Monday, December 31, 2012

Chungu na tamu ya vigogo 2012

BAADHI ya vigogo wa kisiasa hawatasahau yaliyowapata mwaka jana kutokana na mabadiliko makubwa yaliyoigusa medani hiyo na kusababisha kuanguka ama kwa kura au kung’olewa katika nafasi walizokuwa wakizishikilia.
 
Wakati baadhi wakiugulia kwa machungu hayo, kwa upande mwingine lipo kundi la wale wanaosherehekea neema iliyowajia mwaka huohuo, baada ya nyota zao kung’ara kisiasa na kujikuta wakikwaa nafasi za uongozi, pengine ambazo hawakuzitarajia.
Miongoni mwa matukio yaliyowatikisa wanasiasa ni hatua ya Rais Jakaya Kikwete kupangua Baraza la Mawaziri, kutenguliwa kwa baadhi ya matokeo ya chaguzi za wabunge na uchaguzi wa ndani wa CCM ambao uliwaweka kando baadhi ya vigogo wa chama hicho.
Kadhalika, yapo matukio yenye sura ya kipekee ambayo yanawagusa wanasiasa kama Godbless Lema ambaye alianguka kisiasa kwa ubunge wake kutenguliwa na Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha mwanzoni mwa mwaka jana, lakini akaibuka tena shujaa baada ya kurejeshewa nafasi hiyo na Mahakama ya Rufani, Desemba 2012.
Tukio kubwa ambalo lilitikisa siasa za Tanzania ni lile la mabadiliko katika Baraza la Mawaziri ambayo yaliwaweka kando mawaziri sita ambao walikuwa wakiziongoza wizara nyeti zinazosimamia rasilimali za nchi na huduma za afya na uchukuzi.
Waliong’olewa ni Mustafa Mkulo (Fedha), William Ngeleja (Nishati na Madini), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), Omari Nundu (Uchukuzi), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara) Dk Haji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii). Pia panga hilo liliwakumba waliokuwa Naibu Mawaziri, Dk Lucy Nkya (Afya na Ustawi wa Jamii) na Dk Athuman Mfutakamba (Uchukuzi).
Kuanguka kwa Mkulo, Ngeleja na Maige kulitokana na taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyozihusisha wizara zao na ufisadi. Dk Mponda na Dk Nkya, waling’olewa kutokana shinikizo la madaktari ambao walifanya mgomo uliotikisa sekta ya afya nchini.
Kwa upande wake, Nundu naibu wake, Dk Mfutakamba waling’olewa kutokana na kashfa ya ujenzi wa gati bandarini ambao uliwagawa kiasi cha kutofautiana bungeni, wakati Dk Chami naye aliponzwa na ugomvi na aliyekuwa naibu wake, Lazaro Nyalandu. Hata hivyo Nyalandu alipona baada ya kuhamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Walioula
Mabadiliko hayo yalikuwa neema kwa wateule wapya wakiwamo wale ambao hawakuwahi kuwa wanasiasa kama ilivyo kwa Profesa Sospeter Muhongo ambaye aliteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini.
Profesa Muhongo alipewa naibu wawili; George Simbachawene (Nishati) na Stephen Masele (Madini) ambao walikuwa wabunge.
Wabunge wengine walioula ni Dk William Ngimwa ambaye aliteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na kupewa naibu wawili ambao nao hawakuwa katika duru za kisiasa; Saada Mkuya Salum na Janeth Mbene. Ni wakati huohuo ambao Mwenyekiti wa NCCR -Mageuzi, James Mbatia aliteuliwa na Rais kuwa mbunge.

Watanzania waongezeka kutoka milioni 34.4 hadi 45,matokeo ya sensa adhibitisha

RAIS Jakaya Kikwete jana alizindua matokeo ya awali ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, yanayoonyesha kuwa Tanzania sasa ina watu 44,929,002, kati yao 43,625,434 wakiwa wa Tanzania Bara na 1,303,568 Zanzibar.
Akitangaza matokeo ya Sensa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jana, Rais Kikwete alisema takwimu hizo zinaonyesha kuwa Tanzania ina kasi kubwa ya ongezeko la watu.
“Kwa kasi hii, hadi kufikia mwaka 2016 tutakuwa jumla ya watu 51 milioni. Idadi hiyo yaweza kuonekana kuwa haina tatizo kwa nchi kama Tanzania, lakini huo ni mzigo kwa taifa, jamii na kwa uchumi,” alisema.
Alisema kuwa kwa kasi hiyo ya ongezeko la watu hapana budi kuwa na mikakati madhubuti na mipango mipya ya maendeleo kuanzia sasa.
“Kuna umuhimu wa kupanga uzazi, vinginevyo hali ya maisha itazidi kushuka na ushindani katika rasilimali hizi chache tulizonazo utazidi kuwa mkubwa,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Lazima tulipe uzito stahiki suala hili la kupanga uzazi. Lazima ujue utazaa kipindi gani na watoto wangapi ili uweze kuwahudumia.”
Alisema takwimu za matokeo hayo zina maana kwamba Serikali ianze kujipanga kwa ongezeko hilo la watu na jamii kwa upande wake, ianze kujipanga kukabiliana nalo.
“Tukizingatia haya tutaweza kupiga hatua. Sisi serikalini tutaanza kupanga mipango yetu kwa kuzingatia matokeo haya. Nanyi wenzangu anzeni kujipanga kuchukua hatua,” alisema Rais Kikwete.
Alisema matokeo mengine yatatolewa Februari ambayo ndiyo yataonyesha mchanganuo wa jinsia, umri kiwilaya, kikata na kishehia.
Rais Kikwete alisema Sensa ya mwaka 2012, ni ya tano kwa Tanzania, ya kwanza ilifanyika mwaka 1967 na kulikuwa na watu 12,313,054; Tanzania Bara watu 11,958,654 na Zanzibar 354,400.
Sensa ya mwaka 2002 ilionyesha kuwa Tanzania ina zaidi ya watu 34 milioni. Alisema tangu Sensa ya kwanza ilipofanyika hadi ya sasa, kuna ongezeko la watu zaidi ya 33 milioni.
Alisema hatua ya mwisho ya matokeo ya Sensa ya 2012 yanatarajiwa kutolewa Juni, 2013 ikiwa na mchanganuo wa taarifa zote muhimu zikiwamo za kiuchumi kwa kaya.

Books I have read in 2012 #BooksRead2012-Zitto Kabwe,kwa misingi hii kwanini asiwe smart?mie nimesoma vitabu 3 only mwaka mzima.

