Thursday, October 24, 2013

COMING THIS NOVEMBER:FROM tavcom




news
Remember, remember the 5th of November ... and visit our BRAND NEW WEBSITE !

After over a year in design and development our new website is scheduled to go LIVE on November 5th.


tavcom_grab copy 2

Our E-Learning Development team Ollie, Max and Jim have been burning the midnight oil to deliver a site that is not only packed with essential information but is quick and easy to navigate.

Sections of the site featuring company information, traditional 'classroom' training courses, the 'Tavcom Shop' and Technical Services have all been completely revamped and refreshed.

There will be many new sections too, reflecting our ongoing investment in this new interactive era. You will be able to find a selection of Online Courses, a CPD Certificate Course, and individual 'Knowledge Courses', all of which you can purchase and join at the click of a mouse.   

Visit www.tavcom.com after November 5th and put some SPARKLE into your Security Systems career!
divider.gif
 
news
BIG NEWS from Dubai and Saudi Arabia ...

Spectacular success for Tavcom in the Middle East! We have begun an extensive programme of CCTV training for the International Centre for Security and Safety, based at the Dubai Police Academy.

dubai_cctv_400 2

In the first year an estimated 1,000 Dubai engineers will receive Tavcom training in this modern facility designed and built by our own team of experts.

In a purpose-built Training Centre, Tavcom tutors will conduct Foundation and Advanced CCTV courses in partnership with the ICSS. These will enhance skills amongst local engineers,  allowing the Department of Protective Systems of Dubai Police Service to issue licences to those wishing to install and maintain electronic security systems in accordance with international codes and good practices.

If you are in the Middle East in late November please come and meet us at the IFSEC and OSH Arabia Exhibition in Riyadh. Find us at Stand P23 in Hall 4.

1382413_643934675651148_2087679529_n
 
divider.gif
 
news
REGISTER TODAY for the Tavcom 2014 Training Course Prospectus ... !

Don't miss out! Register your interest NOW in our eagerly awaited prospectus which is due to be completed in January.


register_now2 2

Simply email us with your contact details and we will send you an email alert when the online version is published.

Alternatively we would be delighted to post you a traditional hard copy (yes, real paper!) for you to keep close to hand on your bookshelf or desk.

Available in JANUARY ...  


REGISTER YOUR INTEREST HERE TODAY

 
 

NOVEMBER
COURSES

BOOK NOW!



COURSES FOR INSTALLERS

Practical IP
November 4th - 8th

CCTV
System Planning

November 4th - 6th

Electronic Principles
November 7th

Foundation
Intruder Alarms

November 11th - 13th

Practical CCTV
November 11th - 15th

Designing Networks
for Security

November 11th - 15th

Alarm Repair and
Maintenance

November 14th - 15th

Practical
Intruder Alarms

November 18th - 22nd

Foundation CCTV
November 18th - 20th

Intruder Alarm
Legislation

November 21st

Mains Compliance
November 21st

Design and Management of CCTV
November 25th - 28th

Practical
Optical Fibre

November 27th - 28th



COURSES FOR OPERATORS

Working in
Private Security

November 18th - 21st


Advanced Control
Room Skills

November 25th - 26th


Gathering
Video Evidence

November 27th - 29th



COURSES FOR MANAGERS

Managing CCTV
Control Rooms

November 4th - 6th


Managing
Disaster Recovery

November 4th - 7th




iStock_000005894531Small 2

To reserve your place
CONTACT US
TODAY


Telephone
01489 895099

or
Email
sales@tavcom.com

 

enews_01 5


gateway_logo_mini 5
Telephone: +44 (0)1489 895099
Email: sales@tavcom.com

NI KWELI AU CHANGA LA MACHO KAMA KAWAIDA YA CCM

Dar es Salaam. Serikali inatarajia kuandaa hati ya dharura ili kuwezesha kufanyika kwa maboresho ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba ambayo yatajadiliwa upya katika Mkutano wa Bunge unaoanza Oktoba 29 mjini Dodoma.
 
Tayari vyama vya upinzani na chama tawala vimekubaliana taratibu muhimu za kufuata ili maboresho hayo yaweze kupita ndani ya Bunge. Muswada huo haukuwa umepangwa kujadiliwa katika mkutano ujao wa Bunge ndio maana itabidi iombwe hati hiyo ya dharura. Hatua hiyo ni ushindi kwa vyama vitatu vya upinzani vya Chadema, CUF na NCCR- Mageuzi, ambavyo vilipinga muswada huo wakati wa mkutano uliopita wa Bunge Septemba, mwaka huu.
Muswada wa sheria hiyo uliopitishwa Septemba na Bunge ulisusiwa na wabunge wa vyama hivyo wa upinzani kwa maelezo kuwa una kasoro kwenye baadhi ya vipengele.
Hata hivyo, wabunge wa CCM waliamua kuendelea na mjadala na kupitisha muswada huo kitendo ambacho kilisababisha mvutano mkubwa uliomfanya Rais Jakaya Kikwete kukutana na viongozi wa vyama vya siasa vyenye wabunge kumaliza tofauti zao.
Mbatia asoma tamko la vyama
Akisoma tamko la vyama vya siasa mbele ya waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema hatua ya Serikali itakuja baada ya vyama vya siasa kufikia mwafaka wa vipengele vinavyotakiwa kufanyiwa marekebisho kwenye muswada huo. Mbatia alisema kuwa tayari kazi hiyo imefanyika na mapendekezo yao yameshapelekwa serikalini ingawa hakutaka kuingia kwa undani walichopendekeza katika marekebisho hayo.
Vyama vilivyokutana ni pamoja na CCM, Chadema, CUF, NCCR -Mageuzi, TLP. Pia vyama vya UDP na UPDP vilishiriki kwa niaba ya vyama visivyo na wabunge.
Mbatia alisema hatua inayofuata ni vyama kuunda kamati yao na Serikali kuunda yake ili kukubaliana kwa pamoja maeneo muhimu ya marekebisho.
Alisema lengo la hatua hiyo ni kuufanya mchakato wa Katiba kuwa shirikishi baada ya kamati hizo kumaliza kazi yake.
“Baada ya hapo, Serikali itaandaa hati ya dharura ili marekebisho yapelekwe haraka katika Mkutano wa Bunge unaoanza Oktoba 29, “ aliongeza Mbatia.
Mbatia alisema wanataka kabla ya Bunge la Katiba halijaanza basi sheria husika ifanyiwe marekebisho. “Tunawaomba Watanzania hasa wabunge waunge mkono juhudi hizi za vyama na Serikali ili kuhakikisha mchakato wa Katiba Mpya unakuwa shirikishi. Wabunge waridhie marekebisho haya na kuyapitisha,” alisema mbunge huyo wa kuteuliwa na Rais.

