Thursday, January 31, 2013

SIKUJUA KAMA MIALIKO YA HIZI TIMU KUCHEZA NA TAIFA STARS ILITOSWA NDIO IKACHAGULIWA CAMEROON.

.
January 30 2013 ndio nimefahamu kwamba kumbe timu za taifa za Congo Brazzaville, Equatorial Guinea, Rwanda na Swaziland ziliomba mechi ya kirefiki na timu ya taifa Taifa stars lakini zikatoswa.
Baada ya hizo timu za taifa kutoswa, iliyochaguliwa kucheza na Stars ni Cameroon katika mechi ambayo iko kwenye kalenda ya (FIFA) ya mechi za kirafiki zitakazochezwa kote duniani Februari 6 mwaka huu.
.
Hizo timu zote zilizotoswa kasoro Swaziland, zilikua zinataka hiyo mechi na Taifa stars ichezwe kwenye viwanja vya nyumbani kwao na sio hapa bongo lakini hii mechi ya Tanzania na Cameroon itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni.
Kikosi cha Cameroon kilichokamilishwa na wachezaji wengi wa kulipwa wanaocheza katika nchi mbalimbali duniani kitaanza kuwasili bongo Februari 3 mwaka huu ambapo pia TFF imesema Kocha wa Stars Kim Poulsen mwenyewe ndio alichagua stars ichezwe na Cameroon ambayocaptain wake ni staa Samuel Etoo.

HAPA NDIPO ANAPOISHI MCHEZAJI MKENYA AMBAE MAN U INA MPANGO WA KUMSAJILI.


Victor Wanyama ni mchezaji wa Harambee Stars ambae pia anaichezea Celtic ya Scotland, hapa ndipo nyumbani anapoishi ndani ya mji wa Glasgow.
Mtandao wa Ghafla umeripoti kwamba mchezaji huyu amefanya kitendo cha kijasiri cha kukubali kuonyesha nyumba yake kupitia vyombo vya habari kitu ambacho mastaa wengi wa Kenya ni waoga kukifanya, yani huwa hawakubali kuonyesha wanapoishi.
Taarifa zilizosambaa kwa sasa na hata kuripotiwa na Supersport Blitz ni kwamba Club ya soka ya Manchester United inampango wa kumsajili staa huyu Mkenya.

HAYA NDIO MANENO ALIYOYASEMA MWIGIZAJI LULU NJE YA MAHAKAMA KUU, UNAWEZA KUSOMA NA KUMSIKILIZA PIA


.
January 29 2013 ndio msajili amethibitisha kwamba mwigizaji Lulu ametimiza masharti yote ya dhamana juu ya kesi inayomkabili ya kuua bila kukusudia.
Lulu na mama yake mzazi wote kwa pamoja waliangua vilio baada ya dhamana yao kukamilika wakati wakiwa nje ya Mahakama kabla ya kuondoka na Lulu kuingia uraiani.
Haya ni maneno ya Lulu aliyoyatoa akiwa analia…. “Nawashukuru watu wote na nilikua naomba watu waendelee kuniombea sababu hii ni dhamana tu lakini kesi bado ina safari ndefu… nawashukuru wale wote waliokua na mimi kwa hali yeyote ile na zaidi zaidi namshukuru sana Mwenyezi Mungu

Tunajua biashara ya dini inalipa, lakini msiivuruge Tanzania-JK

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa mtindo wa kufanya fujo na kusababisha uvunjifu wa amani kwa visingizio vya dini nchini ni biashara inayolipa na ndiyo maana wakereketwa wa kufanya hivyo hawaishi.

Hata hivyo, akaonya kwamba Serikali katu haitawavumilia wanaotaka kuwavuruga Watanzania kwa kutumia dini zao.

Kikwete aliyasema hayo wakati wa kuwasilisha ripoti ya Mchakato wa Nchi za Afrika Kujitathmini zenyewe katika nyanja za Demokrasia, Utawala Bora na Uchumi (APRM) nchini Ethiopia mwishoni mwa wiki iliyopita.

Alisema ni jambo la kushangaza kuona kuwa wadau wanatumia dini kuiyumbisha nchi kwa vigezo kuwa ni miongoni mwa nchi zilizodumisha amani kwa muda mrefu.
Alisema kutokana na hali hiyo, Serikali yake haitayumba wala kusita kupambana ipasavyo na wafanya fujo hao ikiwa ni pamoja na kutumia njia za busara wakati wa kutoa uamuzi na hatua za kisheria.

“Kuna baadhi ya watu wanatumia vigezo vya kidini kwa ajili ya kufanya vurugu za kuhatarisha amani, Serikali haitaweza kuwavumilia, badala yake tutatumia njia mbalimbali ili kushughulikia matatizo hayo ikiwa ni pamoja na kutumia busara na hatua za kisheria,” alisema Kikwete.

Alisema mapendekezo yaliyotolewa na APRM ya kusimamia kwa uangalifu tofauti za kidini nchini ameyachukua kwa mikono miwili.

Alisema kitendo cha Tanzania kuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ni bahati iliyotokana na kutokuwapo kwa ugomvi wa kikabila, kidini ama yale ya kutokana na rangi za watu. Alisema hali hii inatokana na ukweli kuwa sera iliyopo haina ubaguzi kwa wananchi kwa misingi ya kabila, dini, rangi ama sehemu anakotoka Mtanzania, ni sera nzuri na wanaidumisha.

Kwa mujibu wa Kikwete, uzuri kuhusu dini katika Tanzania ni kwamba kila mmoja ana uhuru wa kuabudu na kwamba Serikali haina dini.

“Tunajua fika kuhusu hatari zinazoweza kusababishwa na baadhi ya wanasiasa na viongozi wa dini wenye malengo ya kuchochea fujo za kidini, hatuwezi kuyumba wala kusita kupambana ipasavyo na watu wa namna hiyo,” alibainisha.

Alisema ikiwa wataona uchochezi wa kidini unafikia kiwango cha kuhatarisha amani ya nchi ama uvunjifu wa amani na sheria na dola itachukua mkondo wake ili haki iweze kutendeka.

Israel yadaiwa kushambulia Syria

Urusi imekuwa ikiunga mkono sana Syria
Urusi imesema ina wasiwasi kuhusu tetesi kwamba Israel imeshambulia eneo fulani nchini Syria, ikisema kwamba shambulio hilo linakiuka Mkataba wa UN.
Jeshi la Syria lilisema mnamo Jumatano ndege za kivita za Israel zilishambulia kituo cha kijeshi cha utafiti Kaskazini-Magharibi mwa Damascus na kuwauwa watu wawili na kuwajeruhi wengine watano.
Lilikanusha habari kwamba malori yaliyokuwa yamebeba silaha na yaliyokuwa yakisafiri hadi Lebanon yalishambuliwa.
Urusi imekataa katakata kumshutumu Rais wa Syria Bashar al-Assad katika miezi 22 ya mgogoro wa kisiasa ambao umesababisha vifo vya zaidi ya watu 60,000.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi ilisema: "Kama habari hizi ni za kweli, basi itakuwa ni jambo la kuweko kwa mashambulizi yasiyo na sababu dhidi ya nchi huru, hata kama washambuliaji watakuwa na sababu zao za kufanya hivyo."
Uhusiano kati ya Urusi na Israel umeimarika katika miaka ya hivi karibuni huku ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi ukikua, asema mwandishi wa BBC aliyeko Moscow, Stephen Rosenberg.
Moscow ni mshirika wa karibu wa Rais Assad. Israel na Marekani wamekataa kutoa taarifa yoyote kuhusu tukio hilo.

Hifadhi ya Serengeti yatwaa tuzo ya kimataifa

HIFADHI ya Taifa ya Serengeti imeteuliwa kuwa mshindi wa Tuzo ya Kimataifa ya Utalii, Hoteli na Huduma za Vyakula kwa mwaka 2013. Uteuzi huu umefanywa na kamati ya uteuzi ya tuzo hizo baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa na waandaaji.

Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Pascal Shulutete alisema Tanapa itapokea tuzo hiyo itakayotolewa kwa Serengeti katika hafla maalumu iliyotarajiwa kufanyika jana mjini Madrid, Hispania.

“Tuzo hizi huandaliwa na taasisi maarufu duniani inayofahamika kama Global Trade Leaders’ Club inayohusisha kampuni zipatazo 7000 duniani,’’ alisema Shelutete.

Alisema tuzo hii ilianzishwa kwa ajili ya kutambua na kuenzi michango inayotolewa na taasisi na kampuni zinazojihusisha na utalii, hoteli pamoja na huduma za vyakula kama njia ya kuthamini mchango na kuhamasisha wale wote wanaofanya kazi katika sekta hii ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa nchi husika.

Shelutete alisema hafla ya utoaji wa tuzo za mwaka huu zilitarajiwa kuhudhuriwa na wadau wa shughuli za utalii kutoka nchi zipatazo 40 duniani na zingeambatana na maonyesho ya kimataifa ya utalii yanayofanyika kila mwaka mjini Madrid, maarufu kama FITUR ambayo Tanzania ni mshiriki.

Hifadhi ya Serengeti ni moja ya hifadhi kongwe nchini ambayo ilianzishwa miaka zaidi ya hamsini iliyopita na ambayo pia ni Eneo la Urithi wa Dunia, kwa sasa hifadhi hiyo ni maarufu kwa wanyama aina ya Nyumbu wahamao kila mwaka katika mzunguko unaohusisha nchi mbili za Tanzania na Kenya. Mzunguko huu wa wanyama wahamao unaaminika kuwa ndiyo pekee uliobakia ulimwenguni unaohusisha wanyama wakubwa wa ardhini.

“Kutolewa kwa tuzo hii ni heshima kwa Tanapa na nchi kwa jumla, ni matokeo ya sera nzuri za uhifadhi zinazosimamiwa na Tanapa katika kuhakikisha kuwa maeneo yaliyotengwa kisheria kama Hifadhi za Taifa yanaendelea kuhifadhiwa vyema kwa ajili ya vizazi vijavyo lakini pia kuhakikisha kuwa viwango vya huduma za utalii katika hifadhi zinakuwa za kiwango cha kimataifa ili kuhudumia wageni watokao sehemu mbalimbali ulimwenguni,” alisema Shelutete.

Tanapa imekuwa katika mchakato wa kuhakikisha inakuza na kutangaza maliasili na hifadhi za Tanzania kwa lengo la kuvutia dunia na watalii katika soko la utalii duniani sambamba na kuingia katika rekodi za kimataifa za masuala ya utalii.

Kufanya majukumu yako kunadumisha ndoa



Wanaume hata hivyo wanoonywa wasitumie utafiti huu kama kigezo cha kutowasaidia wanawake
Wanaume utafiti uliofanywa kwa watu waliooana nchini Marekani umebaini kuwa pale mme na mke wanapozingatia majukumu yao ya kitamaduni ndani ya nyumba huwa na maisha mazuri ya ndoa.
Utafiti huo ulihusisha wanandoa elfu nne na mia tano.
Ulibaini kuwa wakati wanawake wanapofanya kazi za kike pekee kama vile kupika na usafi na wanaume kufanya kazi za kiume kama vile kutengeneza gari na kupanga vitu kabatini hushiriki tendo la ndoa mara 1 nukta sita kwa mwezi zaidi ya wanaume wanaofanya kazi za kike.
Hata hivyo watafiti wamewaonya wanaume dhidi ya kutumia matokeo ya utafiti huu kama sababu ya kutowasaidia wanawake.
Wanasema hii inaweza kusababishha mzozo na pengine kupungua kwa muda wa kujamiiana.

