Thursday, December 6, 2012

Rufaa ya Mnyika kunguruma leo Dar

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika na aliyekuwa mpinzani wake kwenye kinyang’anyiro cha kuwania wadhifa huo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, Hawa Ng’humbi, kwa mara nyingine tena leo wanatarajiwa kupambana mahakamani.
 
Wapinzani hao wa kisiasa, wanatarajiwa kupambana kwa hoja za kisheria, wakati wa usikilizwaji wa rufaa ya Ng’humbi ya kupinga hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, iliyomthibitisha Mnyika kuwa mbunge halali wa Ubungo.
Mnyika, kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alitangazwa na Msimamizi wa uchaguzi katika jimbo la Ubungo, kuwa mbunge wa jimbo hilo, baada ya kupata kura 66,742 huku Ng’umbi akipata kura 50544.
Hata hivyo Ng’humbi kupitia Wakili wake, Issa Maige alifungua kesi Mahakama Kuu kupinga ushindi huo wa Mnyika, huku akiiomba mahakama ibatilishe matokeo na kuamuru uchaguzi huo urudiwe.
Katika hati ya madai ya kesi hiyo namba 107 ya mwaka 2010 na wakati wa ushahidi wake mahakamani, Ngh’umbi alidai kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu na kanuni za sheria wakati wa kampeni, ujumlishaji na utangazaji matokeo.
Hata hivyo Mahakama katika uamuzi wake, ilitupilia mbali madai ya Ng’humbi na badala yake ikamthibitisha Mnyika kuwa mbunge.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa Mei 24, 2012, Jaji Upendo Msuya alisema upande wa madai ulishindwa kuyathibitisha madai yake pasi na shaka, huku akidai kuwa ushahidi wa Ng’humbi ulikuwa ni maneno ya kusikia tu ambayo hakuyashuhudia.
Hata hivyo, Ng’humbi hakukubaliana na hukumu hiyo na kuamua kukata rufaa akiiomba mahakama ya rufani itengue hukumu hiyo ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam. Rufaa hiyo imepangwa kuanza kusikilizwa leo na Jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani; Salum Massati, Katherine Oriyo na Nathalia Kimaro.
Ng’humbi katika rufaa yake hiyo aliyoifungua Oktoba 25, 2012,
Kupitia kwa wakili wake, Maige, ameorodhesha hoja kumi za kupinga hukumu hiyo, akidokeza kile anachokiona kuwa ni udhaifu katika hukumu.
Pamoja na mambo mengine, Ng’humbi anadai kuwa Jaji Msuya alikosea katika kutafsiri sheria na kupima ushahidi wa pande zote.
Baadhi ya hoja zake katika rufaa hiyo, Ng’humbi anadai kuwa jaji alikosea kusema kuwa makosa yaliyobainika katika ujumlishaji na kuhesabu kura na kusababisha kuwapo kwa kura 14,854, zisizohesabiwa hayakuathiri matokeo ya uchaguzi.
Anadai kuwa alithibitsha makosa katika mchakato wa uchaguzi yaliyosababisha kuwapo kwa kura 14, 854 zisizohesabiwa, hivyo  jaji alikose kwa kutokuhamishia kwa mdaiwa, jukumu la kuelezea sababu za kuwapo kwa dosari hizo.
“Jaji alijipotosha kumshutumu mrufani kwa kutokubainisha kuwa makosa ya msingi yaliyobainika katika kujumlisha na kuhesabu kura yalikuwa ni ya nia mbaya,” inasisitiza hati hiyo ya rufaa na kuongeza:

No comments:

Post a Comment