Uswisi sasa kurejesha mabilioni ya mafisadi

Dar es Salaam. Sakata la vigogo kuficha mabilioni ya shilingi katika benki za Uswisi, limechukua sura mpya baada ya Serikali ya nchi hiyo kutunga sheria inayowabana walioweka fedha kwenye benki zake kuzithibitisha, la sivyo zitarejeshwa katika nchi husika.
 
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alifanya mazungumzo na Serikali ya nchi hiyo ambayo imemweleza kuwa imebadili sheria zake ili kuwadhibiti wageni wanaoficha fedha nchini humo.
Akizungumza na gazeti hili, Zitto alisema amepata taarifa hizo juzi baada ya kukutana na Waziri wa Fedha wa nchi hiyo ambaye alimwandalia mazungumzo na watalaamu wake.
Alibainisha kuwa tangu kuibuka kwa sakata hilo mwaka 2012 na Bunge kuiagiza Serikali kufuatilia, Serikali haijaomba taarifa yeyote kutoka Uswisi kuhusu Watanzania waliohifadhi fedha nchini humo.
“Jana nilikutana na Waziri wa Fedha na akatuacha na mazungumzo na wataalamu wake. Wamesema hadi sasa, Tanzania haijasaini mkataba wa kubadilishana taarifa za kikodi (Multilateral convention on administrative assistance in tax matters),” alisema Zitto na kuongeza;
“Kwa kutosaini, Tanzania inajinyima haki ya kupata taarifa hizi na kutoza kodi kwa watu walioficha fedha huku (Uswisi), maana Sheria ya Kodi ya Tanzania inataka kila Mtanzania popote anapopata kipato halali lazima alipe kodi.”
Zitto alieleza kuwa kitendo cha Serikali ya Uswisi kubadili sheria zake, kinaiwezesha nchi hiyo kutoa taarifa za benki za watu walioweka fedha nchini humo wakiwamo Watanzania, ambao sasa watatakiwa kuthibitisha kama fedha hizo ni safi au la.
“Kiufupi, Tanzania haijaomba taarifa yeyote kutoka Uswisi. Ila Uswisi wamebadili sheria yao na sasa mmiliki wa fedha ndiyo anapaswa kuthibitisha kwamba ni safi, na ikithibitika kuwa hazina mwenyewe wala maelezo, zitarudishwa nchi husika,” alisema.
Zitto alisema mbali na kukutana na watendaji hao wa Serikali amezungumza na Umoja wa Mabenki wa nchi hiyo uliobainisha kuwa Uswisi ina Watanzania wachache wenye fedha.
“Wamesema Watanzania wengi wana fedha Uingereza, Jersey, Cayman Islands na Mauritius. Dubai pia imetajwa sana,” alisema Zitto. Zitto alielezea kuwa umoja huo wa benki za Uswisi umeanzisha mkakati wa kusafisha fedha uitwao ‘clean money strategy’, na wamegundua watu wengi ambao ni wanasiasa, wamezuia akaunti zao na kupeleka majina kwenye Serikali zao.
“Tanzania haijafanya maombi rasmi hapa Uswisi na hivyo wao kama benki hawawezi tu kutoa taarifa bila kuombwa. Sheria yao imerekebishwa ambapo sasa ni wajibu wa mwenye akaunti kusema kama fedha zake ni halali au hapana,” alisema Zitto na kuongeza.
Hivi sasa hawapokei pesa kutoka nchi za Afrika au wanapokea kwa tahadhari sana, maana kuna reputational risk (kupoteza heshima),” alisema.

Wednesday, October 23, 2013

Anas al Liby afikishwa mahakamani US


Al Liby anashukiwa kuhusika na mashambulizi ya kigaidi dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania 1998
Mshukiwa wa ugaidi aliyekamatwa na wanajeshi wa Marekani nchini Libya mapema mwezi huu wakati wa operesheni ya jeshi hilo mjini Tripoli, amefikishwa mahakamani kwa mara ya pili mjini New York.
Abu Anas al-Liby anayeshukiwa kuwa mmoja wa viongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeeda aliwakilishwa na wakili wa serikali ya Libya.
Bwana Liby anatuhumiwa kuwa na uhusiano na al-Qaedana pia kuhusika na shambulizi la kigaidi dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 2008.
Hata hivyo amekanusha madai dhidi yake.
Bwana Liby, mwenye umri wa miaka 49, ambaye jina lake halisi ni Nazih Abdul-Hamed al-Ruqai, alifikishwa mahakamani kujadili kuhusu mawakili wake.
Wakati wa kwanza kwa Liby kufikishwa mahakamani, aliwakilishwa na mawakili walioteuliwa na mahakama baada ya kusema kuwa hangeweza kumudu gharama ya mawakili wake.
Hata hivyo inaarifiwa baadaye serikali ya Libya ilimwajiri wakili kuweza kumwakilisha Liby.
Wakili huyo, Bernard Kleinman, alisema kuwa itachukua muda wa miezi kadhaa kudurusu stakabadhi nyingi kabla ya kesi hiyo kuanza rasmi.
Pia alisema sharti Liby arejeshewe Quran yake iliyochukuliwa na wanajeshi hao wakati wa kukamatwa kwake.
Alisema kuwa anawakilisha mshukiwa mmoja anayezuiliwa katika jela la Guantanamo Bay,nchini Cuba.
Bwana Liby anatarajiwa kurejea tena mahakamani tarehe 12 Disemba.
Kumekuwa na ghadhabu nchini Libya kufuatia kukamatwa kwa Al Liby na wanajeshi wa Marekani baadhi wakidai kuwa serikali ya Libya ilihusika.

