasa, baada ya kukamilika kwa jengo la taasisi hiyo, kuanzisha maabara maalumu ya upasuaji na matibabu ya moyo kukamilika.
Ujenzi wa jengo hilo ulianza miaka mitatu iliyopita kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, iliyotoa Sh16.22 bilioni wakati Serikali ya Tanzania ilichangia Sh6 bilioni.
Mei 2008 Hospitali ya Muhimbili ilianzisha Kitengo cha Tiba ya Moyo na Figo, ambacho kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano wa hospitali hiyo, Aminieli Aligaesha alisema kwamba kimeshatoa matibabu kwa zaidi ya wagonjwa 300 tangu kuanzishwa kwake.
 Aga Khan

Kwa upande wa Aga Khan, Dk Dharsee alisema hospitali yake imewekeza kiasi cha Dola za Marekani 4.6 milioni (Sh7.36 bilioni) kuandaa wataalamu wa kuwahudumia wagonjwa wa matatizo ya moyo.
Alisema licha ya maandalizi ya kuleta huduma za upasuaji nchini, hospitali yake imeanza kutoa huduma za kliniki bure kwa vipimo na tiba ndogo ndogo kila Jumatano na Alhamisi.
“Wastani wa wagonjwa 10 wanaofika hospitalini kwetu tumegundua, wanne wana ugonjwa wa moyo,” alisema Dk Dharsee.
Alisema mitindo ya maisha isiyofaa kama uvutaji wa sigara, ulaji wa vyakula usiozingatia afya, ulevi na uzembe wa kutofanya mazoezi mara kwa mara ndiyo vimechochea kwa kiasi kubwa ongezeko la magonjwa ya moyo.
“Hivi sasa takriban asilimia 20 ya watu waishio mijini wanaongezeka uzito kwa kiwango kikubwa jambo ambalo linatishia ongezeko la magonjwa ya moyo kama shinikizo la damu na kupooza,” alisema Dk Dharsee.
“Mwaka 2002 kulikuwa na vifo ya takriban watu 46,000 kutokana na matatizo ya moyo na idadi hiyo inategemewa kuongezeka mpaka 63,000 ifikapo 2015 na 85,400 hapo 2031.
Aliongeza kuwa magonjwa hayo kunaiongezea Serikali mzigo pamoja na kuathiri uchumi wa familia kwa kuwa mwaka 2005 pekee inakadiriwa kuwa Tanzania ilipoteza Dola 100 milioni kwa ajili ya kutibu magonjwa ya kisukari, kupooza na shinikizo la damu.

Rais Mugabe kuwania urais tena

 
RAIS wa Zimbabwe Robert Mugabe  ametangaza kushiriki kwa mara ya sita kwenye uchaguzi wa urais utakaofanyika nchini humo.
Mugabe alisema hayo wakati  wa sherehe ya  kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwake ambapo alitimiza miaka 89.
Katika hafla hiyo kiongozi huyo alisema kuwa, kumekuwa na hila pamoja na shinikizo mbalimbali kutoka Marekani na Uingereza kwa lengo la kumwondoa madarakani yeye pamoja na chama chake cha Zanu PF.
Mugabe ambaye anaiongoza nchi hiyo kwa zaidi ya miaka 33 sasa amepanga kufanya sherehe kubwa zaidi ya kuzaliwa kwake mwezi ujao itakayogharimu kiasi cha Dola 600,000.
Wakati Rais Mugabe akijiandaa kufanya sherehe mwezi ujao, Waziri wa Fedha wa nchi hiyo Tendai Biti alitangaza kuwa, nchi hiyo imebakiwa na hazina ya Dola 300 kwenye Serikali ya nchi hiyo.
Zimbabwe licha ya kukabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi na vikwazo vilivyowekwa na nchi za Magharibi, inatuhumiwa kwa hali mbaya ya ukiukwaji wa haki za binadamu.
Awamu ya tano ya uchaguzi wa Rais nchini humo uligubikwa na ghasia pamoja na vurugu  zilizosababisha Chama cha Zanu PF na kile cha MDC kinachoongozwa na Morgan Tsvangirai kuunda Serikali ya umoja wa kitaifa nchini humo.
Mwanzoni mwa mwezi huu Waziri wa Masuala ya Kikatiba Eric Matinenga alisema  kura  ya uamuzi kuhusu Katiba Mpya itafanyika mwezi Machi.
Serikali hiyo ambayo imefilisika imeomba Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kuisaidia kupata Sh21.48 bilioni kuendesha kura hiyo pamoja na uchaguzi.
“Nilipata ujumbe kutoka kwa Ofisi ya Rais kwamba tarehe ya kura ya uamuzi tayari imeafikiwa. Kura hiyo itafanyika Machi 16,” Matinenga aliwaambia wanahabari mjini Harare.
Katiba ya sasa ya taifa hilo la Kusini mwa Afrika, ambayo imefanyiwa marekebisho mara 19, ilianza kutumika baada ya Zimbabwe kujipatia uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo 1980.

Pinda aunda tume kuchunguza matokeo

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameunda tume itakayochunguza sababu za idadi kubwa ya wanafunzi wa kidato cha nne kuvurunda katika matokeo ya mtihani huo yaliyotangazwa hivi karibuni.
Katika matokeo hayo ambayo yanatajwa kuwa mabovu kuliko yoyote yaliyowahi kutokea katika historia ya Tanzania, asilimia 60 ya wanafunzi waliofanya mtihani huo walipata daraja sifuri.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo alisema kuwa tume hiyo inatarajiwa kuanza kazi wakati wowote wiki ijayo, ambapo itajumuisha Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi.
Lyimo aliwataja wadau wengine watakaohusika katika uchunguzi huo kuwa ni kutoka Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (Tahossa)
“Tume hiyo itahusisha asasi zisizo za kiserikali (NGOs), zinazojishughulisha na masuala ya elimu. Wazazi, walezi na wananchi wote kwa jumla watoe ushirikiano kwa tume, ili ifanye kazi kwa ufanisi,” alisema Lyimo.
Akizungumzia hatua hiyo ya Pinda, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema) alisema wazo hilo ni zuri, lakini kuunda tume bila utendaji hakutakuwa na maana katika elimu nchini.
Alisema kuwa tume nyingi zimeundwa, lakini hakuna tume iliyowahi kuleta mabadiliko na kwamba mara nyingi matokeo ya uchunguzi huwa ni ya kuidhalilisha Serikali.
Msigwa aliongeza kuwa tume hizo hutumia fedha za wananchi na matokeo yake hayatangazwi wala kufanyiwa kazi.
“Serikali ingewaita wadau wa elimu na kuzungumza nao ijue wapi penye matatizo. Halafu maelezo ya wadau hao yajadiliwe bungeni,” alisema Msigwa akiitaka Serikali kuacha kuchanganya ushabiki wa kisiasa pindi zinapowasilishwa hoja muhimu za maendeleo ya taifa na kuongeza:
“Juzi hoja ya Mbatia imetupwa kapuni, hata sisi wabunge tunapeleka hoja nyingi, lakini hazifanyiwi kazi, kwa sababu ya ushabiki.”
Kiongozi wa Jukwaa la Katiba nchini, Profesa Issa Shivji aliwataka Watanzania wasubiri kuona tume hiyo itafanya nini.
Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Benson Bana, alitaka suala la elimu lisichukuliwe kisiasa, badala yake Serikali itatue kero za elimu, alizosema zinajulikana na kwamba hakuna haja ya kumtafuta mchawi.