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA HASEMI UKWELI, ANASIMAMIA UJANJA.


Mradi wa kujenga bomba la kusafirishia gesi MTWARA DSM utalipotezea taifa shs. Trilioni 1 (bilioni 1000) , na fedha hizi zitarudi mikononi mwa mafisadi na baadaye zitakuwa silaha nzito ya wezi hao katika kuhujumu demokrasia na haki za wananchi.

Kuleta GESI kwa bomba DSM ni sawa na ufisadi mwingine wowote ule, wizi ni wizi tu na lazima tuutamke, hata kama wizi huu wa sasa unatetewa na anayejiita "mtoto wa mkulima anayewagharimu wakulima".

Kama suala ni kuwa umeme unapaswa kufikishwa DSM ili kulinufaisha taidlfa zima tujenge mitambo ya umeme Mtwara na tusafirishe umeme wa waya angani ambao ni nafuu na utatumia nusu ya gharama zinazohitajika kutandika bombabla gesi.

Kama hoja ya serikali ni kuileta gesi ya matumizi ya majumbani nchi nzima na kwqmba lazima ifikishwe DSM kuna njia rahisi, bandari ya mtwara imekaa bila kazi yoyote miaka nenda miaka rudi, tunashindwa kuikarabati na kuipanua kwa gharama zisizozidi bilioni 100 kisha tukaanza kusafirisha gesi safi MTWARA hadi DSM kwa njia ya bandari hadi bandari? Nani ameturoga? Nani ametufumba macho tunaoneshwa na hatuoni? Nani ametuziba masikio tunasikilizishwa na hatusikii?

Bomba hili limekuwa bomba, nzi yuko tayari kufia kwenye kidonda. Hawaoni aibu kabisa CCM, hata wizi huu wa wazi wa bomba wanaung'ang'ania kwa nguvu ilimradi tu lengo lao la kupiga "mahela" ya kujipanga na uchaguzi wa 2015.

Watanzania masikini, tunaibiwa hivi hivi na hivi sasa ni kama tuko msibani, vyombo vya habari vimeanza kucheza muziki wa Pinda na kusifia huku vikijua taifa linaliwa na kwamba kuna kila harufu ya rushwa na ufisadi na wizi wa wazi kwenye mradi wa ujenzi wa bomba.....lol...

Yesu wala Mtume Mohhamad hawatashuka kuja kutusaidia katika wizi huu, mungu ametupatia akili na utashi, lazima tuvitumie kudai haki zetu, kupigania maslahi ya nchi yetu, kukataa kuonewa, kukandamizwa na kukubali kutawaliwa bila huruma na "wakoloni weusi".

TAFADHALI "SHARE" HILI TANGAZO -and dont dare to mis it

Monday, January 28, 2013

God's Debt Policy,Lern with me this Masterious truth.

The rich rules over the poor, and the borrower is the slave of the lender (Prov 22:7 RSV). The Bible reveals that you cannot be in debt and be free and yet Jesus came to set us free from all forms of slavery. That is why it is written: You were bought at a price; do not become slaves of men (1 Cor 7:23-24).
To keep us free from the servitude of debt, God has instituted what in today’s terms may be called a consumer protection policy, a kind of policy that modern economies are trying to institute especially where debt has gone bad. That’s why I say, God’s financial system is superior, and, secure!
In Deut 15:1-2, God institutes that all loans must be restricted to a period of no more than seven years, and the lender must forgive and cancel all outstanding loans at the end of the seven years. Exodus 22:26 and 24:6 institutes that a man’s (or a woman’s) livelihood shall not be taken as security for a loan. While as, in Deut 15:6, God lays out His plan regarding debt: I will bless you as I have promised, and you will lend to many nations but will borrow from none. The New Testament echoes this plan perfectly when Paul instructs believers to live God’s debt-free plan by owing no man anything (Rom 13:8 KJV).
Look, when God allows debt, He institutes very restrictive law on debt management. When God expresses his plan regarding debt, He speaks of a no-debt-status kind of plan: “You shall borrow from none”. What I read into God’s debt law is this: “My plan is not for you to be a borrower but for you to be debt-free, and even more than that, a lender”. And that is why I say, God’s debt policy, is a no-debt policy. What do you read into God’s debt law?
source-Nawiri.org

Lern how to come out of debt and to stay out forever.

We have talked about how to come out of debt, but, it is not enough to just come out, you need to stay out. To do so, you need to take five measures:
First measure: Establish a no-debt policy. You may want to make this, one of your money values. To achieve this, you will need to establish some tough measures: 1) stop all borrowing and credit; and 2) stop spending more than you earn- be proud of living within your means. You cannot get to zero debt with a continued culture of borrowing and overspending. It is impossible to control spending without an effective income and expenditure plan. Always plan ahead.
Second measure: Save and invest for expected future needs such as education, child birth, wedding, car repairs, holiday, extra giving, retirement, etc.
Third measure: Set up an emergency fund without which unexpected financial interruptions such as sickness, job loss, etc will push you back into debt. Aim at building a fund equivalent to at least three months worth of expenses.
Fourth measure: Trust and be creative. For capital intensive projects, go creative; think partnership, joint venture, leasing instead of owning, and so on. Also, purpose to trust God to provide what you need debt-free.
Fifth measure: Be debt-wise. God’s own wisdom advises you “Not to be a man who strikes hands in pledge or puts up security for debts because if you lack the means to pay, your very bed will be snatched from under you” (Prov 22:26-27). He also warns you to “Not put up security for another because you will surely suffer for it. Instead, refuse to strike hands in pledge and you will be safe” (Prov11:15). He shows you that “Striking hands in pledge and putting up security for your neighbor amounts to lack of good judgment” (Prov 17:18).
Never borrow money for speculative investments. However, you may borrow money (if you must) for guaranteed opportunities such as financing a business tender. Over the long term nevertheless, I advise that you aim at developing what I call “opportunity savings”.
SOURCE-NAWIRI.ORG

Zitto Kabwe Ahoji Asema serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wa bomba

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amemtaka Rais Jakaya Kikwete aende Mtwara ili kusikiliza malalamiko ya wananchi katika sakata la gesi asili badala ya kuendeleza malumbano ya kumtafuta mchawi.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Bara) na Waziri Kivuli wa Fedha, alisema kuwa kama serikali haitashughulikia suala la Mtwara sasa, yatajitokeza matatizo ya aina hiyo katika mikoa mingine yenye rasilimali zisizonufaisha wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Zitto alisema kuwa, hapa nchi ilipofika ni lazima kwanza kusikiliza kilio cha wananchi wa Mtwara ikiwemo kuelewa madai yao.
“Swali kubwa la watu wa Mtwara na Kusini kwa ujumla ni ‘tunanufaikaje?’ Jibu la swali hili si ahadi za miradi, bali ni vitendo. Hapa ndipo serikali inaposhindwa kushughulikia suala hili, kutoelewa madai ya wananchi na kuyapotosha,” alisema.
Zitto aliongeza kuwa, yafaa viongozi wa kisiasa wenye ushawishi kutoka pande zote, chama tawala na vyama vya upinzani, waende Mtwara kuzungumza na wananchi, lakini wawasikilize kwanza.
Alibainisha kuwa mradi huu wa kutandaza bomba la urefu wa kilometa 542 ni mkubwa sana hapa nchini, na una thamani kubwa zaidi kuliko miradi mingine yote ya miundombinu iliyopata kutokea.
Mradi huu utajengwa kwa mkopo wa dola za Kimarekani 1.2 bilioni kutoka Benki ya Exim ya China.
Alisema kuwa wananchi wa Mtwara kupitia maandamano ya Desemba 27 mwaka jana, wametaka kujua hatma ya maendeleo ya mikoa ya kusini kutokana na mradi huu wa bomba la gesi.
“Serikali imewajibu wananchi hawa kwa kuwaita wahaini, watu hatari na wasioelewa. Imefika mahali inapotosha madai yao kwamba hawataki gesi itoke Mtwara,” alisema.
Katika hilo, Zitto alisema Rais Kikwete ana majibu, hivyo ayatoe sasa kwa wana Mtwara. Kwamba kwa mujibu wa mpango kabambe wa umeme nchini (Power System Master Plan), kulikuwa na mradi wa kufua umeme Mnazi Bay, ambao aliagiza utekelezwe mara moja.
Alisema kuwa serikali ieleze umma kuhusu mradi huo wa kujenga kituo cha kufua umeme 300MW Mnazi Bay, Mtwara na kujenga msongo wa umeme wa 300KV mpaka Singida umeishia wapi?
“Ikumbukwe kuwa Oktoba 12 mwaka jana, Rais Kikwete alipokea ripoti ya ujenzi wa mradi huu kutoka makampuni ya China National Machinery & Equipment Import & Export Corporation (CMEC) ya China na Siemens ya Ujerumani, ambayo kwa pamoja yalitarajia kujenga kituo kikubwa cha kuzalisha umeme kutokana na gesi katika eneo la Mnazi Bay, mjini Mtwara,” alisema.
Zitto aliongeza kuwa, mradi huo ingehusisha kujenga njia ya kusafirisha umeme ya kilomita 1,100 kutoka Mtwara hadi Singida na ungegharimu dola za Kimarekani milioni 684 na kwamba rais aliagiza utekelezwe haraka sana.
“Huu mradi uliishia wapi? Kwa nini serikali ipo kimya kuhusu mradi huu ambao ungejibu kabisa maswali ya watu wa Mtwara?” alihoji.
Zitto alimsifu Rais mstaafu Benjamin Mkapa, akisema ameshatoa kauli kuhusu suala hilo, na kwamba ni wakati muafaka sasa kwa viongozi wengine kumuunga mkono kwa kwenda Mtwara na kukaa na wananchi wa wilaya zote kusikiliza hoja zao na kuona namna ya kupata ufumbuzi wa suala hilo.
Alisema wakati hatua hiyo inachukuliwa, wananchi waombwe kutulia na kuacha vurugu za aina yoyote ile, na serikali isimamishe mradi mpaka hapo suluhu na wananchi itakapopatikana.
“Serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wa bomba, kwani ni dhahiri gharama za mradi huu ni kubwa mno kulingana na uhalisia wa miradi ya namna hii duniani kote. Katika taarifa zote kwa umma serikali imekuwa ikisema kwamba utagharimu jumla ya dola za Kimarekani 1.2 bilioni,” alisema.
Aliongeza kuwa, katika taarifa ya Wizara ya Nishati na Madini, iliyotolewa na George Simbachawene kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini juzi, ilisema mradi utagharimu dola za Kimarekani milioni 875. Kwamba usiri katika mkataba huu unaashiria kwamba serikali inaficha kitu.
Zitto alisema kuwa amelazimika kutoa ufafanuzi huo wakati chama chake kikiandaa tamko, kwa lengo la kujibu kile alichokiita uzushi wa Simbachawene alioutoa kwa wahariri, kwamba yeye anachochea wananchi wa Mtwara na kutumika bila uzalendo.
“Vile vile alitoa vielelezo kadhaa kuonyesha kuwa mradi wa kujenga bomba la gesi ni gharama sawa sawa. Akasisitiza kwamba mimi ni mwongo. Katika kipindi chote cha mgogoro wa gesi Mtwara, sijafika Mtwara. Sijafanya mkutano wowote na waandishi zaidi ya kuandika mawazo yangu, kama Mtanzania kuhusu suala hili,” alisema.
Zitto alisema hataki kubishana na naibu waziri huyo ama kiongozi yeyote ya serikali kwa sasa wakati nchi yetu inaungua. Kwamba huu sio wakati wa kutafuta mchawi bali kutafuta majawabu ya changamoto zilizopo mbele yao.
Mtikila anena
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (DP), Christopher Mtikila, amemtaka Rais Kikwete kutumia hekima katika kumaliza mgogoro wa gesi na maslahi ya Mtwara kinyume chake nchi inaweza kugawanyika.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mtikila alisema kuwa madai ya kwamba umeme wa gesi hiyo ufuliwe kulekule Kusini yanatokana na uchungu wa wananchi wote wa Kusini.
Alisema iwapo moto wa mgogoro huo hautauzimwa kwa hekima, si ajabu ukaimeza mikoa yote ya Kusini ikiwemo Lindi, Ruvuma, Mbeya, Iringa, Morogoro na hata Rukwa ambapo matokeo yake ni kuzaliwa mataifa mawili mpaka ukiwa reli ya kati.
Mtikila alisema wakazi wa Kusini hawazuii gesi hiyo isitoke bali wanachotaka umeme huo ufuliwe kule kule, lengo likiwa ni kuwaletea mapinduzi ya maendeleo.
“Wananchi wa Mtwara wanafahamu kwamba sumaku ya mandeleo ya uwekezaji wa miradi mikubwa ya kuwaletea maendeleo ni nishati na miundombinu, lakini watawala wa CCM waliwanyang’anya reli ya kusini kwa uharamia wa kung’oa mpaka mataruma na kufutilia mbali hata na tuta lenyewe,” alisema.
Aliongeza kuwa Rais Kikwete analazimika pia kutamka bayana kipaumbele kwa uboreshaji wa bandari kuu ya Mtwara, ikibidi hata kwa kusitisha mradi wa bandari ya Bagamoyo.
Kwamba njia pkee ya kuzima moto huo Kusini na kurejesha amani ni rais huyo kutoa tamko la kukubali kufuliwa umeme huo mkoani Mtwara kwa ajili ya maslahi ya taifa.