CAG yet to receive parties audit reports-Zitto na Demokrasia



Chairman of the Parliamentary Public Accounts Committee (PAC),Mr Zitto Kabwe PHOTO|FILE
In Summary
NCCR-Mageuzi chairman James Mbatia refuted reports that the party has not submitted its audit reports for four consecutive years.
Dar es Salaam. The office of the Controller and Auditor General (CAG) said yesterday it was yet to receive audit reports from any of the nine political parties getting subvention.
The remark is in response to a controversy triggered by remarks of the chairman of the Parliamentary Public Accounts Committee (PAC), Mr Zitto Kabwe. His committee has since summoned six of the parties to explain why their accounts were yet to be audited.
The response by the deputy CAG, Mr Francis Mwakapalila, is likely to intensify the subvention controversy which has put the political parties and Mr Kabwe in a face-off in the last one week.
Zitto has accused nine political parties with representation in the Parliament of failing to submit their financial accounts to the CAG for auditing. He directed the registrar of political parties to suspend the subsidies of the parties for their failure to comply with the guiding law.
Zitto claimed that the parties had failed to submit audit reports accounting for a total of Sh67.7 billion in the past four years — a requirement made by the Political Parties (Amendment) Act, 2009.
The deputy CAG told The Citizen that the truth about the controversy will be known on Friday at a joint meeting of all the parties.
He, however, clarified that the CAG’s office had allowed parties to seek the services of external auditors. According to Mr Mwakapalila, the CAG can contract qualified firms to audit the political parties.
“Political parties are expected to maintain proper accounts every year and submit their financial reports, audited by the CAG, to the registrar of political parties,” he detailed.
PAC has summoned the parties on Friday to explain why they failed to submit the said reports. “We will know who was right or wrong, I hope the CAG will also be there. Let’s be patient,” he added.
The nine political parties have been insisting that they have submitted their audited accounts to the CAG and accused Mr Kabwe of overstepping his mandate.
Already, the Civic United Front (CUF) said it would not attend the Friday meeting and accused Mr Kabwe of acting beyond his legal powers.
The party’s deputy secretary general (Mainland), Mr Julius Mtatiro, said his party was not on the list of the parties that have not submitted their audit reports.
The ruling CCM has strongly accused the PAC, saying it was aware of the requirements of the law and that the it had has been submitting its audit reports to the CAG.
Its Publicity and Ideology secretary, Mr Nape Nnauye, said the Tanzania Audit Corporation has audited its accounts from 2003/04 to 2010/2011. “We’re waiting for the 2011/2012 audit report which is still with the external auditors,’’ adding that the report would be forwarded with the CAG once it is ready.
NCCR-Mageuzi chairman James Mbatia refuted reports that the party has not submitted its audit reports for four consecutive years.
“Our accounts were audited and we sent reports to the registrar,’’ he said.
He said, however, that the CAG’s office was cash-strapped and unable to oversee the auditing of political parties.
Chadema Information officer, Mr Tumaini Makene, said his party was playing by the rules as far as financial propriety and transparency were concerned. According to Zitto’s committee, CCM has failed to account for Sh50.97 billion, Chadema (Sh9.2 billion), CUF (Sh6.29 billion), NCCR-Mageuzi (Sh677 million), UDP (Sh33 million), TLP (Sh217million), APPT-Maendeleo (Sh11 million), DP (Sh3.3 million) and Chausta (Sh2.4 million).
Meanwhile, two PAC members yesterday defended Mr Kabwe against attacks by political parties allegedly for personalising the subvention issue, saying the matter was owned by the Committee.
They told The Citizen separately that Zitto had full blessings of members of the PAC before he made the statement to the effect that accounts of nine political parties had not been audited for four years.
“That is the position of our committee and not Zitto’s creations as political parties want the public to believe,” said a member of the committee, Mr Abdul Marombwa.
He said they were wondering why the political parties were personalising the issue while the matter surfaced the committee met registrar of political parties, Mr Francis Mutungi, who revealed the information.
“There is no Zitto’s agenda here, we all sat and agreed on the matter,” he said.
Another PAC member who asked not be named said their team was implementing Political Parties (Amendment) Act, 2009, which requires them to submit the parties accounts to the CAG for auditing and forward the audit reports to the registrar.
“The registrar confirmed to us none of the nine parties fulfilled that legal requirement,” he said.
“That was not Zitto’s statement, it was the outcome of the meeting,” he insisted.
Source: THE CITIZEN http://www.thecitizen.co.tz/News/Cag-yet-to-receive-parties-audit-reports/-/1840392/2041932/-/jwtkmj/-/index.html

New stocked 4WD/SUV - Autorec Enterprise, Ltd

To: All my valued customers


How are you today? I hope you are doing fine!

Today, please let me offer new stocked 4WD and SUV as follows.

http://www.japanesevehicle-sy.com/2013/10/new-stocked-4wdsuv.html

We obtained attractive and excellent selections.
Of course, if you find any your preferable one, please ask me anything.
If you need to receive the contents by e-mail, please feel free to ask me.
I will send it to you by e-mail too.

Thank you very much.

Yours Sincerely,
Shiro Yukimasa (mr)
Autorec Enterprise, Ltd.
---------------------------------------
E-mail: shiro@autorec.co.jp
Cell Phone no: +81-80-3646-2968
Private cell phone:+81-90-9931-3833
Phone: +81-5675-6-6111 (office)
FAX: +81-5675-6-6511 or 3504
---------------------------------------
Website: http://www.autorec.co.jp
My sales promotion blog: http://www.japanesevehicle-sy.com
Skype: shiro-yukimasa
Facebook: http://www.facebook.com/shiro.yukimasa