Friday, February 15, 2013

BREAKING News,TAARIFA KUHUSU KIFO CHA MNIGERIA GOLDIE WA PREZZO



Goldie na Prezzo.
Ni taarifa ambayo kila aliekua karibu na Goldie kwenye page zake za facebook na twitter inakua ngumu kuamini, taarifa rasmi zimeripoti kwamba Goldie ambae ni mwakilishi wa Nigeria kwenye BBA 2012 AMEFARIKI muda mfupi tu baada ya kuwasili Lagos Nigeria akitokea Marekani ambapo bado chanzo cha kifo chake hakijajulikana.
Mmoja wa wasaidizi wake amethibitisha kifo cha Goldie kupitia page ya twitter ya Goldi kwa kusema ni kweli msanii huyo amefariki dunia usiku wa february 14 2013 muda mfupi tu baada ya kuwasili Lagos Nigeria, hali yake ya afya ilibadilika ghafla ikabidi apelekwe hospitali ambako hakuchukua muda mrefu akafariki dunia.

Taarifa nyingine nilizozipata kutoka kwa mtu wake wa karibu wanaeshirikiana kimuziki zimeeleza kwamba mpenzi wake Goldie ambae ni Msanii wa Kenya CMB Prezzo ametua Nigeria usiku huu muda mfupi uliopita kwa ajili ya kuendeleza mipango aliyokua nayo na Goldie ikiwemo kutengeneza show ya TV.
Prezzo alitakiwa kushiriki katika TV show ambayo yeye na Goldie wangekua moja ya wahusika wakuu ambapo mpango ulikua baada ya mwezi mmoja Goldie na Prezzo wangekuja Tanzania, Uganda na Kenya kwa ajili ya kujitangaza na kuipromote single mpya ya Goldie ya ‘Skibobo’ aliyofanya na Ay.

HII NDO CHADEMA, TUMAINI LA WATANZANIA


MKAKATI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kupeleka madaraka kwa wananchi kupitia kanda kumi za kichama zilizoundwa na Baraza Kuu hivi karibuni umeanza kazi rasmi kwa kila kanda kuweka mikakati yake.

Katika mgawanyo huu, Kanda ya Kaskazini ilipangwa kuwa na mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara ambapo Mkoa wa Arusha ulichaguliwa kuwa makao makuu ya Kanda ya Kaskazini.

Taarifa ya kanda hiyo kwa vyombo vya habari jana ilisema kuwa, Februari 16 na 17 mwaka huu, kutakuwa na kikao cha kwanza cha chama Kanda ya Kaskazini ambacho kitajumuisha wabunge wote kutoka mikoa ya kanda hiyo akiwemo Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Freeman Mbowe na viongozi wa chama wa mikoa.

Kwamba kikao hicho pia kitahudhuriwa na wenyeviti na mameya wa halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA pamoja na wajumbe wa kamati kuu ya chama, wanaoishi kwenye Kanda ya Kaskazini pamoja na mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei.

Aidha, Februari 17 mwaka huu, kikao kitajumuisha viongozi kutoka majimbo yote ya Kanda ya Kaskazini takriban majimbo 30 na kuleta wajumbe zaidi ya 200 katika Jiji la Arusha.

Siku hiyo hiyo kutakuwa na uzinduzi wa kanda yenyewe na kuitambulisha timu ya uratibu, utakaohitimishwa na mkutano mkubwa wa hadhara.

Taarifa hiyo iliwaomba wananchi, wakazi wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini wajitokeze kwa wingi kwa ajili ya uzinduzi wa kanda yao na kuunga mkono mpango huu wa chama ambao mbali ya kukifanya kuwa karibu zaidi na wananchi pia katika kufanya shughuli za kisiasa kwa ufanisi wa hali ya juu.

Tuesday, February 12, 2013

wajue wagombea Urais wa Kenya kwa ungani wao.

Uhuru Muigai Kenyatta

Naibu waziri mkuu wa Kenya tangu mwaka 2008, Uhuru Kenyatta, alizaliwa tarehe 26 Oktoba mwaka 1961 kwa Mama Ngina na Mzee Jomo Kenyatta, ambaye alikuwa Rais wa kwanza wa Kenya, kati ya mwaka 1964-1978, na akaitwa "Uhuru", neno la Kiswahili linalomaanisha ukombozi kutoka kwa wakoloni.
Mrithi wa mashamba makubwa Kenya, anatajwa kuwa nambari 23 katika orodha ya watu matajiri zaidi Afrika akiwa na thamani ya dola milioni miatano.
Uhuru, anayejulikana na wafuasi wake kama "Njamba" neno la Kikikuyu, linalomaanisha, Shujaa, ni mgombea wa urais wa muungano wa Jubilee, ambao ni muungano wa vyama vya TNA chake Kenyatta, (URP) na (Narc). Mgombea mwenza wake ni William Ruto wakisaidiana na Charity Ngilu,
Mwalimu wake wa siasa ambaye ni Rais mstaafu, Daniel Moi alimuingiza katika siasa kwa mara ya kwanza na kumpendekeza kuwa mgombea wa urais licha ya kutokuwa na uzoefu wa kisiasa wakati wa uchaguzi wa mwaka 2002.
Hata hivyo, Uhuru alishindwa pakubwa na mpinzani wake, Rais mwai Kibaki na hivyo kumfanya kuwa kiongozi rasmi wa upinzani bungeni.
Uhuru aliungana na Raila kupinga rasimu ya katiba iliyopendekezwa na Kibaki mwaka 2005, lakini baadaye wakatengana huku Uhuru akimuunga mkono Kibaki katika kugombea muhula wa pili.
Kibaki, alitangazwa mshindi katika uchaguzi uliokumbwa na utata mkubwa na punde baadaye akamteua uhuru kama waziri wa serikali za mitaa.
Baada ya kibaki na odinga kutia saini makubaliano kusitisha mapigano, Uhuru aliteuliwa kama mmoja wa manaibu wawili wa waziri mkuu na kisha baadaye akateuliwa kuwa waziri wa fedha. Lakini alijiuzulu baadaye baada ya kupatikana na makosa ya kujibu katika kesi yake ICC ya uhalifu wa kivita kuhusu ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007.
Uhuru na mgombea mwenza wake William Ruto. Wote wanakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC
Kenyatta atafika mahakamani baada tu ya uchaguzi wa mwezi Machi, kwa kosa la uhalifu wa kivita ICC. Mgombea mwenza wake, William Ruto, pia anakabiliwa na makosa hayo hayo.
ICC, inamtuhumu kwa kupanga mashambulizi yaliyofanywa na kundi haramu ya Mungiki, Kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya kabila la wjaluo baada ya wale wa kabila lake wakikuyu kushambuliwa katika mkoa wa Rift Valley.
Ruto na Uhuru walijitetea vikali dhidi ya tuhuma za ICC, na kusema kuwa waziri mkuu Rail Odinga anapaswa kuwajibikIa ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi mwaka 2007/2008
Kama Waziri wa Fedha, Kenyatta alikuwa katika Msitari wa mbele kuleta mageuzi katika wizara ya fedha na ambavyo serikali hufanya biashara zake. Hasa katika kupanga makadirio ya matumizi ya pesa za serikali kupitia mitandao ya kijamii.
Alikuwa waziri wa kwanza wa Kenya kuzindua ruwaza iliyoundwa kwa kuhusisha wananchi na kutilia mkazo katika kutumia mitandao ya kijamii katika uundaji wa sera za chama chake.
Kenyatta anaahidi kuleta mageuzi ya kijamii,kisiasa na kiuchumi na anawaalika wakenya wote kuhusika na uundaji wa sera za chama chake.
Pia anaahidi kutoa hekari milioni moja ya mashamba kwa ajili ya ukulima wa unyunyiziaji maji mimea na kupanua kilimo katika kipindi cha miaka mitano.