‘Sumu’ ya DK Slaa yaitesa CCM Moshi

Mwita alisisitiza kuwa kamwe CCM haiwezi kujibu hoja kwa kusukumwa na mikutano ya Chadema bali watafanya hivyo kunapokuwa na hoja na CCM iko katika mchakato wa kujibu mapigo.
Katika mkutano huo, Dk Slaa, Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), John Heche walimwaga sumu inayokifanya CCM kuweweseka.
Katika mkutano huo viongozi hao pamoja na Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema wanadaiwa kutumia maneno makali kumshambulia Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama.
Viongozi hao wa Chadema waliwachongea Gama, Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Bernadette Kinabo na Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Ibrahim Msengi kuwa wanaingilia utendaji wa Halmashauri.
Kauli za viongozi hao zilitokana na hotuba ya Meya wa Manispaa ya Moshi kuwashtaki viongozi hao wa serikali ya CCM kuwa wanazuia utekelezaji wa maamuzi ya baraza kwa masilahi ya kisiasa.
Meya huyo alisema viongozi hao wamekuwa wakitumia vibaya vikao vya ushauri mkoa (RCC) na vile vya wilaya(DCC) kuingilia uamuzi halali wa Manispaa ya Moshi inayoongozwa na Chadema.
Alitoa mfano wa viongozi hao kumwagiza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Bernadette Kinabo kuendesha operesheni dhidi ya wafanyabiashara wadogo ili kuichonganisha Chadema na wananchi.
Kwa mujibu wa Meya huyo, Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo limekuwa katika wakati mgumu kutokana na Kinabo kukataa kutekeleza maazimio ya vikao halali ili tu kuinufaisha CCM kisiasa.
Mathalan alisema, sera ya Chadema Moshi Mjini ni kuwalipia ada wanafunzi wote wa sekondari ambao wazazi wao hawana uwezo, lakini mkurugenzi huyo amekataa kuidhinisha fedha hizo.
Meya huyo alisema mwaka 2011/2012, Halmashauri hiyo inayoongozwa na Chadema ilitenga Sh196 milioni kulipa ada hizo na mwaka 2012/2013 imetenga Sh216 milioni ambazo zote hazijaidhinishwa.
“Ukimuuliza anasema sera ya elimu bure siyo sera ya Serikali.Tunaomba hoja hiyo uipeleke bungeni tujue ni wakati gani vyama vinaweza kutekeleza sera zake kwa halmashauri inazoziongoza,”alisema.
Meya huyo alisema vitendo vinavyofanywa na viongozi hao wawili ni dhahiri vina lengo la kuidhoofisha Chadema kisiasa katika Jimbo la Moshi na pia kuwagombanisha na wananchi.

Wakati bunge linatarajiwa kuanza kesho,Wabunge watano kuwasilisha hoja binafsi

 
WAKATI Kikao cha Kumi cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinatarajiwa kuanza kesho, Wabunge watano wamejitokeza kuwasilisha hoja binafsi katika kikao hicho.
Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Zanzibar Habib Mnyaa anakusudia kuwasilisha maombi ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara kupinga gesi iliyogundulika mkoani humo kusafirishwa kwenda jijini Dar es Salaam.
Naye Waziri Kivuli wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo  Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alisema atawasilisha hoja binafsi kutaka kujua fedha zinazotumika kulipia vipindi vya runinga vinavyoelezea mafanikio ya Serikali.
Mbilinyi ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) alisema atafanya hivyo ili kujua fedha hizo zinalipwa na nani kwa malengo gani.
Kwa upande wake, Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba anatarajiwa kuwasilisha hoja ya kuitaka Serikali kupeleka bungeni muswada wa sheria, wa kuanzisha Mfuko wa Elimu ya Juu. Lengo kuu ni kuhakikisha kila mwanafunzi aliyepata nafasi ya kujiunga na elimu ya juu anakopeshwa kwa asilimia 100.
Naye Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa anatarajiwa kuwasilisha hoja binafsi kutaka Bunge liunde Tume ya kuchunguza vitendo vya ujangili vinavyoendelea hapa nchini.
Kwa upande wake Mbunge wa Msoma Mjini (Chadema), Vincent Nyerere atawasilisha hoja binafsi kuhusu matukio ya kigaidi na mauaji holela ya raia wasio na hatia yanayotokea hapa nchini.
Nyerere alisema hivi sasa vitendo vya mauaji vinaendelea, utasikia polisi kauawa na wananchi au wananchi wamemuua polisi lakini hakuna hatua zaidi.Analitaka Bunge kutoa maadhimio kuhusu vitendo hivyo vinavyohatarisha usalama wa raia na mali zao.

Vurugu Mtwara: Wabunge waangua vilio

WABUNGE waliochomewa nyumba na mali zao katika vurugu zilizotokea Mtwara juzi; Anna Abdallah na Mariam Kasembe, jana waliangulia vilio walipotakiwa na gazeti hili kuzungumzia tukio hilo.
moja ya nyumba ya mbunge iliyochomwa juzi huko mtwara
Nyumba za wabunge hao wa Viti Maalumu na mali zingine kadhaa za taasisi mbalimbali, ni miongoni mwa vitu vilivyoharibiwa katika vurugu hizo ambazo pia zilisababisha vifo vya watu wanne wilayani Masasi.
Akizungumza kwa huzuni,  Anna alisema hajui sababu za uharibifu huo, hasa ikizingatiwa mwenyewe amekuwa huko kwa karibu siku tatu na hakuona dalili za uhasama wowote dhidi yake.
Anna ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho alisema: “Nina siku ya tatu hapa Masasi na nimeshiriki mkutano wa halmashauri kwa mwaliko na wakati wote, sikuhisi chochote hivyo siwezi kujua sababu ya chuki iliyofanya nyumba yangu ichomwe moto,” alisema.
Alipotakiwa aeleze hali ilivyokuwa, alisema, “Wavamizi hao walipora kila kitu nyumbani kwangu yakiwamo mapazia, kabla ya kumwaga petroli kila chumba na kuwasha moto.”
Aliendelea kueleza,” Kila kitu kiliteketea. Inatia uchungu kwani nyumba hiyo niliijenga kwa kudunduliza fedha kidogo kidogo nikiwa mkuu wa mkoa.”
Anna alisema, kundi hilo la vijana lilivamia nyumbani kwake saa 4:00 asubuhi na kuanza kupora mali kwa kupita chumba kimoja baada ya kingine.
“Hali si nzuri. Kila kitu kimeibwa na nyumba imechomwa moto, hakuna kilichobaki. Walichukua kila kitu na itanichukua muda mwingi kujua thamani halisi ya hasara iliyopatikana,” alisema.
Kauli ya Kasembe
Naye Kasembe alipokea simu ya mwandishi wa habari hii kwa kilio na kuikata huku akisema, “Jamani niacheni… Mwenzenu naumia…!”
Alipopigiwa tena baadaye, alisema anashangazwa na tukio hilo ambalo limemfika bila kutarajia na kumtia hasara kubwa.
“Wamepora kila kitu katika nyumba na kuichoma moto, sijui atakuwa nani huyu, kwani sina tatizo na wapiga kura wangu na sina mgogoro na mtu yeyote. Nashindwa hata kuhisi nani kafanya uchochezi,” alisema Kasembe.
Alisema wakati wa vurugu hizo, ndugu zake akiwamo mama yake, walikimbia na kwenda kujihifadhi hotelini, lakini mpaka sasa hawajui wataishi vipi baada ya nyumba hiyo kuteketezwa kwa moto.
“Jana wanafamilia walilala hotelini na leo tupo nje ya gofu la nyumba yangu ambayo imeteketea kabisa kwa moto, tunasubiri majaaliwa mengine, lakini nimechanganyikiwa kwa kweli na sijui ni kitu gani hiki, siamini,”alisema.
Polisi waeleza uharibifu
Watu 44 wanashikiliwa na polisi wilayani Masasi kufuatia vurugu hizo.
Kamanda wa Polisi Mkoa  wa Mtwara, Maria Mzuki alisema watu hao wamekamatwa kwa wakituhumiwa kujihusisha na vurugu hizo zilizosababisha uhalibifu mkubwa mali.

BREAKING: PICHA 8 ZA LULU MAHAKAMANI LEO JAN 28 PAMOJA NA MAELEZO YA MASHARTI YA DHAMANA YAKE.