Books I have read in 2012   – Zitto Kabwe

  1. Mother India : A political biography of Indira Gandhi – Pranay Gupte
  2. The Assassination of Lumumba – Ludo De Witte
  3. The Malay Dilemma – Mahathir Mohamad
  4. The Correct Line? Uganda under Museveni – Olive Kobusingye
  5. Start with Why: How great leaders inspire every one to take action – Simon Sinek
  6. Game Change -  J Heilemann and M Halperin
  7. Everyday Coruption and the State – G Blundo and J – P Olivier de Sardan
  8. Defeating Dictators: fighting tyranny in Africa and around the world – G Ayittey
  9. India’s Economy : Performances and challenges – S Acharya and R Mohan (ed)
  10. The Shadow World: Inside the Global Arms Trade – Andrew Feinstein
  11. Historia ya Mwalimu Nyerere na maisha yangu katika Utumishi wa Umma-Pius Msekwa
  12. The New Machiavell: How to wield Power in the modern world – Jonathan Powell
  13. The Oil Kings: How the US, Iran and Saudi Arabia changed the balance of power in the Middle East – Andrew Scott Cooper
  14. Dreams that matter: Egyptian Landscapes of the Imagination – Amira Mittermaier
  15. Kenya: Between Hope and Despair, 1963 – 2011- Daniel Branch
  16. How to win an election: An Ancient Guide for modern politicians – Quintus Tullius Cicero
  17. Dictator’s learning curve: Inside the battle for democracy – W Dobson
  18. Eight Days in September: The removal of Thabo Mbeki – Frank Chikane
  19. End Game: Secret Talks and the end of Apartheid – W Esterhuyse
  20. Africa’s Odius Debts: How foreign loans and capital flight bled a continent – L Ndikumana and J Boyce
  21. Treasure Islands: Tax Havens and the men who stole the world – N Shaxson
  22. La Roja: A journey through Spanish Football – J Burns
  23. The Open sore of a continent: a personal narartive of the Nigerian crisis- Wole Soyinka
  24. How Rich countries got rich….and Why Poor countries stay poor – Erik Reinert
  25. Why Nations Fail: The origins of Power,prosperity and poverty – D Acemoglu and J Robinson
  26. Why Africa fails: the case of growth before democracy – E Kamugisha
  27. The Oil Curse: How Petroleum wealth shapes development of Nations – M Ross
  28. Radio Congo: signals of hope from Africa’s deadliest war – B Rawlence
  29. Che in Africa: Che Guevara’s Congo Diary – W Galves
  30. S for Samora: a lexical biography of Samora Machel (still reading)
  31. Antihills of the Savannah  (still reading)

Friday, December 28, 2012

Madaktari 30 wasimamishwa

BARAZA la madaktari Tanganyika limewasimamisha kwa muda madaktari 30, kutoa onyo kwa madakari 289 na kuwafutia mashtaka madaktari 49 baada ya kupitia malamamiko ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kufuatia mgomo wa madaktari uliotokea Juni 23 hadi 28 mwaka huu.
 
Taarifa iliyotolewa jana na Msemaji wa Wizara hiyo, Nsachris Mwamwaja imeeleza kuwa Baraza lilipitia malalamiko yote na limetoa adhabu stahiki kwa kila daktari aliyethibitishwa kushiriki katika mgomo huo.
Alisema mashtaka yaliyoahirishwa kutokana na wahusika kuhitaji ushauri wa kisheria ni madaktari wanne na mashtaka yasiyosikilizwa kutokana na wahusika kutofika walipoitwa na Baraza ni madaktari 22.
“Wizara inakamilisha taratibu za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni za  Utumishi wa Umma kwa Madaktari wote waajiriwa ambao walipatikana na hatia mbele ya Baraza la Madaktari,”aliseleza Mwamaja na kuongeza
“Wizara pia imeridhia kuwapa madaktari waliokuwa katika mafunzo kwa vitendo fursa nyingine ya kuendelea na mafunzo hayo katika hospitali za Umma walizokuwepo kabla ya kuondolewa.”
Hata hivyo alisema fursa hiyo haitawahusu madaktari wote waliopewa adhabu za kusimamishwa na Baraza la Madaktari, hadi hapo watakapomaliza kutumikia adhabu zao.
Alisema kwa taarifa hiyo madaktari wote waliofutiwa mashtaka na wale waliopewa onyo na onyo kali wanatakiwa kuwasilisha kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii barua kutoka kwa msajili wa Baraza la Madaktari ikithibitisha kurejeshewa usajili  na kuruhusiwa kuendelea na mafunzo kwa vitendo.
Vile vile madaktari waajiriwa(Registrar) wanatakiwa pia kuripoti kwa Katibu Mkuu ili kupewa
barua zao kulingana na Adhabu walizopewa.

New Simba Coach to jet in today

                                                                        Newly appointed head coach for Simba FC Patrick Liewing
The Newly appointed head coach for Simba FC Patrick Liewing is expected to jet in the country today.

Speaking in a telephone interview, Simba SC chairman Aden Rage said the former manager of the Paris Saint Germain Academy coach main task will be to develop youth football at the club.

He said his club management is very delighted to have landed the services of Liewing who has a very good understanding of African football and youth football development.

“He is coming to coach our senior team as the head coach of Simba SC, but he will also be responsible for youth football development at our club, his background speaks a lot of his achievements as a youth football coach.

“Simba SC is the only team in the country with all youth development structures, we have Under 14, 16, 17 and Under 20, the coming of Liewing will help us a lot” he said.

He said the coach will join the team training tomorrow at   TTC Chang’ombe in Dar es Salaam, where all players are expected to be present.

Simba is undergoing intensive training to prepare for the second round of the Vodacom Premier League and also Confederation of African Football (CAF) games early next year. 

Liewig replaces Serbian Milovan Cirkovic, who guided the club to league glory last season.

The French tactician coached Asec Mimosas of Cote D'Ivoire between 2004 and 2009, winning a couple of domestic cups and leading the club to the semi-finals of the African Champions League in 2009 in 2006 he was nominated with the coach of the Egyptian national team and the coach of Al Ahly for the award of the best coach of Africa.

Meanwhile, Simba SC said they have given their youth team 500.000/- prize money to share among themselves, the youth team was given the money for emerging third in the just ended Uhai Cup which involves under 20 players from premier league clubs.




SOURCE: THE GUARDIAN

Lema amsikitikia anayedaiwa kuwa askari JWTZ Monduli

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), amesema kama angekuwa ndiye mwenye uamuzi ya mwisho ndani ya Chadema, angempokea kwenye chama hicho askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), aliyepiga naye picha kama kitendo hicho kitamfanya afukuzwe kazi.
 
