Friday, November 30, 2012

Dk. Slaa ampa somo Mangula

SIKU chache baada ya Makamu Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Philip Mangula, kujibu mapigo ya wapinzani wake akisema wanaombeza wanasahau historia yake, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, amemtaka aweke mikakati hiyo katika vitendo.
Dk. Slaa alidai kuwa kwa sasa Watanzania wamechoka kusikiliza historia, hivyo kama Mangula ana uthubutu aanze kusafisha chama chake kwa kuwaondoa watuhumiwa magwiji wa ufisadi kabla ya kuhangaika na wale waliotoa rushwa kwenye uchaguzi wao.
Wakati Dk. Slaa akitoa somo hilo kwa Mangula, naye mwanasiasa mkongwe nchini, Thomas Nyimbo, amemvaa kigogo huyo wa CCM akisema kuwa ni kama anashindana na kivuli chake kwa kujidanganya kuwa ataitokomeza rushwa ndani ya chama hicho.
Kauli hizo zinakuja siku chache baada ya Mangula kakaririwa na vyombo vya habari akitamba kuwa wanaombeza kuwa hawezi kuitokomeza rushwa CCM wanasahau rekodi yake akiwa Katibu Mkuu wa chama hicho.
Mangula bila kumung’unya maneno aliwataja wafanyabiashara Yusuf Manji na Thomas Nyimbo kuwa ni miongoni mwa watu aliowafutia ushindi wasigombee ubunge baada ya kubainika kujihusisha na rushwa katika kura za maoni mwaka 2000.
Mwanasiasa huyo pia alikumbushia jinsi chama kilivyofuta matokeo ya baadhi ya washindi katika majibo 32 na kuamuru uchaguzi urudiwe baada ya kubaini uwepo wa mizengwe ya rushwa, hivyo akaahidi kuwa wanaombeza wangoje waone ndani ya miezi sita atakavyochukua hatua.
Hata hivyo, katika mahojiano yake na gazeti hili jana, Dk. Slaa aliendelea kumbeza Mangula akisema kama anajisifu kuwa anaweza kuondoa wala rushwa katika CCM, basi aanze na watuhimiwa sugu walioshindikana kung’oka kwenye falsafa ya kujivua gamba.
Alisisitiza kuwa anamshangaa Mangula kwa kujisifu kwa jambo hilo, na kwamba kama kweli anaweza basi atekeleze sera ya kujivua magamba iliyomshinda mtangulizi wake Pius Msekwa na Wilson Mukama.
Alisema kuwa watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho ambao wametajwa hadi na wana-CCM wenyewe bado wapo na wanaendelea vema na kazi za kila siku.
“Hivyo kama Mangula ana ubavu aanze na hawa aache kujisifia historia, mambo anayoyataja kwanza Watanzania wengi hawayajui, wanataka kuona sasa,” alisema.

Palestina yapandishwa hadhi na UN,Palestinian Statehood: Tanzania Votes YES At UN


Wapalestina walisherehekea sana kufuatia tangazo hilo
Baraza la umoja wa mataifa limepitisha kwa kauli moja kwa wingi wa kura kupandisha hadhi ya eneo la Palestina.
Nchi mia moja thelathini na nane ziliunga mkono hatua ya kuitambua Palestina kuwa nchi ambayo si mwanachama wa Umoja wa mataifa lakini itaruhusiwa kushiriki katika shughuli za umoja wa mataifa.
Mataifa tisa yakijumuisha Isarael na Marekani yalipiga kura ya kupinga mpango huo huku mataifa arobaini na moja yakisusia shughuli hiyo.
Kura hiyo yenye umuhimu mkubwa sasa inaiwezesha Palestina kuwa na ushirika na umoja wa mataifa na mashirika mengine kama vile mahakama ya ICC.
Mwandishi wa BBC amesema kuwa wapelestina wanaweza kutumia nafasi hayo kuishataki Israel kwa kusababisha visa vya dhulma dhidi ya ubinadamu katika ngome yake.

 

Bunge la USA kujadili vikwazo dhidi ya Iran

Bunge la Senate nchini Marekani litajadili vikwazo vipya vilivyowekewa Iran kwa lengo la kuikomesha nchi hiyo kuendelea kuzalisha madini ya uranium ili itengeneze silaha za kinyuklia.
Vikwazo hivyo vipya, vilivyowasilishwa katika bunge la Senate la Marekani hapo jana, ni pigo kwa sekta ya kawi nchini Iran.
Vikwazo vya awali vilipunguza kwa kiasi kikubwa mauzo ya mafuta nje ya Iran na kuathiri uchumi wake. Tehran inasisitiza kuwa mpango wake wa kinyuklia ni kwa manufaa ya wananchi wa Iran.

Bakwata yamkana Sheikh Ponda mahakamani

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), limemkana Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake, baada ya kudai mahakamani kuwa eneo walilovamia wakidai ni mali ya Waislamu linamilikiwa kihalali na kampuni ya Agritanza.
 

Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Suleiman Lolila alisema hayo jana wakati akitoa ushahidi katika kesi ya jinai inayomkabili Ponda na wenzake 49 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakidaiwa pamoja na mambo mengine kuvamia na kupora ardhi na wizi wa vifaa vya ujenzi.

Akitoa ushahidi wake jana huku akiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka, Lolila ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka alidai kuwa eneo hilo awali lilikuwa likimilikiwa kihalali na Bakwata.

Hata hivyo, alidai kuwa baadaye Bakwata walibadilishana na Kampuni ya Agritanza Limited baada ya kuona eneo lililobaki halifai kujengwa chuo kikuu kutokana na ufinyu wake.
Alidai kuwa awali eneo hilo lilikuwa kubwa lakini miaka ya 2000 lilianza kumegwa na kuzigawia baadhi ya taasisi na wafanyabiashara na kwamba tume iliundwa na kubaini kwamba hayo yalifanyika kinyume na utaratibu.

“Baada ya kumegwa eneo lililobakia ni finyu ambalo halitoshi kujengwa chuo kikuu. Mimi nilikuwapo wakati Baraza la Wadhamini wa Bakwata wakijadili jinsi ya kupata eneo kubwa na kuijadili Kampuni ya Agritanza iliyokuwa na eneo la ekari 40 Kisarawe ili tubadilishane,” alidai.

Shahidi huyo aliongeza kuwa Agritanza ilikubali kubadilishana maeneo na kwamba wao walichukua ekari nne zilizopo Markaz (Chang’ombe) na Bakwata ikachukua ekari 40 zilizopo Kisarawe.

“Hayo yalifanyika baada ya kupata baraka kutoka katika Baraza la Maulamaa lililokaa na kuamua hivyo Januari 22, 2011,” alisema shahidi huyo na kuongeza:
“Baada ya kufanyika mabadilishano, Agritanza walianza kushughulikia usajili wa kiwanja namba 311/3/4 na walipata. Hivyo kwa sasa ni wamiliki halali, tulishamalizana nao.”

Shahidi huyo aliendelea kudai kuwa eneo hilo Serikali ililitoa kwa Wamisri kwa ajili ya kujenga chuo chini ya usimamizi wa Bakwata.
Alidai kuwa kwa mujibu wa mkataba huo uliosainiwa mwaka 2003, endapo Wamisri wataondoka Tanzania watarejesha eneo hilo katika umiliki wa Bakwata.
Shahidi huyo pia alitoa kielelezo cha makubaliano ya Baraza la Wadhamini wa Bakwata na Agritanza, kuhusu kubadilishana uwanja.

Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Juma Nassoro alipinga kwa madai kwamba kisheria walitakiwa kutoa notisi kabla ya kuwasilisha kielelezo hicho mahakamani.

Akijibu hoja hizo, Wakili Kweka alidai kuwa barua halisi wanayo na kwamba ipo katika kumbukumbu za Bakwata, huku akisisitiza kuwa shahidi anastahili kutoa kielelezo hicho kwa sababu saini yake ipo.

Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa anayesikiliza kesi hiyo, alikikataa kielelezo hicho akisema Serikali ilitakiwa kutoa notisi kabla ya kuwasilisha kielelezo hicho.

Hakimu Nongwa alisema kwa kuwa barua halisi ipo wanatakiwa kuiwasilisha mahakamani, lakini akasema endapo barua halisi haipo, basi taarifa ya jana itatambulika kuwa notisi na wataruhusiwa kuiwasilisha.

Hatutoi sasa majina ya walioficha fedha Uswiss

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika (Chadema) amesema licha ya kuwa na orodha ya vigogo walioficha fedha Uswiss, lakini hawezi kutoa orodha ya majina hayo kama Serikali inavyotaka kwa vile orodha ya vinara wa ufisadi ambayo ilitajwa Mwembe Yanga bado haijashughulikiwa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Sahara jijini Mwanza, Mnyika alisema kwamba kama Serikali ya CCM inasisitiza kutaka majina ya walioficha fedha huko Uswiss yatajwe, wanapaswa kusimama na kueleza ile orodha ya mafisadi ambayo Chadema waliitaja pale Mwembe Yanga imefanyiwa kazi gani.

“Watu wanapotutaka tutaje majina, na sisi tunawambia kwanza wasimame na kutueleza ile ‘list’ (orodha) ya mafisadi ambayo tuliitaja kwa majina wameishughulikia vipi?” alihoji Mnyika na kuongeza kwamba wanajua jinsi ambavyo CCM wanalivyonufaika na ufisadi kupitia Kampuni ya Kagoda jambo ambalo linadhihirisha kuwa haiwezi kuwa rahisi kwao kushughulika na vita ya ufisadi.

Alisisitiza kuwa wanaotaka majina yatajwe wanayo ajenda yao na wao wameshaifahamu hivyo hawatashughulika nayo na kusema ukifika wakati ambao wao wanautambua wataweka kila kitu nje, lakini siyo kwa kushinikizwa na Serikali ya CCM.

“Tunajua serikali hii inayoundwa na Chama Cha Mapinduzi haina dhamira ya kushughulika na ufisadi, na hili ndilo litakalowaondoa madarakani,” alifafanua.

Hata hivyo mkutano huo uliingia dosari wakati Mnyika akiendelea kuhutubia ambapo mawe yalianza kurushwa na vijana wanaodaiwa kuwa ni vijana wa Diwani wa Kata ya Kitangiri kwa tiketi ya Chadema, Henry Matata aliyevuliwa uanachama.

Kutokana hali hiyo vijana wa Chadema walizungumza katika maeneo mbalimbali na kufanikiwa kuwanasa vijana wawili ambao walishambuliwa na kueleza na kunusuriwa na Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje aliyeita polisi na kuwaomba waache kuwashambulia.

Awali akizungumza katika mkutano huo Mbunge wa Jimbo la Nyamagana,Wenje alieleza wananchi kuwa katika mkakati wake wa kuboresha elimu ya msingi na sekondari amefanikiwa kutengeneza madawati mengine 400 baada ya madawati ya awali 500 kugawiwa katika shule.