Raila Amolo Odinga

Raila Odinga alizaliwa Januari tarehe 7 mwaka 1945 Magharibi mwa Kenya mkoa wa Nyaza. Raila, anayejulikana kwa wafuasi wake kama "Agwambo" kumaanisha mwenyekiti kwa lugha yake asili ya Dholuo, ni waziri mkuu wa kwanza wa Kenya , wadhifa ulioundwa kufuatia mkataba wa kitaifa ulioafikiwa baada ya ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007-2008 kama ishara ya kugawana mamlaka.
Alitia saini mkataba wa kugawana mamlaka na Rais Mwai Kibaki ili kumaliza ghasia za miezi miwili zilizokumba nchi baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata.
Raila mwenye umri wa miaka 68 wa chama cha ODM ingawa kwa sasa anagombea urais kwa muungano wa CORD, ameamua kushirikiana na makamu wa Rais Kalonzo Musyoka, ambaye pia alikuwa hasimu wake miezi miwili tu kabla ya uchaguzi wa mwaka 2007.
Aliondoka kutoka chama cha ODM na kuunda chama chake ODM-Kenya na hata kuitikia uteuzi wake kama makamu wa rais wa serikali ya Rais Mwai Kibaki.
Kama hayati babake, Jaramogi Oginga Odinga, Raila ambaye ni waziri mkuu wa kwanza wa Kenya, kwa miaka minane aliishi kukamatwa na kuachiliwa mara kwa mara tangu mwaka 1982 hadi 1991 kwa harakati zake za kupigania mageuzi wakati wa muhula wa pili wa utawala wa rais Daniel arap Moi.
Kufuatia kuundwa kwa katiba mpya, mwezi Agosti, mwaka 2010, amekuwa akisema kwenye kampeini zake kuwa nia yake ni kuleta mageuzi ya kisiasa.
Raila ni mwanasiasa anayesifika sana kwa ushawishi wake kisiasa na ambaye amekuwa katika msitari wa mbele kuunda vyama vya miungano na wanasiasa ambao ni mahasimu wake.
Baada ya uchaguzi wa mwaka 1997 ambapo Raila alishikilia nafasi ya tatu, kufuatia kuundwa kwa muungano wa chama chake (NDP) na chama cha rais wa zamani Daniel moi (KANU), aliteuliwa kama waziri wa kawi katika serikali ya muhula wa mwisho wa Moi.
Mwaka 2002, baada ya Moi kumuunga mkono uhuru Kenyatta, kama mrithi wake, Raila na maafisa wengine wa KANU ikiwemo Kalonzo Musyoka na wafuasi wengine, walipinga ungwaji mkono wa Kenyatta kugombea Urais. Waliungana na kiongozi wa upinzani Mwai Kibakina na kuunda muungano wa National Rainbow Coalition (Narc) ambao baadaye ulishinda uchaguzi wa mwaka 2002.
Raila aliungana na Rais Mwai Kibaki kuunda serikali ya Muungano ya NARC baada ya kumuondoa mamlakani rais mstaafu Daniel Moi
Mwaka 2005 aliungana na Uhuru Kenyatta aliyekuwa kama kiongozi rasmi wa upinzani, ili kushinda kura ya maoni kuhusu rasimu ya katiba chini ya serikali ya rais kibaki .
Wakati Kibaki alipomfuta kazi na washirika wake, aliunda chama cha ODM ambacho kilipiga kura ya La dhidi ya rasimu ya katiba mpya. Aliongoza kampeini mwaka 2007 na kwa shingo upande kukubali ushindi wa rais Kibaki
Katika uchaguzi uliokumbwa na utata , ghasia na mauaji. Lakini hatimaye alilazimika kujiunga na Kibaki katika serikali ya Muungano.
Disemba mwaka 2012, Raila alilazimika kupiga moyo konde na kurudiana na Kalonzo Musyoka chini ya muungano wa CORD, kwani daima husema katika siasa, hakuna maadui wa kudumu.
Raila anaamini kuwa wakenya wanastahili kuhudumiwa vyema zaidi kuliko ahadi wanazopewa na kwamba chini ya utawala wake, Raila anaahidi kuleta mageuzi na kuhakikisha uongozi bora. Anaahidi kuwa serikali yake itaekeza katika viwanda vya kisasa , mabohari pamoja na vituo vya teknolojia ya mawasiliano katika maeneo ya kuvulia, ushirikiano na sekta ya kibinafsi ili kuimarisha kilimo.

Martha Wangari Karua

Alizaliwa tarehe 22 Septemba mwaka 1957 mkoa wa kati. Na yeye ndiye mgombea wa pekee mwanamke katika uchaguzi huu. Aliajiriwa kama hakimu akiwa na umri wa miaka 24 kabla ya hata kuwa mbunge miaka kumi baadaye.
Mgombea wa muungano wa National Rainbow Coalition (Narc-Kenya), Karua alimteua mwanauchumi Augustine Chemonges Lotodo kama mgombea mwenza wake. Lotodo pia amewahi kuwa mbunge katika bunge la Afrika Mashariki
Karua mwenye umri wa miaka 55, alikuwa mwanachama wa upinzani ambao walipigania siasa za vyama vingi nchini Kenya mapema miaka ya tisini chini ya utawala wa rais mstaafu Daniel Moi aliyekua anaongoza kimabavu chini ya chama kimoja.
Mkereketwa wa demokrasia na maswala ya wanwake nchini Kenya, Karua alihusika na kupigania haki za wanawake kwa kutaka uungwaji mkono katika maswala yanayowahusisha wanawake wenyewe.
Karua alikuwa mfuasi mkubwa wa rais Mwai Kibaki na sera zake hadi tarehe sita Aprili mwaka 2009 wakati alipojiuzulu kama waziri wa sharia, akielezea kuwa kazi yake ilikuwa inaingiliwa sana na baadhi ya maafisa wakuu serikalini.
Aliongoza upande wa serikali wakati wa mapatano kati ya Raila Odinga na Kibaki ili kumaliza ghasia za baada ya uchaguzi.
Pia aliwahi kuhudumu kama waziri wa maji aliyepigia debe sana sheria ya maji ya mwaka2002 ambayo ilichochea mageuzi katika sekta hiyo.
Karua anaahidi kuleta mageuzi katika sekta ya afya, elimu, uongozi bora kubuni nafas za kazi, kuhusisha vijana katika maswala ya uongozi na kuhakikisha serikali yake inafanya kazi kuboresha maisha ya wananchi.

