Sunday, December 16, 2012

NAMNA YA KUPATA MWENZI MZURI WA MAISHA. (HOW TO FIND/GET A GOOD MARRIAGE PARTNER)


*Mithali 19:14, 21
1.      Mweleze Mungu vizuri, zile haja za moyo wako. (Mwa 2:18)
Mungu anaheshimu sana haja za moo wako ambazo zitakupa wewe furaha ya maisha.
(Mathayo 7:7-11;  Wafilipi 4:6-7 ; Zab 145:17-18) Hii ni kwasababu, Mungu anaheshimu sana matakwa na mahitaji ya watoto wake, maana anapenda kuiona furaha ya watoto wake.
Isa 45:11 ; 1Kor 7:39; Yak :16,  Luk 18:1,  Kol 4:2.
2.      Mwombe Mungu akuonyeshe au akukutanishe na mwenzi wako. (*Yer 33:3)
Kumwomba Mungu kusababisha mazingira ambayo yatawakutanisha na mtatambuana baada ya kupata ufahamu wa Mungu kwamba ‘you belong together’ yaani mnaendana, mnafanana, mnafaana na hivyo mnaweza kuishi pamoja vizuri. Hiyo ndiyo maana halisi ya kufunuliwa au kuonyeshwa. Japo Mung5 anaweza kukupa maono katika ndoto au katika maombi, lakini si lazhma iwe hivyo. Si kila mtu anaweza kupata maono kuhusu mwenzi wake. Soma Efe 1:15-19, Jab 32:,  Isa 43:26,  Isa 45:11
3.      Tengeneza marafiki. (*Mith 18:24, Mith 17:17)
Watu wengi humwomba Mungu kwa uaminifu sana ili wapate mwenzi wa maisha. Lakini wanfanya makosa ya kujifungia katika kisiwa cha upekee. Ni ngumu sana kuOnekana na kujulikana tabia na utu wako wa ndani kama hudachangamana na jumuiya za ma2afiki. MunGu ndiye chanzo cha urafiki. Hat Yesu alikuwa na marafiki wa kiume na waki kike pia. (Yoh 11:5).  Jithidi kufanya marafiki mvalimbali ila mwombe Mungu akupe marafiki wazuri. Mk 5:25 – (30) – 34; inasema, wengi walimgUsa Yesu na kumsUkuma-sukuma, lakini ni mmoja tuambaye atakuwa na mguso wa tofauti katika moyo wako.
ISHARA ZA KUTAMBUA (UPENDO WA) PENZI LA KWELI.
1.      Mtu huyo atakamata umakini wako na atakuvutia (attention).
2.      Atajaa moyoni na mwazoni mwako kuliko kawaida na wengine.
3.      Utatamani sana uwepo wake wakati wote (kuwa naye).
4.      Utapenda kuwasiliana naye mara kwa mara (kama hamko wote).
5.      Utakuwa na moyo wa kumjali, wema, zawadi na kujitoa sana kwa ajili yake.
6.      Utakuwa na heshima ya juu sanA, adabu, uTii na uaminifu sana kwake.
7.      Utakuwa na maneno mazuri, maneno laini, na maneno ya upendo kwake.
8.      Utakuwa na moyo/uwezo wa kumvumilia au kuchukuliana naye vile alivyo.
9.      Utakuwa na hamu ya kumgusa au kumshika kwa upendo (si tamaa).
10.  Utakuwa na moyo na utayari wa kumlinda Na kumhifadhi.
11.  Uhusiano wenu utapendeza mbele za watu wengi (si lazima wote)
12.  Utakuwa na amani na furaha ya ajabu moyoni mwako/mwenu.
Mungu alisema kwa mkono wa Mtume Paulokuuelezea Upendo kwA namna hii;
1 Cor 13 : 4-8(a)
*          Upendo huvumilia/subira  (Love is patient)
*          Upendo hufadhil)/hufania wema (Love is kind)
*          Upendo hauna husuda (Love doesn’t Envy)
*          Upendo haujivuni (Love is not proud)
*          Upendo haukosi adabu (Love is not rude)
*          Upendo hauna ubinafsi (Love is not selfish)
*          Upendo hauna uchungu (Love is not easily angered)
*          Upendo hauhesabu mabaya (Love doesn’t count wrongs)
*          Upendo haufurahii uovu (Love doesn’t rejoice with evil)
*          Upendo hufurahia ukweli (Love rejoices in truth)
*          Upendo unalinda (love always protects)
*          Upendo huamini yote (Love always trusts)
*          Upendo hutumaini (Love always hopes)
*          Upendo hustahimili (Love always perseveres)
5.  Omba ushauri kwa watu wanaokujua/wanaomjua huyo umpendaye.
2Kor 13:1; Zab 73:24; Mith 15:22
Ushauri kutoka kwa watu werevu wanaomjua Mungu na wanaowajua ninyi wawili utakuhibitishia kwamba ulichsikia mooni juu ya huyo mtu ni sahihi. Mashauri ya watu yanaweza kukusaidia kufanya maamuzi magumu nay a muhimu.
(Math 18:16;   1Tim 5:19;   Ebr 10:28; Fil 4:6-7, Kol 3:15 na Isa 55:12
6.  Mwendee na Useme naye kwa hekima.   (*Wimbo 3:1-4)
Baada ya maombi na subira, Mungu akuongoze kusema naye kwa wakati utakaoongozwa na Mungu. Uwe jasiri na muwazi. Lakini usemi wako uwe wa kawaida (simple). Usichague maneno magumu wala misamiati wala mafumbo. Uwe wazi na wa kawaida.
7.    Thibitisha uhusiano wako/wenu (kiofisi).  (*Wimbo 3:4)
Baada ya kuongea na kulitafakari pamoja kwa muda mtakaoona unatosha au unafaa, ni muhimu sana sasa mpelekane mbele, katika mamlaka zenu za kifamilia na kikanisa. Uhusiano mzuri usiwe wa mafichoni. Tunaona huyu mpenzi katika kitabu cha Wimbo anasema, anataka kumtafuta mpenzi wake, amshike mkono, wapelekane kwa wazazi. Huo ndio utaratibu mzuri kibiblia. Familia na kanisa watawasaidia kufuata taratibu za kiutamaduni na kiroho ili mhalalishwe kuwa mume na mke. Ndipo ndugu na marafiki mtawashirikisha mipango yote ili kuandaa harusi na makazi. 

NINA AMINI UMEELEWA.....NA HUO NDIO UPENDO BORA(QUALITY LOVE)
for more go http://quality-love.blogspot.com/   by chavala claun

No comments:

Post a Comment