Alisema madawati hayo yatagawanywa kwa shule 30 za wilaya ya Nyamagana na kubainisha kwamba kutokana na madaati ya awali 500 kutolewa bila utaratibu na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza,Wilson Kabwe hivyo madawati haya alieleza kuwa yatasambazwa na madiwani wa Chadema katika shule pamoja na katibu wa ofisi yake ili kuhakikisha yanafika katika shule husika iliyopangwa.

Mmiliki gari lililomuua Sharo Milionea aibuka na kukubali asara hatamdai mtu.

MMILIKI wa gari ambalo lilikuwa likiendeshwa na msanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ na kupata nalo ajali iliyosababisha kifo chake huko Muheza, Tanga, Mohammed Ismaili maarufu kwa jina la Mudi Suma, ameibuka na kueleza uhusiano wake na marehemu, huku akisema amekubali hasara.

Akizungumza kwa simu kutoka Muheza jana Suma alisema hana mpango wa kudai fidia au kupeleka malalamiko yoyote kwa ndugu wa marehemu kwa kuwa; “Kilichotokea ni kazi ya Mungu.” “Siwezi kudai hata kidogo hivyo ni vitu vya kupita tu. Marehemu alikuwa ni zaidi ya ndugu yangu, gari ni kitu kidogo sana katika uhusiano tuliokuwa nao,” alisema Suma na kuongeza kwamba hata Marehemu Sharo Milionea naye alikuwa amemwachia mali zake kadhaa ikiwamo gari.

“Siyo gari tu alilokuwa ameniachia. Kuna mikataba yake ya kazi, Bajaji yake na funguo za chumbani kwake. Nasubiri kukabidhi vitu hivyo baada ya kukaa na ndugu zake. Vitu viko kwenye mikono salama,” alisema.

Kuhusu gari lake lililopata ajali, Suma alisema lilikuwa na bima ndogo, lakini anapanga kwenda TRA atakaporejea Dar es Salaam kufuatilia baadhi ya mambo.
“Kabla ya kuondoka bima ile kubwa ilikuwa imekwisha kwa hiyo nikaamua kuikatia bima ndogo. Nitakapofika kesho (leo) Dar es Salaam, nategemea kwenda ofisi za bima kuzungumza nao,” alisema Suma.

Alipoulizwa kama kuna mtu mwingine atakayeathirika kutokana na gari hilo kuharibika katika ajali mbali na yeye, alijibu: “Hakuna tofauti na mimi mwenyewe na familia yangu.”

Kabla ya ajali
Suma alieleza kuwa kabla ya kuanza safiri yake, Sharo Milionea alifika nyumbani kwake mchana na kumweleza kuwa afya yake haikuwa nzuri.

“Kabla ya kuondoka aliniambia kuwa hajielewi elewi na kifua kilikuwa kinambana. Nikamshauri asiondoke peke yake, atafute mtu wa kuondoka naye ambaye atamsaidia kuendesha gari njiani,” alisema Suma na kuongeza:

“Tulianza kuwapigia simu jamaa zetu wanne wa kusafiri naye lakini kila tuliyemwambia hakuwa tayari. Ilikuwa ni changamoto mpaka ilipofika saa 10:45 hivi jioni, akaamua kuondoka peke yake. Wakati anatoa gari getini kwangu, nikamwambia, basi jaribu kuwa mwangalifu sana, maana alikuwa kweli anasumbuliwa na kifua. Tukakubaliana kwamba atakaporudi aende hospitali kucheki afya yake.”

Kuhusu uhusiano wake na marehemu, Suma alisema: “Mimi ni mfanyabiashara na yeye alikuwa msanii, lakini ilitokea tukawa marafiki sana mpaka ikafikia wakati nikaona kuwa ni ndugu yangu. Nilimwamini nikamtambua kama sehemu ya familia.”

Alisema marehemu alikuwa akitumia gari hilo kila alipolihitaji na safari ya kwenda nalo Tanga kwa wazazi wake ilikuwa ni ya tatu.“Siyo mara ya kwanza kuitumia gari lile, nilikuwa nimemwamini sana. Safari ya kwanza alichukua na kusafiri nalo mwenyewe, halafu safari ya pili ikafuata na hii ilikuwa safari ya tatu,” alisema Suma.

Eneo la ajali wakimbia makazi
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Songa Kibaoni mahala ambako Sharo Milionea alipatia ajali, wamezikimbia nyumba zao baada ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu kutoa siku moja kwa waliopora mali za marehemu huyo kuzisalimisha mara moja.

Mgalu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Muheza alisema jana kwamba usiku wa kuamkia jana, baadhi ya nyumba kijijini hapo zilikuwa tupu baada ya wakazi wake kuzikimbia.

‘Serikali imezidi kudhihirisha udhaifu’ asema Mnyika

MBUNGE wa Ubungo (Chadema), John Mnyika amesema ukiukwaji wa sheria wa matumizi ya Sh96 bilioni katika ununuzi wa mafuta mazito ya uendeshaji wa mitambo ya kufua umeme wa dharura ni matokeo ya Serikali kuwa dhaifu.
 

Amesema udhaifu huo unatokana na Serikali kushindwa kuzingatia utawala wa sheria, huku akilishukia Bunge kwamba nalo limefanya uzembe katika kusimamia utekelezwaji wa maazimio yake.

Kauli hiyo ya Mnyika ambaye ni Waziri kivuli wa Nishati na Madini imekuja siku chache tangu gazeti la East African kutoa taarifa kwamba jumla ya Dola54milioni zimegundulika kuibwa, watumishi waandamizi wa Wizara ya Nishati na Madini na Tanesco kupitia manunuzi ya mafuta ya kuendeshea mtambo wa umeme wa IPTL.

Gazeti hilo lilinukuu taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh ikieleza kuwa kuna kikundi ambacho kazi yake ni kujinufaisha na mpango huo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mnyika alimtaka Rais Jakaya Kikwete aagize ripoti ya CAG iwekwe wazi, kuchukuliwa hatua kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa waziri wa Wizara hiyo, William Ngeleja.

“Spika wa Bunge anatakiwa kuifuatilia wizara hii pamoja na ile ya Fedha kuhusu ufisadi huu,” ilieleza taarifa hiyo na kuongeza;
“Rais Kikwete atumie mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba ibara za 33, 34, 35, 36 na 143 (4), aagize kuwekwa hadharani kwa ripoti ya ukaguzi maalum (Special Audit) uliofanyika mwaka 2011 kuhusu tuhuma za ufisadi na ukiukwaji wa sheria katika ununuzi wa mafuta mazito ya kufua umeme wa dharura katika mitambo ya IPTL.”

Katika taarifa hiyo Mnyika amemtaka Rais Kikwete azielekeze mamlaka na vyombo husika kumchunguza Ngeleja kwa kuwa tuhuma hizo zilitokea wakati akiwa waziri.
“Ripoti ya ukaguzi maalumu (special audit) ya mwaka 2012, ile ya uchunguzi wa Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA) kuhusu suala hilo ziwekwe wazi” ilieleza taarifa hiyo.

Mbunge huyo alimtaka Spika Makinda naye anatakiwa kuitisha haraka kikao cha kamati mojawapo ya kudumu ya Bunge ili kuepusha udhaifu na uzembe unaoendelea kwa sasa kwa kuwa moja ya mamlaka ya Bunge ni kuisimamia Serikali.
“Juhudi hizi zinatakiwa kufanyika kwa haraka ili wizara husika itueleze kinachoendelea” ilieleza taarifa hiyo.

Mbunge huyo aliwahi kumuandikia barua Spika wa Bunge mwezi mmoja uliopita akimtaka atumie madaraka yake kukabidhi usimamizi na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme katika moja ya Kamati za kudumu za bunge.

Inaeleza kuwa sasa anakusudia kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Spika kuhusu tuhuma za baadhi ya wabunge na na umuhimu wa hoja ya kutaka Bunge liazimie kuunda kamati Teule kuchunguza masuala yote ya ukiukwaji wa sheria, matumizi mabaya ya madaraka na tuhuma za ufisadi.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa uchunguzi huo umhusishe Mkaguzi mkuu ili kuchunguza malipo yaliyofanywa kampuni za BP (Sasa PUMA Energy), Oryx na Camel Oil ili kubaini kama kuna vigogo zaidi wa Serikali waliojinufaisha kwa kisingizio cha dharura ya umeme.

Ushahidi mpya wa mauaji ya Mau Mau

Baadhi ya wapiganaji wa Mau Mau waliodhulumiwa na wakoloni wa Uingereza
Stakabadhi za Serikali zilizotolewa huko Uingereza zinaonyesha kwa ukamilifu namna wafungwa wengi waliuawa wakati wa uasi wa kundi la Mau Mau nchini Kenya.
Wakenya kumi na mmoja walipigwa na walinzi hadi kufa katika kambi walikozuiliwa ya Hola huku wengine wakijeruhiwa mwaka 1959.
Mzee moja manusura wa mauaji hayo kwa sasa ameshtaki serikali ya Uingereza akidai aliteswa.
Stakabadhi hizo zinaonyesha mkutano uliongozwa na aliyekuwa gavana wa Kenya na maafisa wakuu wa magereza kumbukumbu zinazoonyesha kuwa maafisa hao walikiuka haki za binadamu lakini hawakufunguliwa mashtaka.

Makaburi zaidi ya 100 yafukuliwa nchini Benin

                    Voodoo nchini Benin
Zaidi ya makaburi 100 yamefukuliwa katika eneo la makaburi karibu na mji mkuu wa Benin, Porto-Novo, polisi wamesema.
Wahalifu hao, waliofanya kitendo hicho, pia walivikata vichwa vya miili hiyo na kuiba baadhi ya viungo vyao vya ndani.
Mwandishi habari wa BBC Vincent Nnanna, aliyeko Benin, alisema inashukiwa kwamba uhalifu huo una uhusiano fulani na itikadi za kichawi zijulikanazo kama Voodoo, zinazotumia viungo vya miili ya wanadamu kama hirizi.
Hii ndiyo mara ya kwanza kwa kisa kama hiki kutokea nchini humo, ambapo Voodoo ni dini rasmi, Nnanna aliendelea kusema.
Kuna zaidi ya Voodoo 100 zinzaowakilisha maswala tofauti. Kwa mfano, Gou huwakilisha vita na masonara, na Sakpata huwakilisha ugonjwa, uponyaji na dunia.
Kuhuzunishwa
Mwandishi wetu anasema makaburi hayo yalipatikana na mwashi aliyekuwa amesahau ala zake za kazi katika eneo hilo la makaburi lililoko Dangbo, karibu na Porto-Novo.
Ndugu za maiti hao wamehuzunishwa sana kwa sababu wanaamini kwamba baada ya kufariki roho ya mtu huweza kuzaliwa tena katika kiumbe kingine. Wanahofia kwamba wapendwa wao watazaliwa upya pasipo na viungo vilivyibwa.
Kasisi mkuu wa Voodoo aliiaambia BBC kwamba visa kama hivyo havikubaliki katika imani hiyo – na akashutumu uhalifu huo.
Wafuasi wa Voodoo – ambao ni asilimia 40 ya idadi ya watu wote nchini Benin – wanaamini kwamba maisha yote huendeshwa na nguvu za pepo ya malihai kama maji, moto, dunia na hewa.