“Ingawa wanaofaa kutoa kauli kama hizi ni viongozi wakuu kama Mwenyekiti na Katibu wa Taifa kupitia vikao halali vya chama, lakini binafsi, ningekuwa na uwezo, ningempokea mara moja askari huyu kwenye chama kama ishara ya walio tayari kujitoa mhanga kupoteza vyote ikiwemo kazi kwa ajili ya ukombozi wa taifa iwapo atafukuzwa kazi,” alisema Lema.
Hata hivyo, Lema aliyekuwa akizungumza katika mahojiano maalumu akiwa mjini Moshi kwa mapumziko ya Sikukuu ya Krismasi, alisema kitendo cha JWTZ kuanza kumwandama na pengine kumfukuza kazi askari huyo, kitafumua chuki kubwa kati ya askari wa vyeo vya chini na wenye vyeo vya juu ambao wengi wanaitumikia CCM kwa nafasi zao, ukiwemo ukuu wa mikoa na wilaya.
Alitoa mfano Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Samuel Ndomba ambaye kabla ya kuhamishiwa Makao Makuu ya jeshi alikoshika nyadhifa mbalimbali na hatimaye kuteuliwa kushika nafasi yake ya sasa, alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, cheo kilichompa fursa ya kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu na Kamati ya siasa mkoa wa CCM, Mkoa wa Arusha.
“Askari huyu mdogo akifukuzwa kazi kwa sababu ya picha aliyopiga na sisi, basi itathibitisha double standard (undumila kuwili)  ya utawala katika taifa letu. Huyu kapiga picha na taarifa ya kusakwa inatolewa na JWTZ , lakini wako wengi ambao ni wanajeshi wa vyeo vya juu ambao siyo tu wanapiga picha na viongozi wa chama tawala bali ni wafanyakazi wa CCM kwa nyadhifa zao wakiwa bado wako jeshini,” alisema Lema.
Alisema ujasiri wa mtu huyo anayeamini kuwa kweli ni askari wa JWTZ kujitokeza kupiga naye picha huku akijua anahatarisha kazi yake, ni ushahidi kuwa wapo askari wengi nchini  waliochoshwa na mwenendo wa CCM.
Alisema ukweli huo unathibitishwa na matokeo ya kura katika vituo vilivyokuwa ndani au jirani na vituo vya polisi na kambi za jeshi wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, ambapo wagombea wa upinzani walipata kura nyingi ikilinganishwa na wale wa CCM.
Lema aliyepiga picha na askari huyo akiwa na mbunge mwenzake wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema), alitoa changamoto kwa watu wenye mapenzi mema na taifa hili, kufanya utafiti wa maofisa wa juu wa JWTZ na vyombo vingine vya ulinzi na usalama wanaotumikia chama tawala kwa siri au kwa uwazi kupitia vyeo na nyadhifa zao.
“Hawa ni pamoja na wakuu wa mikoa, wilaya na maofisa wa ngazi mbalimbali ndani ya CCM ambao tunashuhudia wakirejea jeshini wakitokea kwenye utumishi wa chama lakini hatujawahi kusikia tamko la kutafutwa wala kuchunguzwa na jeshi kwa kushiriki siasa,” alisema Lema
Alisema hata ikitokea kweli askari aliyepiga naye picha akafukuzwa kazi hatajuta kumsababishia madhila hayo bali atajisikia faraja kwa sababu kitendo hicho kitafungua ukurasa mpyae katika harakati za ukombozi kwa watu kuelewa kuwa siyo kila jaribu au makosa ni mkosi, bali ni hatua muhimu katika kufikia mafanikio ya unachokiamini.
Alisema askari huyo atakuwa ameshinda hofu, vitisho na uoga alivyosema ni miongoni mwa dhambi kuu katika maisha ya mwanadamu na kuwataka Watanzania kutoogopa lolote, hata ikibidi kifo wakati wakipigania haki zao kwani hakuna atakayeishi milele kwa kuogopa kufa.
“Ni heri mtu kuishi miaka michache duniani na Jina lake kubaki linaishi kwa haki na wema kuliko kuishi miaka mingi akatoweka kama mzoga” alisema Lema akimkariri Mwana mapinduzi Steve Biko na kuongeza  “Ni dhambi kubwa katika demokrasia kuupuuza ukweli eti kwa sababu anayesema uongo amejifunza kupiga na kuua,”
Lema aliishauri JWTZ kutekeleza ahadi ya kulinda Taifa hata kwa kukemea kwa maneno wizi wa mali na rasilimali za umma zikiwemo fedha na wanyapori wanaotoroshwa kwenda nje kwa msaada wa waliokabidhiwa dhamana ya kuvilinda na kuvitunza kwa faida ya wote.

Padri aliyepigwa risasi Z’bar aikana Polisi

PADRI Ambrose Mkenda ambaye alipigwa risasi Jumanne iliyopita, mjini Zanzibar na watu wasiojulikana amekana maelezo yaliyotolewa na polisi yakimtaja kuwa ni Mhasibu wa Kanisa Katoliki, Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako amelazwa, Padri huyo alisema wadhifa wake ni Mkurugenzi wa Idara ya Uchungaji anayeshughulikia masuala yote ya Kanisa Katoliki visiwani humo.

Alisema hakuwa mhasibu wa kanisa hilo kama inavyoelezwa na kwamba taarifa hizo siyo za kweli.Hata hivyo, Padri Mkenda alisema alikuwa akimsaidia mhasibu kwa kipindi cha miezi mitatu.

“Mimi sikuwa mhasibu wa kanisa kama inavyoelezwa na watu. Napinga vikali taarifa hizo kwani mimi nilikuwa namsaidia mhasibu kwa muda tu kwani hakuwapo,” alisema.

Alipoulizwa jana kuhusu madai hayo mapya ya Padri Mkenda, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Aziz Juma Mohamed alisema asingeweza kuzungumza lolote kwa kuwa alikuwa nje ya kituo chake cha kazi licha ya kuwa na jibu la madai hayo.

“Sasa nipo Dar es Salaam kikazi. Naogopa kuandikwa kwamba nimetoa ufafanuzi juu ya suala uliloniuliza. Japokuwa majibu ninayo, lakini cha msingi ni kwamba jaribu kumtafuta kaimu wangu Haji Hana anaweza kuwapa majibu,” alisema Mohamed.

Alipoulizwa Kamanda Hana alisema inawezekana madai ya Padri Mkenda yakawa ya kweli kwa kuwa baada ya tukio hilo hakuweza kuzungumza lolote na badala yake maelezo yake yalitolewa na wasaidizi wake ambao ndiyo waliosema kwamba alikuwa mhasibu.

“Padri alikuwa akizungumza kwa ishara, hivyo hakuweza kusema chochote. Wasaidizi wake ndiyo wakatoa taarifa hizo kwamba ni mhasibu wa Kanisa.”

Akizungumzia hali yake Padri Mkenda alisema anaendelea vizuri lakini bado ana maumivu makali katika sehemu za mwili wake ikiwa ni pamoja na kichwani.

