Friday, October 26, 2012

AIRTEL WAZIDI KUPAGAWISHA WATEJA WAKE

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, imezindua ofa ya kuongea bure mara tano ya wastani wa matumizi ya kupiga simu kwa siku nzima, kwa wateja wake nchini
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Sam Elangalloor, alisema wametoa ofa hiyo kwa wateja wao kwa wastani wa kiwango cha fedha watakayotumia kila siku.
Alisema wateja watatumia bonasi hiyo ya muda wa maongezi,kupiga simu kwenda mtandao wowote  kwa siku hiyo.
”Tumefanya hivi ili kuendelea kuboresha huduma zetu na pia kuendelea kudhibitisha dhamira yetu ya kuwapatia wateja wetu nchini nzima, uhuru wa kuongea,” alisema Elangalloor.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Beatrice Singano, alisema mteja anayetumia mtandao huo ameshaunganishwa katika bonasi hiyo na kwamba kinachotakiwa ni kupiga simu ili apate salio la bure mara tano kwa wastani wa matumizi yake.
“Kadri mteja anavyotumia simu yake kwa kupiga simu, ndivyo atakavyojipatia  nafasi  zaidi ya kuzawadiwa asilimia 500 ya bonasi ya muda wa maongezi bure,”alisema.

 “Mfano mteja anaweka vocha ya Sh 500 kwa siku nzima, hivyo akatumia na kuisha saa 6:00 mchana muda huo atapewa bonasi ya maongezi ya bure ambayo itakuwa mara tano ambapo ataongezewa salio la Sh2,500 litakalotumika siku hiyo kabla ya saa 6 usiku”alisema Singano

No comments:

Post a Comment