Wednesday, November 28, 2012

Obama meets with business leaders and middle class Americans

President Barack Obama, Vice President Joe Biden and Secretary of the Treasury Tim Geithner meet Wednesday with business leaders to discuss ways to avoid the "fiscal cliff" and keep the economy growing. The group includes Frank Blake of The Home Depot, Lloyd Blankfein of Goldman Sachs Group, Joe Echeverria of Deloitte, Muhtar Kent of Coca Cola and Marissa Mayer of Yahoo.
Obama delivers remarks earlier in the day at an event with middle class Americans who would see their taxes go up if Congress fails to extend the expiring George W. Bush-era tax cuts.
The tax cuts, set to end Jan. 1, and deep spending cuts, scheduled to go into effect Jan. 2, make up the fiscal cliff.
 President Barack Obama gestures as he speaks in the Eisenhower Executive Office Building, on the White House campus in Washington, Wednesday, Nov. 28, 2012, about how middle class Americans would see their taxes go up if Congress fails to act to extend the middle class tax cuts. The president said he believes that members of both parties can reach a framework on a debt-cutting deal before Christmas.  (AP Photo/Susan Walsh)
Members of the Campaign to Fix the Debt, including Erskine Bowles, former co-chair of the National Commission on Fiscal Responsibility and Reform, will be on Capitol Hill on Wednesday for meetings with House Speaker John Boehner and Republican leadership, and with House Minority Leader Nancy Pelosi and Democratic leadership. The mission: Urge member members of Congress to reach a deal on avoiding the fiscal cliff during the lame duck session.
And that's not the extent of the fiscal cliff talk on Wednesday. Back at the White House, Vice President Biden will meet with the AFL-CIO Executive Council for talks on deficit reduction and tax cuts.
And then there is this: First lady Michelle Obama will welcome military families to the White House on Wednesday for the first viewing of the 2012 holiday decorations. This year's White House Blue Room Christmas Tree pays tribute to armed forces and features ornaments decorated by children living on U.S. military bases all over the world.
And this: Minnesota Democratic Sens. Amy Klobuchar and Al Franken will host a remembrance event marking the 10th anniversary of the plane crash that killed Sen. Paul Wellstone, his wife, their daughter, and three campaign staffers.

2013 Postgraduate Diplomas Scholarships Open for Application!

THE MOMENT OF TRUTH: 2013 Postgraduate Diplomas Scholarships Open for A... http://t.co/e9K4tJrI
themomentoftruthtz.blogspot.com

Obama, Romney to meet at White House Thursday

WASHINGTON (AP) — President Barack Obama will host his former political rival Mitt Romney for a private lunch at the White House Thursday, their first meeting since the election.
 FILE - In this Oct. 16, 2012 file photo, President Barack Obama and Republican presidential candidate, former Massachusetts Gov. Mitt Romney exchange views during the second presidential debate at Hofstra University in Hempstead, N.Y. President Barack Obama will host his former political rival Mitt Romney for a private lunch at the White House Thursday, Nov. 29, 2012, their first meeting since the election. (AP Photo/David Goldman, File)
Obama promised in his victory speech earlier this month to engage with Romney following their bitter campaign and consider the Republican's ideas.
"In the weeks ahead, I also look forward to sitting down with Gov. Romney to talk about where we can work together to move this country forward," Obama said at the time.
Obama aides said they reached out to Romney's team shortly before Thanksgiving to start working on a date for the meeting. The two men will meet in the White House's private dining room, with no press coverage expected.
In the days after his loss, Romney told top donors that the president was re-elected because of the "gifts" Obama provided to blacks, Hispanics and young voters, all of which are core Obama constituencies.
"The president's campaign, if you will, focused on giving targeted groups a big gift," Romney said.
Many Republican officials, eager to move on quickly after the loss, disputed Romney's comments and urged the party to focus on being more inclusive.
White House spokesman Jay Carney said Obama was looking forward to having a "useful discussion" with his former competitor. But he said there was no formal agenda for the lunch.
While in Washington, Romney will also meet with his former running mate, Wisconsin Rep. Paul Ryan, according to a Romney campaign aide. Ryan is back on Capitol Hill, where he's involved in negotiations to avert a series of automatic tax increases and deep spending cuts that have come to be known as the "fiscal cliff."
Much of that debate centers on expiring tax cuts first passed by George W. Bush. Obama and Romney differed sharply during the campaign over what to do with the cuts, with the Republican pushing for them to be extended for all income earners and the president running on a pledge to let the cuts expire for families making more than $250,000 a year.
The White House sees Obama's victory as a signal that Americans support his tax proposals.
Obama and Romney's sit-down Thursday will likely be their most extensive private meeting ever. The two men had only a handful of brief exchanges before the 2012 election.
Even after their political fates became intertwined, their interactions were largely confined to the three presidential debates.
Romney has virtually disappeared from politics following his loss in the Nov. 6 election. He's spent the last three weeks largely in seclusion at his family's southern California home. He has made no public appearances, drawing media attention only after being photographed at Disneyland in addition to stops at the movies and the gym with his wife, Ann.
Former aides confirm that Romney is expected to move into an office at the Boston-area venture capital firm Solamere Capital. The firm was founded by his oldest son, Tagg Romney, and Spencer Zwick, who served as his presidential campaign's national finance chairman.
It's unclear what role, if any, Romney will play at the firm. Former aides said Romney was subletting office space from Solamere.

Dk. Slaa kinara urais 2015 • Matokeo kura za maoni yawataja Lowassa, Membe na Zitto Kabwe

WAKATI mjadala wa nani anafaa kuwa Rais wa awamu ya tano wa Serikali ya Jamhuri ya Mungano unashika kasi kila kona ndani na nje ya nchi, jina la Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa limeng’ara, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Pamoja na uwepo wa vyama 18 vya siasa vyenye usajili wa kudumu, mjadala wa nani anafaa kuwa Rais ajaye, umejikita kwenye vyama vikubwa viwili, kikiwemo Chama tawala cha Mapinduzi (CCM) na Chama Kikuu cha Upinzani cha CHADEMA.
Kwa mujibu wa kura za maoni zilizoendeshwa na mtandao maarufu dunaini wa Jamii Forum kwa kuuliza “Nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA na CCM”, majina manne yalipambanishwa, mawili kutoka CCM na mawili CHADEMA.
Waliopambanishwa kutoka CCM ni pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, ambao wamekuwa wakitajwa kuibua makundi yanayosigana kutaka urais mwaka 2015.
Licha ya kuwapo majina mengine yanayotajwa kufaa kuwania urais ndani ya CCM, wapambe wa Lowassa na Membe, wamekuwa katika mvutano mkali na wa wazi na kuibua mpasuko mkubwa ambao ulionekana wazi hata wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma.
Baadhi ya majina mengine yanayotajwa kuutaka urais CCM ambayo hayakushindanishwa kwenye kura hizi za maoni ni pamoja na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuri, Steven Wassira, Dk. Emmanuel Nchimbi, Frederick Sumaye na Dk. Asha Rose Migiro ambaye hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete alimteua kuwa mjumbe wa Sekretarieti ya CCM, akiongoza idara ya mambo ya nje.
Nafasi hiyo inampa sifa Dk. Migiro kuingia kwenye vikao muhimu vya chama vya Halmashauri Kuu (NEC) na Kamati Kuu (CC).
Kwa upande wa CHADEMA, kura za maoni zilizoanza Julai, mwaka huu, ziliwakutanisha Katibu Mkuu na mgombea urais mwaka 2010, Dk. Slaa na Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, Zitto Kabwe.
Katika siku za hivi karibuni, Zitto amekuwa akijinasibu kutaka kuwania urais mwaka 2015 na kupendekeza sifa ya umri wa kugombea kiti hicho upunguzwe kutoka miaka 40 hadi 35.
Hata hivyo majina mengine yanayotajwa kufaa kuwania urais ndani ya CHADEMA na ambayo hayakushirikishwa kwenye kura hizo za maoni ni pamoja na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, ambaye yuko nyuma ya mafanikio yote ya CHADEMA hadi kufikia hatua hii. Katika ordha hiyo, pia yumo Mbunge wa Singida Vijijini, Tundu Lissu.
Matokeo ya kura hizo za maoni, yanaonyesha kuwa jumla ya wapiga kura 1188 walishiriki kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA, Dk. Slaa na Zitto, wakati wapiga kura 375 walishiriki kuwapigia Lowassa na Membe, wote kutoka CCM.
Kwa upande wa CHADEMA, matokeo yanaonyesha kuwa Dk. Slaa alipigiwa kura 1,007, sawa na asilimia 84. 76% wakati Zitto, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, aliibuka na kura 181, sawa na asilimia 15.
Kwa upande wa CCM, jumla ya washiriki 375 walipiga kura na kati yao, washiriki 164, sawa na asilimia 43.73 walimpigia Lowassa wakati Waziri Membe aliibuka na kura 67, sawa na asilimia 17.87.
Aidha kwa mujibu wa matokeo hayo, wapiga kura 144 walipiga kura ya kutomuunga mkono mgombea yeyote kati ya Membe na Lowassa.
Matokeo ya jumla yanaonyesha kuwa Dk. Slaa aliibuka na ushindi mkubwa wa kura 1,007 kwa kupigiwa kura nyingi zaidi kuliko majina ya washiriki wengine waliopendekezwa kuingia kwenye mnyukano huo.
Mshindi wa pili ni Zitto mwenye kura 181, watatu ni Lowassa mwenye kura 164 na Waziri Membe anashika nafasi ya nne kwa kura 67.
Licha ya kupata kura chache kwenye mchuano huo, jina la Waziri Membe limekuwa likitajwa zaidi tangu alipoibuka mshindi kwenye nafasi ya ujumbe wa NEC kupitia kundi maalum (Kundi la Kifo), licha ya kupigiwa kampeni chafu na mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM), Hussein Bashe, ambaye bila kumung’unya maneno alitamba kumpigia kampeni za kumwangusha asishinde nafasi hiyo.
Hata hivyo matokeo ya kura hizo za maoni sio rasmi kwani kati ya majina yote yaliyoshirikishwa kwenye kura hizo, hakuna hadi sasa aliyekwishatangaza nia ya kuwania urai 2015.

Agizo la Magufuli kukamata magari ya Serikali utata

UTEKELEZAJI wa zoezi la kukamata watumishi wa Serikali wanaotumia namba za kiraia kwenye magari ya umma kinyume cha sheria na utaratibu, unasuasua kutokana na kuwapo kwa taarifa za kutatanisha kuhusu kufanyika kwa kazi hiyo.
 

Taarifa zilizopatikana zinaeleza kuwa tangu Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli atangaze kufanyika kwa zoezi hilo akishirikiana na polisi, baadhi ya maofisa wa Serikali walibadilisha namba kimyakimya bila kutolewa taarifa yoyote.