SMZ yatoa tamko
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imesema inafanya uchunguzi wa kina juu ya tukio la kupigwa risasi na watu wasiojulikana kwa Padri Mkenda.

Akizungumza na waandishi wa habari jana muda mfupi baada ya kumjulia hali Padri Mkenda, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mohamed Aboud alisema Serikali inafanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo cha tukio hilo.

Alisema kwa sasa ni mapema kujua chanzo cha tukio hilo kwani tayari vyombo vinavyohusika ikiwa ni pamoja na Jeshi la Polisi Zanzibar na Tanzania Bara vimeshapewa jukumu la kufanya uchunguzi.

“Tukio hili ni kubwa na limetuhuzunisha. Kwa kutambua umuhimu wa watumishi wa dini nchini, Serikali inafanya uchunguzi wa kina ili kutambua chanzo cha tukio hilo haraka,” alisema Aboud na kuongeza:
“Kwa sasa ni vyema tukawaachia madaktari ili wandelee na uchunguzi wa afya yake lakini ifahamike wazi kwamba Serikali ipo makini na pindi wahusika watakapopatikana watachukuliwa hatua kali za kisheria.”

Utafiti: Mfumo mbovu wa mawasiliano wachochea migogogo Bodi ya Mikopo

Mfumo  mbovu wa mawasiliano, hasa ya mtandao wa intaneti katika Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), ndiyo tatizo kuu linalosababisha kuibuka kwa migogoro kati ya wanafunzi wa vyuo vikuu na serikali katika upatikanaji wa mikopo ya kugharimia masomo yao na hatimaye kufanyika migomo na maandamano ya mara kwa mara.

Tatizo hilo na mengine, limegundilika kufuatia utafiti uliofanywa na Mtafiti, ambaye ni Mhitimu wa Stashahada ya Juu ya Mawasiliano ya Umma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Ally Kileo.

Utafiti huo, ambao matokeo yake yalitangazwa na Kileo katika mkutano wake na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana, ulifanywa kwa lengo la kuchunguza matatizo ya msingi yanayoikabili bodi hiyo hasa katika eneo la mawasiliano kupitia teknolojia ya ‘intaneti’ katika kuwahudumia wadau wake wakuu, ambao ni wanafunzi.

Pia ulilenga kutoa mapendekezo ya kitaalamu ili kuiwezesha bodi hiyo kutoa huduma bora zaidi.

Kileo alisema matatizo yaliyochunguzwa zaidi katika utafiti huo, yalikuwa katika mawasiliano wakati wa maombi ya mikopo ya karo na gharama za shughuli za kimasomo, hasa pesa kwa ajili ya kufanyia utafiti na mafunzo kwa vitendo.

Alisema katika utafiti huo, asilimia 55 ya washiriki wote 45 walisema matumizi ya intaneti, vipeperushi, matangazo ya kubandikwa, matangazo ya redioni na katika televisheni kama njia za mawasiliano, bado hazijaiwezesha bodi kutoa au kufanya shughuli za mawasiliano vizuri na kwa wakati baina yake na wadau wake katika kutoa huduma sahihi na kwa haraka.

Kileo alisema katika kuchunguza matumizi ya mtandao wa intaneti kama chombo kikuu cha mawasiliano, upungufu mkubwa zaidi umegundulika; mmojawapo ikiwa ni kukosekana kwa ubunifu na matumizi madogo ya njia ya mawasiliano ya intaneti.

Mwingine ni urasimu usio wa lazima, kuchelewa kwa majibu ya maswali au maelezo yanayotokana na zoezi la usajili, kukosekana kwa uwazi na ukweli katika mchakato wa kupanga mikopo na kukosekana kwa ushirikiano katika mawasiliano katika mawasiliano kati ya bodi na wadau wake.

Alisema katika nchi zilizoendelea kwenye teknolojia ya utoaji wa mikopo ya elimu kwa kutumia mtandao wa intaneti, kama vile Afrika Kusini na Botswana, shughuli zinazochukua siku mbili Tanzania, huko huwachukua saa chache kuzikamilisha.

Kileo alisema utafiti huo ulibaini pia kuwa siyo tu uzembe wa watendaji katika vitengo vya bodi kufanya huduma za bodi kuwa duni na mbaya, lakini pia kukosekana kwa nia ya dhati ya kuboresha huduma za bodi kunafanya zoezi lote la matumizi ya mtandao wa intaneti kutoa huduma kuwa kama mchezo wa kuigiza usio na waigizaji wala watazamaji sahihi.

Alipendekeza bodi kuimarisha na kuboresha huduma za mawasiliano ya mtandao wa intaneti kwa kuongeza taaluma ya mawasiliano ya umma kwa watendaji wake katika zama hizi za utandawazi na kujenga kituo cha mawasiliano ya huduma kwa wateja kwa njia ya simu na inataneti itakayopatikana kwa saa 24 kwa gharama za mtumiaji wa hudum
ac hiyo.
CHANZO: NIPASHE

Msigwa: CCM mnapoteza muda Iringa

MWENYEKITI wa Chadema Mkoa wa Iringa Mchungaji Peter Msigwa ameponda mikakati iliyotangazwa na viongozi wa (CCM) wa Mkoa wa Iringa ya kutangaza dhamira ya kurejesha jimbo hilo mikononi mwa chama hicho akisema kitendo hicho si utatuzi wa kero za wakazi wa Mkoa wa Iringa.
Msigwa alihoji ikiwa chama hicho tawala kitafanikiwa kurejesha jimbo lilikuwa likishikiliwa na CCM kwa miaka mingi kabla ya wananchi kuchagua upinzani mwaka 2010 kama ndiyo njia ya utatuzi wa kero za wananchi.

Akizungumza na gazeti hili alisema anashangazwa na mawazo ya viongozi hao wanaofikiria leo kurejesha jimbo badala ya kushugulikia kero za wananchi ambazo alisema zinakwamishwa na utendaji mbovu wa Serikali ya CCM.

“Leo Iringa gunia mmoja la Mahindi Sh80,000, wananchi wa kipato cha chini hawana uwezo wa kununua, yote haya ni matokea ya Serikali ya CCM ya kushindwa kusimamia na kujali wananchi wake, ikiwa watachukua jimbo hili wanataka kusema ndilo litakuwa suluhisho la migogoro na kero za wakazi wa Iringa mjini?,” alihoji Msigwa na kuongeza:

“Hadi sasa ndani ya CCM hakuna mgombea anayeweza kusimama na kupambana na nguvu ya umma katika jimbo hilo na si lazima nipitishwe mimi na chama changu kugombea bali mtu yeyote atakayeteuliwa wananchi watamchagua ili mradi atapitishwa na Chadema” alisema.