Lulu akiwa anaingia Mahakamani leo january 28 2013 akiwa na shauku ya kupata dhamana.
Mahakama kuu leo imetangaza dhamana ya mwigizaji Lulu lakini iwapo atatimiza masharti aliyopangiwa ambayo ni pamoja na kuwasilisha hati yake ya kusafiria, kutosafiri nje ya Dar es salaam, kujiwakilisha au kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila mwezi pamoja na wadhamini wake wawili ambao kila mmoja adhamini kwa shilingi milioni 20 za kitanzania.
Upande wa familia ya Lulu umesema masharti yote yaliyotajwa wanaweza kuyatimiza leo leo hivyo wanasubiri tu jibu la msajili ambae ndio anatakiwa kuhakikisha hayo masharti yametimia kisha ruhusa ya kumkabidhi Lulu kwa familia yake itolewe.
Taarifa za ndani ni kwamba uwezekano wa Lulu kuachiwa upo kuanzia january 29 2013 ambayo ni kesho kwa sababu kuna watumishi wawili wa serikali ambao wapo kikazi mkoani Pwani na ndio walitakiwa kutia saini dhamana ya Lulu wakiwa ni sehemu ya masharti.
.
.
.
.
Hapa ni wakati alipocheka sana pale mwandishi mmoja wa kike ambae pia alikua akimpiga picha alipokua akimlainisha Lulu kwa maneno baada ya mwigizaji huyo kuficha uso wake alipokua akipigwa picha, alisema alikua anaumizwa macho na mwanga wa kamera.
.
.
Mama mzazi wa Lulu ni mwenye nguo nyeupe na nyeusi.
chanzo-millardayo.com

Friday, January 25, 2013

MATOKEO YOTE YA MECHI ZA AFCON LEO JAN 25 2013 NA MAJINA YA WAFUNGAJI.

.
.

Manumba apelekwa kutibiwa Afrika ya Kusini

HATIMAYE Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba (picha ndogo chini) amesafirishwa kupelekwa nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Jaffer Dharsee ambako Manumba alikuwa amelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU) tangu Januari 13, mwaka huu, amethibitisha kusafirishwa kwa kiongozi huyo wa Polisi.
“Ni kweli amesafirishwa jana (juzi),kwenda Afrika Kusini, akiwa katika hali ya kuridhisha, ila sijajua bado jina la hospitali aliyopelekwa,”alisema Dk Dharsee.
Akizungumza na gazeti hili juzi mchana, kabla ya kusafirishwa Manumba, Dk Dharsee alieleza kuwa hali ya kiongozi huyo sasa inatia matumaini kwani ameweza kujitingisha baadhi ya viungo vya mwili wake, tofauti na awali alipofikishwa hospitalini hapo.
“Anaendelea vizuri, licha ya kwamba yupo ICU, lakini anatia matumaini kwa sababu kwa sasa naweza kusema amepata ufahamu, kwani anaonyesha kuwa ana maumivu,hata uso wake sasa umebadilika tofauti na awali alipokuwa hajitambui,” alisema Dk Dharsee.
Awali Dk Dharsee alithibitisha kuwa Manumba anasumbuliwa na malaria kali baada ya kumfanyia uchunguzi na kukutwa na wadudu 500 wa ugonjwa huo hatari, hali ambayo ilisababisha apoteze fahamu na figo zake zote mbili kushindwa kufanya kazi.
Kwa upande wa Mganga Mkuu Mwelekezi wa Polisi, Dk Ahmed Makata aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu jana kuwa, kusafirishwa kwa Manumba kumefanikiwa baada ya afya yake kuimarika vyema tofauti na ilivyokuwa awali.
“Mimi kwa sasa nipo Tanga, lakini imewezekana kumsafirisha kwa kuwa afya yake imeimarika, yaani presha, mzunguko wake wa damu kwa kifupi ni kwamba imewezekana kwa sababu yupo vyema sasa tofauti na awali, ambapo ilishindikana kumsafirisha,”alisema Dk Makata.
Msemaji wa Polisi, Advera Senzo alipohojiwa kuhusu kusafirishwa kwa Manumba, alithibitisha, lakini hakuwa tayari kueleza amesafirishwa wakati gani, ndege iliyomsafirisha, wala hospitali aliyopelekwa.
“Taarifa ninayokupa ni hii, amesafirishwa jana (juzi) kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi basi hayo mengine mimi sikwambii kwa sasa, lakini amefika salama,” alisema Senso.
Tangu alipolazwa katika Hospitali ya Aga Khan chumba cha ICU, akiwa hajitambui huku akipumua kwa msaada wa mashine, viongozi mbalimbali wakiwamo wa Serikali walimtembelea ili kumjulia hali.
Miongoni mwa viongozi waliomtembelea ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete, Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mke wake mama Tunu Pinda.

Vurugu tupu Tanzania,NI JUU YA GESI YA MTWARA

MAENEO ya mikoa ya Morogoro, Mtwara na Dar es Salaam, jana yaligeuka uwanja wa fujo na vurugu zilizosababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali, huku polisi wakitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi.
 
Vurugu hizo zimehusisha wakulima na wafugaji wa jamii ya Kimasai kwa upande mmoja wa Morogoro, Mtwara Mikindani wananchi waliizingira nyumba ya Diwani wa Kata ya Mikindani kwa madai ya kuwahifadhi watu wanaodaiwa kuwa washirikina ndani ya nyumba yake, huku Dar es Salaam eneo la Kariakoo, polisi na Wamachinga wakipambamba na Mgambo wa Jiji.
Mkoani Mororgoro mtu mmoja aliyefahamiwa kwa jina la Mohamed Msigara (60) amefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya kutokea vurugu kati ya wakulima na wafugaji Kijiji cha Dumila, wila yani Kilosa, baada ya wafugaji wa Jamii ya Kimasai kuingiza mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima yaliyo katika Kitongoji cha Mfulu, Kilosa.
Pamoja na mauaji hayo, wasafiri waliokuwa wakitumia Barabara ya Morogoro – Dodoma, nao walionja machungu ya vurugu hizo, baada ya kukwama kwa saa 5 kutokana na wananchi wa kijiji hicho, kufunga barabara kwa mawe, magogo ya miti na kuchoma magurudumu ya gari.
Wananchi hao walichukua hatua hiyo huku wakisisitiza kutaka kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, ili kumaliza mvutano huo.
Katika vurugu hizo wanakijiji hao walivunja vioo vya madirisha ya baadhi ya nyumba tano za kulala wageni, kuharibu gari dogo aina ya Landcruser pamoja na kupora mali mbalimbali zi nazodaiwa kumilikiwa na wafanyabiashara wa jamii ya Kimasai.
Kabla ya kufanya uharibifu huo saa 2:30 asubuhi, wananchi hao walifanya maandamano sambamba na kusimama katikati ya barabara, hali iliyosababisha polisi kufika eneo hilo kwa ajili ya kuwadhibiti.
Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU), walifika eneo la tukio 5:20 asubuhi na kufanikiwa kuwatawanya wananchi hao kwa kutumia mabomu ya machozi, hatimaye kufungua barabara hiyo.
Pamoja na barabara hiyo ya Morogoro – Dodoma, wananchi hao pia walifunga barabara ya Dumila- Kilosa, hivyo kuyafanya magari yaliyokuwa yakitumia barabara hiyo kukwama kwa zaidi ya saa sita na kusababisha usumbufu kwa wasafiri waliokuwa wakitumia barabara hiyo.
Wakati vurugu hizo zikiendelea, wafugaji wa jamii ya Kimasai wakiwamo wanawake na watoto walionekana kukimbilia kwenye kituo kidogo cha Polisi Dumila kwa lengo la kujihami na kupata msaada wa polisi kutokana na hofu ya kushambuliwa na wananchi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyekuwepo kwenye eneo la tukio, mkulima aliyefahamika kwa jina Mauya Hamadi alisema kuwa wananchi wamelazimika kufanya vurugu hizo baada ya wafugaji wa jamii ya Kimasai kuingiza mifugo kwenye mashamba ambayo tayari yameshapandwa mazao na kufanya uharibifu.
Alisema kuwa tayari suala hilo walishalifikisha kwa uongozi wa kijiji, kata, wilaya hadi mkoa, lakini hakuna jitihada zozote zinazofanywa na viongozi, hivyo kulazimika kumtaka Mkuu wa Mkoa Joel Bendera, kwenda kuzungumzia suala hilo, ambapo hata hivyo mkuu huyo wa mkoa hakuwahi kufika eneo hilo hadi walipoamua kufanya maandamano hayo.

TAMKO LA NDUGU BENJAMIN WILLIAM MKAPA.KUHUSU VURUGU ZA MTWARA


Katika wiki za hapa karibuni kumekuwa na mijadala na mazungumzo mengi kuhusu mikakati ya maendeleo ya mikoa ya Kusini hususan Mkoa wa Mtwara.  Mazungumzo hayo yamekuwa na lugha kali na yameambatana, hatimaye, na maandamano na mikutano ya hadhara.  Kiini chake ni matumizi ya gesi iliyogunduliwa mkoani kwa ajili ya miradi au mipango ya maendeleo ya mkoa huo, mipango iliyopo mbioni kutekelezwa au inayotarajia kutekelezwa.  Mwenendo wa mazungumzo, maandamano na mikutano ya hadhara imeelekea kuashiria shari na kuvunjika kwa amani.
Aidha vituko na kauli hizo zimekaribia kujenga kutokuelewana kati ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali, kati ya wanachama wa vyama vya siasa na viongozi wao, kati ya wananchi na viongozi wa Serikali.  Mtafaruku huu haufai kuachwa uendeleee na kutishia usalama.  Mipango ya maendeleo siyo Siri.  Mikakati na mbinu za Utekelezaji wake siyo Siri.  Maelezo yake mazuri yanaweza kutolewa yakadhihirisha namna na kasi ambayo raslimali zitawanufaisha wananchi wa eneo zilizomo na Taifa zima.  Utekelezaji wa miradi unategemea masharti kadhaa, k.m. Uwapo wa mitaji na teknolojia.  Lakini pia mwekezaji, awe Serikali au Sekta binafsi, atataka iwepo hali ya utulivu na usalama wa watu, hali na mali.  Hayo yatadaiwa na wawekezaji wa ndani na wa nje.  Vurugu, fujo, vitisho havivutii uwekezaji.
Nikiwa Mwana Mtwara na raia mwema mpenda nchi, nimefadhaishwa sana na matukio haya ya siku za karibuni Mtwara.  Kwa sababu hiyo natoa wito kwa wadau wote wa maendeleo ya Mtwara kusitisha harakati hizi na maandamano na mihadhara na badala yake wajipange KUKAA PAMOJA katika meza moja, kupitia historia, kutathmini mipango, kuchambua kwa kina mikakati ya utekelezaji wake, na hatimaye kufikia muafaka wa Ujia wa maendeleo. Fujo, vitisho, kupimana nguvu na malumbano kamwe si masharti ya maendeleo.  Mazungumzo yataboresha sera, ya uwekezaji ya mkoa na nchi.
Linalowezekana leo lisingoje kesho.
Benjamin William Mkapa
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Monday, January 21, 2013

Manchester United yavutwa shati.

Mshambuliaji wa Van Persie akishangilia goli
Vinara wa ligi kuu ya England, Manchester United imeambulia pointi moja baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Tottenham.
Mshambuliaji Robin Van Persie aliiwezesha timu yake ya Manchester United kuongoza kipindi cha kwanza baada ya kufunga bao katika dakika ya 25.
Van Persie alipata goli hilo akiunganisha krosi ya Tom Cleverly.
Man United wakiamini kuwa tayari wamepata ushindi katika mechi hiyo, walijikuta wakigawa pointi baada ya Clint Dempsey kufunga katika dakika za majeruhi na kuamsha shangwe kwa mashabiki wa Tottenham katika uwanja wao wa White Hart Lane.
Matokeo hayo bado yanaiacha Manchester United kileleni mwa ligi hiyo ikiwa na pointi 56, huku ikifuatiwa na Manchester City yenye pointi 51.
Tottenham iko katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 41, pointi nne nyuma ya Chelsea yenye pointi 45, ikikakalia nafasi ya tatu ya ligi kuu ya England.
Timu zote hizo nne zimecheza mechi 23 kila moja.