Tanzania yang’ara maajabu saba,imepata tuzo tatu za maajabu saba ya africa

TANZANIA imepata tuzo tatu za maajabu saba ya Afrika kupitia vivutio vyake bora vya utalii vya Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Serengeti ambayo viliongoza kwa kupata kura nyingi kuliko nchi nyingine yoyote.
Akitangaza matokeo hayo jana mjini hapa, rais wa taasisi iliyoandaa tuzo hiyo Dk. Phillip Imler wa Marekani, mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema ushindi huo umetokana na kuwa Tanzania ina vivutio vya kipekee.
Akielezea hifadhi ya taifa ya Serengeti, alisema kuwa ndiyo hifadhi ya kipekee iliyopata kura nyingi kutokana na tabia ya misafara ya wanyama wanaohama kwa msimu.
Naye Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo alisema kuwa nchi za Afrika zina vivutio vingi vya utalii na fursa kubwa ya kukuza pato kupitia utalii huo.
Alisema anaamini kutokana na sifa ambayo Tanzania imeipata kupitia vivutio vyake vitatu itaendelea kuvitunza kuhakikisha kuwa vinavutia zaidi watalii na kuongeza pato la taifa.
“Afrika ina vivutio vingi vyenye kuvutia hivyo kila nchi ni lazima ijivunie rasilimali hizo kwa kuvitunza na kuviendeleza,” alisema.
Alisema kwa Tanzania ni bahati ya pekee kuweza kupata tuzo tatu za maajabu saba ya Afrika ambazo ni Mlima Kilimanjaro, Bonde la Ngorongoro pamoja na hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo ni wajibu wa kuvitunza na kuviendeleza.
Alisema kuwa iwapo Watanzania wataendeleza tabia ya utunzaji wa vivutio vilivyoko nchini, nchi itaendelea kupata sifa duniani kote.
Naye Mkurugenzi wa Hifadhi za Taifa (Tanapa), Dk. Alan Kijazi, alisema Mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu barani Afrika na hivyo una kila sababu ya kushinda na Watanzania waendelee kuutunza.
Kuhusu hifadhi ya Ngorongoro alisema kuwa imeshinda kwa kuwa na wanyama wa kila aina kama Big Seven: simba, tembo, viboko, nyati, vifaru, sokwe na mamba.
Mbali na Tanzania Dk. Imler alivitaja vivutio vingine vilivyoshinda kuwa ni Red sea Reefs, Okavango Inland delta iliyoko nchini Botswana, Sahara Desert na River Nile.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, alisema ushindi huo ni historia kubwa duniani na kwamba ni jambo la Watanzania wote kujivunia.

Mchungaji auawa kwenye vurugu Geita

MCHUNGAJI wa Kanisa la Pentecoste Assemblies of God Tanzania (PAGT) Buseresere, Wilaya ya Chato, Mathayo Kachila (45) amefariki dunia huku watu wengine 15 wakijeruhiwa kwa mapanga kufuatia vurugu kutokana na mgogoro wa bucha.
Tukio hilo lilitokea jana saa 2:27 asubuhi kwenye Soko la Buseresere baada ya kundi la wananchi kuvamia bucha iliyokuwa na maandishi ya ‘Bwana Yesu Asifiwe, Yesu ni Bwana’, kuwataka waliokuwa wakiuza kuifunga hali iliyozusha vurugu.
Chanzo cha vurugu
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, wananchi hao wanaodaiwa kuwa waumini wa Kiislamu walikuwa wamechukizwa na kufunguliwa kwa bucha hiyo, ndiyo wakachukua uamuzi wa kwenda kuamuru ifungwe.
Inadaiwa kabla ya kufunguliwa kwa bucha hiyo, Wakristo walifanya mkutano wa Injili Uwanja wa CCM Katoro na kutangaza kuwa, watachinja nyama yao na kuiuza kwenye bucha maalumu.
“Tulipata taarifa za kufunguliwa kwa bucha hii na tulipofika kuwaomba waache kuuza nyama yao, waligoma na kuendelea kuuza, baada ya kuona hilo wafuasi wa Dini ya Kiislamu walikimbilia msikitini na kuunda kikosi cha kupambana nao,” alisema Mwenyekiti wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) Wilaya ya Chato, Yusuf Idd.
Alisema licha ya kuwasihi hawakumsikiliza, waliamua kwenda kupambana.
Katika vurugu hizo, duka la Idd lilivunjwa na kuporwa simu na fedha, huku pikipiki mbili ambazo hazijafahamika wamiliki zilichomwa moto.
Katika vurugu hizo nyama ndani ya bucha hiyo ilimwagiwa maji, ikiwamo kuharibiwa kwa madirisha na milango yake.
Licha ya majeruhi kutajwa kuwa 15, waliotibiwa Kituo cha Afya Buseresere na kuruhusiwa ni Abdallah Shaaban (25), Abubakar Shaaban (27), Faruk Shaaban (14), Kassim Almasi (23), Yusuf Shaaban (18), Bilal Hassan na Abdallah Ibrahim.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Geita, Dk John Lumona alisema majeruhi wengine waliofikishwa ni Yasin Rajabu (56), Said Taompangaze (47), Masoud Idd (21), Ramadhan Pastory (36), Haruna Rashid (61) na Sadiq Yahya (40), ambaye hali yake ameieleza kuwa mbaya na alipelekwa Hospitali ya Rufani Bugando.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geira, Paul Katabago alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa rasmi baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa.
Mkuu wa Wilaya ya Chato, Rodrick Mpogolo aliwataka wananchi kutulia kwa vile suala hilo linashughulikiwa na serikali na litapatiwa ufumbuzi.