Msigwa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini alitoa kauli hiyo jana kufuatia viongozi wa CCM wa Mkoa wa Iringa wakiwa ni wa chama na jumuiya zao kueleza mikakati waliyonayo kuwa ni pamoja na kurejesha Jimbo hilo mikononi mwa chama chao.

Mbowe atumia siku nzima kukiokoa Chadema Karatu

KATIKA kile kinachoonyesha kuwa mgogoro na mpasuko kati ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),wilayani Karatu ni ngoma nzito,Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe jana alijifungia siku nzima akifanya vikao vya ndani wilayani humo.
Mbowe aliyewasili Karatu jana asubuhi, alikutana na wajumbe wa kamati ya utendaji wa wilaya ambapo alitarajiwa kutafuta ufumbuzi na suluhu ya mpasuko huo uliosababisha kamati hiyo kusimamishwa kwa muda na Kamati Kuu ya Taifa iliyokutana karibuni jijini Dar es Salaam.
Hakuna kiongozi yeyote wa Chadema wilaya au mkoa aliyekuwa tayari kuzungumzia yaliyojiri kwenye vikao kati yao na mwenyekiti huyo wa Taifa.
“Kikao bado kinaendelea. Siwezi kukueleza lolote kwa sababu ndivyo tulivyokubaliana kutozungumza yanayoendelea hadi taarifa ya pamoja itakapotolewa na viongozi,”alisema mmoja wa viongozi aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina.
Hata hivyo, habari za kuaminika kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji Wilaya ya Karatu walioomba kutotajwa majina, zimeeleza kuwa pande mbili zinazovutana ziliamua kutumia kikao chao na Mbowe kila upande kuweka mambo yote hadharani ili mbivu na mbichi zijulikane.
“Wenzetu (upande mwingine) walikuwa wanajaribu kuficha udhaifu wao kwenye suala la mradi wa maji kama chanzo cha mtifuano. Sasa tumeamua kueleza ukweli uchungu ambao hawakupenda uelezwe kuwa tatizo hapa ni uongozi mbovu wa halmashauri ya wilaya inayoongozwa na chama chetu,” alisema mjumbe mmoja.
Akifafanua, alisema kinacholeta mgogoro ni baadhi ya viongozi waliokaa madarakani muda mrefu kwenye halmashauri hiyo kulewa madaraka na kuanza kutumia nafasi zao kujineemesha binafsi.
Alisema viongozi hao walioamua kugeuza ugomvi wao binafsi na wananchi wasioridhishwa na matendo yao kuwa suala la kisiasa wanatuhumiwa kujichukulia uamuzi wa
kugawa au kumiliki ardhi bila kujali maslahi ya umma uliowapa fursa ya kuongoza.
Kutokana na uzito wa hoja zilizowasilishwa kwenye kikao kati ya Mbowe na wajumbe wa kamati ya utendaji,
Mwenyekiti huyo alilazimika kufanya kikao kimoja tu badala ya viwili kama ilivyopangwa awali. Jana, Mbowe alipaswa kukutana na kamati ya utendaji pamoja na madiwani kabla ya leo kukutana na wadau wa maendeleo Karatu.

Secondary school abandoned, It has never enrolled a student since construction was finished Four primary schools surround it

A building at Kiwalani Secondary School in Ilala Municipality, Dar es Salaam, which has lain literally abandoned for several years now reportedly because not even a single student has been selected to study there. Our roving photographer captured the scene yesterday. (Photo: Omar Fungo)
A Ward secondary school built at Yombo- Kiwalani in Dar es Salaam under the secondary school education programme lies idle since 2007 for lack of students, thus attracting vandals who have stripped it of its vital fixtures.

The Guardian team which visited the partially built school found out that no students were enrolled there despite four classrooms, laboratory building, staff room and toilets being ready and its being in the proximity of four primary schools.

The students from the four primary schools could have been enrolled at the abandoned school, but are instead forced to attend schools far from their home.

Residents near the school blamed the government for misuse of resources used to construct the school which is now abandoned, with windows, doors and other important fixtures stolen by vandals.

A resident of Yombo Matangini, Mzee Kabale said the area where the school has been constructed was not proper as it became waterlogged when it rained.

“At the beginning when we were informed about the construction of the school we were surprised …but because it was to meet our long time need to have a secondary school in the area, we agreed with the idea, expecting that they would use qualified contractors to do the job…,” he said.

Ramadhani Kimosa, a “local” security guard at Kiwalani Primary school, claimed to have volunteered for the work, to keep out youths and children who damaged the building.

“I have been guarding here since 2005, hoping that one day my children will be among others attending this school. I couldn’t stay aside and watch while things went wrong…our children are suffering by having to study far from home, while we have a school nearby,” he said.

He added: “A lot of money has been spent for the construction of this school, yet it has been turned into a hiding place for robbers and playground for children.”

Kiwalani ward executive officer Adeltus Kazinduki told The Guardian that he knows nothing about the construction f the school because when he started work last year, he learnt that documents on the project had been burnt.

“This project is not implemented by my office. The right person to speak to is the ward councilor who participated in the full council meeting which discussed various development projects including the construction of secondary schools,” he said.

He added: “We all wish the school to operate as the country is facing shortage of classrooms …once the construction is completed we will not send our children to schools which are far.”
For his part, Kiwalani ward councillor Said Kitambulio attributed the delay to complete construction of the school to lack of funds.

He said about 39m/- had been spent during phase one of the project and that additional 150m/- was needed to complete it and repair the rooms which have been vandalised and to remove the stagnant water.

Speaking on the stagnant pool of water, he said: "When construction of the school started we dug a trench to drain the water from the area, but after only six months, people who live near the school started throwing garbage into the trench, thus blocking it.

The government established ward based community school under secondary school education programme with the aim of increasing the number of students pursuing secondary school education. However the schools have been facing a number of challenges including shortage of teachers, classrooms and leaning materials.
SOURCE: THE GUARDIAN

Hukumu kesi ya Lema yaibua mapya

MWANAZUONI aliyebobea katika sheria, Profesa Issa Shivji na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Francis Stolla wamekosoa hukumu ya Mahakama ya Rufani, iliyomrejesha bungeni, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi, wanasheria hao walisema hukumu hiyo iliyotolewa na majaji watatu wakiongozwa na Nathalia Kimaro, Salum Massati na Bernard Luanda, inapingana na sheria.

Hata hivyo, mmoja wa mawakili wa Lema, Method Kimomogoro amepinga madai hayo akisema wanaoipinga pengine hawajapata nafasi ya kuliangalia kwa undani suala la haki ya mpiga kura kupinga matokeo mahakamani.