CAMPUS NIGHT 2013 @ MOSHI & ARUSHA ILIKUWA BAM BAM.

https://fbcdn-sphotos-e-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash4/321458_473751066022255_1525025522_n.jpg

Dk Slaa: Tutaipeleka puta CCM hadi 2015

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa amesema kuwa kuanzia mwaka huu hadi 2015, chama chake kitaipeleka mchakamchaka CCM, kwa kuwa chama chake kimefanikiwa kuwaamsha Watanzania.
Alisema kwamba Watanzania sasa wameamka na kutambua utajiri wa nchi yao na jinsi   rasilimali zinavyotoroshwa nje ya nchi na kuanza kudai kufaidika nazo kwa nguvu. Hivyo Chadema kitaitumia fursa hiyo kuipeleka puta CCM, lengo likiwa kuhakikisha kila Mtanzania anaishi maisha bora.
 
Dk Slaa alisema hayo alipokuwa akizungumza katika kongamano la Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini, ambao ni wafuasi wa chama hicho (CHASO), lililofanyika Dar es Salaam jana.
Alieleza kuwa kinachotokea mikoa ya Lindi na Mtwara, pamoja na maandamano ya hivi karibuni ya wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) ni majibu tosha kwa CCM, kwamba mikutano ya Chadema iliyofanyika mikoa mbalimbali nchini imewaamsha wananchi.
Wanafunzi zaidi ya 500 walihudhuria kongamano hilo kutoka  IFM, Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU), Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) na  Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (DIT), pamoja na vyuo mbalimbali vilivyopo Dar es Salaam na mikoani.
Desemba 18 mwaka jana Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe alisema kuwa mwaka huu utakuwa ni wa kuunganisha nguvu ya umma kitaifa, baada ya Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuzifanyia kazi hoja mbalimbali zinazotolewa na chama hicho.
Dk Slaa ambaye alitumia saa 1:06 kuzungumza na wanafunzi hao, alisema kuwa elimu ya uraia waliyoitoa kwa wananchi katika mikutano ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), pamoja na Operesheni Sangara, wamefanikiwa kwa asilimia 99.
“Tumewapa elimu ya uraia wananchi katika mikoa yote nchini na sasa wanajua haki zao,.Hiyo ni kazi na mikutano yetu pamoja na maandamano tuliyoyafanya” alisema Dk Slaa na kuongeza:
“Nawapongeza wanafunzi wa IFM kwa kuandamana, najua wapo watakaosema nachochea maandamano, lakini wanatakiwa kujua kwamba wanafunzi hawa walikuwa na haki, haiwezekani wanabakwa kisha wakae kimya, tena wametoa taarifa polisi na hakuna kilichofanyika.”
Mbali na kutaka Mkuu wa Jeshi la  Polisi nchini, IGP Said Mwema na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova kujiuzulu kwa kitendo cha kuamuru  wanafunzi wa IFM kupigwa wakati walikuwa wakililia usalama wao, alisema kwamba kuna tofauti kubwa kati ya vurugu na kudai haki za msingi.
“Inakuwaje polisi wanawapiga mabomu wanafunzi wanaofanya maandamano, lakini wanashindwa kuzuia Twiga wanaotoroshwa nje ya nchi, tuungane, tushirikiane na tupige kelele, ili mali zetu zirudi,” alisema Dk Slaa na kuongeza:

Msafara wa Mangula wazomewa Mwanza

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Taifa Philip Mangula jana alionja machungu aliyowahi kupata Waziri Mkuu Mizengo Pinda baada ya msafara wake kuzomewa jijini Mwanza.
Msafara huo wa Mangula ulizomewa jana muda mfupi baada ya kumaliza mkutano wake katika uwanja wa michezo Nyamagana.

Katika msafara huo mbali na Mangula pia walikuwapo Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, Naibu Waziri wa Ujenzi, Grayson Lwenge na Katibu Itikati na Uenezi, Nape Nnauye.  
Mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo, baadhi ya wananchi waliokuwa katika mkutano huo ambao hawakuwa wamevalia sare za CCM, walijipanga kando ya barabara ya Posta na wakati viongozi hao wakipita waliwazomea huku wakionyesha ishara ya vidole viwili.
Kutokana na hali hiyo, vijana wa CCM maarufu kama Green Guard walianza kuvamia wazomeaji hao na kuanza kutembeza kipigo ambapo vijana wawili ambao majina yao hayakufahamika walijeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili.
Septemba 17, mwaka jana, ndani ya uwanja wa Sahara, Pinda alizomewa na wananchi wakati akihitimisha ziara yake jijini Mwanza, kutokana  na kero nyingi zinazowakabili wakazi wa jiji hilo, huku kiongozi huyo akiwataka waachane na ushabiki wa kisiasa.
Awali, akihutubia mkutano huo, Mangula alisema pamoja na kwamba wapinzani wamekuwa wakibeza mafanikio ya ya CCM lakini ukweli utabaki palepale kwamba katika kipindi cha miaka 50 ya utawala huo nchi imepiga hatua za maendeleo.
Mangula alitoa mfano kuwa wakati wa miaka ya nyuma kulikuwa na ghorofa moja la hospitali ya Bugando na sasa yapo ‘mabugando’ mengi.
Mbali na kuelezea mafanikio hayo pia aliwataka wanachama wa CCM kutumia vikao katika mashina kuzungumza na wanachama kubainisha matatizo yanayowakabili badala ya kuzungumza nje ya vikao, jambo ambalo limekuwa likikigawa chama.
Hata hivyo, Mangula ambaye alikuwa akisubiriwa kwa hamu katika mkutano huo, tofauti na matarajio ya wengi hakuzungumza zaidi ya dakika tano.
Wakati akiondoka baadhi ya wananchi hao walisikika walilalamika kuwa walitarajia kusikia mengi lakini hakuna walichosikia.
Kutokana na hali hiyo wananchi hao waliamua kukaa kando ya barabara ya Posta, nje ya uwanja huo na kuanza kuwazomea viongozi waliokuwa wakipita.

Mtwara : Serikali inavunja nchi kwa kutosikiliza Wananchi

Mtwara : Serikali inavunja nchi kwa kutosikiliza Wananchi
Kwa wiki ya tatu mfululizo kumekuwa na malumbano kuhusiana na suala la ujenzi wa Bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam. Kumekuwa na madai yenye nguvu ya hoja kutoka kwa wananchi wa Mtwara dhidi ya porojo kutoka kwa viongozi wenye dhamana ya kujibu madai haya ya watu wa Mtwara. Watu wa Mtwara kwa umoja wao na kwa kuungwa mkono na viongozi wa dini zote wamekuwa wakitaka Serikali ifikirie upya suala la mradi wa ujenzi wa Bomba la gesi na badala yake kujenga mitambo ya kufua umeme mkoani Mtwara na kusafirisha umeme huo kwenda maeneo mengine ya nchi. Kwenye moja ya maandishi yangu (Serikali iwasikilize watu wa Mtwara) nimeshauri kuwa Taifa liwe na gridi nyingine ya Taifa ambayo itatokana na Gesi tu na ianzie Mtwara.
Ikumbukwe kwamba katiba ya nchi, ibara ya 9 katika mabano J inataka mamlaka ya dola na vyombo vyake vyote kuhakikisha ya kwamba shughuli zote za kiuchumi zinaendeshwa kwa namna ya kwamba pasiwe mrundikano wa utajiri au shughuli za uzalishaji kwa watu wa chache. Katiba inaendela kwa kuelekeza kwamba uchumi wa nchi upangwe katika uwiano sawia (9, d). Watu wa Mtwara wanatekeleza matakwa haya ya katiba kwa kukataa mrundikano wa shughuli za kiuchumi wa nchi na utajiri wa nchi kua kwenye mikoa michache na hasa mkoa wa Dar-Es-Saalam.
Serikali imekuwa ikitoa majibu ya porojo na kuwatusi watu wa Mtwara na kama ilivyozoeleka Rais Jakaya Kikwete na Mawaziri wake wamekuwa wakisema suala la Mtwara linatumika na wanasiasa kujitafutia umaarufu. Inasikitisha sana kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwaambia mabalozi wa nchi za kigeni waliopo hapa nchini kuwa yanayoendelea mkoani Mtwara yanachochewa na Wanasiasa tuliosimama na wananchi wanaodai haki ya kufaidi utajiri wa nchi yetu. Rais Kikwete na Mawaziri wake wameshindwa kabisa kuonyesha uongozi katika suala hili na hatimaye kuhatarisha umoja wa kitaifa.
Kwa udhaifu wa serikali na tabia ya kutafuta mchawi badala ya kutatua tatizo la msingi, wananchi wameendelea kukutana na hata wengine sasa kuanza kusambaza ujumbe wa kukata kipande cha nchi na kuanzisha Jamhuri ya Kusini. Nimeona kwenye mabango ya mkutano wa hadhara uliofanyika 19/1/2013 wananchi wakibeba mabango yanayoaishiria kuchoka kuwa sehemu ya Tanzania na kuanzisha Jamhuri ya Makonde kuanzia jiwe la Mzungu wilayani Kilwa mpaka mto Ruvuma. Haya yanatoka na kiburi cha Serikali kujishusha na kuwasikiliza wananchi wanao dai haki yao ya kikatiba.
Ni Serikali iliyokosa uhalali wa kutawala inayoweza kudharau hisia hizi za wananchi. Serikali ielewe kwamba kamwe haitaweza kulinda kila nchi ya bomba hili iwapo italijenga kwa nguvu. Badala ya kuzungumza na vyombo vya habari Serikali ifanye mazungumzo na wananchi wa Mtwara na kukubaliana na matakwa yao. Kitendo cha Serikali kung’ang’ania msimamo wake dhidi ya watu wa mtwara ni kitendo kinacho weza kuipasua nchi na hivyo kwenda kinyume na masharti ya katiba ibara ya 28 ambayo inasema: “kila raia ana wajibu wa kulinda uhuru wa nchi, uhuru mamlaka na umoja wa taifa.”ibara ya 28, 1.
Inawezekana Serikali inaogopa kuvunja makubaliano na Wachina ya mkopo wa dola za kimarekani 1.2 bilioni ambao imeuingia bila hata kushirikisha Bunge. Inawezekana Serikali na hasa watendaji wa Serikali waliojadili mkopo huu wameshapata chao na hivyo kuogopa kusikiliza madai halali ya wananchi. Lakini yote hayo hayawezi kuwa zaidi ya Umoja wa nchi yetu. Hatuwezi kukubali nchi yetu ipasuke vipande vipande kwa sababu tu ya kulinda mkataba wa bilioni 1.2 tuliokopa China, ambayo serikali inang’ang’ania.
Tunafahamu kwamba ubalozi wa China umeandika barua serikalini kuwaondoa raia wa China waliopo Mtwara kwa hofu ya maisha yao. Serikali inaficha ukweli huu kama ilivyoficha ukweli kwamba Naibu Waziri wa Nishati na Madini bwana George Simbachawene alifukuzwa na wananchi wa Mtwara alipokwenda hivi majuzi. Serikali itaficha ukweli mpaka lini? Lazima tupate majawabu.
Kwanza Serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wa Bomba hili. Kamati ya Bunge ya POAC ilipokuwa inapitia mahesabu ya TPDC iliomba mkataba na kwa mshangao mkubwa wabunge wakaambiwa Mkataba haupo TPDC bali upo Wizarani. Kwa nini Mkataba huu wa matrilioni ya Fedha unafichwa? Mkataba huu ulisainiwa pamoja mikataba mingine 2, mmoja wa kujenga nyumba za wanajeshi wa thamani ya dola za kimarekani 400 milioni na mwingine wa mawasiliano jeshini wa dola za kimarekani 110 milioni, na mikataba yote mitatu imesainiwa kimya kimya bila kushirikisha wananchi kupitia Bunge. Lazima mikataba yote hii iwekwe wazi.
Pili, Mkataba huu uchunguzwe kama unalingana na thamani ya fedha maana kwa utafiti wa awali inaonyesha kuwa bei ya ujenzi wa bomba imepandishwa maradufu. Wastan wa kujenga bomba la gesi duniani ni dola za kimarekani 1.2 milioni kwa maili moja. Mradi huu wa Tanzania utagharimu dola za kimarekani 2.2 milioni kwa kilomita moja (maili 1 ni sawa na kilomita 1.6).
Tatu, Serikali ibadilishe Mkataba huu kuwa wa mkopo wa kujenga Mitambo ya kufua umeme Mtwara na ujenzi wa Msongo wa Umeme kama gridi ya pili ya Taifa. Kwa sasa Tanzania ina gridi moja ambayo inabebwa na bwawa la Mtera linalo tegemea mto Ruaha ambao hivi sasa unakauka miezi 5 katika miezi 12 ya mwaka. Ni dhahiri kwamba kwa usalama wa Taifa na hata kwa gharama Nchi itafaidika zaidi kwa kujenga gridi nyingine kutokea Mtwara badala ya kusafirisha gesi kuja Dar-Es-Salaam.
Serikali haitashinda vita hii kwa kuzusha kwamba ama wanasiasa wanaopinga wanatumika na makampuni mengine au kwa mataifa ya magharibi kutaka kuvuruga nchi. Serikali ijitazame yenyewe. Bila kufanya hayo tunayo pendekeza hapo juu, wananchi wataendelea kupigania hako yao. Hii ni vita ya uwajibikaji. Wananchi wanataka kufaidika na rasilimali za nchi yao. Kwa vyovyote vile upande wa wananchi utashinda. Vita ya uwajibikaji kwenye rasilimali za nchi sio ya vyama vya siasa, ni vita ya wananchi. Chama cha siasa kitakachokwenda kinyume na matakwa ya wananchi, kinajichimbia kaburi.
chanzo-

