Tuesday, November 13, 2012

Tigo yawakumbuka wateja waishio vijijini

ILI kuwaongezea wateja wake uwanja mpana wa kutumia mawasiliano ya simu, Kampuni ya simu za Mkononi ya Tigo, imezindua kifaa maalum cha kuchaji simu kinachotumia nishati ya jua.

Kifaa hicho kitawafanya wananchi hasa wanaoishi vijijini ambako  hakuna nishati ya umeme kuweza kuchaji simu zao, hivyo kuongeza idadi ya watumiaji wa mawasiliano ya simu nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana, Ofisa Masoko wa Kampuni hiyo, Jaqulini Nnunuma  alisema Tanzania ina idadi kubwa ya watu ambao wanatumia simu za mikononi na asilimia 50 ni wateja wa tigo, hivyo wameamua kuanzisha vifaa vya nishati ya jua vyenye uwezo wa kuchaji simu kwa lengo la kurahisisha huduma zao.

‘’Tanzania ina idadi kubwa ya watu ambao hawana njia ya moja kwa moja ya kupata umeme, hivyo leo tumeamua kuzindua rasmi kifaa maalum cha nishati ya jua kwa ajili ya kuchaji simu za mikononi’’alisema Nnunduma.

Pia aliongeza  kuwa pamoja na kuwapa wateja nishati rafiki na endelevu kwa matumizi ya kila siku, watakaonufaika na mradi huu ni wale  wanaoendesha maisha na biashara zao katika maeneo yasiyo na umeme .

‘’Kwa kuwapa wateja wetu nishati rafiki na endelevu  kwa matumizi ya kila siku watakaonufaika na mradi huu ni wale wale wanaoishi na kuendesha biashara zao katika maeneo yasiyo na umeme tu’’ aliongeza Nnunduma.

Naye Meneja Miradi , Yaya Ndoje alisema kuwa watakaonufaika na huduma hiyo endelevu  kwa ajili ya kutoa huduma hiyo ya kusambaza vifaa hivyo ni wale walio mawakala wa tigo tu, pamoja na wauzaji wa bidhaa za tigo kama simu na chaji pekee katika mikoa yote nchini Tanzania Bara na Visiwani.

Aidha aliongeza kuwa kwa kupitia vifaa vya nishati ya jua huduma hii bunifu itarahisisha na kufanya na  upatikanaji wa huduma ya tigo iwe rahisi pamoja na kuongeza kipato ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma kwa kipindi kwa wateja wetu.

No comments:

Post a Comment