Profesa Shivji kwa upande wake alieleza kushangazwa na maelezo ya Mahakama ya Rufani kuwa mpiga kura hana haki ya kufungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kusema hiyo ni sawa na kutunga sheria mpya na si kutafsiri zilizopo.
Alisema Sheria ya Bunge ya Uchaguzi, Katiba ya nchi na Mahakama, vinampa haki mpiga kura kufungua kesi kupinga matokeo ya uchaguzi.

“Sheria ya Bunge na Mahakama Kuu katika kesi ya Mgonja (Chediel ya mwaka 1980), vinampa haki mpiga kura kufungua kesi mahakamani kupinga matokeo. Sijaona hoja nzito ya Mahakama ya kufuta haki hiyo ya mpiga kura,” alisema Profesa Shivji.

Katika shauri hilo namba 84 la mwaka 1980 lililofunguliwa na William Bakari na mwenzake dhidi ya Mgonja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mahakama Kuu Tanzania iliamua kuwa, mpiga kura ana haki kufungua kesi mahakamani kupinga matokeo. Walalamikaji walishinda.

Hata hivyo, Mahakama ya Rufani katika kesi ya Lema, iliamua kwamba hukumu katika kesi ya Mgonja ilikosewa kwani si sahihi kwamba mtu yeyote bila kujali mahali alipojiandikisha na kupiga kura anaweza kupinga matokeo katika jimbo lolote nchini hata kama haki zake hazijakiukwa kwa namna yoyote.

Lakini Profesa Shivji aliitetea hukumu hiyo ya Mgonja akisema imekuwapo kwa zaidi ya miaka 30 sasa na kwamba kwa muda wote huo imekuwa ikifuatwa katika uamuzi wa mashauri mbalimbali, huku akisisitiza kuwa Mahakama haiwezi kuifuta kirahisi tu.

Profesa Shivji alisema mpiga kura ni mwananchi na kwa vyovyote ana masilahi katika uchaguzi husika na hivyo anatarajia kuona uchaguzi ambao ni huru na wa haki.
“Hivyo huwezi kusema hahusiki na nani kashinda au kashindwa kwa kuwa uchaguzi ni muhimu katika kujenga na kukuza demokrasia,” alisema Profesa Shivji.

Chama cha Wanasheria
Kwa upande wake, Stolla alisema: “Nimesikiliza hata maoni ya wanasheria mbalimbali wakizungumzia kutofurahishwa na tafsiri ya Mahakama ya Rufani kuhusu haki ya mpiga kura ‘ku-challenge’ (kupinga) matokeo ya uchaguzi mahakamani,” alisema na kuongeza:
“Katika uamuzi wa kisheria, inaonekana Mahakama imetunga sheria mpya na wengi tunajiuliza kama siyo, sababu ya kuwa mpiga kura ni ipi nyingine inampa haki mpiga kura kupinga matokeo?”

Stolla alisema Sheria ya Bunge ya Uchaguzi ya tangu mwaka 1985, ambayo ilifanyiwa marekebisho mwaka 2002, kabla ya kutungwa upya mwaka 2005, inampa haki mpiga kura kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.

“Mwaka 2002, sheria zote zilifanyiwa marekebisho na baadaye mwaka 2005, Bunge likatunga sheria mpya inayoitwa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, ikafuta ya mwaka 1985. Sheria hiyo na marekebisho yake, ndiyo inayotawala uchaguzi hadi sasa,” alisema.

Alisema hata kabla ya kutungwa kwa sheria hiyo ya Uchaguzi ya mwaka 1985, tayari kulikuwa na uamuzi wa Mahakama Kuu katika kesi ya Mgonja ambayo iliamua kuwa mpiga kura ana haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.

Mtwara villagers want to know how they're to benefit


Mtwara residents demonstrate in the municipality yesterday to protest what they described as likelihood of being �bypassed� and therefore not benefiting much from the installation of a pipeline to pump natural gas found in Mtwara Region to Dar es Salaam. (Photo: Guardian Correspondent)
Thousands of Mtwara residents yesterday staged a nine-kilometre march to protest against the government decision to construct a gas pipeline from the region to Dar es Salaam while it is yet to clear the air about how the local people are going to benefit.

The demonstration started from Mtawanya village where the gas is being extracted and ended on Msimbati Street in Mtwara municipality.

The peaceful demonstration, which also attracted wananchi from Tandahimba and Newala districts, was well guarded by the police.
According to reports issued by the coordinators of the demonstration, Mtwara Regional Commissioner Joseph Simbakalia had been asked to receive the marchers in the municipality but reportedly declined. They were instead received by chairman of the Union of Political Parties in the region Hussen Mussa Amiri.

Parties forming the union are Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), NCCR-Mageuzi, SAU, Tanzania Labour Party, APPT Maendeleo, Alliance for Democratic Change, United Democratic Party and DP.

The slogan of the union is “Gas first, political parties later.'
The main market and roads here were closed for some time to allow traders to take part in the demonstration. The demonstrators held placards to convey their messages, which protested transporting gas from Mtwara to Dar es Salaam.

Reading out a statement by political parties, secretary of the union Seleman Litope said for a long time southern regions have been denied various development opportunities, citing the uprooting of a railway, poor supervision of cashewnut sales and lack of infrastructure such as roads and extraction of gas.

He said the situation had caused southern regions to lag behind in development, adding that they were not ready to see history repeating itself.

"We want the construction of the gas pipeline to be suspended …the government is not transparent on how the residents of Mtwara are going to benefit from the resource. The decision to transport gas to Dar es Salaam is contrary to President Kikwete's promise when he visited the region, saying Mtwara should prepare to become an industrial zone," Litope said.

“We are worried due to what happened to Songosongo residents in Lindi region. They have been left in abject poverty while they produce gas. We want to supervise our resources so we can get development,” he said.

The statement, which contained nine recommendations, queried why power generators were not installed in Mtwara while it has enough space for such projects.

They called on President Jakaya Kikwete to sack Mtwara RC Simbakalia, claiming that he has insulted them for mounting the protest against the construction of the gas pipeline to Dar es Salaam.

Announcing new power connection charges earlier this month, Energy and Minerals Minister Prof Sospeter Muhongo said residents in Lindi and Mtwara regions would be the first to start enjoying the lower rates. They will for the next six months be paying only 99,000/- connection fee for both single and three-phase power, a steep reduction from 455,104.76/- for single phase and 912,104.74/- for three phase.

According to the minister, residents in Lindi and Mtwara have been given such lower prices as an offer to enable more people access electricity. He said the residents had for a long time complained about high power connection fees despite the regions being major producers of gas in the country.
SOURCE: THE GUARDIAN

Saturday, December 22, 2012

HAYA NDIO MAGAZETI YA DEC 23 2012, MICHEZO NA HARDNEWS.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Kontena la kondom mbovu lakamatwa

KONTENA lililosheheni kondomu za kiume kutoka nchini India imekamatwa na kuzuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam, baada ya kubainika kuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu.
 