Chanzo chetu cha habari kutoka Wizara ya Ujenzi, kimeeleza kuwa katika kazi hiyo, Dk Magufuli alitaka liwe linatangazwa na kufanyika mara moja.
Kilisema, badala yake inafanyika kwa siri na hakuna taarifa zinazotolewa waziwazi juu ya utekelezaji.

“Sijui nini kimetokea, tunaona zoezi liko kimya taarifa hazieleweki, tulisikia kuwa taarifa kuhusu zoezi hilo lilikuwa limeandaliwa na wizara, lakini mpaka sasa haijatolewa na hakuna kitu kinaendelea, nadhani kutakuwa kuna kitu kimetokea,”kilisema chanzo hicho
na kuongeza;

“Kila mtu wizarani ukimuuliza kuhusu zoezi hilo haelewi kinachoendelea.”
Lakini taarifa zilizopatikana kutoka vyanzo vingine vya habari zilieleza kuwa karibu magari 400 yamejiandikisha kupata namba za Serikali tangu zoezi la kakamatwa litangazwe.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Jerryson Lwenge alipoulizwa juu ya zoezi hilo alisema kuwa atafutwe naibu katibu mkuu wa wizara hiyo, John Ndunguru kwa kuwa ndiye anashikilia ofisi ya katibu mkuu kwa sasa.
“Sisi tupo Kenya kwenye mambo ya Afrika Mashariki mtafute naibu katibu mkuu ndiye anayeweza kukupa taarifa,” alisema Lwenge.

Hivi karibuni, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, John Ndunguru alivieleza vyombo vya habari kwamba Serikali iliweka utaratibu unaozuia matumizi ya namba za kiraia kwenye magari yake isipokuwa kwa kibali maalumu.

Alisema kuwa hali ya kuzuia namba hizo iliibuka baada ya kubainika kwamba kupitia namba hizo, magari ya umma yanatumika vibaya na baadhi kupotea.

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga alisema Waziri alitarajiwa kutoa ripoti jinsi zoezi hilo linavyoendelea kwa kuwa Waziri mwenyewe ndiye anatakiwa kuzungumzia suala hilo.

Alisema zoezi la ukamataji magari linaendelea kwa muda wa miezi mitatu mfululizo lakini hakusema idadi ya magari yaliyokamatwa hadi hivi sasa.

Safari ya mwisho ya Sharo Milionea

MAELFU ya waombolezaji jana walijitokeza kushiriki mazishi ya msanii Hussein Ramadhan maarufu kwa jina la Sharo Milionea, huku mamia wakizirai baada ya kushindwa kujizuia wakati mwili wake unawekwa kaburini.
Maelfu ya waombolezaji jana walijitokeza kushiriki mazishi ya msanii Hussein Ramadhan maarufu kwa jina la Sharo Milionea, huku mamia wakizirai baada ya kushindwa kujizuia wakati mwili wake unawekwa kaburini. 

Mwili wa msanii huyo ulizikwa jana kijijini kwake Lusanga wilayani Muheza saa 7 mchana, katika tukio lililomshirikisha Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye ambaye alimwakilisha mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.

Waombolezaji walianza kumiminika kijijini Lusanga tangu juzi jioni na idadi yao iliongezeka zaidi jana asubuhi. Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi.Sala ya mazishi iliongozwa na Sheikh Twaha Juma ambaye baadaye aliamuru jeneza hilo kupelekwa makaburini, ambako waombolezaji kadhaa walipoteza fahamu.

20 wapelekwa hospitali
Miongoni mwa matukio yaliyojitokeza katika msiba huo ni baadhi ya waombolezaji kupoteza fahamu msibani.Matukio tofauti ya watu kuzirai yalitokea wakati mwili wa msanii huyo ulipokuwa unapelekwa nyumbani kwao kijijini Lusanga ukitokea Hospitali Teule ya Wilaya ambako ulihifadhiwa tangu alipopata ajali Jumatatu usiku na wakati wa mazishi.

Miongoni mwa waliopoteza fahamu katika msiba huo ni wasanii na waigizaji wa filamu waliokuwa wakiigiza na Sharo Milionea wakati akiwa katika kundi la AL Riyam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na MC wa shughuli hiyo, Steve Nyerere, zaidi ya watu 20 walipoteza fahamu katika msiba huo na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

DC Mgalu aliwaomba waombolezaji kutokuwa na shaka juu ya waliopoteza fahamu kwa kuwa madaktari maalumu walikuwa wameandaliwa hospitalini hapo kwa ajili ya kuwapa huduma.
Mwananchi lilifika katika hospitali Teule na kukuta waliokuwa wamepoteza fahamu, wengi wao wakiwa ni wasichana, wakipata huduma huku wengine wakiomba kupewa ruhusa ili wakahudhurie maziko.

JK atuma rambirambi
Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kutokana na vifo vya wasanii watatu vilivyotokea hivi karibuni, kikiwamo cha Sharo Milionea.

Taarifa iliyotolewa jana Dar es Salaam na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilisema kuwa Rais Kikwete ameshtushwa na vifo hivyo vya ghafla.
Wasanii hao ambao walifariki dunia katika mazingira tofauti ni Mwigizaji wa Kundi la Kaole, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ aliyefariki dunia hivi karibuni kutokana na maradhi yaliyokuwa yanamsumbua kwa muda mrefu.

Msanii mwingine ni mwigizaji wa filamu, John Maganga aliyefariki Novemba 24, 2012 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu.
“Nimeshtushwa na kuhuzunishwa mno kutokana na taarifa za vifo vya wasanii hawa ambao kwa hakika mchango wao mkubwa katika tasnia ya muziki na maigizo hapa nchini ulikuwa unatambuliwa na kuthaminiwa na wananchi wengi,” ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.

Vile vile, mke wa Rais Kikwete, Mama Salma alituma salamu za rambirambi zilizosomwa na DC Mgalu, kuwa ameguswa na msiba huo na kuwataka ndugu wa marehemu na wasanii wengine kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu.
Kwa mujibu wa Mgalu, Mama Salma alituma salamu hizo akiwa Mwenyekiti wa Mfuko wa Wanawake na Maendeleo (WAMA).

“Mke wa Rais kama mnavyojua ni mama wa Watanzania wote na ni mama wa wasanii, hivyo msiba huu wa Sharo Milionea umemgusa sana na ameitaka familia ya marehemu kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki cha majonzi,” alisema Mgalu.

Wenye sare za CCM
wazomewa
Katika msiba huo watu waliokuwa wamevalia sare za CCM walijikuta katika wakati mgumu baada ya kuzomewa na waombolezaji ambao walisema hakukuwa na haja ya kujitambulisha kiitikadi katika msiba huo.

Kundi la vijana waliokuwa kando ya barabara ielekeayo kitongoji cha Jibandeni, nyumbani kwa mama mzazi wa marehemu, waliwazomea watu hao huku wakisema kuwa huo haukuwa msiba wa CCM bali ni wa wasanii wa filamu.

Vijana hao walieleza kushangazwa kwao na kitendo cha makada hao kuvaa sare katika msiba huo wakati kiongozi wao ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye aliwasili msibani hapo akiwa amevaa nguo za kawaida.

Noti za zamani zachanganya wananchi

MATUMIZI ya noti mpya na za zamani katika mzunguko kwa karibu miaka miwili sasa, yanatajwa kuwa kashfa nyingine kwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), baada ya ile ya wizi uliofanyika katika Akaunti ya Madeni ya Nje, (EPA).

Baada ya BoT kuzindua noti mpya za Sh1,000, 2,000, 5,000 na 10,000 Januari 2011, Gavana Benno Ndullu alitangaza kuwa noti za zamani zenye thamani sawa na hizo, zingeondolewa kwenye mzunguko ndani ya kipindi cha miezi sita, ahadi ambayo mpaka sasa haijatekelezwa.

Akizungumzia hali hiyo mwanzoni mwa wiki, Gavana Ndullu alisema, hawezi kusema lini noti za zamani zitakwisha matumizi yake kwa kuwa hili litategemea kumalizika kwa noti hizo kwenye mzunguko.

Tangu noti mpya zilipoingia katika mzunguko, taifa limekuwa likitumia noti za aina mbili kwa pamoja, kitendo ambacho kimezua mjadala, huku baadhi ya watu wakieleza kuwa kinahatarisha uchumi wa taifa.

Watu wa kada mbalimbali waliozungumza na gazeti hili wameitupia lawama BoT, wakisema imeshindwa kuweka usimamizi mzuri wa fedha ama kwa makusudi au uzembe, hivyo kutoa fursa kwa watu wasio waaminifu kuingiza fedha chafu kwenye mzunguko.

“Biashara ya noti bandia inaonekana kama halali…, wanasema ukipeleka Sh100,000 unauziwa noti bandia za Sh200,000 namna ya kuzibadilisha utajua mwenyewe,” alieleza meneja wa benki moja mjini Moshi, ambaye hakutaka atajwe gazetini.

Kwa nyakati tofauti maofisa wengine wa benki kutoka mikoa ya Dare es Salaam, Mbeya, Arusha, Mwanza na Kilimanjaro, walidokeza kuwa noti za zamani ni bora ikilinganishwa na noti mpya.

Mbali na kuchakaa haraka, maofisa hao wamesema noti mpya ni rahisi kughushiwa na maeneo salama ya kuzipeleka fedha hizo ni vijijini.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alisema kimsingi hakuna athari zozote kiuchumi kama nchi itaendelea kutumia noti mbili zenye thamani moja, lakini hii inatoa mwanya wa kusambaa noti bandia kwenye mzunguko wa fedha.
“Kama moja ya noti hizo zinaghushika kirahisi, watu wataghushi na kuziingiza kwenye mzunguko. Huu ni udhaifu wa Benki Kuu katika kusimamia suala hilo. Fedha hizo zinatakiwa zifike benki na zikienda huko, zisitolewe tena kwa wananchi,” alisema.
“Kuna uwezekano noti hizo kutokubalika kwenye baadhi ya maeneo,” alisema.
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi katika Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), Moris Oyuke pamoja na kusema kuwa kutumika kwa noti tofauti zenye thamani moja hakuna madhara kiuchumi, alisisitiza kuwa hali hiyo inapaswa kudhibitiwa.

“Kama BoT inapata Sh10,000 iliyochakaa na kuiharibu, kisha kutoa Sh10,000 mpya, hapo hakuna madhara. Tatizo linakuja kama BoT itaharibu kiasi kidogo cha fedha na kuingiza katika mzunguko fedha nyingi zaidi, hii italeta mfumko wa bei,” alisema.

Mkuu wa Idara ya Fedha katika Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Esther Ishengoma alisema kuwa kuwepo kwa noti mbili katika mzunguko kunaleta mkanganyiko katika jamii.

Dk Ishengoma alibainisha kuwa noti za zamani ni ubora zaidi ya noti mpya na inawezekana Serikali imeliona hilo ndiyo maana inashindwa kuziondoa katika mzunguko.

Jaji chande aikwepa kesi ya Lema,INAONESHA INAUTATA MWINGI.

JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande amejitoa kusikiliza rufaa ya kesi ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, badala yake nafasi yake imechukuliwa na Jaji Bernard Luanda.
 
Kujitoa kwa jaji mkuu kumekuja ikiwa zimebaki siku tano kusikilizwa upya kwa rufaa hiyo Desemba 4, mwaka huu, baada ya awali Mahakama ya Rufani, kuona rufaa hiyo ilikuwa na dosari.
Mahakama hiyo ilikubali hoja ya wajiburufaa kuwa rufaa hiyo ilikuwa na dosari kutokana na tofauti ya vifungu vya sheria vilivyotumika katika hukumu iliyomvua ubunge Lema na vilivyotumika katika hati ya kukaza hukumu, iliyowasilishwa mahakamani sambamba na rufaa hiyo.
Hata hivyo, kilichomwokoa Lema ni kifungu cha 111 cha Kanuni za Mahakama, ambapo mahakama hiyo ilisema kuwa chini ya kanuni hiyo, dosari hizo zinaweza kurekebishwa.
Jaji Chande ndiye aliyekuwa kiongozi wa jopo la majaji watatu katika kesi hiyo akiwamo Salum Massati na Natalia Kimaro.
Jaji Mkuu aliingia kwenye kesi hiyo akichukua nafasi ya Jaji Mbarouk Salim Mbarouk aliyekuwa amepangwa awali, ambaye sababu za kuondolewa hazikuwekwa wazi.
Wakili wa  Lema, Method Kimomogoro alithibitisha kuwa amepata taarifa kuwa jaji mkuu hatasikiliza rufaa hiyo na badala yake Jaji Luanda ndiye atachukua nafasi yake.
“Ni kweli jaji mkuu hatakuwapo kusikiliza rufaa ya Lema nimewasiliana na Msajili Dar es Salaam ameniambia hatokuwepo kwenye hilo jopo,” alisema Kimomogoro na kuongeza:
Hata hivyo, Wakili Kimomogoro alisema “Huu ni utaratibu wa kawaida wa mahakama kwa kuwa huenda jaji mkuu akawa amesafiri au ana shughuli nyingine.”
Wakili wa wajiburufaa, Alute Mughwai alisema hajapata taarifa kama Jaji Mkuu ameondolewa kwenye jopo hilo kwa kuwa huo si utaratibu wa mahakama kutoa taarifa hizo.
“Mahakama huwa haitoi taarifa, zinawekwa (taarifa) kwenye ubao wa mahakama siku ambayo rufaa inasikilizwa,” alisema.
Aliendelea, “Jaji yeyote atakayepangwa sisi hatuna tatizo kwa kuwa wote ni majaji, wewe uko huko Dar na mimi niko huku bara (Arusha), hivyo unaweza ukazipata taarifa zaidi huko kwa kuwa ndiyo uko jikoni Dar.”

SHARO MILIONEA ALIMPENDA MAMA YAKE KUPITA MAELEZO …ILIKUWA AMFUNGULIE DUKA

MAJRANI wa familia ya marehemu Sharo Milionea kijijini Jibandeni, Lusanga, wanasema hawajawahi kuona mtu aliyekuwa anampenda mama yake kama Hussein (Sharo Milionea).
Mzee mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mzee Saidi akiwa na kundi la majirani wenzake, aliiambia Saluti5 kijijini hapo kwamba haujawahi kupita mwezi mmoja bila Sharo kuja kumtembelea mama yake.
“Alijua vilivyo majukumu yake, alijua kuwa yeye ndio mhimili wa familia yao, alihakikisha kila mwezi lazima aje mara moja au zaidi kumsalimia mama yeke” alisema mzee huyo na kuongeza kuwa msanii huyo alikuwa mtu wa watu kijijini hapo “Hakulewa sifa, aliendelea kuwa Hussein yule yule tuliyemlea hapa”.
Inaaminika Sharo Milionea alikuwa na mipango ya kumfungulia duka mama yake ili kujikimu kwa shida ndogo ndogo na inasemekena hata miongoni mwa vitu vilivyoibiwa kwenye gari lake ikiwa ni pamoja na pesa milioni sita kulikuwepo pia bidhaa kibao mahususi kwa ajili ya duka alililotaka kumfungulia mama yake.
Mama yake ambaye ana ulemavu wa mguu inaaminika atakuwa amepata pigo kubwa sana kwa vile Sharo alikuwa ndio kichwa cha familia.
Kwa kulewa hilo, Msanii mkongwe, Mzee Majuto aliiambia Saluti5 kuwa atapambana kadri awezavyo kuhakikisha kuwa mama huyo anapata matunda ya kazi za mwanae.
Sharo alifariki kwa ajali ya gari akiwa njiani kwenda kumsalimia mama yake ambapo alitaka akae nae kwa usiku mmoja kisha kesho yake arejee Dar kwa ajili ya mazishi ya msanii mwenzake John Stephano Maganga.

MZEE MAJUTO AZIRAI MSIBANI,SHARO ALIKUWA MANAGER WA MZEE MAJUTO

MMOJA wa watu waliokaribu sana na marehemu Sharo Milionea, Mzee Majuto jana alizirai msibani wakati mwili wa marehemu ukiwa njiani kuletwa nyumbani kutoka hospitali tayari kwa mazishi.
Majuto ambaye kwa wakati fulani alionekana kujitahidi kuwa imara, alijikuta akichotwa na hisia kali na kudondoka chini na kisha kupoteza fahamu kwa dakika kadhaa.
Hatimaye baada ya juhudi ningi za kumpepea, Mzee Majuto alizinduka na kupumzishwa kando ili aweze kurejea katika hali ya kawaida.
Akiongea na Saluti5 baadae, Mzee Majuto alisema kifo cha Sharo kimemuumiza sana “Nahisi kama nusu ya mwili wangu umechukuliwa, ni mtoto mdogo lakini alikuwa rafiki yangu sana, alikuwa zaidi ya mwanangu” alisema kwa uchungu mzee Majuto.
Kwa miaka ya hivi karibuni Mzee Majuto na Sharo Milionea wamekuwa ndio wasanii wanao-oana zaidi kikazi kiasi cha kupelekea makampuni kadhaa kuwatumia kwenye matangazo yao ya biashara.

MAZISHI YA MSANII SHARO MILIONEA NI MAZISHI YA KIHISTORIA TANGA

INAAMINIKA kuwa mazishi ya Mchekeshaji na mwanamuziki, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ hayajawahi kutokea mkoani Tanga.
Mzee Rajabu (mwenye kofia pichani juu) ni mmoja wa watu wanaomini hivyo, anasema tangu azaliwe hadi kufikia utu uzima alionao, hajawahi kushuhudia mazishi makubwa namna ile.
“Nashukru nimeishi miaka mingi na nimetembea sehemu kadhaa za nchi hii, lakini sijawahi kuhudhuria msiba wenye watu wengi kama waliojitokeza kuja kumzika kijana wetu”
“ Amezikwa na watu wengi sana tena wa kila aina inaonyesha kuwa ni mtu aliyeishi na watu vizuri alikuwa ni kijana mwema sana aliyependa wenzake,”anasema Babu huyo mkazi wa Lusanga, wilayani Muheza.
Sharo amepumzishwa jana kwenye nyumba yake ya milele katika makaburi ya familia yao kijijini Jibandeni, Lusanga. Umati mkubwa ulihudhuria mazishi yake na inakadiriwa zaidi ya nusu ya waliohudhuria, walitoka Dar es Salaam.
Kitu pekee ambacho unaweza kujifunza kwenye msiba huu ni kwamba WASANII ni watu wakubwa sana, labda hawajijui tu, ni watu wakubwa na mashuhuri pengine kuliko hata wanasiasa wakubwa.
CHANZO-SALUTI5

‘SHARO MILIONEA HAKUFA’ ,ndivyo anavyodai msanii mwenzake

PENYE wengi hapokosi mengi, katika mazishi ya msanii nyota, Sharo Milionea yaliyofanyika jana Lusanga, Muheza, zilipenya mbegu mbaya za imani za kishirikina.
Msanii mmoja mkongwe ambaye Saluti5 haioni busara kulitaja jina lake, alithubutu kusema Sharo Milionea hakufariki bali amechukuliwa kama msukule.
“Sina la kufanya kwa kuwa mimi si mwanafamilia lakini ndani ya nafsi yangu naamini Sharo hakufa, yupo hai amechukuliwa msukule” alisema msanii huyo.
Sharo Milionea alifariki Jumatatu usiku kwa ajali mbaya ya gari wakati akielekea kwao Lusanga kumsalimia mama yake mzazi.
chanzo- Saluti5

Four Dimensions of Management - Developing an Appropriate Management Model

Four Dimensions of Management - Developing an Appropriate Management Model http://t.co/znmBk0n4 via @Mind_Tools
mindtools.com
Use this framework to develop a management model that suits the way that you want to do business.

Monday, November 26, 2012

Rais Zuma awachinjia Ng'ombe wahenga

Bwana Zuma, ambaye ana wake zaidi ya mmoja na watoto 21, anasifika sana kama mwenye kufuata itikadi za utamaduni wa Zulu.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amewataka wazee wa jadi au wahenga kumsaidia katika kushikilia uongozi wa chama tawala (ANC).
Bwana Zuma alihudhuria sherehe moja kijijini siku ya Jumapili, ambako ng'ombe 12 walichinjwa na huku ubani ukichomwa watu wakimuombea achaguliwe tena.
Wapinzani wake wanataka ang'olewe kutoka katika uongozi wa chama, huku kongamano la chama likitarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Bwana Zuma, ambaye ana wake zaidi ya mmoja na watoto 21, anasifika sana kama mwenye kufuata itikadi za utamaduni wa Zulu.
Alimshinda mtangulizi wake Thabo Mbeki katika kinyang'anyiro kikali kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka
2007 ili kuongoza chama cha ANC.

Mkuki na Ngao

Ushindi wake ulimaanisha kuondoka mamlakani kwa bwana Mbeki na kumweka Kgalema Motlanthe kama rais wa mpito, hadi mwaka 2009 ambapo uchaguzi mkuu ulifanyika na kumuingiza madarakani.
Tawi la vijana wa chama tawala pamoja na maafisa wengine wa serikali sasa wanamfanyia kampeini bwana
Motlanthe, ambaye ni makamu wa rais, kumenyana na bwana Zuma katika kongamano litakalofanyika mwezi ujao, mjini Mangaung.
Wawili hao watakuwa wakigombania uongozi wa chama.
Familia ya Zuma ilichinja ng'ombe 12 na kuchoma ubani katika kijiji chao cha Nkandla mkoani KwaZulu-Natal siku ya Jumapili kuwataka wahenga kumpa mwongozo kabla ya uchaguzi.
"tuko hapa kumtakia kila keri baba yetu. Baada ya sherehe hii tuna imani kuwa ana ulinzi wa kutosha na tuna uhakika atarejea kusherehekea nasi.'' alinukuliwa akisema mwanawe Zuma , Nomthandazo Zuma
Kiongozi wa kijamii alimpa Zuma mshale na ngao akiwa amevalia nguo yenye madoa doa na kumtaka atumie silaha hiyo kujikinga kutokana na wapinzani wake katika chama cha ANC.
Bwana Zuma amekumbwa na kashfa za ufisadi tangu alipochukua mamlaka lakini kulingana na duru za kisiasa huenda akachaguliwa tena.