Dk Salim, Nchimbi, Tibaijuka waula CCM

HARAKATI za kupanga safu za uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimehitimishwa usiku wa kuamkia leo baada ya Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC) kuchagua wajumbe wa Kamati Kuu (CC).
Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya kikao cha NEC jana, walioula kuingia katika chombo hicho kikuu cha uamuzi ndani ya CCM ni pamoja na Waziri Mkuu wa zamani, Dk Salim Ahmed Salim na mawaziri kadhaa kutoka Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.
Dk Salim ambaye aligombea urais dhidi ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika Uchaguzi Mkuu wa 2005, aliteuliwa jana kuwa mjumbe wa NEC na baadaye jina lake kupendekezwa kuwa miongoni mwa waliopigiwa kura za kuwa wajumbe wa CC.
Makada 14 wa CCM, saba kutoka kila upande wa muungano walipigiwa kura katika uchaguzi huo ambao matokeo yake yalitangazwa usiku wa manane.
Kutoka Tanzania Bara, waliochaguliwa ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira.
Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Alhaji Adam Kimbisa, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa na Mbunge wa Viti Maalum, Pindi Chana.
Kutoka Tanzania Zanzibar mbali na Dk Salim, wengine ni Waziri wa Ulinzi, Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi.
Pia wamo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan, Naibu Waziri wa zamani wa Mawasiliano na Uchukuzi, Dk Maua Abeid Daftari pamoja na  Khadija Aboud.  Wajumbe hao wapya wanaunda Kamati Kuu pamoja na wengine wanaoingia kwa nyadhifa zao.
Vigogo urais watoswa
Uteuzi wa makada waliopigiwa kura uliwaweka kando vigogo ambao wamekuwa wakitajwa kuusaka urais kupitia chama hicho katika Uchaguzi Mkuu ujao wa 2015.
Miongoni mwa waliowekwa kando ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na mawaziri waandamizi wawili katika Serikali ya Rais Kikwete, Samuel Sitta (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) na Bernard Membe (Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa).
Kadhalika, majina makubwa ndani ya chama hicho kama vile January Makamba, Martin Shigela, Willison Mukama, Mohamed Seif Khatib, Omar Yusufu Mzee na wengineo hayakuwamo kwenye orodha ya waliopigiwa kura.
Baadhi ya makada walioanguka Balozi Ali Karume, Gwaride Jabu, Dk
Raphael Chegeni, Dk Cyril Chami, Michael Lekule Laizer, Ramadhan Madabida, Hassan Wakasuvi, Dk Fenella Mukangara, Shamsa Mwangunga na Said Mtanda.

Monday, February 11, 2013

Njia Kilimanjaro Marathon 2013 zatangazwa

WAANDAAJI wa Kilimanjaro Marathon 2013 wametangaza kwamba mbio za mwaka huu zitafanyika katika njia zile zile zilizotumika mwaka jana.
Mbio za mwaka huu zinatarajiwa kurindima mjini Moshi mkoani Kilimanjaro Machi 3.
John Addison, Mkurugenzi Mtendaji wa Wild Frontiers, waandaaji wa tukio hilo, alisema katika taarifa jana kwamba njia zitakazotumika kwa ajili ya Kilimanjaro Marathon 2013 ni kuanzia Uwanja wa Chuo cha Ushirika (MUCCoBS) kuelekea katikati ya mji na kisha kufuata barabara kuu ya kwenda Dar es Salaam kwa takriban kilomita 8 hadi 9.
Baadaye watageuka na kurudi Moshi mjini kupitia katikati ya mji na baadaye watapandisha mwinuko kidogo kuelekea Mweka.
“Wanariadha watafurahia zaidi sehemu hii, kwa sababu ina mandhari ya kuvutia na kutakuwa na washangiliaji wengi kando ya barabara,” alisema na kuongeza.
Sehemu ya kupandisha kuelekea Mweka inahitaji kupanda kwa taratibu, lakini kwa sababu Mlima Kilimanjaro ni kivutio na uwepo wa wananchi wanaoshangilia muda unaenda haraka na kuwasaidia wakimbiaji kumaliza mapema.
Alisema kuwa hadi kituo cha Mweka ambako wanaridha wanageukia kurudi Uwanja wa Ushirika, inakuwa ni takriban kilometa 32 tangu kuanza mbio ndefu ya kilomita 42.
Baada ya hapo kipande kilichobaki kinakuwa ni mteremko kuelekea uwanjani mwisho wa mbio na njia nzima ni mteremko tu.
Aliongeza kuwa kwa wale watakaoshiriki Nusu Marathon, mbio zitaanzia Uwanja wa MUCCoBS, mahali ambapo ni tambarare na baadaye watapandisha kwenye mwinuko kidogo kuelekea Mweka kama ilivyo zile mbio ndefu kabla ya kurudi takriban kilomita 10, kuelekea tena uwanjani.
“Kutakuwa na meza za maji kama ilivyo kawaida na magari maalumu ya kunyunyizia maji mithili ya mvua kando ya barabara, huduma ambazo zimeandaliwa maalumu kuwafanya wanariadha waendelee kuwa na nguvu wakati wote wa mbio hizo,” alisema.
Kuhusu burudani, Addison alisema kuwa hali ya uwanjani itakuwa ya kusisimua kutokana na burudani za uhakika kutoka bendi za muziki wa nyumbani zitakazokuwepo, chakula cha kutosha, nyama choma, vinywaji na bila kusahau mbio za kujifurahisha za Vodacom 5km Fun Run ambazo pia zinatarajiwa kuleta msisimko wa aina yake.
“Ili kuhakikisha usalama wa wakimbiaji, baadhi ya barabara zitakuwa zimefungwa asubuhi siku ya mbio, lakini kutakuwepo na njia mbadala kuzunguka mji kwa ajili ya wakazi wa Moshi. Wakazi wa Moshi ambao wanatarajia kukimbia pamoja na wakimbiaji wengine watakaofika Moshi mapema, wanaweza kuanza mazoezi katika njia hizo hili kupata uzoefu wa njia na kujiandaa vizuri kwa ajili ya mbio,” alisema.
Mbio hizo zinaratibiwa na Executive Solutions na kudhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, huku wadhamini wengine wa tukio hilo wakiwa ni pamoja na Vodacom Tanzania (5km Fun Run), GAPCO (Nusu Marathon Walemavu), Tanga Cement, CFAO Motors, KK Security, Keys Hotel, TPC Sugar, TanzaniteOne, New Arusha Hoteli, Kilimanjaro Water, FastJet na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA).

