Friday, November 23, 2012

Mark Huges afutwa kazi ni Kocha wa QPR

Mark Hughes
                                               Mark Hughes
Kocha wa QPR, ambayo kwa sasa iko mkiani kwenye msururu wa ligi kuu ya Premier ya England Mark Hughes amefutwa kazi.
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo, kocha huyo amefutwa kazi kutokana na matokeo mabaya tangu kuanza kwa msimu huu.
Baada ya mechi 12 kuchezwa QPR haijashinda hata mechi moja.
Taarifa hiyo imesema kuwa, bodi hiyo inajadili mipango ya kutangaza wasimamizi wapya wa klabu hiyo muda mfupi ujao.
Mark Bowen na Eddie Niedzwiecki watasimamia klabu hiyo wakati wa mechi ya ya kesho Jumamosi dhidi ya Manchester United katika uwanja wa Old Trafford.
''Bodi ya wakurugenzi ingependa kutoa shukrani kwa Mark, kutokana na juhudi zake wakati alikuwa kocha wa klabu hiyo kwa muda wa miezi kumi iliyopita'' taarifa hiyo iliongeza.
Wakurugenzi hao wamesema watangaza mipango mipya ya klabu hiyo muda mfupi ujao na aliyekuwa kocha wa Tottenham Harry Redknapp anatarajiwa na wengi kuteuliwa kuwa kocha mpya wa QPR.

No comments:

Post a Comment