Maofisa wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wamelazimika kufanya msako mkali kwenye baadhi ya maduka ya dawa jijini Dar es Salaam baada ya kubainika kwamba tayari kondomu hizo zipo sokoni.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Leandri Kinabo alizitaja kondomu hizo kuwa ni aina ya Melt Me zenye thamani ya Sh222.1   milioni zilizokamatwa tangu Oktoba 23 mwaka huu na kuzuiliwa bandarini hapo kwa taratibu zaidi za kisheria.
“Jambo lililotushtua ni kwamba zimebainika kwamba zipo madukani, tukajaribu kufuatilia tena bandarini tukifikiri kuwa huenda zimetolewa kinyemela licha ya kuzuiliwa ili ziteketezwe au zirejeshwe nchini India kwa gharama zao wahusika.
Tulipokwenda bandarini tukabaini kwamba bado zipo katika hali ile ile, kumbe  zimeingizwa nchini kwa njia ya panya, kwa kweli ni mbovu na ndiyo maana tumelazimika kuwajulisha wanahabari ili muwape taarifa wananchi wawe makini,” alisema Kinabo.
Alifafanua zaidi kwamba kondomu hizo ni mbovu kwani zimebainika kuwa na vitundu, pia zinapasuka haraka, hazina kabisa viwango vya ubora wa bidhaa unaotakiwa na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO).
Kinabo alisema kuwa TBS bado wanaendelea kufanya mawasiliano na kampuni iliyotengeneza kondomu hizo, lakini kwenye kasha  lake inaonyesha kuwa inaingizwa nchini na kampuni ya Fair Deal Exim ya Dar es Salaam. 

PICHA 10 ZA USHAHIDI JINSI MBUNGE GODBLESS LEMA ALIVYOPOKEWA ARUSHA DEC 23 2012.

Mapokezi ya Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema katika jiji la Arusha leo, Lema ameshinda rufaa jana ya kesi yake iliyomfanya avuliwe ubunge na Mahakama.
.
.
.
.
.
.
Jamaa nae anadai anachukua video.
Godbless Lema na mbunge Joshua Nassari wa Arumeru Mashariki.
Mke wa Godbless Lema na mtoto wao kwenye mapokezi. (Picha zote zimepigwa na Mroki wa mrokim.blogspot.com)

Eti kipofu kaona Mwezi-Tanzania yaifunga Zambia 1-0

Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars imeilaza timu ya taifa ya Zambia, Chipolopolo kwa bao moja kwa bila katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa katika uwanja wa taifa mjini Dar es Salaam, Tanzania.
Katika mechi hiyo bao pekee la washindi, lilipatikana sekunde chache kabla ya kumalizika kipindi cha kwanza likitiwa kimiani na mshambuliaji Mrisho Ngassa.
Tanzania wakimenyana na Zambia jijini Dar es SalaamTimu ya Zambia, ambayo ni mabingwa wa Afrika ikiwa pia timu bora ya mwaka barani Afrika na yenye mchezaji bora wa mwaka wa BBC, Christopher Katongo, ilitawala mpira kipindi cha kwanza lakini ikokosa umakini katika umaliziaji.
Kwa upande wa timu ya Tanzania, ambao walionekana kutojiamini katika kipindi hicho, taratibu walibadilika, na kumiliki sehemu ya kiungo.
Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto,Frank Domayo na Salum Abubakar waliichosha ngome ya Zambia kwa kuelekeza mashambulizi mengi, langoni mwa Chipolopolo.
Mrisho Ngassa kama angekuwa makini zaidi angeweza kuipatia timu yake bao la mapema zaidi.
Timu ya Zambia ilichezesha nyota wake wengi akiwemo Christopher Katongo na Stopila Sunzu ambaye anatarajiwa kujiunga na timu ya Reading ya England.

Ndugu ukoo wa Lissu walivyoumana kortini

MIONGONI mwa mambo yatakayokumbukwa katika kesi iliyotengua na baadaye kumrejeshea ubunge, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ni mawakili wa pande mbili zilizokuwa zikipambana katika kesi hiyo ya kuhistoria.


Kwanza ni mawakili ndugu; Tundu Lissu ambaye alikuwa akimtetea Lema na Alute Mughway ambaye alikuwa wakili wa makada wa CCM waliofungua kesi kupinga ushindi wa Lema.

Lissu ambaye ni kada wa Chadema na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wakili mwenzake, Method Kimomogolo walishirikiana kumtetea Lema ambaye ni kada wa Chadema.

Lakini kaka yake (Mughway) alikuwa anawatetea warufaniwa (wajibu rufaa) ambao ni makada wa CCM; Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel.

Alute na Tundu wote ni watoto wa Mzee Augustino Lissu Mughwai na Bibi Alu Alute Tundu ambao wote sasa marehemu. Wakati Alute ni mzaliwa wa pili katika familia hiyo ya watoto 12, Tundu ni mzaliwa wa tano.

Alute hivi sasa ni wakili wa kujitegemea akifanyika kazi zake mkoani Arusha wakati mdogo wake Tundu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki ni wakili akifanyia kazi zake jijini Dar es Salaam.

Ndugu hawa walikuwa kivutio katika kesi hiyo kwani wote walionekana kuwa mahiri katika kujenga na kupangua hoja pale walipokuwa wakiishawishi mahakama kuwapa ushindi wateja wao.

Ndugu hawa wawili wamekuwa wakipambana mahakamani kwenye kesi ya Lema tangu ifunguliwe Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, wakipinga matokeo yaliyompa ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka  2010.

Hukumu ya kesi hiyo ndiyo iliyomvua ubunge Aprili 5, 2012 lakini Lissu na wakili mwenzake Method Kimomogolo awalikata rufaa ambayo jana ilimrejeshea Lema Ubunge.

Hii inatoa picha kwamba katika fani ya ya sheria hasa kwenye uwakili mahakamani huweza kuwakutanisha maadui kutoka pande mbili, mtu na mwanaye katika pande hizo mbili lakini kila mmoja akisimamia kile anachokiamini ili kufanya kazi yake.

Baba anaweza kuwa upande wa utetezi na mtoto anaweza kuwa upande wa mashtaka, kila mmoja akitaka kuonyesha uwezo wake kwa mteja wake.

Wakati mwingine watu huweza kusema kwa nini huyu asizungumze na mwanaye ili asitoe hoja nzito au mtoto asizungumze na baba yake ili asitoe hoja nzito ili kurahisisha kesi. Lakini hayo hayana nafasi pale watu hawa wanapokuwa katika kazi zao hasa za kitaaluma.