CHADEMA yawasha moto- Yamtaka Makinda kuamua kujadili hoja au Bunge lisiwepo

CHAMA cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa masharti mazito mawili kwa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kikimtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda, kuamua ama aliache Bunge lijadili hoja muhimu kwa taifa au lisiwepo kabisa.
Msimamo huo umekuja zikiwa ni siku chache baada ya kuibuka mvutano mkubwa bungeni kati ya wabunge wa upinzani na kiti cha Spika kutokana na maamuzi yake kuegemea upande mmoja wa kuibeba serikali na kuzika hoja za wapinzani.
Wakizungumza jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Temeke Mwisho, viongozi wakuu wa CHADEMA kwa nyakati tofauti waliwaeleza wananchi kile kilichojiri bungeni na kuwataka kuwaunga mkono ili kuondoa udhalimu.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, alisema kuanzia sasa wabunge wao hawatatoka bungeni kama njia ya kupingana na ubabe wa kiti cha Spika badala yake watahakikisha Bunge halifanyi kazi mpaka lijadili hoja za msingi kwa maslahi ya Watanzania.
Akihutubia maelfu ya wananchi waliofurika mkutanoni baada ya kuhitimishwa kwa maandamano ya kuwapokea wabunge wao yaliyoanzia eneo la Ubungo River Side na msafara wake kupita maeneo mbalimbali hadi Temeke, Mbowe alisema wamegundua janja ya CCM.
“Tumegundua janja yao. Walidhani watatuchakachua kila mara, tutatoka Bungeni; sasa tumeamua. Wasipotusikiliza hatutoki hadi kieleweke,” alisema.
Mbowe alisema wakati wa Watanzania kulalamika juu ya mustakabali wa nchi yao umekwisha na kilichobaki ni kuchukua hatua dhidi ya serikali na wao kama wabunge weameanza kwa kuwagomea kutoka nje hali iliyoifanya serikali iombe kukaa nao mezani kwa ajili ya mjadala wa namna ya kuendesha Bunge hilo kwa usawa.
Aliongeza kuwa ni wakati wa Watanzania kutoa kauli moja kama watu waliokasirishwa na ugumu wa maisha bila kujali dini kabila wala sehemu atokayo mtu.
“Ni ujinga kugombana kwa misingi ya udini, ukabila na ukanda badala ya kushughulikia matatizo ya msingi ya nchi yetu leo watawala wanatugawa kwa dini zetu makabila yetu na hata tutokako ili wapate kuendelea kutunyonya katika rasilimali zetu sasa tuamke na mwaka 2015 uwe mwisho wa msiba wa CCM,” alisema.
Dk. Slaa amuonya JK
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alikumbushia sababu za kwa nini alimwambia Rais Kikwete kuwa akifanya mchezo nchi haitotawalika.
Alisema miaka miwili iliyopita akiwa katika moja ya mikutano ya chama wakiwa wanaomba dua, askari polisi waliwapiga mabomu na hata alipochukua hatua ya kuwasiliana na Msajili wa Vyama vya Siasa hakuweza kupokea simu yake.
Aliongeza kuwa leo baada ya miaka miwili dhuluma na uonevu ukiwa umetamalaki wananchi wameamua kuchukua hatua za kuiwajibisha serikali kupitia maandamano.
Kuhusu Bunge, Dk. Slaa alisema kinachofanyika sasa chini ya uongozi wa Spika Makinda na Naibu wake Job Ndugai ni kutaka kuwadhoofisha wabunge wa upinzani ili wasiweze kuzungumzia shida za wananchi.
Tundu Lissu atoboa siri
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, alisema kuwa Makinda na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge chini ya Mwenyekiti wake, Brigedia mstaafu Hassan Ngwilizi, walikuwa wameleta hukumu bungeni ya kuwasimamisha ubunge wabunge wanne wa CHADEMA kwa miezi sita.
Lissu alisema kuwa waligundua wananchi wataandamana hivyo Spika alimwita na kumshauri Ngwilizi aache kusoma hukumu hiyo.
“Walikuwa wameleta hukumu kutushtaki eti Lissu, Pauline Gekul, Joshua Nassari na John Mnyika tufungiwe kwa miezi sita lakini wakagundua mitaani hapatakalika wakaamua kuahirisha kuisoma.
“Tutumie nguvu ya umma kulazimisha utaratibu wa kupata Katiba mpya. Haki isipotendeka tuingie barabarani, tuikomboe nchi yetu kwa miguu yetu na mikono yetu,” alisema Lissu.
Katika mkutano huo, Lissu pia amesema kuna njama za kuchakachua maoni ya Katiba kutokana na idadi ya wabunge wa CCM, na muundo wa mabaraza uliotangazwa wa sasa, ambao wajumbe watateuliwa na kupitishwa na vikao vya maendeleo vya kata, ambavyo wenyeviti wengi ni wa CCM.
Msigwa amvaa Kinana
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, alimtuhumu Katibu Mkuu wa CCM kuwa ni mmoja wa watuhumiwa kwa ujangili na kwamba serikali haimchukulii hatua, hivyo kuwaasa Watanzania wamweke mbali na tembo.
Alisema afadhali apige kelele ili tembo wasichukuliwe, twiga wasisafirishwe, apige kelele watu wapate maji, kuliko kukaa kimya aonekane ana nidhamu twiga na tembo wauawe au wasafirishwe.
Zitto: Spika lazima ang’oke
Naibu katibu mkuu wa CHADEMA (bara) Zitto Kabwe, alisema wanaandaa hoja binafsi ya kutokuwa na imani na Spika Makinnda na naibu wake Ndugai huku akiwataka wananchi waanze kuwawajibisha viongozi hao kuanzia sasa kwa kuwatumia ujumbe wa kulaumu namna wanavyoendesha Bunge kibabe.
Alisema Spika Mkinda hatumii akili zake alizojaaliwa na Mwenyezi Mungu kufanya kazi bali anashikiliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi.
Zitto alitoa namba za simu za viongozi hao kwa wananchi na kuwataka waanze kuwatumia ujumbe wa maandishi au kumpigia kuonyesha kuwa hawakubaliani na utendaji wao bungeni. Mapema katika taarifa yake Zitto alipinga uamuzi wa Spika wa kuifuta Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) kwa kuiunganisha na ile ya Hesabu za Serikali, akidai hayo ni maamuzi ya hovyo.
Zitto alisisitiza kuwa ni lazima Spika adhibitiwe kwa kuondolewa katika nafasi hiyo haraka iwezekanavyo vinginevyo nchi itaumia.
Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema kuwa maamuzi haya yameleta sintofahamu kwa wananchi wengi na wafuatiliaji wa masuala ya Bunge na uwajibikaji katika nchi yetu.
Mbunge huyo ambaye kamati yake ilikuwa mwiba kwa serikali katika kuibua kashfa za ufisadi aliweka bayana kuwa maamuzi ya Spika ni kinyume cha kanuni za Bunge, sheria ya ukaguzi na Katiba ya nchi.
“Maamuzi ya Spika yanavuruga Bunge, ni ya hovyo na yanapaswa kupingwa na kila mdau wa uwajibikaji nchini.
Baada ya Tanzania kuingia kwenye zoezi la ubinafsishaji, mashirika mengi ya umma yaliuzwa na mengine kufa kabisa,” alisema.
