Friday, November 16, 2012

Historia ya Boko Haram kwa ufupi sana

Mwanzilishi wa kundi hilo, Mohammed Yusuf, aliuawa na maafisa wa ulinzi mwaka wa 2009.

Kiongozi wa Boko Haram
Kiongozi wa Boko Haram
Kwa sasa kundi hilo linasemekana kuongozwa na Abubakar Shekau.
Msemaji wa jeshi Luteni Kanali Sagir Musa, ameiambia BBC kuwa Bwana Ibrahim, alikuwa mshirika wa karibu wa Bwana Shekau na amekuwa na sifa ya nguvu na ushawishi mkubwa.
Kanali Luteni Kanali Musa ameongeza kuwa operesheni ya kuwaska wapiganaji hao katika eneo hilo la Maiduguri inaendelea.
Tayari jeshi hilo la serikali limenasa shehena kubwa ya silaha ikiwa ni pamoja na vilipuzi, alisema Luteni Kanali Musa.
Aidha amedai kuwa Bwana Ibrahim alihusika na kifo cha Generali Shuwa baada ya kupokea agizo kutoka kwa Bwana Shekau.
Gen Shuwa ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao jeshi la Nigeria, linawaona kuwa mashujaa wa vita, kutokana na juhudi zake katika harakati za kumaliza vita kati ya jeshi la serikali na waasi wa Biafra waliotaka kujetenga miaka ya sitini.

No comments:

Post a Comment