Dk Slaa amwagiza Lema ‘ambane’ Pinda bungeni

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemuagiza Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya chama hicho, Godbless Lema wakati atakapokwenda Bungeni, kufufua hoja kuhusu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kulidanga Bunge Febuari 10 mwaka huu.

Dk Slaa alitoa agizo hilo jana makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wafuasi walioandamana wakishangilia Lema kurejeshewa ubunge wake jana na Mahakama ya Rufaa.

Dk Slaa alisema huu ni wakati wa Lema kwenda kufufua hoja ya kwamba Waziri Mkuu alilidanganya Bunge kwani tayari udhibitisho wa jambo hilo ulikuwepo.

“Nakuagiza sasa Lema utakapo kwenda Bungeni uende ukambane Waziri Mkuu kwa kulidanganya Bunge kwani Spika wa bunge alisema hoja hiyo imefungwa kwa sababu ya wewe kutokuwepo bungeni,” alisema Slaa.

Waziri Mkuu Pinda akijibu swali bungeni aliseme chanzo cha vurugu zilizosababisha vifo mjini Arusha ni ni uamuzi wa madiwani wa Chadema  kutokubali kushindwa katika uchaguzi wa jiji hilo.

Pinda alitoa kauli hiyo Febuari 10 mwaka huu wakati akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe  aliyetaka kujua msimamo wa Serikali kuhusu mauaji ya raia yaliyofanywa na Polisi wakati wa vurugu zilizotokea Arusha.

Kutokana na majibu hayo, Lema kabla ya ubunge wake kutenguliwa na mahakama, aliomba kupewa mwongozo wa spika akidai kwamba Pinda alikuwa amelidanganya Bunge.

Spika wa Bunge Anne Makinda hajawahi kutoa mwongozo kuhusu suala hilo na aliwahi kusema kuwa suala hilo limefungwa kwani aliyeuliza hayupo tena bungeni.

Lema spidi 120 kwenye kona shaaaaa.

LEMA, jembeee, jembe limerudi, wamebana wameachia.” Ni baadhi ya maneno yaliyosikika kutoka kwa maelfu ya wafuasi wa Chadema, kumsifia Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa mapokezi makubwa ya mbunge huyo mjini Arusha jana.

Aidha, Chadema kimetangaza kuwadai Sh250 milioni, wanachama watatu wa CCM waliomfungulia kesi Lema, ikiwa ni gharama za kesi hiyo.
Mapokezi hayo yalifunika na kusababisha shughuli mbalimbali kusimama kwa takriban saa 5, huku barabara nyingi na mitaa ikifungwa.
Lema alikuwa akirejea Arusha kutoka jijini Dar es Salaam, baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kumrejeshea ubunge wake, aliovuliwa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Aprili 5, mwaka huu.
Jaji Gabriel Rwakibarila alimvua Lema ubunge, baada ya kuridhika na ushahidi wa wanachama watatu wa CCM, Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo na mashahidi wao kuwa mbunge huyo alitoa kauli za kashfa dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk Batilda Burian.
Mbali na nyimbo za kumsifu Lema, wafuasi hao wa Chadema walikuwa wakikiponda Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Msafara wa mapokezi ya Lema aliyevaa fulana nyeupe iliyokuwa na maandishi kifuani yaliyosomeka; ‘Usiogope, Mungu yupo kazini G. Lema’, ulianzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ukiwa na magari na pikipiki zaidi ya 100 za wanachama na wapenzi wa Chadema, waliojitolea kuzijaza mafuta na kupakia abiria bila kulipwa.
Shughuli zote za kijamii, zikiwamo safari za magari na biashara katika barabara zote ulipopitia msafara wa Lema, zilisimama kwa muda kupisha msururu huo wa magari na watu kupita, huku waliolazimika kuegesha magari yao pembeni kupisha msafara wakionyesha alama ya vidole viwili inayotumiwa na Chadema.
Msafara kuelekea KIA ulianzia eneo la Phillips jijini Arusha, ukiongozwa na viongozi wa Chadema wilaya na mkoa wa Arusha.
Waliokosa nafasi katika magari ya wanachama na wafuasi wa chama hicho waliamua kusimamisha magari aina ya Coaster, yanayofanya safari kati ya Arusha-Moshi na kuyakodi kwa kujilipia Sh5,000 kama nauli ya kwenda na kurudi KIA.
Baada ya kufika KIA, msafara kutoka Arusha uliungana na uliotoka mkoani Kilimanjaro na kuanza safari ya kurejea Arusha Saa 4:00 asubuhi, safari iliyochukua zaidi saa tano, ambao uliwasili Uwanja wa Soko la Kilombero jijini Arusha saa 9:30 alasiri.
Kwa kawaida, safari kutoka KIA hadi Arusha mjini huchukua dakika 40 hadi 45, lakini jana, safari hiyo ilichukua muda mrefu kutokana na msururu mrefu wa magari, pikipiki na watu waliokuwa wakijitokeza njiani kuusimamisha wakishinikiza kusalimiana na Lema.
Kutokana na  hali hiyo, Lema, alilazimika kusimama katika vituo zaidi ya 20 ili kusalimiana na wananchi, ambao wengi wao walishika matawi ya miti mikononi kuashiria amani.
Vituo ambavyo Lema alilazimika kusimama baada ya wananchi kufunga barabara ni pamoja na Njia Panda ya KIA, King’ori, Kikatiti, Maji ya Chai, USA-River, Tengeru, Chama, Kwa Pole, Shangarai, Kambi ya Chokaa, Kwa Mrefu, Ngulelo, Kimandolu, Phillips, Mount Meru Hotel na Sanawari.
Mbunge huyo aliyepanda gari la wazi ili kukata kiu ya wananchi waliokuwa na hamu ya kumwona tangu KIA hadi Arusha mjini pia alisimama katika maeneo ya Clock Tower, Metro Pole, Friends Conner, Kilombero Sokoni kabla ya kuingia kwenye uwanja wa Kilombero National Housing, alikohutubia mkutano mkubwa wa hadhara.
Mapokezi hayo yalihudhuriwa na viongozi kadhaa wa kitaifa wa Chadema akiwamo Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (Bavicha), John Heche na wabunge Israel Natse wa Karatu, Joshua Nassari wa Arumeru Mashariki, Cecilia Paresso na Grace Kiwelu wa Viti Maalumu.
Katika hatua nyingine, Chadema, kimetangaza kudai fidia ya zaidi ya Sh250 milioni kwa wanachama watatu wa CCM, waliofungua kesi dhidi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
chanzo-Mwananchi

Mapokezi ya lema arusha leo ilikuwa hivi

Add caption

magazeti ya leo 22/12/12

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.