Zitto na Demokrasia

Rais Obama awatukuza Lincoln, Luther King

RAIS Barack Obama wa Marekani ameapishwa rasmi kushika muhula wa pili wa urais, katika sherehe maalumu iliyofanyika kwenye Ikulu ya nchi hiyo jana.
 
Obama ambaye ni Rais wa 44 wa Marekani, aliingia madarakani katika uchaguzi wa kihistoria mwaka 2008 uliomfanya kuwa Rais wa kwanza mwenye asili ya Afrika katika taifa hilo kubwa duniani.
Sherehe za kuapishwa kwake Ikulu jana zilikuwa za faragha na zilihudhuriwa na watu wachache maalumu, leo ataapishwa katika sherehe za jumla zitakazowajumuisha watu wote kwenye Uwanja wa National Mall.
Katika kiapo chake, Obama atatumia Biblia mbili, moja iliyokuwa ikitumiwa na Martin Luther King na nyingine ilikuwa ikitumiwa na aliyekuwa Rais wa 16 wa Marekani, Abraham Lincoln.
Lincoln aliongoza taifa hilo kuanzia Machi 1861 hadi alipouawa Aprili 1865.
Akiwa Ikulu jana, alitumia Biblia iliyowahi kutumiwa na Lincoln, katika sherehe za leo  atatumia Biblia ya Martin Luther King.
Lincoln, ndiye aliyeliongoza taifa hilo kipindi kigumu cha kusimamia umoja na kufuta biashara ya utumwa.
Martin Luther King ambaye alikuwa mchungaji na mwanaharakati wa haki za watu wenye asili ya Afrika nchini Marekani, aliuawa Aprili 4, 1968, muda mfupi baada ya kutoa hotuba yenye nguvu ya I have a Dream (Nimeota ndoto).
Hotuba hiyo ikuwa ikieleza ndoto yake kwamba muda siyo mrefu watu wenye asili ya Afrika watapata nguvu na kupata haki yao kama raia wa Marekani.
Viongozi hao wawili wana historia ya pekee, Lincoln ndiye aliyetumia muda wake mwingi akiwa Ikulu ya Marekani kuhakikisha watu wenye asili ya Afrika ambao walikuwa watumwa wananasuliwa utumwani.
Luther alikuwa mwanaharakati aliyechochea mabadiliko kwa kushinikiza Serikali kuwapa haki zao za msingi.
Obama aliapishwa rasmi jana ikiwa ni siku ya kwanza kati ya siku mbili zilizopangwa, leo ataapishwa mara ya pili katika viwanja maalumu vya Nationa Mall mjini Washington, ambako maelfu ya watu watapata fursa ya kushuhudia.
Hotuba ya kuapishwa kwake  itakayotolewa leo inatarajiwa kuweka historia mpya, pia kuhitimisha matukio ya siku mbili hizi za kuapishwa, ataweka wazi mtazamo wake wa kipindi cha miaka minne ijayo.
Mkusanyiko utakaoshuhudia kuapishwa kwake na kusikiliza hotuba yake moja kwa moja katika uwanja huo unakadiriwa kupungua kutoka ule wa watu 1.8 milioni mwaka 2009 na kufikia kati ya 600,000 na 800,000, huku mamilioni wakishuhudia kupitia televisheni.

Moto wa gesi wazidi kushika kasi Mtwara,Zitto ampinga Kikwete

SAKATA la kupinga ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam limechukua sura mpya baada ya wananchi zaidi ya 30,000 kusaini katika fomu maalumu kupinga gesi hiyo kusafirishwa.
Wakati wananchi hao wakikamilisha shughuli hiyo na kukabidhi fomu hizo kwa wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), umoja wa vyama tisa vya siasa mkoani umemwomba Rais Jakaya Kikwete kusitisha mradi huo ili kuepusha uvunjifu wa amani unaoweza kujitokeza.
Pia, umoja huo umewataka wabunge wote wa Mkoa wa Mtwara kutangaza msimamo wa kila mmoja juu ya gesi kwenda Dar es Salaam au kukubaliana na uamuzi wa Serikali ili wajue nani msaliti kwao.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika Uwanja wa Sabasaba mjini hapa, viongozi hao kwa nyakati tofauti wamemtaka Rais Kikwete kutokutumia ‘jazba na mabavu’ katika kulipatia suluhu jambo hilo, badala yake busara zitawale kwa kusitisha mradi huo.
“Sisi Watanzania hatujazoea vita, bali tumezoea kupata hasara… katika hili naomba Kikwete akubali kupata hasara kama tunavyokubali hasara nyingine…Sisi wananchi tupo radhi tuingie kwenye deni kubwa kama hilo, lakini gesi haiwezi kwenda Dar es Salaam,” alisema Uledi Abdallah Makamu, Mwenyekiti wa umoja huo na kuongeza:
“Hizo trilioni tatu kama anaona hawezi kuzilipa iwapo gesi itabakia Mtwara...Basi atafute njia nyingine za kulipa… Atambue kuwa hakuna fedha yenye thamani ya amani na utulivu wetu…akumbuke kuwa mafahali wawili hawakai zizi moja.”Naye Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Mtwara Mjini, Mustafa Nchia aliwataka wabunge kutoa misimamo yao ili wananchi wajue ni mbunge yupi anawaunga mkono na yupi msaliti kwao.
“Hadi sasa ni Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini), George Mkuchika, (Newala), Asnain Murji (Mtwara Mjini) na Clara Mwatuka (Viti Maalum CUF), wametoa misimamo yao, vipi ninyi wengine…Tunataka kusikia msimamo wa kila mmoja,” alisema Nchia huku akishangiliwa na mamia ya watu waliohudhuria mkutano huo.
Zitto ampinga Kikwete
Wakati Rais Kikwete akisisitiza kuwa mgogoro kuhusu gesi unachochewa na wanasiasa kwa lengo la kukwamisha juhudi za Serikali za kumaliza tatizo la mgawo wa umeme,  Mbunge wa Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amesema huo ni uzushi. Katika taarifa yake jana, Kabwe alisema Serikali haitashinda vita hii kwa kuzusha kwamba wanasiasa wanaopinga wanatumika na kampuni nyingine au kwa mataifa ya magharibi kutaka kuvuruga nchi.
“Serikali ijitazame yenyewe. Bila kufanya hayo tunayo pendekeza, wananchi wataendelea kupigania haki yao...Hii ni vita ya uwajibikaji. Wananchi wanataka kufaidika na rasilimali za nchi yao.
Kwa mujibu wa Zitto, Serikali imekuwa ikitoa majibu ya porojo na kuwatusi watu wa Mtwara, na kama ilivyozoeleka Rais Kikwete na mawaziri wake wamekuwa wakisema suala la Mtwara linatumika na wanasiasa kujitafutia umaarufu.
“Inasikitisha sana kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwaambia mabalozi wa nchi za kigeni waliopo hapa nchini kuwa yanayoendelea mkoani Mtwara yanachochewa na wanasiasa tuliosimama na wananchi wanaodai kufaidi utajiri wa nchi yetu. Rais Kikwete na mawaziri wake wameshindwa kabisa kuonyesha uongozi katika suala hili na hatimaye kuhatarisha umoja wa kitaifa.”
Aliongeza kuwa anafahamu kwamba Ubalozi wa China umeandika barua serikalini kuwaondoa raia wa China waliopo Mtwara kwa hofu ya maisha yao. Serikali inaficha ukweli huu kama ilivyoficha ukweli kwamba Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene alifukuzwa na wananchi alipokwenda huko hivi majuzi. Serikali itaficha ukweli mpaka lini?” alihoji.
Waziri na wanasiasa
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene amesisitiza kuwa mgogoro na vurugu zinazoendelea mkoani Mtwara kuhusu gesi unachangiwa na wanasiasa.
Alisema kuwa watu hao aliodai wanakosa uzalendo na utaifa, wanalenga kuhakikisha tatizo la umeme linaendelea kuwepo nchini hadi uchaguzi mkuu ujao ili wapate ajenda ya kisiasa jukwaani.

Friday, January 18, 2013

Obama Inauguration Limo to Carry ‘Taxation Without Representation’ License Plate

It’s poised to be a colossal event: over 100 parade horses, miles of electric cable, at least 50,000 volunteers, hundreds of thousands of free tickets — and at least one limo bearing the slogan “taxation without representation.”


That limo will carry President Barack Obama from the Capitol along a 1.5-mile route on Pennsylvania Avenue as part of inauguration ceremonies next Monday, Jan. 21. On its license plates: the phrase used by frustrated colonists in the years leading up to the American Revolution.