Sunday, October 20, 2013

Boko Haram waua madereva 19 Nigeria


Wanamgambo waliokuwa wamevaa nguo za kijeshi, wamewaua watu 19 katika kuzuizi cha barabarani walichokuwa wameweka kukagua magari katika jimbo la Borno.
Wanaume hao waliokuwa wamejihami , waliwasimamisha madereva na kuwaamrisha kuondoka kutoka katika magari yao kabla ya kuwapiga risasi na kuwaua.
Walioshuhudia tukio hilo waliambia BBC kuwa wanaume hao walikuwa wanachama wa Boko Haram, ingawa kundi hilo bado halijatamka chochote kuhusu mauaji hayo.
Jimbo hilo la Kaskazini mwa Nigeria liko chini ya sharia ya hali ya hatari, huku Boko Haram wakiwa vitani na serikali kutaka utawala wa kiisilamu.
Kundi hilo huwalenga raia na wanajeshi kwa mashambulizi ikiwemo shule na makabiliano ya mara kwa mara na jeshi la taifa.
Shambulizi la hivi karibuni, lilifanyika Jumapili, asubuhi karibu na mji wa Logumani, ambao hauko mbali sana na mpaka na Cameroon.
Walionusurika shambulizi hilo walisema kuwa washambuliaji walivaa nguo za jeshi na walikuwa wanaendesha pikipiki kabla ya kuwashambulia waathiriwa.
"Takriban wanaume 9 walituamuru kuondoka kwenye magari yeu na kulala chini,’’ alisema mwanamume
"Waliwaua watu 5 kwa kuwapiga risasi na kasha kuwanyonga wengine 14 kabla ya mtu mmoja kuwapigia simu na kuwambia kuwa wanjeshi wanakuja.’’
Alisema washambuliaji baadaye walitoroka na kujificha msituni kwa pikipiki zao.
Manusura mwingine alisema kuwa alisikia mtu aliyekuwa karibu naye akiuawa kwa kisu. Alisema ana uhakika kuwa washambuliaji walikuwa Boko Haram kwa sababu ya kuwa na ndevu.
Mwandishi wa BBC Tomi Oladipo alisema kuwa ni jambo la kawida kwa polisi kuweka vizuizi barabarani hasa katika maeneo yenye misukosuko na huenda washambuliaji waliiga mbinu hioyo ya jeshi ili kuwanasa waathiriwa. I,
Boko Haram limezua mgogoro mkubwa wa kisiasa Nigeria tangu mwaka 2009, nia yao kuu ikiwa kuunda utawala wa kiisilamu, hasa katika maeneo ya kaskazini mwa nchi
Kundi hilo limelaumiwa kwa mashambulizi kadhaa ambao yamesababisha takribna vifo 2,000 tangu mwka 2011.

Zitto aenda Uswiss na Uingereza kuhusu utoroshaji wa fedha

Shirika la Kimataifa la Mtandao wa Ulaya wa Madeni na Maendeleo, European Network on Debt and Development (Eurodad)  watafanya ziara ya kiuchunguzi kuhusu masuala ya uwazi katika kodi katika nchi za Ulaya kuanzia tarehe 20 Oktoba mpaka tarehe 5 Novemba mwaka 2013. Uchunguzi huo utaendeshwa na wataalamu waliobobea wa masuala ya kodi na maendeleo. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali wa Bunge la Tanzania Zitto Zuberi Kabwe ameteuliwa kuongoza Jopo la uchunguzi huo.
Eurodad ni Mtandao wa Mashirika yasiyo ya kiserikali yapatayo 48 kutoka nchi 19 za Ulaya ambayo yanajihusisha na masuala ya kufutia madeni nchi zilizoendelea, misaada yenye maana na kodi za haki. Mashirika haya yamekuwa kwenye kampeni ya kupinga utoroshwaji wa fedha kupitia ukwepaji kodi unaofanywa na mashirika ya kimataifa kwa nchi zinazoendelea. Zitto amekuwa mmoja wa wabunge wanaosimamia hoja ya kutaka Watanzania waliotorosha fedha kwenda nje warejeshe na kufunguliwa mashtaka. Mwaka 2012 aliwasilisha hoja binafsi Bungeni na kupitishwa kuwa Azimio la Bunge ya kutaka uchunguzi kuhusu utoroshwaji wa fedha na kufichwa nje kama Uswiss. Kikosi Kazi cha Serikali kutekeleza Azimio hilo la Bunge kinatarajia kuwasilisha taarifa yake katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Bunge. Siku ya Jumatatu tarehe 21 Oktoba Zitto atakutana na Waziri wa Fedha wa Uswiss na maafisa wa mabenki na asasi zisizo za kiserikali zilizopo jijini Geneva. Pia Zitto atahudhuria mkutano wa Kamati ya Kodi ya Umoja wa Mataifa katika kampeni ya kubadili mfumo wa kodi za kimataifa ili kuzuia unyonyaji wa nchi za Kiafrika unaofanywa na Makampuni makubwa ya Kimataifa.
Baada ya Geneva Zitto atatembelea nchi za Luxembourg na Brussels kabla ya kwenda Norway ambapo atamalizia ziara yake kwa Jopo la Wataalamu wa masuala ya kodi na Maendeleo kuandika taarifa maalumu yenye mapendekezo kuhusu kuzuia utoroshaji wa fedha kutoka Afrika.
Zitto atakwenda jijini London kutoa mada kuhusu masuala ya kodi za kimataifa katika mkutano wa Uwazi (Open Government Partnership). Mwenyekiti wa PAC Tanzania atafanya mazungumzo na Mwenyekiti wa PAC Uingereza Bi Margaret Eve Hodge, Lady Hodge MBE, PC, MP  kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano wa mabunge mawili na kuendeleza wito wake kwa makampuni ya kimataifa kulipa kodi zao barani Afrika na kuacha tabia ya kutumia ‘Tax Havens’ kukwepa kodi na kufukarisha nchi za Kiafrika.
Zitto invited to annual OGP Summit
The Kigoma North Member of Parliament and Chairman of the Public Accounts Committee (PAC), Hon Zitto Kabwe has been invited for the annual Open Government Partnership (OGP) Forum which kicks off in London at the end of the month.
The OGP Summit is a chance to promote tax and illicit issues to new audiences, to encourage new commitments in country action plans.
Hon Zitto, who also serves as Deputy Leader of Official Opposition in the Parliament, will serve in the panel which will discuss tax and illicit flows, which is among themes to be deliberated during the summit.
The OGP is a global platform for domestic reformers committed to making their governments more open, accountable, and responsive to citizens. Tanzania is among countries which have signed its membership to the OGP.
Hon Zitto has great interest on tax avoidance through illicit transfers and last year he tabled private motions which lead to the adoption of a Parliament Resolution compelling the government to investigate a number of individuals who have illicitly stashed billions of dollars abroad.
The fact finding mission will see its members interact with UN Tax Committee, OECD, EU as well as key European governments. They will visit a number of European cities namely Geneva, Paris, Luxembourg, Brussels and Oslo.
Ends
Issued by;

Parliamentary Office of Hon. Zitto Kabwe MP
Dar es Salaam
October 19, 2013

WANAVYOWEZA KUIBA PESA KUPITIA MITANDAO YA SIMU

Kumetokea matukio kadhaa ya wizi kwa njia ya mtandao unaohusisha simu za mikononi katika utoaji wa fedha ingawa pesa nyingi zimetolewa kwa ushirikiano wa wafanyakazi wa kampuni za simu .


