Thursday, October 18, 2012

Je wajua jumuiya ya uamsho ilitoa ujumbe gani katika maadhimisho ya Nyerere?soma hapa uone wanayo yasambaza kwa wanachama wao,jinsi hawataki kuliona kanisa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla


 ufuatao ndo ujumbe wao

JE WAJUA KAMA UISLAMU UMEINGIA TANZANIA TOKA KARNE YA 8
JEE wajua kama UKIRISTO ni DINI MPYA TANZANIA kwa kuwa iliingizwa katika KARNE YA 18 na wamisionari.

Wamisionari hawa walipotia mguu pwani ya Africa ya Mashariki,nia yao hasa ilikuwa ni kuufuta Uisalamu na kuingiza UKIRISTO ili upate nguvu na utawale Tanzania.Wakaazi wa pwani hii iliyokuwa ikijulikana kama ZENJI waliuona UKIRSTO kwa mara ya kwanza mwaka 1498 Wareno walipofika sehemu hizo.
Mwaka 1567 wamisionari wa Augustinian waliingia AFRICA ya MASHARIKI ili kupambana na UISALAMU ili UKIRISTO uwe dini ya DUNIA NZIMA NA DINI YA TANGANYIKA,Kwahiyo wakati UKURISTO unaingia AFRICA ya Mashariki Uislamu ilikuwa ushafika kwa KARNE 1O nyuma.
Kadinali Lavigirie alianzisha The White Fathers,taasisi ya Kanisa Katoliki kwa kusudi maalum la kuupiga vita UISLAMU. Wakati huo huo Church Missionary Society (CMS) ilikuwa imijitwisha kazi ya kuondoa ulimwengu kutokana na Uislamu.Hadi hii leo White Father wapo Tanzania wakiendelea kufanya kazi iliyowaleta zaidi ya miaka mia iliyopita ya kuupiga vita UISLAMU na UKIRISTO kukapata hatamu zote katika SERIKALI na wakiristo ndio wawe na nguvu Tanzania hili likisimamiwa kwa ukamilifu na NYERERE baada ya uhuru kabla ya MKAPA kukamata kiti hicho.

Wajerumani walipofika Tanganyika waliwakuta Waislamu wanafahamu kuandika,kusoma na wamekuwa wameilimika katika hesabu na herufi walizokuwa wakitumia zilikuwa za kiarabu.Wajerumani kwa ajili hii basi waliwajiri WAISLAMU kuwa waalimu,wakalimani na Makarani Serikalini.Wamisionari na Wakoloni waliona wivu kwa maendeleo hayo kwa waislamu.
Baada ya hapo njama zikapangwa tena kuwafisi waislamu na uislamu na kuanzia wakaanza kupiga marufuku herufi za KIARABU kutumika badala yake wakazalimisha kujifunza herufi za KIRUMI.
Muislamu ambae jana alipoingia kulala alikuwa ameelimika akaamka asubuhi yake mjinga,hana elimu,hajui kusoma wala kuandika.

Njama hizi zote dhidi ya Uislamu ilikuwa sehemu ya makubaliano kama ilivyoandikwa katika kifungu 1V cha Mkutano wa Berlin mwaka 1884.Kifungu hicho kilikuwa kinasema kuwa UKIRISTO NI LAZIMA ILINDWE DHIDI YA UISLAMU.
Kati ya mwaka 1888-1889 kifungu hicho kilianza kusimamiwa na Imperial British East Africa Company ilitumia nguvu za kisiasa na kijeshi kuulinda UKIRISTO Afirica Mashariki.
Kwa kipindi cha zaidi ya miaka 100 KANISA likaelekeza nguvu zake katika kuwataarisha raia ambao wengi wao walikuwa WAKIRISTO,watakao kuwa watiifu na kulitumikia KANISA katika SERIKALI ambao ndio huu mfumo tulio nao sasa tunaouita (MFUMO KRISTO).
Ni katika mtandao huu ndiyo Wakiristo WANAYOIMILIKI Serikali ya chama cha Mapinduzi kwa upande wa TANGANYIKA NA ZANIBAR, na ndio KANISA inafanya inavyopenda na kuambrisha katika serikalia ya CCM, Wakati Waislamu na Uislamu ukifanywa kama vitu visivyokuwa na maana yoyote.

EWE muisalmu bado utaendelea kumfanya kafiri kuwa ndio rafiki yako na kipenzi chako wakati yeye ndie anae upiga vita dini yako?

Ewe Musilamu bado unaimani na wana siasa kuwa ndio watakaoleta mabadiliko katika nchi hii wakati wao wote wanafata ule mfumo wa serikali ya Kanisa inayoongozwa na CCM.
Ewe muislamu zinduka KANISA NDIO LINALOTAKA MUUNGANO NA DEMOCRACY Ilikuweza kuwa na nguvu Zanzibar Muungano wowote tutakao funga tujue tunaungana na KANISA SIO NCHI.
 

20Like · 

No comments:

Post a Comment