Dk Slaa: CCM wasubiri majibu 2015

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema CCM watazunguka nchi nzima lakini majibu yatajulikana 2015 kwani ndiyo utakuwa mwisho wao.

Pia Dk Slaa amesema Chadema hakiyumbishwi na kuahimia CCM kwa waliokuwa madiwani wake mkoani  Arusha, na badala yake kinapata nguvu ya kuweza kusimamia maadili ya viongozi wake.
Dk Slaa alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili kuhusu mambo mbalimbali ya kisiasa yanayoendelea nchini, ikiwa ni siku moja tangu uongozi wa juu wa CCM ukiongozwa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahaman Kinana umalize ziara yake ya kwanza katika Mikoa ya Mtwara, Rukwa, Geita na Arusha.
Alisema Chadema siku zote kitabaki kuwa mwalimu na vyama vingine vitafuata kwa kuiga mambo ambayo chama hicho kimeyaanzisha.
“CCM kuzunguka huku na huko na ni kutuiga sisi kwani tumeanza muda mrefu, baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 tumekuwa tukizunguka na kuwaeleza wananchi mambo mbalimbali,” alisema Dk Slaa na kuongeza;
“Wao (CCM) wazunguke tu lakini mambo yote yatajulikana 2015 kwani Watanzania wa sasa siyo wa kudanganywa tena.”
Dk Slaa alisema anashangaa kwa nini CCM wanazunguka huku wakilalamika wakati wao ndiyo wanaiongoza nchi hivyo majibu ya matatizo ya wananchi wanayo.“Chadema ni mwalimu na wao hufuata, waendelee na mzunguko wao lakini waache kulalamika kama sisi bali watoe majibu kwa kuwa wao ndiyo wanaongoza Serikali,”alisema Dk Slaa.
Akizungumzia baadhi ya madiwani wa chama hicho waliohamia CCM, Dk Slaa alisema kuwa hawakiyumbisha chama chao na kwamba hata kama wamehama wasipolipa Sh15 milioni kama amri ya mahakama ilivyotolewa watakwenda jela.
Juzi katika mkutano wa CCM Arusha, madiwani wa Chadema walitangaza kujiunga na CCM huku wakipinga hatua ya Dk Slaa, kuwa alikuwa akitaka kuwafunga baada ya kuwatimua ndani ya chama hicho.
Madiwani hao ambao walitimuliwa na Chadema kutokana kitendo chao cha kumtambua Meya wa Jiji la Arusha Gaudensi Lyimo wa CCM ni Rehema Mohamed, Simba Salum wa Kata ya Kati na Frank Joseph Takachi wa Kata ya Olasiti.
Jana Dk Slaa alisema kitendo hicho kinaonyesha jinsi gani kuna wanasiasa ambao ni matapeli hapa nchini kwani madiwani hao walikwenda mahakamani kutaka warudishiwe uanachama wao sasa wamekimbilia  CCM. “Watanzania sasa wanajua aina ya wanasiasa matapeli, kama walienda mahakamani kuomba uanachama wanahangaika nini,”alisema Dk Slaa na kuongeza; “Chama hakitayumba na tutaendelea kusimamia maadili ndani chama kama ilinavyotakiwa.” Alisema baadhi ya madiwani wameshaanza kulipa fedha ambazo mahakama imesema, hivyo hao waliokimbilia CCM wasipolipa fedha hizo ndani ya miezi miwili watakwenda jela kama mahakama ilivyosema.
NCCR wanena
Katika hatua nyingine Chama cha NCCR-Mageuzi kimemtaka Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara,  Philip Mangula kushughulikia rushwa ndani ya chama hicho kwa muda wa siku saba na siyo miezi sita kama alivyoahidi.
Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Faustin Sungura amesema vinginevyo chama hicho kitawahamasisha wananchi waikatae CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Sungura alisema wahusika wa rushwa wanafahamika na ametoa siku hizo kutokana na kuona miezi sita ni mingi na watendaji wa vitendo hivyo wanafahamika katika chama na Serikali na kwamba kinachokosekana ni dhamira ya dhati ya kuchagua viongozi wenye mikono safi.

Kesi ya Kakobe Aprili mwakani

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imepanga kuanza kusikiliza ushahidi wa walalamikaji katika kesi ya ubadhirifu inayomkabili Askofu Mkuu wa Kanisa la Full  Gospel Bible Fellowship (FGBC), Zakaria Kakobe Aprili 2, mwakani.
 
Pia, mahakama hiyo imetoa siku 14 kwa pande zote kukubaliana na kuwasilisha mahakamani hoja au mambo yanayobishaniwa, ambayo ndiyo yatakayotolewa ushahidi.
Amri hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Jaji Iman Abood, aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo wakati wa mkutano wa makubaliano wa jinsi ya kuendesha kesi hiyo.
Jaji Aboud amepangiwa kusikiliza kesi hiyo baada ya juhudi za usuluhishi zilizofanywa na Jaji Augustine Shangwa kushindikana, kutokana na Askofu Kakobe kukataa usuluhishi huo.
Katika mkutano huo wa makubaliano ya kuendesha kesi hiyo, kila upande ulitaja idadi ya mashahidi wake.
Upande wa walalamikaji unaowakilishwa na Wakili Barnabas Luguwa, ulidai utakuwa na mashahidi watano licha ya walalamikaji wenyewe.
Upande wa utetezi unaowakilishwa na Wakili Miriam Majamba, ulidai utakuwa na mashahidi wanane, zaidi ya mlalamikiwa mwenyewe.
Kesi hiyo namba 79/2011 ilifunguliwa Mei 26, mwaka jana na wachungaji watatu wa kanisa hilo; Deuzidelius Patrick, Angelo Mutasingwa na Benedict Kaduma.
Hata hivyo, baadaye Mchungaji Kaduma alilazimika kujitoa kutokana na ushauri wa ndugu na daktari, baada ya kupata ajali na kulazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa.
Baadaye, msimamizi wa kanisa hilo wilayani Liwale, mkoani Lindi, Mchungaji Ignas Innocent naye aliwasilisha maombi kutaka kujiunga katika kesi hiyo.
huku akidai ameamua kupigania haki na kwamba, kuna mambo ambayo anataka kuyaweka wazi.
Wachungaji hao wanamtuhumu Askofu Kakobe licha ya mambo mengine, kwa ubadhirifu wa mali na fedha zaidi ya Sh14bilioni na ukiukwaji wa katiba ya kanisa hilo.
Awali, Askofu Kakobe kupitia kwa wakili wake, Miriam Majamba aliwawekea pingamizi la awali walalamikaji hao  akidai hawana haki ya kumfungulia kesi, lakini juhudi zake ziligonga mwamba baada ya mahakama kulitupilia mbali.
Katika pingamizi lake hilo, licha ya kudai walalamikaji hawana haki ya kisheria kumfungulia kesi, kwamba si wachungaji wa kanisa hilo kwani walishafukuzwa tangu mwaka 2010.

Chadema uongozi balaa

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitafutia dawa migogoro inayotokana na baadhi ya makada wake kuonyesha nia ya kuwania urais na ubunge mwaka 2015, baada ya kuanzisha utaratibu maalumu wa wanachama wake kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gageti  hili, mpango huo unakuja wakati Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe ametangaza nia ya kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao, kitendo ambacho kiliwashtua vigogo wa chama hicho akiwamo mwasisi wake, Edwin Mtei.

Mara kadhaa Mtei amekuwa akimwonya Zitto kuwa kitendo chake cha kutangaza nia yake ya kugombea urais kitasababisha mzozo na mpasuko ndani ya chama hicho.

Mtei amekuwa akisema kuwa Zitto anatakiwa kuwaunganisha wanaChadema na siyo kuwagawa, au kuwavuruga na kwamba siyo shida kuonyesha hisia za kuwania urais, lakini tatizo ni kuwa hali hiyo inatengeneza mzozo mkubwa.

Mtei ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Fedha na Gavana wa Benki Kuu (BOT) enzi za utawala wa Mwalimu Julius Nyerere, alisema wakati mwafaka ukiwadia, Chadema kitaamua ni nani mwenye sifa za kugombea urais akisema kina utaratibu wake wa kuwapata wagombea mbalimbali wa uongozi.

Akizungumza wakati akijibu hoja mbalimbali katika mtandao wa Jamii Forum katikati ya wiki hii, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema viongozi wa chama hicho walikutana mjini Morogoro hivi karibuni na kutengeneza utaratibu wa watu kutangaza nia wanapotaka kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

“Nadhani huu ni uamuzi mzuri wa chama maana watu wengine wana wasiwasi usio na msingi wowote kwamba kuwa na wagombea wengi kwenye chama ni kuvuruga chama,” alisema Zitto na kuongeza:

“Lakini watu haohao wanashangilia kweli wakiona demokrasia inavyotekelezwa kwenye nchi nyingine kama Marekani.”

Alisema kuwa tatizo la Watanzania wanapenda kuona demokrasia inatekelezwa, lakini wao wanaogopa kuitekeleza, hivyo mwongozo kwa wagombea ambao walipitisha Morogoro utasaidia sana.

“Uamuzi wa Morogoro kuhusu mwongozo kwa wagombea utatusaidia sana kuondoa mashaka kama haya,” alisema Zitto.

Mwananchi Jumapili lilipomuuliza Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika kuhusu jambo hilo  alionyesha kutofahamu lolote kuhusu utaratibu huo, wala ulipofanyika huo mkutano wa Morogoro.

“Mkutano upi wa Morogoro?” alihoji Mnyika. Alipoelezwa kuwa suala hilo lilizungumzwa na Zitto katika Mtandao wa Jamii Forum alisema: “Muulize kwanza Zitto akupe ufafanuzi ni kikao gani cha chama, pia juu ya huo utaratibu, akikueleza ndiyo urudi tena kwangu.”

Juhudi za kumpata Zitto kueleza kwa undani kuhusu utaratibu huo hazikuzaa matunda, kwani simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita bila majibu, baadaye kuzimwa kabisa.

Akizungumzia azma yake ya kuachana na ubunge kama alivyoahidi mwaka 2005 kuwa, atagombea vipindi viwili pekee Zitto, alisema kuwa aliwaambia wapigakura wake kwamba nia yake ni kuwa rais wa nchi.

“Nia yangu ni kupisha wengine nao wakimbize kijiti cha maendeleo ya jimbo letu na mkoa wetu,” alisema Zitto na kufafanua, “ Nimeshasema mara kwa mara kwamba ukiachana na siasa kazi ninayoipenda zaidi ni ualimu.”

Alisema kuwa akiachana na ubunge atakwenda kufundisha kwa kuwa anapenda kufanya tafiti, kusoma, kuandika na kufundisha.