No, it’s not some seditious prank planned by Obama’s political foes, it’s actually a symbolic decision endorsed by the President himself. In fact the phrase will soon appear on all of the presidential vehicles for the remainder of Obama’s four-year term, says the White House.
Mike Theiler / Reuters“President Obama has lived in the District now for four years, and has seen first-hand how patently unfair it is for working families in D.C. to work hard, raise children and pay taxes, without having a vote in Congress,” said the White House in a statement. ”Attaching these plates to the presidential vehicles demonstrates the president’s commitment to the principle of full representation for the people of the District of Columbia and his willingness to fight for voting rights, home rule and budget autonomy for the District.”
The District of Columbia was founded when George Washington signed the Resident Act on July 16, 1790; in 1801, D.C. was placed under the exclusive jurisdiction of Congress. Since the capital district isn’t formally beholden to a U.S. state, it lacks a voting member in Congress. And yet D.C. residents still must pay Federal taxes: a sore subject for many of the city’s residents, who number over 630,000 — more than the entire population of Vermont or Wyoming.
Something you might not recall: President Bill Clinton put the phrase on the presidential limo during his last days in office, but President George W. Bush chose to remove it in 2000.
(MORE: The Manti Te’o Hoax: 6 Questions About the ‘Fake’ Girlfriend That Has the Sports World Reeling)

STATE OF THE NATION ADDRESS BY H.E PAUL KAGAME,PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF RWANDA

STATE OF THE NATION ADDRESS BY H.E PAUL KAGAME,PRESIDENT OF THE REPUBLIC OF RWANDA
Distinguished leaders of our country’s high institutions
Members of the Diplomatic Corps and representatives of International Organisations
Distinguished Guests
Fellow Rwandans
Good afternoon to you all.
I am pleased to be here at Parliament for two important reasons: the first is to share with all Rwandans, friends of Rwanda and our partners, where Rwanda stands today. The second is to wish you all a Happy New Year, as is tradition during this period.
I want to begin by thanking every Rwandan who participated in the population census that took place this year. This survey enabled us to determine the number of Rwandans in the country as well as their socio-economic status.
The census will ensure that government planning and the services are more in line with Rwanda’s population. Importantly, the results showed that population growth has decreased from 2.9% in 2002 to 2.6%. This is a clear indication that efforts to slow down population growth have been effective and, if we continue along this path, will ensure that our economy and the wellbeing of Rwandans are not negatively affected.
There is no denying the progress and development our nation continues to make. Various data show that Rwanda’s economy continues to grow.
As we end the year, our economy is predicted to grow by 7.7% mainly as a result of good yields in the service and industry sectors, which increased by 13.5% and 6% respectively in the first three quarters of the year. This is encouraging.
Our economy would have grown even faster had there not been two external mitigating factors. The first is the global economic downturn which had repurcussions on Rwanda’s economy. The second is the consequence of conflict in a neighbouring country that has been blamed on Rwanda when this is not true. We are not the cause of or contributing factor to this conflict, even those who claim this know it. Those who accuse us are actually the cause of the conflict.
Click here for the Kinyarwanda version
As you know there is a report based on falsehoods which some of our longtime partners have used as the basis to suspend development aid, in a manner that violates agreed principles of international development partnerships.
I would say that these actions did not come as a surprise because we have known all along, from experiences we have had, that external support does not depend on us and can be stopped at anytime. They don’t even need to have a reason, let alone one based on the truth. Our goal must remain to work hard in order to reduce our dependence on aid. What is important is not get discouraged as we move forward towards this objective. Suspension of development assistance may slow down the progress we are making but it should not stop us from doing our best to improve our wellbeing and to lift our citizens out of poverty as we have already done for one million Rwandans in the last five years.
There is no doubt that if we continue to work with full commitment, and with the right mindset, to take our country forward and grow our economy, the aid suspension may prove to be a valuable lesson for Rwanda.
The foundation has been laid. In addition to the hard work that has characterised Rwandans this year and in the years before, we have peace, security and good governance in our country. There is much more we have managed to achieve that I will talk about.
The number of banks and their branches continue to grow throughout the country. Cooperatives and SACCOs have also increased in number and proven to be of great value for their members and for the country’s economy in general. It is not just the numbers, the quality of services also continue to improve.
Rwandans accessing financial services increased from 48% in 2008 to 72% this year. In total, banks and other financial institutions have given a total of 440 billion Rwandan francs worth of loans, which marks a major increase from 339 billion of last year. If we maintain and further improve our savings culture and make use of financial services, there is no doubt our economy will grow even more.
In 2012, Rwandan exports grew at 74% while their value increased by 22%. Our imports grew by 29% while their value increased by close to 14%. Although exports grew, there is still a big deficit, judging by how much we spend on imports. We must therefore increase the size and value of our exports in order to maximize benefits.
Investment in Rwanda, both internal and foreign, has increased this year. In the first three quarters of 2012, investments reached a total of $570 million, compared to $483 million last year. It is encouraging to note that investments are being made in projects that have a direct and positive impact on our economy. These include investments in electricity distribution, international hotels, and Rwandair which connects Rwanda to the rest of the world.
The incentives we have put in place to motivate businesses have contributed in a major way to this growth in investment. This partly explains why Rwanda was ranked first in “Doing Business” in the East African Community and third in Africa.
This year we continued to construct new roads including Kigali-Musanze, Kigali-Gatuna, Rusizi-Rubavu, Ntendezi-Huye, and also rehabilitated others. Big and small towns and trading centers around the country continued to be transformed and renewed. Water and electricity are more widely distributed in the country, although additional efforts are needed to ensure that many more Rwandans are able to access these utilities.
The mining sector continues to play a big role in growing our economy. This year, revenue from mineral resources totaled close to $128 million and is expected to rise which will result in more benefits for Rwandans, including additional employment.
The tourism industry also continued to advance and is now the biggest foreign currency earner. Rwanda’s security and stability attracts visitors keen to see what is being done here and enjoy the country’s various attractions.
By October this year, tourism generated $232 million compared to $204 million last year. It is critical that we strive to provide excellent service and customer care so that visitors to Rwanda leave as good ambassadors who will return and also encourage others to visit.
We should also be encouraged by the progress we have made in advancing Information and Communication Technology. It is now easier than ever to access numerous services, including news and information, send and receive money, get market prices of food stuff both within Rwanda and beyond.
We encourage all Rwandans, especially the youth, to take advantage of available technology as this will add value to our work and lead to increased revenues.
In the social sector, more Rwandans today are enrolled in formal education than in previous years, and more citizens are able to access appropriate health care.
This year, the number of schools at every level, as well as the number of students has increased. In primary school, the number of students increased by 2.3% from 2,341,146 last year to 2,394,674. In secondary schools, the number of students increased by almost 10%, up from 486,437 last year to 534,712. The number of students in universities increased by 4% from 73,674 in 2011 to 76,629 this year.
We also launched the 12-Year Basic Education to improve on the 9-Year Basic Education program we already had in place.
Furthermore, we are pleased with the increased number of technical vocational schools established, as well as the number of students, which has risen from 67,919 to 74,320. These students are acquiring skills that will enable them to work in industries, agriculture and also create their own jobs. We must continue to invest in and build the capacity of these schools so that Rwanda can benefit even more from the skills and knowledge of well-trained and greater numbers of graduates.
We have a duty to encourage Rwandan youth to acquire vocational training because Rwanda’s economy will continue to depend on practical knowledge. But in order to motivate young people, leaders here today as well as parents everywhere must understand the value of vocational training.
We also note the number of international universities that have set up branches in Rwanda, such as Carnegie-Mellon University from the United States. This contributes to high quality education in general and allows Rwandans to access specialised knowledge previously only available abroad.
In the health sector, in 2012 we concentrated on increasing the number of hospitals and skilled medical professionals. You may know about a new program to bring doctors from abroad particularly from renowned American universities and hospitals to build capacity of Rwandan doctors and hospitals.
We reformed the community health insurance scheme so that every Rwandan is now able to access medical care anywhere in the country.
Diseases like malaria that had afflicted Rwandans for a long time, as well as child and maternal mortality continue to reduce significantly. Statistics show that deaths of children under the age of five has fallen from 152 of every 1000 in 2005 to 54. Maternal mortality has dropped from 750 of every 100,000 in 2005 to 134, while the number of deaths caused by malaria reduced greatly, from 54% in 2005 to 6%.
We will continue efforts to fight malnutrition that is often the result of bad mentality and illiteracy. It is not right that our country has attained self sufficiency in food and yet some parts of our country continue to experience malnutrition. We will continue to give our doctors advanced and specialised training as well as continue to manage and fight HIV/AIDS.
In the justice sector, laws continue to be reviewed where it is deemed necessary, based on international best practices. It is in recognition of this development that some international courts are sending back suspects living in their countries who may have committed crimes in Rwanda.
We have reduced the length of sentences and are working to transform prisons into correctional institutions. This initiative has resulted in a reduction in the number of detention facilities and detainees.
The Abunzi system of justice has taken root and citizens play a major role in this program that is based on Rwandan historical tradition. This system has been key in reducing cases that would have otherwise gone to courts of law. We have also established centres for access to justice in every District to provide legal advice to Rwandans.
Gacaca Courts that concluded this year did an outstanding job of delivering reconciliatory justice. These courts provided solutions for huge challenges faced by Rwandans as a result of the genocide. This also is evidence that Rwandans have the capacity to find solutions to challenges that we face, even in the future.
I would like to take this opportunity to thank Rwandans from all walks of life, both in the country and abroad as well as friends of Rwanda for contributing to the Agaciro Development Fund, which we created.
We will continue to work closely with other African nations and beyond in pursuit of long-term stability for our region, as well as work for development and improved wellbeing of all Africans.
We will also continue to offer our contribution to peace and stability in Africa and elsewhere in the world when needed and within our means.
In conclusion, I would like to reiterate that Rwanda is on the right path; what we need to do now is stay focused on our vision, implement the plans we have made, and never get discouraged in the struggle to take our country and our people forward even in the face of adversity – and I can assure you that we will have challenges. But we have to commit to facing these challenges head on and overcoming them. These obstacles should not discourage but energise us and strengthen our determination.
Let us show our resolve and commitment in this New Year, so that it may be even better than the year that just ended. May our economy grow and may we lift many more Rwandans out of poverty.
Starting with our own plentiful capacities in addition to our energy, let us continue to work for good results. On this, all leaders need to understand that they must be fully involved and committed. I wish to not only remind but also request this again of leaders.As I said earlier, this is an opportunity to wish all Rwandans and friends of Rwanda a Happy New Year.
May it be a year of abundance and productivity for you all and your families, and may it also be a year of continued joint work to take our country forward to where we deserve to be.
Thank you, have a good evening and God bless you.

Manumba hali tete,yasemekana figo zake hazifanyi kazi

HALI ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Robert Manumba bado ni tete na jana Rais Jakaya Kikwete alikwenda tena ikiwa ni mara ya pili mfululizo katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam alikolazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), kumjulia hali.
 

Mbali na Rais Kikwete, viongozi wengine waliofika hospitalini hapo kumjulia hali DCI Manumba ni Mke wa Rais, Salma, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP, Said Mwema na Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni. Pia walikuwapo ndugu, jamaa na marafiki ambao walikusanyika hospitalini hapo takriban siku nzima jana wakifuatilia afya yake.

Rais Kikwete alifika hospitalini hapo jana saa 11:15 na alitumia takriban dakika 10 tu kwani alitoka saa 11:26 huku akionekana mnyonge na alielekea kwenye gari lake na kuagana na IGP Mwema na Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Jaffer Dharsee kisha kuondoka.

Juzi, Rais Kikwete alikwenda hospitalini hapo mara baada ya kumsindikiza Uwanja wa Ndege mgeni wake Rais wa Benin,Thomas Boni Yayi aliyekuwa nchini kwa ziara ya siku moja.
Jana, Mke wa Rais alikuwa wa kwanza kufika hopitalini hapo saa 10:20 na aliondoka saa 10:45 muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kufika.