Aliongeza kwua Bunge lilikuwa na Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na kamati hiyo ilifutwa mwaka 1997 kufuatia hatua za ubanafsishaji na ukweli kwamba mashirika ya umma hayatakuwapo na hivyo hapakuwa na haja ya kuwapo kwa kamati hiyo.
Zitto alisema kuwa mwaka 2007, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alifanya mkutano wa uwajibikaji na kulieleza taifa kuwa kimsingi mashirika ya umma bado yapo na mahesabu yake, kwa kuwa hayaangaliwi, ni mabaya sana na fedha za umma zinapotea.
Alisema kuwa kwa hali hiyo, CAG aliomba Bunge liunde Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma ili liweze kupokea, kujadili na kutoa maelekezo kuhusu mahesabu ya mashirika hayo na kusimamia ufanisi wake.
“Kamati ya POAC iliundwa rasmi mwaka 2008 mwezi Februari. Nilipewa dhamana ya kuwa mwenyekiti wa kwanza wa kamati hii.
“Sababu za kuanzishwa kwa POAC bado zipo na kimsingi sababu hizo ni za maana sana sasa kuliko ilivyokuwa kabla,” alisisitiza.
Alifafanua kuwa katika kipindi cha miaka mitano, POAC imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa umahiri na kwa uwazi kuliko kamati nyingine zote za Bunge.
“Taarifa ya mwisho ya POAC katika Bunge iliyowasilishwa katika mkutano wa saba wa Bunge, mwezi Aprili mwaka 2012 ulipelekea kutolewa kwa hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu ambayo ilisababisha mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri,” alisema.
Zitto alisema kuwa wakati kamati inajiandaa na taarifa yake ya mwaka 2012 kwenye Mkutano wa Kumi na Moja, Spika ameivunja.
“Ikumbukwe maagizo ya mwisho ya Kamati ya POAC yalikuwa ni kuzuia mifuko ya hifadhi ya jamii kutoa mikopo kwa serikali bila ya kuwapo kwa mikataba,” alisema.
Aliongeza kuwa hivi sasa serikali imekopa zaidi ya sh trilioni 1.2 kutoka mifuko ya hifadhi ya jamii kwa ajili ya miradi mbalimbali, mikopo hiyo ya fedha za wafanyakazi haina mikataba yoyote na POAC iliona hatari ya fedha za wafanyakazi kupotea na kuleta madhara makubwa kwa wastaafu nchini.
Zitto anaamini kuwa POAC ilipaswa kuongezewa nguvu zaidi ili kufikia uwekezaji wa serikali kwenye makampuni binafsi badala ya kuifuta. Uwekezaji wa serikali kwenye makampuni kama BP, Airtel, Kilombero Sugar, SonGas hauna uangalizi wowote.
“Spika anasema kazi za POAC zitafanywa na Kamati ya PAC; Tanzania ina jumla ya mashirika ya umma 258 yenye thamani ya sh trilioni 10.2 mpaka Juni mwaka 2012, hata kamati ya POAC ilikuwa haiwezi kushughulikia mashirika yote ya umma katika mwaka mmoja, PAC itawezaje kusimamia wizara za serikali, mikoa na wakala wa serikali na wakati huohuo mashirika ya umma 258?” alihoji.
Zitto alisema kuwa taifa linarudi miaka ya kabla ya 2008 ambapo mashirika ya umma yalikuwa kichaka cha kuiba fedha za umma.
Hivi karibuni POAC iligundua mtindo wa wizara za serikali kupeleka fedha kwenye mashirika na kutumia kifisadi ili kukwepa ukaguzi kwenye wizara; mfano ukiwa ni Wizara ya Utalii kupeleka zaidi ya sh milioni 600 Bodi ya Utalii mwaka 2010/2011.
Mnyika kumvaa Maghembe
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alitoa wiki mbili kwa Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghebe kuwa endapo hatachukua hatua kujibu hoja tisa ambazo alikuwa aziwasilishe bungeni basi ataongoza maandamano ya wananchi wa Dar es Salaam kwenda ofisini kwa waziri.
Mnyika alieleza kusikitishwa kwake kwa kuondolewa hoja yake, akisema ni kwa kuwa Rais Jakaya Kiwete alidanganya kuwa 2013 tatizo la maji katika jiji la Dar es Salaam litakuwa historia.
Aliongeza kuwa hoja yake iliondolewa kinyume cha utaratibu wa kanuni, japo ilikuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa Dar es Salaam.
Maandamano na mkutano huo yaliwashirikisha takriban wabunge zaidi ya 20 wa chama hicho, viongozi waandanizi wa kitaifa na maelfu ya wananchi waliokuwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali na kuungwa mkoni kila mahali ulipopita msafara huo.
Askofu amkaanga Makinda
Naye askofu wa kanisa moja kubwa nchini ambaye aliomba kuhifadhiwa jina ili kuepusha malumbano, alisema kuwa Spika Makinda na Naibu wake, Job Ndugai, wanayumba na wanaliyumbisha Bunge.
Akizungumza na gazeti hili kwa simu, askofu huyo alisema kuwa viongozi hao wawili wametumwa na wanatumika. Na kwamba wale waliowatuma wanaona kuwa wanafanya vizuri kwani ndilo hasa lengo.
Alisema ni juhudi za wabunge pekee, tena wenye maono ya kizalendo, ndizo zinaweza kuwaondoa madarakani kwani ni vibaraka.
“Ukimlinganisha huyu Spika na wenzake waliowahi kuongoza Bunge, huyu ni balaa. Amevaa itikadi zaidi. Lakini tunatafsiri kuwa anatumika na Rais.
“Huwezi kuwa na Bunge imara kama una serikali dhaifu. Ndiyo maana katika nchi yetu sasa, mtu hawezi kuwa Spika kama Rais hajamkubali,” alisema.
Alisema hayo tunaweza kujifunza kutokana na kauli ya Makinda ya hivi karibuni alipotoa maoni yake kwenye tume ya kukusanya maoni ya Katiba, pale aliposema kwamba anapendekeza Spika asitokane na chama cha siasa.
Hiyo ina maana anashinikizwa na chama chake kufanya mengi ambayo kama si shinikizo, asingeyafanya. Hata haya yanayotokea ni shinikizo la chama chake.
“Hali ni hiyohiyo hata katika mahakama. Serikali inaingilia sana uhuru wa mahakama. Ndiyo maana hata Jaji Mkuu alipotoa maoni yake katika Tume ya Marekebisho ya Katiba alisema angependa mahakama iwe huru.
“Maana yake anajua kuwa kwa sasa kuna shinikizo kutoka serikalini au chamani katika uendeshaji wa maamuzi ya mahakama nchini. Hii ni hatari,” alisema.
Askofu alibainisha kuwa Makinda ni tofauti na Spika aliyepita Samuel Sitta; kwamba Sitta alikuwa na mwelekeo, alisimamia ukweli, japo mwelekeo wake haukupendwa na watawala.
Aliongeza kuwa Sitta alikuwa mpigania haki, mpenda mabadiliko na aliweza kuonyesha kuwa anawajali wanyonge. Hakuliyumbisha Bunge na aliweza kusimamia maamuzi.
“Bunge haliongozwi kitaasisi, bali linaongozwa kwa matashi ya mtu binafsi au kikundi cha watu.
“Sisi tunapaswa kuwa makini katika kuchagua watu wa aina hii na tunapaswa kuwaelimisha Watanzania ili wapambane kuondoa mfumo wa aina hii,” alisema.
chanzo-mtanzania daima

