Monday, October 8, 2012

Samata awania tuzo mwanasoka bora wa Afrika

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limemteua mshambuliaji wa  TP Mazembe na Tanzania, Mbwana Samata kuwa miongoni mwa nyota 32 watakaowania tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani ya Afrika.Hii ni mara ya kwanza kwa mchezaji wa Tanzania kuingia kwenye orodha hiyo ya wachezaji wanaowania tuzo ya Afrika kwa wachezaji wa ndani.Katika taarifa iliyotolewa mwishoni mwa wiki na CAF, ilivitaja vigezo vilivyotumika kumjumuisha Samata kwenye orodha yake kuwa ni mchezaji kijana aliyeibuka na kuwa nyota katika kikosi cha TP Mazembe tangu alipojiunga nayo mwaka 2011
Pia, lilimtaja Samata kama miongoni mwa wachezaji tegemeo katika kikosi cha TP Mazembe akiwa ameifungia mabao sita katika mechi mbalimbali za michuano ya kimataifa.
Hivi karibuni Samata aliingia kwenye  orodha ya wafungaji bora 71, duniani sambamba na Lionel Messi, Neymar na Cristiano Ronaldo.Mbali ya Samata, TP Mazembe imefanikiwa kuingiza jumla ya wanandinga watano kwenye kinyang'anyiro hicho cha kumsaka mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.Wengine ni mshambuliaji raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Tresor Mputu, beki Stoppila Sunzu, kiungo Rainford Kalaba na mshambuliaji Given Singuluma wote raia wa Zambia.

Orodha kamili ya nyota 32 wanaowania tuzo hiyo na klabu zao na nchi wanazotoka ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Tanzania),  Abdelmoumen Djabou (Club Africain, Algeria), Ahmed El-basha(Al-Merreikh, Sudan), Ahmed Zuway (CA Bibertin, Lybia), Abdoulrazak Fiston (Lydia Adacademic, Burundi), Alou Bagayok (Djoliba, Mali), Moxolisi Mthethwa (Royal Leopard, Swaziland) na Oboaboa Godfrey (Sunshine Stars, Nigeria).Pia yupo Alula Girma (St George, Ethiopia), Azuka Boko Izu (Sunshine Stars, Nigeria), Boubacar Bangolula (Djoliba, Mali), Edward Sadomba (Al Hilal, Zimbambwe), Essam El Hadary (El Merreikh, Misri), Emmanuel Clottey (Esperance, Ghana), Given Singuluma (TP Mazembe, Zambia), Omar Mohamed Bakheet(Al Hilal, Sudan), Rainford Kalaba (TP Mazembe, Zambia) na Razak Yakubu (Al Ahly Shandy, Ghana).Wengine ni Amouda Ahmed Elbashir (Al Ahly Shandy,Sudan), Arrison Affur (Esperance,Ghana), Ismailia Diara (Cercle Olympique de Bamako,Mali), Joao Hernani (Interclub,Angola), Mohamed Aboutreika (Al-Ahly,Misri), Mongezi Bobe (Black Leopards,Afrika Kusini), Mudather El-Taieb (Al Hilal, Sudan) na Solomon Asante (Berekum Chelsea, Ghana).Orodha hiyo inakamilishwa na Stopila Sunzu (TP Mazembe, Zambia), Taboko Eric Nyemba (AC Leopard Dolisite, DRC Congo), Tresor Mtupu (TP Mazembe, DRC Congo), Walid  Hicheri (Esperance, Tunisia),  Yannick N'Djeng (Esperance,Cameroon) na Youssef Msakni (Esperance, Tunisia).

No comments:

Post a Comment