Habari zilizopatikana jana zilieleza kwamba kutokana na afya yake kuwa mbaya, wageni wengi wakiwamo viongozi waandamizi, walizuiwa kuingia kumwona.
Uongozi wa Aga Khan watoa tamko
Jana mchana, uongozi Aga Khan ulitoa taarifa rasmi kuzungumzia afya ya kiongozi huyo wa Polisi huku ukieleza kuwa kimsingi siyo nzuri na bado anahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari.

“Uongozi wa Hospitali ya Aga Khan ungependa kuujulisha umma kwamba Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, DCI Robert Manumba bado yupo hospitalini Aga Khan ambako anaendelea kupatiwa matibabu. Hali yake bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Juzi, Dk Dharsee alisema Manumba alifikishwa katika hospitali hiyo akisumbuliwa na malaria huku hali yake ikiwa mbaya na hajitambui.

Msemaji wa familia atoa mafumbo
Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo jana, msemaji wa familia ya DCI Manumba, James Kilaba alisema: “Maisha ndivyo yalivyo, huwezi kuzua ugonjwa na huwezi kubadili uhalisia wa mambo. Sisi kama familia, tunaamini Mungu yuko na ndugu yetu na ndiye atatenda yake na naomba Watanzania wamuombee.”

Hata hivyo, alikataa kuzungumzia ugonjwa wake zaidi ya kusema kuwa alipelekwa Jumanne iliyopita hospitalini hapo kwa ajili ya vipimo zaidi.

Mdhamini wa Bakwata amruka Ponda kortini

MWENYEKITI wa Baraza la Wadhamini la Bakwata, Masoud Ikome (72), amemkana Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Shekhe Ponda Issa Ponda, mshirika wake, Shekhe Mukadam Abdallah Swalehe (45) na wafuasi wao kuwa hawatambui hata kwa sura.

Shekhe Ponda, ambaye ni mwanaharakati maafuru wa kutetea kile anachokiita haki na mali za Waislamu anakabiliwa na mashtaka ya wizi wa mali yenye thamani ya Sh59.6 milioni.

Ikome ambaye ni shahidi wa nne wa upande wa mashtaka, jana alikana kumfahamu Shekhe Ponda na wafuasi wake mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Victoria Nongwa.

Hatua hiyo ilikuja baada ya kuambiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumain Kweka awaangalie washtakiwa hao kwa jumla yao na aieleze mahakama kama anawatambua.
“Hata mmoja simtambui na hakuna hata mmoja aliyewahi kuwa mjumbe wa Baraza la Maulamaa,” alidai Ikome.

Ikome alidai kuwa amekuwa akifanya kazi Bakwata tangu Mei 15 mwaka 2010 na kwamba majukumu yake ni kudhibiti mali za Bakwata zinazohamishika na zile zisizohamishika.
Alizitaja mali hizo kuwa ni pamoja na nyumba, viwanja, magari na vifaa vya maofisini.

Alidai kuwa mamlaka ya utendaji kazi huo anayapata kutoka, katika Baraza la Maulamaa na kwamba anakifahamu kiwanja namba 311/32 kwa sababu aliwahi kuitisha kikao kupitia Baraza la Wadhamini na kukijadili kuhusu kubadilishwa na kiwanja kilichokuwa kinamilikiwa na Kampuni ya Agritanza Ltd huko Kisarawe mkoani Pwani.
“Mabadilishano hayo yalikuwa yana lengo la kupata kiwanja kikubwa ambacho kingeweza kujengwa Chuo Kikuu cha Kiislamu. Tulipata ekari 40 zilizokwishapimwa huko Kisarawe ambapo tulibadilishana na ekari nne za Malkazi Chang’ombe.” alisema shahidi huyo.
Alisisitiza kuwa nguvu ya kufanya mabadilishano ya kiwanja cha ekari nne na ekari 40 walizipata kutoka katika Baraza la Maulamaa ambalo lilikaa na kuamua kibadilishwe na kwamba hayo yalifanyika Januari 24.
Shahidi huyo wa upande wa mashtaka alidai kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maulamaa ndiyo katibu wa Baraza la wadhamini Bakwata, Suleiman Said, hivyo habari za utekelezaji wa mabadilishano hayo walikuwa wakizipata kutoka kwake.

Alibainisha kuwa kwa sasa eneo la Chang’ombe Malkazi, linamilikiwa kihalali na Kampuni ya Agritanza Ltd baada ya kukamilishwa kwa taratibu zote za mabadilishano hayo.
Kwa upande wake shahidi wa tano wa upande wa mashtaka, Hafidhi Othman (42), alidai kuwa aliwahi kukutana na Shekhe Ponda ambaye ana mgogoro na Bakwata wa muda mrefu.
Alidai kuwa katika mazungumzo yake na Ponda alimweleza kuwa walichokifanya siyo sahihi kwa sababu wao kama Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, hawakushirikishwa katika mabadilishano hayo.
Shahidi huyo, anadaiwa kuwa baada ya kuambiwa hivyo na Shekhe Ponda, alimweleza kuwa kama wanaona Bakwata wamenufaika na ekari 40 na wao watafute ekari nyingine 40 ili aweze kuwanunulia.
Alidai kuwa Shekhe Ponda alikwenda na mzee mmoja ambaye alisema ana eneo la ekari 30 huko Mkuranga ambapo Ponda alimwambia kuwa “Tuache tukaangalie tutakujibu mwishoni mwa wiki na lakini usijenge ukuta.”
Hafidhi alidai kuwa ilipofika Alhamisi alipata habari kuwa Ponda na wafuasi wake watakwenda kuvamia, baada ya kupata taarifa hiyo.
Alidai kuwa ilipofika siku ya Ijumaa baada ya swala nilipita katika eneo hilo la Malkazi Chang’ombe, kweli nikawakuta watu wengi wakiwa wamening’iniza mbao na mabati katika eneo tunalolimiki bila ya idhini yetu.
Aliongeza kudai kuwa alikwenda katika kituo cha Polisi cha Kati kutoa taarifa juu ya tukio hilo.
Alidai kuwa katika eneo hilo kulikuwepo na mchanga lori tatu, kokoto tani 36, matofali 2,000, nondo na mifuko 50 ya simenti na kwamba baadhi ya vitu hivyo viliibwa.
Pia shahidi huyo alibainisha kuwa fedha zilizotumika kununua ekari 40 za Kisarawe zilitolewa na Kampuni mama ya Agritanza Ltd, Kampuni ya Ali Hillary Ltd.
Hakimu Nongwa aliiahirisha kesi hiyo hadi Januari 31, mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa.

Kampuni ya Tigo yagoma kupunguza gharama za simu

WAKATI Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwasilisha rai ya kupunguza gharama za mwingiliano wa simu , Kampuni ya Tigo imekataa kufanya hivyo kwa madai kuwa itahatarisha uwekezaji wake kwa punguzo la asilimia 69.
 

Msimamo huo wa Tigo, umekuja baada ya TCRA kukutana na wadau wa mawasiliano jana jijini Dar es salaam, ili kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya kupunguza gharama ya mtandao mmoja kwenda mwingine. Hatua hiyo inalenga katika kuwasaidia wananchi kumudu gharama za mawasiliano ya simu.

Naibu Mkurugenzi wa Utekelezaji wa Kanda wa TCRA, Victor Nkya, alisema punguzo hilo ni la kutoka asilimia 35 hadi asilimia 69 na kwamba litaanza kutumika Machi mosi mwaka huu na kukoma Desemba 31 mwaka 2017 .

Nkya alisema punguzo la gharama ya kupiga mtandao mmoja kwenda mwingine kwa mwaka 2013 litakuwa asilimia 34.92, mwaka 2014 asilimia 32.40, mwaka 2015 asilimia 30.18, mwaka 2016 asilimia 28.57 na mwaka 2017 ni asilimia 26.96.

“Lengo letu ni kupunguza gharama za mwingiliano wa simu, mfano mwananchi ambaye yupo Tigo anapiga kwenye mtandao wa Vodacom hizi gharama atazilipa mwenye kampuni ya Vodacom kuilipa kampuni ya Tigo badala ya kulipa mwananchi kama ilivyo sasa,” alisema.
Alisema maoni yanayotolewa na wadau yatachukuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mawasiliano na kuyafanyia kazi.

Ofisa Mdhibiti wa Kampuni ya Tigo, Levocatus Nkata, alisema punguzo hilo ni kubwa hivyo wawekezaji watashindwa kuendesha kampuni zao.
Alisema Kampuni ya Tigo inatoa huduma zake hadi vijijini na kwamba hatua hiyo itaifanya ishindwe kupeleka na kutoa huduma kwenye maeneo hayo.

Nkata alisema itachukua muda mrefu kurudisha gharama walizotumia kuendeshea kampuni yao kutokana bei ya kuendesha mitambo.

“Sisi hatukubaliani na hayo mapendekezo yaliyoletwa na TCRA, punguzo hilo kwa sisi wawekezaji ni kubwa sana, tunachoomba wasipunguze ibaki kama ilivyo na kwa mwaka 2017 tunaomba ipunguze kufikia asilimia 45 tu, “alisema Nkata.

Kampuni za Airtel, Vodacom , Benson na Dovetel zimekubali punguzo hilo lakini zimeiomba TCRA ipunguze asilimia chache.

Bavicha yasisitiza kumtimua Shonza

BARAZA la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), limesisitiza kuwa Juliana Shonza amevuliwa nafasi aliyokuwa akiishikilia ya umakamu mwenyekiti wa baraza hilo baada ya kukamilisha taratibu zote za kumuondoa.
 

Kauli hiyo imekuja kufuatia Shonza kunukuliwa kwenye vyombo vya habari akisema yeye bado ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo kwa maelezo kuwa hakuwa amepewa barua yoyote ya kumsimamisha.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa BAVICHA, John Heche alisema Shonza alitumiwa barua ya kumvua nafasi hiyo kwa njia ya posta januari 6, hata hivyo amekuwa akikataa kuipokea.

“Lakini sio hivyo tu siku aliyokuwa anazungumza na vyombo vya habari, tulimtumia barua akakataa kuipokea, taratibu zinatuambia kumpatia barua lakini kama ameikataa bado haiwezi kubadili maamuzi ya chama,”alisema Heche.
Baada ya kumtafuta Shonza ili kutoa ufafanuzi juu ya tarifa za kupokea kwa barua hiyo zilishindikana.

Siku mbili zilizopita Shonza alikunukuliwa kwenye vyombo vya habari akisema kikao cha kamati ya utendaji cha Bavicha kilichokutana na kupitisha umamuzi wa kumfukuza kilikuwa sio halali huku akiwatupia lawama Heche na Mwenyekiti wa Chama hicho Freemon Mbowe kwa madai ya kumdhalilisha.

Shonza alisema yeye bado ni Makamu Mwenyekiti wa Bavicha na mwanachama halali wa chama hicho. Aidha alisema anafanya mkakati wa kuwashtaki wale anaowalalamikia kwa kumuita msaliti ndani ya chama hicho.

Shonza alimtuhumu Heche kutengeneza mipango ya kutukuza ukanda waziwazi ndani ya chama hicho huku akiwataka kutoa ufafanuzi wa kikatiba juu ya shutuma zinazotolewa dhidi yake.