“Hivi sasa tunaandaa mpango wa kuanzisha Chuo Kikuu cha Ziwa Tanganyika (Lake Tanganyika) mkoani Kigoma, nitafurahi kama nitakuwa mmoja wa wahadhiri wa mwanzo wa chuo hiki,” alisema Zitto.

Katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe alisimama kugombea nafasi ya urais akishindana na Rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwa akisimama kwa mara ya kwanza.

Mwaka 2010, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa aligombea nafasi hiyo na kuibuka mshindi wa pili kwa kupata asilimia 26.34 nyuma ya Rais Kikwete ambaye alipata asilimia 61.17.

Hivi sasa tayari kumetokea maneno ya chinichini miongoni mwa wabunge waliopo madarakani wakiwatuhumu baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao wameaanza kuingia katika majimbo yao kutaka kugombea viti hivyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Wabunge hao wanahoji kama wanachama hao wanaofanya hivyo wanataka kugombea ubunge katika uchaguzi ujao ili kukifanya chama kiongeze idadi ya wabunge bungeni, kwa nini wasiende kugombea katika majimbo ambayo hayana  wabunge wa chama hicho?

Vilevile, chama hicho kilipata msukosuko katika mchakato wa kupata wabunge wa Viti Maalumu katika uchaguzi uliopita na kulazimika kuweka vigezo ambavyo viliondoa manung’uniko hayo.

Baadhi ya vigezo hivyo ni elimu, mchango wa mgombea katika chama, wanawake waliogombea katika majimbo na uzoefu katika ubunge.

E & P


Zitto afichua siri yake na JK

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amefichua siri ya uhusiano wake na Rais Jakaya Kikwete kuwa, unatokana na kuheshimu mchango wake anaoutoa kwa taifa.
 
Kutokana heshima hiyo, Zitto anasema ndiyo maana Rais Kikwete hakufika jimboni kwake katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2005 na mwaka 2010 kumnadi mgombe wa CCM.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema alisema hayo katika mahojiano maalum na Mtandao wa Jamii Forum juzi.
Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, jana alilithibitishia gazeti hili kwamba alihojiwa na mtandao huo kwa saa nane.
“Kweli ni mahojiano baina yangu na Jamii Forum. Kwa Kfupi ni kwamba, yalikuwa  mahojiano ya saa nane, kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa kumi jioni na walionihoji kwa njia ya mtandao walikuwa wakituma maswali na mimi nawajibu,” alisema Zitto.
Alisema yeye na Rais Kikwete wana uhusiano nje ya siasa na hata siku moja hawajadili mambo ya vyama vyao wanapokutana na kwamba, Rais anaamini katika uzalendo wake.
Zitto alisema kutokana Rais Kikwete kuthamini mchango wake, ndiyo maana hajawahi kwenda kwenye jimbo lake kumfanyia kampeni mgombea wa chama chake cha CCM katika chaguzi za mwaka 2005 na 2010.
“Hatuna makubaliano yeyote, bali anaheshimu mchango wangu kwenye nchi yangu. Mwaka 2005 hakuja Kigoma Kaskazini na 2010 pia hakuja Kigoma Kaskazini,” alisema.

Alisema kama ilivyo kwa wengine wenye uamuzi ya kuthamini kazi za wagombea wa vyama vingine, Rais Kikwete naye anayo haki ya kuheshimu na kuthamini kazi zake.
Aithdha, Zitto alisema anamheshimu Rais Kikwete kama mzee wake na kwamba, kuwaita kuwa wao ni marafiki ni kukosea.
“Kuita sisi ni marafiki ‘is understatement’, yeye ni mzee wangu. Tunaheshimiana, lakini ninaiheshimu zaidi Tanzania na ninaipenda zaidi Tanzania,” Zitto alisema.
Alichokifanya Rais Kikwete kutokuja katika jumbo langu si jambo geni, kwani hata vyama vingine vimewahi kuvifanya.
Alitoa mfano wa aliyekuwa mgombea wa urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu mwaka 2005, Freeman Mbowe alipofika katika Jimbo la Musoma Mjini, alimpigia kampeni mgombea wa CUF.

Ridhiwan, Lowassa waelezea utajiri wao

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwan wamezungumzia tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwao kwamba wanamiliki rasilimali zenye thamani ya mabilioni ya shilingi.
 
Lowassa kwa upande wake amekuwa akidaiwa kuwa tajiri anayemiliki kampuni kubwa za kibiashara na kumekuwa na taarifa kwamba ana ukwasi ambao vyanzo vyake vinatia shaka na siyo rahisi kuvitolea maelezo.
Kwa upande wake Ridhiwan naye amekuwa akidaiwa kuwa na utajiri mkubwa na amekuwa akihusishwa na biashara za kampuni za kusafirisha mafuta ambayo hupelekwa kwenye migodi, umiliki wa hoteli na majengo kadhaa ya kifahari.
Wote wawili wamekuwa wakidaiwa kwamba baadhi ya mali zao wamekuwa wakiziendesha chini ya kivuli cha wafanyabiashara wengine wakubwa nchini ili kukwepa kuhojiwa walikotoa utajiri huo, taarifa ambazo hata hivyo imekuwa vigumu kuzithibitisha.
Hata hivyo jana kwa nyakati na mazingira tofauti, Lowassa na Ridhiwan walijitokeza hadharani na kukanusha madai kwamba wao ni matajiri wa kupindukia.
Lowassa kwa upande wake akiwa mjini Mbeya alisema yeye siyo tajiri kama ambavyo imekuwa ikidaiwa lakini wakati huohuo akasema “sijafilisika”.
“Wengi wanasema kuwa mimi ni tajiri siyo kweli, lakini sijafilisika kutokana na kuchangia makanisa kwani nina marafiki wengi ambao wananisaidia katika kuchangia makanisa nao pia hawajafilisika,”alisema Lowassa.
Lowasa alitoa kauli hiyo alipokuwa akiendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa hosteli ya wanachuo wanawake ambao ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Theofilo Kisanji cha mkoani Mbeya, kinachomilikiwa na Kanisa la Moraviani Tanzania, Jimbo la Kusini Magharibi.
Kiongozi huyo ambaye alichangia kaisi cha Sh25 milioni, alisema kila mtu ana wajibu wa kuchangia elimu na kwamba mwanamke anapaswa kutazamwa kwa karibu zaidi kwani ndiye anayebeba jukumu kubwa la kutunza familia.
Kwa upande wake Ridhiwan alisema: “Ikiwa mimi ni tajiri wa kiasi kinachosemwa, basi mimi ninamzidi Bakhressa (Said Salim, mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki), maana nimepewa kila hoteli hapa mjini, kampuni za mafuta na kila biashara kubwa inayoanzishwa hapa mjini ni ya Ridhiwan”.
Said Salim Bakhressa ni mfanyabiashara ambaye anatajwa kuwa tajiri kuliko wote nchini na anashika nafasi ya pili katika nchi za Afrika Mashariki na Kati, huku akiwa miongoni mwa wafanyabiashara 10 wanaonyemelea kuingia katika nafasi za juu za utajiri Afrika.
Hata hivyo Ridhiwan ambaye hivi karibuni alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), aliongeza: “Ninaweza kuwa nafanya biashara moja au mbili, lakini siwezi kuwa mmiliki kiasi chote hicho cha mali.
Mtoto huyo wa Rais Kikwete alikuwa akijibu tuhuma kwamba magari yake kumi ya kusafirisha mafuta yamekamatwa na kuzuiwa katika mpaka wa Kenya na Tanzania, Namanga mkoani Arusha kutokana na kukwepa kodi, taarifa ambayo aliikanusha.

WAFANYABIASHARA watano, Said Bakhressa Gulam Dewji, Rostam Aziz, Reginald Mengi na Ali Mufuruki, wametajwa na Jarida la Ventures Africa linalozungumzia masuala mbalimbali ya uchumi wa Afrika kuwa ndiyo matajiri zaidi nchini.


Anayeongoza katika orodha hiyo ni Bakhressa anayemiliki mali na fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 620 milioni sawa na Sh992 bilioni (Dola moja Sh1,600) akifuatiwa na Dewji ambaye utajiri wake ni Dola 560 milioni (Sh896 bilioni). Wengine na kiasi cha mali na fedha wanazomiliki kwenye mabano ni Rostam (Sh672 bilioni- Dola 420 milioni) Mengi (Sh448bilioni- Dola 280 milioni) na Mufuruki (Sh176 bilioni - Dola 110 milioni).

Matajiri hao wamepatikana baada ya kuangalia nafasi zao kifedha, ufanisi wa kampuni zao katika soko la hisa, mfumo wa wanahisa katika soko la hisa na mtiririko mzima wa fedha katika akaunti zao kwenye benki mbalimbali.

Jarida hilo linalotoka mara moja kwa mwezi kutoka Afrika Magharibi, limesema matajiri hao wa Tanzania ni kati ya Waafrika wenye utajiri ambao ni mabilionea 4,800 kutoka mataifa 17.
Asilimia kubwa ya watu 1,523 ni mamilionea na wamo katika ripoti ya watu matajiri Afrika.
Jarida hilo linataja jinsi matajiri hao walivyokuwa wajasiriamali wadogo kabla ya kuibuka na kuwa mabilionea.

Said Salim Bakhresa
Jarida hilo limesema chanzo cha utajiri wa Bakhressa ni mapato yanayotokanana uzalishaji wa bidhaa mbalimbali kwenye viwanda vyake.

Mfanyabiashara huyo aliacha shule akiwa na umri wa miaka 14 na kuanzisha biashara zake. Alianza kuuza urojo Zanzibar na baadaye alifungua mgahawa miaka ya 1970.

Mgahawa huo ulipanuka na alitumia faida yake kufungua mashine ya kusaga pamoja kiwanda za usindikaji vyakula, huku akiunda Kundi la Makampuni ya Bakhressa.
Aliendelea kusindika vyakula mbalimbali na kutengeneza unga wa mahindi na baadaye kuanzisha kiwanda cha kuoka mikate na baadaye kutengeneza chocolate, ice cream, vinywaji na makasha ya kufungashia bidhaa. Kutokana na shughuli hizo, kwa mwaka huingiza Sh800 milioni.
Kampuni zake kwa sasa zinafanya biashara mbalimbail katika nchi za Tanzania, Uganda, Malawi, Rwanda na Msumbiji na ameajiri zaidi ya wafanyakazi 2,000.

Gulam Dewji
Mfanyabiashara huyo ana utajiri unaokadiriwa kufikia Dola 560 milioni kutokana na kuzalisha bidhaa na kutoa huduma mbalimbali.
Ni mmoja wa mataikuni wa Tanzania tangu miaka ya 1970 na kazi yake kubwa ilikuwa kuingiza bidhaa mbalimbali kutoka nje.

Alianza na kampuni ndogo aliyoiita Mohammed Enterprises Tanzania, ambayo kwa sasa ni kati ya kampuni kubwa Afrika Mashariki na Kati.
Miongoni mwa mali zake ni Kiwanda cha 21st Century Textiles, moja ya viwanda vikubwa vya nguo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kampuni yake ina viwanda vinne, Tanzania na Msumbiji huku ikizalisha Dola 100 milioni kwa mwaka. Pia kampuni hiyo husindika juisi kwa matunda ya Tanzania, mafuta ya kula, sabuni na tishu.