JK amjibu Lowassa tatizo la ajira

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete katika hali inayoashiria kumjibu rafiki yake, Edward Lowassa ameponda makada wa chama hicho ambao wamekuwa wakipanda jukwaani kuhubiri kuwa ajira ni tatizo pasipo kupendekeza suluhisho la tatizo hilo.
Rais Kikwete ambaye alikuwa akifungua semina ya siku mbili ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM mjini Dodoma jana, alisema kusimama jukwaani na kusema kwamba ajira ni tatizo hakuna maana ikiwa mhusika hatoi pendekezo la jinsi ya kumaliza tatizo hilo.
Ingawa hakutaja majina ya wanasiasa ambao wamekuwa wakizungumzia suala hilo lakini Lowassa, ambaye alijiuzulu wadhifa wa Waziri Mkuu mwaka 2008,  amenukuliwa mara nyingi akiitaka Serikali kuchukua hatua za kukabiliana na tatizo la ajira kwa maneno kwamba ‘ni bomu linalosubiri kulipuka’.
Lowassa, ambaye ni Mbunge wa Monduli kupitia CCM,  aliwahi kuingia hata kwenye malumbano makali na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.
Kabaka akiwa bungeni mjini Dodoma, Machi 21, 2012 alilazimika kutoa takwimu za namna Serikali ilivyokuwa inatengeneza ajira kwa nia ya kumjibu Lowassa, ambaye alikuwa ameeleza tatizo la ajira linavyowaathiri vijana kwenye moja ya hafla.
Lowassa ameendelea kuzungumzia suala hilo mara kwa mara kila anapopata fursa ya kuhutubia.
“Ndiyo ajira ni tatizo, hapa mkakati ni ajira itapatikana vipi? Ni tatizo kweli, tunafanyaje na tunalitatua vipi? Tunataka mtu anayesema kwamba ni tatizo na apendekeze pia suluhu yake,” alisema Rais Kikwete, ambaye aliwahi kutamka kuwa Lowassa ni rafiki yake na anafahamika kuwa alishirikiana naye katika harakati zake za kuwania urais mwaka 2005, na baadaye akamteua kuwa Waziri Mkuu.
Lowassa, ambaye ni miongoni wa makada wa CCM wanaotajwa kuwania urais mwaka 2015, alikaririwa akisema Oktoba 19,  2011 kuwa; “Sijakutana na Rais Kikwete barabarani, watu waache kunichonganisha naye.” Ilikuwa katika mkutano na waandishi wa habari jimboni kwake Monduli.
Suala la ajira nchini ni moja ya mada zinazotarajiwa kuwasilishwa kisha kujadiliwa katika semina hiyo ya CCM, na Rais Kikwete aliwataka wajumbe kupendekeza jinsi ya kuongeza ajira nchini wakati mjadala husika utakapowadia.
Hata hivyo, Rais Kikwete alisema hivi sasa ajira katika sekta ya umma ni kama hakuna, kwani zimebaki sekta za afya na elimu na kwamba hivi sasa suluhu ni kukuza sekta binafsi ili kuongeza ajira.
Alitoa mfano kwamba wakati yeye alipohitimu kidato cha nne, cha sita na chuo kikuu hakukuwa na tatizo la ajira kwa kuwa idadi ya wasomi ilikuwa ndogo ikilinganishwa na mahitaji ya sasa ya soko hilo.
Kikwete alisema wakati huo Serikali ilikuwa haijajitosheleza, tofauti na sasa ambapo imefikia ukomo wa kuajiri isipokuwa kwa sekta mbili tu.
“Kwa sasa Serikali haina uwezo tena wa kuajiri, ilifika mahali kila kiongozi anaenda kuomba serikalini na kupeleka watu wake, unakuta anatoka Kikwete anaomba mtoto wake aajiriwe, mara Katibu Mkuu naye anapeleka watu wake, ikafika mahali mashirika yakajaa tukapata kazi ya kuwapunguza,” alisema Rais Kikwete.

Papa Benedict XVI ametangaza kuachia madaraka


KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Benedict XVI ametangaza kuachia madaraka ya kuongoza kanisa ifikapo mwishoni mwa mwezi huu, uamuzi ambao ni wa kwanza tangu karne ya 15 kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Habari la AFP.
Katika taarifa yake, Papa amesema amefikia uamuzi huo ambapo sasa ana umri wa miaka 85.
Msemaji wa Papa, Federico Lombardi amesema kiongozi huyo wa juu kabisa wa Kanisa Katoliki duniani, ataachia ofisi rasmi tarehe 28 Februari, mwaka huu saa mbili kamili asubuhi.
Wachambuzi mbalimbali wa masuala ya Vatican wanasema safari hii, kuna uwezekano mikoba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI ikarithiwa na Kardinali kutoka Afrika.
Kardinali Peter Turkson wa Ghana ametajwa kama mrithi-mtarajiwa wa nafasi hii nyeti ndani ya Kanisa Katoliki, linalokadiriwa kuwa na waumini zaidi ya bilioni moja dunia nzima.
Mwingine ni Kardinali Francis Arinze; mzaliwa wa Nigeria ambaye alichukua nafasi ya Benedict XVIkama Kardinali-Askofu wa Velletri-Segni alipoteuliwa kuwa Papa miaka nane iliyopita.
SOMENI STATEMENT YAKE HIYO HAPO
 Dear Brothers,

I have convoked you to this Consistory, not only for the three canonisations, but also to communicate to you a decision of great importance for the life of the Church. After having repeatedly examin
ed my conscience before God, I have come to the certainty that my strengths, due to an advanced age, are no longer suited to an adequate exercise of the Petrine ministry.

I am well aware that this ministry, due to its essential spiritual nature, must be carried out not only with words and deeds, but no less with prayer and suffering. However, in today’s world, subject to so many rapid changes and shaken by questions of deep relevance for the life of faith, in order to govern the bark of Saint Peter and proclaim the Gospel, both strength of mind and body are necessary, strength which in the last few months, has deteriorated in me to the extent that I have had to recognise my incapacity to adequately fulfil the ministry entrusted to me.

For this reason, and well aware of the seriousness of this act, with full freedom I declare that I renounce the ministry of Bishop of Rome, Successor of Saint Peter, entrusted to me by the Cardinals on 19 April 2005, in such a way, that as from 28 February 2013, at 20:00 hours, the See of Rome, the See of Saint Peter, will be vacant and a Conclave to elect the new Supreme Pontiff will have to be convoked by those whose competence it is.

Dear Brothers, I thank you most sincerely for all the love and work with which you have supported me in my ministry and I ask pardon for all my defects. And now, let us entrust the Holy Church to the care of Our Supreme Pastor, Our Lord Jesus Christ, and implore his holy Mother Mary, so that she may assist the Cardinal Fathers with her maternal solicitude, in electing a new Supreme Pontiff. With regard to myself, I wish to also devotedly serve the Holy Church of God in the future through a life dedicated to prayer.

From the Vatican, 10 February 2013
BENEDICTUS PP XVI.