Tukio kubwa sana ni lile la kampuni moja kupoteza karibu bil 2.5 kwa mkupuo , ambapo walihusika wafanyakazi zaidi ya 5 huku mmoja wao akiwa ameacha kazi kabla ya tukio nitaeleza tukio hili kwa ufupi .

Hii kampuni haina tabia ya ufanya utaratibu wa kufuta rekodi za mtu aliyeacha kazi ndani ya muda mfupi haswa zile taarifa zake za kuingia kwenye kompyuta au anapotaka kuingia kwenye database na program nyingine za kiofisi .

Kilichotokea huyu kijana alivyoacha kazi , wenzake wakajua hivyo walijua kuna taarifa Fulani zimeachwa kwahiyo wakafanya utaratibu wa kufanya recovery ya password za huyu kijana aliyeacha kazi .

Password zilipatikana zote kwa ushirikiano wa kijana mwingine wa kitengo cha Tehama , kwahiyo wakaingia kwenye kompyuta ya huyu kijana aliyeacha kazi na kutengeneza wakala feki wa kutoa fedha , wakafungua zaidi ya 10 halafu wakaweka watu wao .

Wakaanza kutoa fedha kupitia hao wakala feki , kilichofanya washtukiwe ni kitendo cha kutaka kuhamisha zaidi ya mil 400 kwenda kwenye akaunti ya mmoja wao ndio hapo benki walipopiga simu kwenye kampuni hiyo ili kupata taarifa zaidi kwa bahati nzuri alipokea mtu wao , kesho yake benki ikapiga tena ndipo mwenzao hakuwepo , ndipo mchezo wao uliishia hapo walikamatwa lakini sasa wako nje sijui kesi yao iliishia wapi .

………………………………………………………………………………………..

Siku nyingine mfanyakazi mmoja wa kampuni ya simu alienda kwa dada mmoja kuomba namba yake ya uwakala akamwambia atamwingizia hela kiasi cha mil 1 kila siku kwa siku 3 yeye achukue laki 3 kwa kila hamisho .

Huyu mfanyakazi aliwasiliana na mawakala zaidi ya 50 kwa makubaliano hayo , kumbe huyu mfanyakazi alikuwa anafanya taratibu za kuacha kazi na kweli aliacha kazi akaenda kufuata zile fedha .

Kampuni ya simu ikashtuka hela zimehamishwa kwenda kwa mawakala hao na mfanyakazi ameacha kazi , walikuwa wameshachelewa sana , waliopata shida ni mawakala kwa kufungiwa huduma zao wengine kupelekwa polisi .

……………………………………………………………………………………..

Ukiwa unatoa huduma za uwakala wa kutoa fedha basi usipende kuzoeana sana na watu , kama unapenda sikiliza kisa hiki .

Mtu mmoja alizoeana na wakala Fulani kiasi kwamba aliweza kujua hata bosa wa yule wakala majina yake na namba zake za simu na hata vitu vingingine vidogo vidogo .

Siku moja huyu jamaa kwa kutumia program ya kompyuta akamwandikia huyu wakala sms . NAOMBA UTUME KIASI CHA LAKI 4 KWENYE NO 98686 JINA LAKE NI SSSS .Wakala kuangalia namba ni ya bosi wake kweli hakutaka kuhakiki hiyo sms vizuri yeye akahamisha hela akaibiwa .

Siku ya pili huyu mhalifu alienda kwa mtu mwingine kwa kutumia hiyo program akaandika ujumbe wa kutoa fedha  kiasi cha laki 4 ,wakala kuona sms akajua kweli yule mtu katoa hela kampa mhalifu hela kumbe ile ilikuwa sms tu , siku nyingine akajifunza mtu akitoa hela hakikisha nae anapokea sms ya kuthibitisha kutoa hela .

HIVI NDIVYO FACEBOOK INAVYOPATA PESA KUPITIA KWAKO


Kuwa na Akaunti ya Facebook ni kwa manufaa yako na manufaa ya Facebook

Facebook ambayo kwa sasa inapatikana katika lugha 70 ulimwenguni, ni mtandao wa jamii ambao unaongoza kwa kuwa na watumiaji wengi zaidi duniani. Wewe na mie kama watumiaji wa Facebook tunainufaisha kampuni hiyo ya Facebook, kwani kupitia kuitumia kwetu kunaiwezesha Facebook kuingiza mapato kwa njia ya moja kwa moja au nyingine.

Makala hii inakuchambulia namna ambavyo Facebook inaingiza "vijisenti" vyake:-


1. Kupitia Matangazo: Kwakuwa inao watumiaji wa mtandao wengi, ni rahisi kwa Facebook kushawishi watu binafsi na makampuni kutangaza bidhaa zao kupitia aina mbalimbali za matangazo yanayorushwa hewani na Facebook. Mfano , kampuni inaweza kudhamini POST yake, ili ionekane kwa watu wengi zaidi na mara nyingi. Pia kuna matangazo ya biashara ambapo unaweza kutengeneza tangazo lako la biashara na kulirusha hewani kupitia Ukurasa wako wa Facebook (Facebook Page).  Ili kutengeneza tangazo Facebook, unaweza kuenda sehemu maalum ukiwa Facebook imeandika 
CREATE AN AD.Unahitaji kuwa na Credit Card au Umejisajili na unayo akaunti ya Paypal ili kuweza kulipia huduma hii.

Mfano wa Matangazo yanayoipatia fedha facebook
 
 

2. Salio maalum la Facebook ( Facebook Credit)

Ni kama vile unavyonunua salio la simu yako ili utumie salio hilo kupiga simu, ila kwa Facebook, unaponunua Facebook Credit, ni kwa ajili ya kuweza kutumia credit hiyo kulipia kucheza Games, au hata kununua vitu katika baadhi ya maduka yanayouza bidhaa zao ndani ya Facebook.

Unahitaji kuwa na Credit Card au Umejisajili na unayo akaunti ya Paypal ili kuweza kununua Facebook Credit.