Kampuni hiyo pia inamiliki kampuni ya bima, makontena, kampuni za kuuza mafuta ya petroli na maduka ya kuuza bidhaa mbalimbali zaidi ya 100 Tanzania nzima.
Hata hivyo, Gulam alisema jana kwamba takwimu zilizotolewa zimekosewa. Alisema kwa sasa yuko nje ya Dar es Salaam na atatoa taarifa sahihi atakaporejea.
“Kuna baadhi ya tarakimu zimekosewa niko Morogoro kuangalia biashara zangu nikirudi Dar es Salaam nitazungumza,” alisema Dewji.

Rostam Aziz
Ameelezwa kuwa utajiri wake umetokana na kuendesha shughuli zake mbalimbali ikiwamo kampuni za mawasiliano ya simu, madini na biashara za usafiri wa meli.
Mwanasiasa huyo mwenye asili ya Asia, alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa Mbunge wa Igunga mwaka 1993 na alishinda kwa vipindi viwili.

Aliachana na ulingo wa siasa mwaka 2011. Anamiliki asilimia 19 ya Hisa za Kampuni ya Vodacom ambayo ina wateja zaidi ya milioni nane.

Ameelezwa pia kuwa anamiliki Kampuni ya Ujenzi ya Caspian na sehemu ya Bandari ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Kampuni ya Hutchison Whampoa ya Hong Kong.
Akizungumzia utafiti huo, alisema: “Umefanyika kwa umakini isipokuwa tu kwa upande wangu wanasemas ninamiliki asilimia 19 ya Kampuni ya Vodacom kitu ambacho si sawa kwani ninamiliki asilimia 35.”

Reginald Mengi
Mengi anakimiliki kampuni mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, viwanda vinavyozalisha vinywaji baridi vya Coca-Cola na ana mgodi wa dhahabu.

Mfanyabiashara huyo baada ya kufanya kazi ya uhasibu ambayo ndiyo taaluma yake, alifanya biashara ya kutengeneza kalamu za wino zilizopata soko kubwa Afrika Mashariki.
Leo hii, IPP Group ambayo Mengi ni mwenyekiti wake, inamiliki magazeti mbalimbali ikiwemo Financial Times, ThisDay na The Guardian, televisheni mbili kubwa Afrika Mashariki na Kati EATV na ITV na vituo vya redio. Anamiliki Kampuni za IPP Gold na Handeni Gold.

Ali Mufuruki
Utajiri wake unatokana na biashara mbalimbali za rejareja na za ushirika.
Ni mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Tanzania Infotech Investment Group.
Kampuni hiyo inajumuisha Watanzania na Waganda kwa ajili ya kuuza bidhaa za Afrika Kusini za Woolworth.

Infotech hufanya kazi ya uendelezaji makazi na ukodishaji, matangazo na shughuli za mawasiliano.

HAYA NI MAMBO MACHACHE MUHIMU YA KUYAZINGATIA KILA SIKU.


.
Nimepita kwa dada yangu Monica nikakuta karatasi lililoandikwa mambo machache ya binadamu yeyote kuyazingatia kwenye mzunguko wa maisha wa kila siku.
1. Hakikisha unapoongea na simu unatumia sikio la kushoto
 2.Usinywe dawa na maji baridi
 3. Usile heavy meals baada ya saa kumi na moja jioni
 4. Kunywa maji mengi wakati wa asubuhi, usiku kunywa kidogo
 5. Wakati mzuri wa kulala ni kuanzia saa nne usiku mpaka saa kumi usiku
 6. Wakati simu yako imeisha charge na kubaki bar moja, usipokee simu yoyote utakayopigiwa kwa sababu simu inapoisha charge kama hivyo, radiation is 1000 times stronger.

MAGAZETI YA LEO NOV 27 NDIO HAYA.siasa na uchumi

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

MAGAZETI YA LEO NOV 27 NDIO HAYA.

.
.
.
.
.

Mashabiki wa West Ham matatani

  West Ham

                               West Ham
West Ham imetangaza kuwa itao adhabu kali kwa mashabiki wake ambao watapatikana na hatia kutumia lugha ya ubaguzi wa rangi wakati wa mechi yao siku ya Jumapili, dhidi ya Tottenham.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa klabu hiyo mashabiki watakaopatikana na hatia huenda wakapigwa marufuku ya kutohudhuira mechi yoyote ya klabu hiyo maishani.
Shirikisho la mchezo wa soka nchini Uingereza, FA limesema linachunguza uwezekano wa kuanzisha uchunguzi kufuatia ripoti kuwa mashabiki kadhaa wa Tottenham walidhulumiwa.
Inadaiwa kuwa baadhi ya mashabiki wa Westham, waliimba nyimbo za ubaguzi kuhusiana na kujeruhiwa kwa mashabiki wa Tottenham mjini Rome wiki iliyopita ambako baadhi yao walidungwa visu.
Tayari malalamisha kadhaa yamewasilisha kwa idara ya polisi na klabu hiyo imetangaza kuwa itachukua hatua kali zaidi dhidi ya mashabiki watakaopatikana na hatia.
Msemaji wa FA, amesema wanasubiri ripoti ya maafisa waliosimamia mechi hiyo, ili kuamua hatua watakayochukua.
Baadhi ya mashabiki wa Westham, wanadaiwa kuwakejeli mashabiki wa Tottenham, ambao tangu jadi wamekuwa na uhusiano wa karibu na jamii ya Wayahudi wanaoishi mjini London.

PRESS RELEASE: Shilingi Bilioni 86 zaibwa Wizara ya Nishati/TANESCO, Gridi ya Taifa hatarini

Gazeti la The East African la Novemba 24 – 30, 2012 limetoa taarifa kwamba jumla ya dola za kimarekani milioni 54 zimegundulika kuibwa na watumishi waandamizi wa Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la TANESCO kupitia manunuzi ya Mafuta ya kuendesha mtambo wa Umeme wa IPTL. Gazeti hili limenukuu taarifa ya ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Tanzania (Controller and Auditor General). Taarifa hiyo inasema kuna kikundi (racket) ambacho kazi yake kubwa ni kujifaidisha binafsi na mpango wa umeme wa dharura kupitia manunuzi ya Mafuta mazito ya IPTL.
Itakumbukwa kwamba toka mwaka 2011 kumekuwa na shinikizo lililotolewa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini kwamba zabuni za ununuzi wa mafuta ya kuendesha mpango wa umeme wa dharura na mchakato mzima wa manunuzi ya mafuta haya ufanyiwe uchunguzi wa kina (forensic audit).
Katika mkutano wa 3 wa Bunge la Kumi (April 2011) niliuliza swali Bungeni kuhusu kashfa hii ya ununuzi wa mafuta ya kuendesha mtambo wa IPTL na baadaye tarehe 16 Aprili 2011 nilimwomba Spika airuhusu Kamati ya Nishati na Madini kufanya uchunguzi kuhusu kashfa hii. Kamati ya Nishati na Madini chini ya aliyekuwa Mwenyekiti ndugu January Makamba ililitaka Bunge kuazimia kufanyika kwa uchunguzi kuhusu suala hili kwenye Taarifa yake ya mwaka 2011 iliyowasilishwa Bungeni mwezi Aprili mwaka 2012. Waziri Kivuli wa Nishati na Madini ndugu John Mnyika katika Hotuba yake ya Bajeti ya Wizara hiyo mwaka 2011 alipendekeza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu kashfa hii pia. Juhudi zote hizo hazikuzaa matunda.
Kipindi hicho kiwango kilichokuwa kinahojiwa kuibwa ni shilingi bilioni 15 tu. Taarifa ya The East African kama walivyonukuu kutoka kwenye taarifa ya CAG inaonyesha fedha zilizoibwa ni shilingi bilioni 86.
Zabuni za kununua mafuta ya kuendesha umeme wa dharura zimekuwa zikitolewa bila kufuata utaratibu wa zabuni kwa mujibu wa Sheria ya manunuzi. Hivi sasa kila mwezi Tanzania inatumia dola milioni 70 kununua mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme. Fedha hizi zinatoka Hazina na sehemu ndogo kutoka TANESCO. Wakati fedha hizi bilioni 112 zinachomwa kila mwezi kununua mafuta mazito na dizeli ya kuendesha mitambo ya umeme, Taarifa za kitaalamu zinaonyesha kwamba Bwawa la Mtera hivi lina kina cha maji chini ya kiwango kinachotakiwa na uzalishaji wa umeme ni asilimia 20 tu ya uwezo (installed capacity). Iwapo TANESCO wataendelea kutumia zaidi maji yaliyopo Mtera, Mitambo itashindwa kazi na Gridi nzima itasimama maana Mtera ndio nguzo kuu ya Gridi ya Taifa. Hali hii ni hatari sana kwa uchumi na ulinzi na usalama wa Taifa. Kimsingi Gridi ya Taifa ipo hatarini kutokana na kiwango cha Maji kilichopo Mtera hivi sasa na kuendelea kupungua kwa kina hicho cha maji.
Wananchi wanapaswa kuelezwa kinaga ubaga nini kinaendelea katika sekta ndogo ya umeme hapa nchini;
1.      Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kuhusu zabuni za manunuzi ya Mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme wa dharura iwekwe wazi na ‘racket’ inayosemekana kuiba jumla ya shilingi bilioni 86 ionyeshwe na hatua za kisheria zichukuliwe mara moja na bila kuchelewa.
2.      Waziri wa Nishati na Maadini auleze umma hali yalisi ya sekta ya umeme nchini, uzalishaji wa umeme upoje, hali ya maji katika bwawa mkakati la Mtera na nini hatma ya mitambo ya IPTL, kesi zake na utekelezaji wa mapendekezo ya Bunge kuwa kesi za kampuni hii zimalizwe nje ya mahakama. Pia Taifa lielezwe Mpango wa Dharura wa umeme unakwisha lini maana muda uliotolewa na Bunge mwezi Agosti mwaka 2011 tayari umekamilika. Waziri aeleze hatua agni amechukua baada ya kukabidhiwa taarifa na CAG kuhusu maafisa waandamizi wa Wizara waliohusika na wizi wa shilingi bilioni 86 za kununua mafuta ya IPTL.
3.      Waziri wa Fedha na Uchumi aueleze umma ni kiwango gani cha fedha Hazina imetoa kununua mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme wa dharura kati ya Mwezi Novemba mwaka 2011 na Oktoba mwaka 2012 na kama taratibu zote za zabuni zilifuatwa na pale ambapo hazikufuatwa ni hatua gani PPRA wamechukua dhidi ya waliokiuka sheria ya manunuzi na kuleta hasara ya mabilioni ya fedha kwa Serikali.

Kabwe Zuberi Zitto, Mb
Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Waziri Kivuli wa Fedha
Dar es Salaam. Novemba 25, 2012