Thursday, August 20, 2015

WASIFU WA KINGWENDU KWA KIFUPI-NI MCHEKESHAJI MAARUFU NA MGOMBEA UBUNGE KUPITIA CUF

KINGWENDU's PROFILE.!
Majina yake halisi ni Rashid Mwinshehe, na jina lake la kisanii ni "Kingwendu". Kabila ni Mzaramo mzaliwa wa Kisarawe. Elimu yake ni Stashahada ya Uhasibu (Diploma in Accounting) kutoka chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA).
Kitaaluma Kingwendu ni Mhasibu. Amefanya kazi ya uhasibu ktk taasisi mbalimbali kabla hajaamua kuachana nayo na kujiingiza kwenye sanaa za maigizo ambapo anafanya vizuri ktk sanaa za vichekesho (Physical and Character Comedy).
Kwa sasa anagombea Ubunge jimbo la Kisarawe kupitia chama cha wananchi CUF akiwakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). Yeye mwenyewe anasema "mwaka huu CCM watageuka mapepe Kisarawe, wanaosema sijasoma waende TIA kuuliza records zangu.."
Alipoulizwa kwanini amechagua UKAWA na sio CCM kama wasanii wengine amesema "UKAWA ndio habari ya mjini, Ukijiunga UKAWA unapata raha duniani, aluu".

No comments:

Post a Comment