3. Kupitia Kuuza bidhaa mbalimbali

Facebook inayo huduma ya kuuza bidhaa mbalimbali kwa mtindo wa "Gift" ambapo wewe mtumiaji unachagua nani unataka kumnunulia bidhaa , kisha unaenda kwa profile ya huyo unayetaka kumuuzia bidhaa. Utaona sehemu imeandikwa GIVE GIFT, ukibofya hapo utakutana na aina mbalimbali za zawadi na maelekezo. Hata hivyo huduma hii ya kutoa zawadi kwa watu haipataki kwa kila nchi. Inabidi ucheki Profile ya mtu husika unayetaka kumpa zawadi kuona kama GIVE GIFT ipo katika profile yake.
 

TAHADHARI KWA WATUMIAJI WA KOMPYUTA ZENYE WINDOW XP


 

Watumiaji wa  programu ya komputa iitwayo Window XP wamepewa tahadhari na kampuni ya Microsoft ambayo ndiyo iliyotengeneza program hiyo kuwa hapatakuwa na matoleo mapya (updates) zaidi kuhusu Window XP Service Pack 3 baada ya mwezi wa nane mwaka 2014.

Akizungumza na wataalamu mbalimbali wa masuala ya ulinzi mtandao Agosti 16,mwaka huu Mkurugenzi wa kitengo kijulikanacho kwa jina la Microsoft Trustworthy Computing,Tim Rains anasema kuwa ingawa Window XP wakati inatolewa ilikuwa na ubora huku ikipendwa na watumiaji wengi wa kompyuta,kwa sasa imeonekana kuwa dhaifu kutokana na kuongezeka kwa uhalifu wa kimtandao.

Amesema kumekuwepo na wimbi kubwa la wahalifu wanaotumia mianya mbalimbali kuingilia kompyuta za wateja wanaotumia Window XP na kuongeza kuwa hali hiyo ya uhalifu itaendelea hasa kwa wale wataoendelea kutumia aina hiyo ya window.

Rains amesema wanaendelea kutafuta ufumbuzi pale itakapobainika wahalifu wameweza kupenya katika kompyuta za wateja wao wanaotumia aina mpya za window ambapo kwa sasa kupitia kituo cha kuangalia usalama wa kompyuta cha kampuni hiyo kinaendelea kutoa maelezo ya jinsi ya kuwalinda wateja wao.

Amesema kampuni ambazo bado zitakuwa zinatumia Window XP,zitasababisha wahalifu kutafuta mapungufu katika window hiyo na kuleta athari ambapo kampuni ya Microsoft haitakuwa na msaada ama wa bure au wa kulipia dhidi ya hali hiyo,kwani itakuwa imeshaacha kutoa msaada wa kuhusu Window XP


Chanzo:Gazeti la Mwananchi

Friday, October 18, 2013

CHADEMA wamkana Zitto • Yeye asema anawangoja makatibu wakuu Oktoba 25

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa kimewasilisha taarifa zake za fedha kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na zilizokaguliwa kwa mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12.
Kwamba, hilo linathibitishwa na barua ya Msajili wa Vyama yenye kumb. Na CDA.112/123/01a/37 ya Septemba 4, 2012, iliyopelekwa kwa makatibu wakuu wa vyama vyote vya siasa.
Uthibitisho huo umetolewa kukanusha taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, iliyosema kuwa vyama vya siasa vinavyopata ruzuku kutoka serikalini havijawasilisha taarifa yake ya mapato na matumizi kwa ajili ya kufanyiwa ukaguzi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa kipindi cha miaka minne mfululizo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana huku akionesha nyaraka za vielelezo, Katibu wa Baraza la Wadhamini wa CHADEMA, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Anthony Komu, alisema wamesikitishwa na taarifa ya PAC.
Alisema kuwa wameamua kuchukua jukumu la kuufahamisha umma kuwa wapo tayari kutoa ushirikiano wa dhati ili sheria hiyo ifanye kazi yake kwani tangu itungwe mwaka 1992 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2009, CHADEMA kimekuwa kikifuata utaratibu kama ulivyoelekeza.
Komu alisisitiza kuwa taarifa za PAC si sahihi na hazina ukweli wowote kuhusiana na CHADEMA labda kwa vyama vingine.
Alifafanua kuwa hesabu za mwaka wa fedha zilizokaguliwa za 2009/2010, CHADEMA kiliwasilisha kwa msajili kwa barua yenye kumb. C/HQ/ADM/MSJ/04/71 ya Oktoba 2011.
Komu alionesha barua ya Msajili wa Vyama ya Septemba 4, 2012, ambayo ilionesha vyama vilivyowasilisha hesabu zilizokaguliwa kwake kuwa ni CHADEMA na NCCR-Mageuzi tu.
Kwa mujibu wa barua hiyo, CUF waliwasilisha hesabu kwa msajili bila kukaguliwa. Vyama ambavyo havikuwasilisha hesabu zao kabisa ni CCM, TLP, APPT- Maendeleo, UDP na DP.
Komu alifafanua kuwa taarifa ya fedha iliyokaguliwa kwa mwaka huu 2012/2013 bado hawajaiwasilisha kwenye ofisi ya msajili.
Alisema hatua hiyo ni baada ya ofisi ya msajili yenyewe kutoa maelekezo kwa barua yenye kumb. Na. DA.112/123/16A/97 ya Novemba 26, 2012.
“Tumefanya mawasiliano na CAG kwa ufafanuzi wa jambo hili na tutawafahamisha ipasavyo kuhusu malipo/gharama mliyotakiwa kulipa katika ukaguzi wa mahesabu hayo,” ilisomeka barua hiyo ya msajili.
Hadi jana wakati CHADEMA wanatoa utetezi huo, Komu alisema ofisi ya msajili ilikuwa haijatuma hata mkaguzi au maelekezo yoyote kama walivyoelekezwa walipe kiasi gani na wapi kwa kazi ya ukaguzi wa hesabu za mwaka 2012/2013.
Komu aliilaumu PAC kujitokeza hadharani kuzungumza mambo mazito pasipokuwa na ushahidi wala kuwashirikisha wahusika ambavyo ni vyama vya siasa, badala yake ikajumuishwa na CHADEMA katika kapu hilo.
“CHADEMA tuna hadhi yetu, ni chama makini, hatuachi mambo yaende yalivyo, ndiyo maana kuliko kuanza kujibizana na mtu mmoja mmoja katika simu, tumewaita waandishi ili kutoa taarifa hii kwa umma kuwa taarifa ya PAC si sahihi,” alisema.
Alisisitiza kuwa kama kweli tangu mwaka 2009 hesabu hazijakaguliwa, basi aulizwe CAG, ofisi yake inafanya nini ikiwa fedha zinatolewa mwaka wa kwanza hazikaguliwi hadi mwaka wa nne.
“Ofisi ya CAG ituambie wanafanya kazi gani, kwanini wanaendelea kutoa ruzuku kama hesabu hazikaguliwi?
“Sisi CHADEMA tuko wazi, tunapopata hata misaada kutoka nje huwa tunamuarifu msajili, maana yake ni hatari kama chama kinapokea misaada hakisemi kwa msajili,” alisema.
Komu aliongeza kuwa chama kinaweza kupokea hata misaada ya Al- Shabaab au mambo mengine kama ya EPA, ndiyo maana wanawataka PAC waende mbele zaidi ili utaratibu wa uwazi uende kwenye vyama vyote kama wanavyofanya CHADEMA.
“Tulipata fedha kutoka Denmark ukiwa msaada kwa ajili ya kujenga uwezo, tulimwandikia msajili, naye akatujibu kwa barua Na. DA/112/123/16a/10 ya tarehe 19, Agosti 2013.
“Tunashukuru kwa taarifa hii ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa,” ilisomeka barua hiyo.
Juzi, vyama vya CCM, CUF na NCCR-Mageuzi navyo vilimjia juu Zitto vikidai anatafuta umaarufu, kwani hesabu zao zimekaguliwa.
Zitto azidi kukomaa
Alipotafutwa kujibu ufafanuzi huo wa vyama, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, alisema vinapoteza muda kuongea na waandishi, badala yake viongozi wao wajiandae kujieleza mbele ya kamati yake.
“Wanapoteza muda tu. Badala ya kufanya mikutano na waandishi, wajiandae kujieleza mbele ya kamati, niweke wazi utaratibu wa kisheria.
“Vyama vinapewa ruzuku, vinafunga mahesabu ya mwaka, vinawasilisha mahesabu kwa mkaguzi. Akishakagua vyama vinawasilisha hesabu zilizokaguliwa kwa msajili, naye anachapisha mahesabu kwenye gazeti la Serikali (GN),” alisema.
Zitto alisisitiza kuwa hadi kufikia juzi, hakuna chama ambacho kilikuwa kimepeleka mahesabu yaliyokaguliwa kwa msajili.
Alisema kuwa PAC inasimamia sheria, hivyo kumuonya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, aliyemshambulia, akisema aache kelele wakati kamati hiyo ikiwa inamsubiri Katibu Mkuu wake, Abdulrahaman Kinana kuhojiwa.
Zitto alisema yupo tayari kunyongwa akitetea masilahi ya umma, huku akiwataka viongozi wa CHADEMA na CCM kutoendeleza malumbano kuhusiana na hoja ya zuio la ruzuku, la sivyo atawafunga.
Akizungumza na waandishi, alisema vyama hivyo vinatakiwa kufika mbele ya kamati yake Oktoba 25, mwaka huu.
Zitto alisema anayo mamlaka kama mwenyekiti wa kamati hiyo kuwafunga jela wote wanaoendeleza malumbano hayo ilhali agizo lilishatolewa, na kusema kuwa hilo ni onyo kwa CHADEMA na CCM, aliodai ni vinara wa malumbano.
“Mimi sifanyi siasa hapa, natekeleza jukumu langu kama mwenyekiti wa kamati, kwa hiyo hili ni onyo kwao, nipo tayari kunyongwa nikitetea masilahi ya umma,” alisema.
Alieleza kuwa ni vema vyama hivyo vikapeleka ripoti kwa msajili na kuachana na malumbano yasiyo na tija, huku akiwashukia waliokuwa wakidai kuwa anatafuta umaarufu kwa maelezo kuwa tayari ni maarufu.
Alisema vyama hivyo vinavyotakiwa kufika kwenye kamati yake ni CCM, TLP, CHADEMA, NCCR-Mageuzi, UDP, CUF, APPT-Maendeleo, UPDP na Chausta.
Aliwataka wanasiasa kutochukulia suala hilo kama ni la Zitto binafsi bali limeamuliwa na Kamati ya Bunge.
Alifafanua kuwa anafahamu fika kuwa ana masilahi katika hilo, kwa kuwa ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, lakini uamuzi alioutoa ni kwa niaba ya kamati na si binafsi.
Zitto alisisitiza kuwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita, ofisi ya msajili pamoja na waliokuwa wajumbe wa kamati hiyo kabla yake, walikuwa wakiogopa kuviwajibisha vyama hivyo.
Alisema inashangaza kuona katika hicho, msajili hakuwahi kuitwa katika kamati wala suala la ruzuku za vyama kuzungumziwa.
Vyama hivyo vinadaiwa kutowasilisha ripoti hiyo kwa miaka minne kuanzia mwaka 2009, ambapo tayari serikali imeishavilipa jumla ya sh bilioni 67.7 kama ruzuku.
Ruzuku hiyo imelipwa kwa CCM sh bilioni 50.9, CHADEMA sh bilioni 9.2, CUF sh bilioni 6.3 na NCCR-Mageuzi sh milioni 637.
Vingine ni UDP sh milioni 333, TLP sh milioni 217, DP sh milioni 3.3, APPT-Maendeleo sh milioni 1.1 na Chausta sh milioni 2.4.

Utata wagubika ujio wa Alex Massawe

HATUA za kumrejesha nchini mfanyabiashara maarufu, Alex Massawe, aliyefikishwa mahakamani nchini Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) kwa tuhuma za mauaji, zimegubikwa na utata mkubwa, huku Tanzania ikidaiwa kushindwa kutimiza masharti ya Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol).
Kwa mujibu wa chanzo chetu kutoka Dubai, Interpol iliipa Tanzania hadi kufikia Septemba 4, mwaka huu, iwe imewasilisha vielelezo vya kuthibitisha tuhuma zake.
Chanzo hicho kiliongeza kuwa muda huo umemalizika bila Tanzania kuwasilisha uthibitisho huo na kwamba Massawe ameachiwa huru nchini humo.
Massawe alikamatwa Dubai kati ya Juni 20 na 25. Kwa mujibu wa Mkuu wa Interpol, Tawi la Tanzania, Gustav Babile, ombi la kumleta mhalifu nchini kutoka nje ya nchi (extradition request) lina hatua ndefu.
Alisema kuwa kuna mlolongo wa taratibu za kutekeleza ili Massawe aletwe, akasisitiza kuwa ilikuwa ni lazima kwanza Polisi wa Tanzania watoe tangazo kwa Interpol kuhusu kumsaka mtu huyo ili aletwe.
Jeshi la Polisi nchini limekanusha taarifa hizo za kuachiwa kwa Massawe, likisema halina taarifa za suala hilo, na kwamba taratibu za kisheria zinaendelea kufanyika.
Msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso, alisema: “Mambo ya kusikia sisi hatuyafanyii kazi, kwanza vyanzo vingine vya habari ni vya kutiliwa shaka. Sisi tukijiridhisha tukawa na taarifa kamili tutawaambia.”
Naye Mkuu wa Interpol Tanzania, Babile, alisema kuwa Jeshi la Polisi limeshafanya taratibu zote za kiuchunguzi, limepeleka jalada kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Eliezer Feleshi.
Babile alisema kiutaratibu Jeshi la Polisi linapomaliza uchunguzi na kuandikia, kinachofuata ni jalada kupelekwa kwa DPP, ambaye akishajiridhisha hulipeleka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ili taratibu za kuanza kumrejesha mtuhumiwa nchini ziweze kufanyika.
Hata hivyo taarifa ya awali iliyotolewa na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, baada ya kukamatwa Massawe, ilisema kuwa sheria inasema mtu akikamatwa nchi nyingine, anashtakiwa nchini humo, huku taratibu za kisheria za kumrejesha zikiendelea kwa nchi ambazo zina utaratibu wa kubadilishana wafungwa kama ilivyo Tanzania na UAE.
Taarifa za kukamatwa Massawe nchini Dubai zilipatikana Julai 11, mwaka huu, na kuthibitishwa na Babile, aliyesema mtuhumiwa huyo alikamatwa kati ya Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.
Aprili 4, mwaka huu, Massawe alitajwa mahakamani katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara, Onesphory Kituly, ambaye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 akiwa nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam.
Katika kesi hiyo mshtakiwa wa kwanza ni mfanyabiashara maarufu, Abubakar Marijani ‘Papaa Msofe’ na mshtakiwa mwingine ni Makongoro Joseph Nyerere.
Dar es Salaam. Wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe akisisitiza kuwa hesabu za Chadema ni miongoni mwa ambazo hazijakaguliwa, chama hicho kimeishutumu kamati hiyo kwa kuagiza kusitishwa kwa ruzuku kwa vyama vya siasa na kusema hatua hiyo ni ubabe.
Wakati Chadema wakitoa kauli hiyo, jana Zitto alisema vyama vya siasa tisa vikiwamo Chadema, CCM na CUF vinatakiwa kufika mbele ya PAC Oktoba 25 mwaka huu, kwa ajili ya kujieleza na kwamba chama kitakachokaidi, sheria za Bunge zinaeleza wazi, kwamba wahusika wanaweza kufungwa jela siku saba.
Chadema kilisema kuwa PAC kabla ya kuchukua hatua, ilipaswa kuwapa nafasi ya kuwasikiliza viongozi wa vyama husika, kumhoji Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Msajili wa vyama vya Siasa ambao wameshindwa kutimiza wajibu wa kukagua hesabu hizo kwa miaka minne.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chadema, Anthony Komu alisema jana kuwa, uamuzi wa PAC utaviathiri vyama kwani bajeti zake zimezingatia kuwapo kwa ruzuku.
“Kuna vyama ambavyo vinategemea ruzuku kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, Chadema ingawa tuna vyanzo vingine vya mapato, tunaitegemea kukamilisha bajeti yetu kwa fedha za ruzuku ambazo zinatusaidia kwa asilimia 45. Ni tabia mbaya kuchukua uamuzi kwa kibabe na kuhukumu kabla ya kutusikiliza siyo haki hata kidogo,” alisema Komu.
Alitetea chama chake kwamba kimekuwa na utaratibu wa kuwasilisha hesabu zilizokaguliwa ambapo alitoa ushahidi wa barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa ya April 16, 2012 ikithibitisha kwamba hesabu zao zipo sawa baada ya kuziwasilisha katika ofisi hiyo.
“Chadema tunataka ukaguzi wa hesabu usijikite katika fedha za ruzuku pekee bali katika vyanzo vyote vya mapato ya vyama, tatizo CAG alitueleza kwamba anakabiliwa na upungufu wa rasilimali watu kwa hiyo PAC walipaswa kuliangalia tatizo hilo na kutafuta ufumbuzi,” alisema Komu.
Zitto juzi alikaririwa na vyombo vya habari akieleza kuwa Serikali ilitoa kiasi cha Sh67.7 bilioni kama ruzuku kwa vyama tisa vya siasa tangu mwaka 2009, lakini vyama hivyo havijawahi kuwasilisha taarifa za ukaguzi wa hesabu zake kwa msajili kama sheria inavyoagiza.
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema), aliamuru Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kusimamisha utoaji wa ruzuku hadi hapo vitakapowasilisha ripoti ya ukaguzi na makatibu wake wakuu kuhojiwa.
Miongoni mwa vyama vilivyotajwa ni APPT-Maendeleo lakini jana Rais Mtendaji wa Chama hicho, Peter Mziray alisema chama chake hakijawahi kupewa kiasi cha Sh217 milioni kama inavyodaiwa na PAC.
Mziray alikiri walianza kupata ruzuku 2009 ila inasema ilikuwa kidogo kiasi cha Sh 50,000 kwa mwezi na baadae kupanda Sh 275,000 kwa mwezi.
Alisema kiasi walichopata kuanzia mwaka 2009 ni kiasi cha Sh12 milioni tu. “APPT-Maendeleo haina uwakilishi bungeni kwa hiyo haiwezi kupata kiasi hicho kikubwa cha fedha,” alisema Mziray.

Simba noma Jumapili pale Taifa

Yanga inaendelea kushikilia rekodi ya jumla baada ya ushindi mara 38, Simba 32, huku mara 32 zilitoka sare
 
Dar es Salaam.  Huku zikiwa zimesalia siku mbili, rekodi za miaka 13 iliyopita, zinaonyesha Simba imeibuka na ushindi mara nyingi zaidi ya Yanga katika mapambano baina ya timu hizo iliyopigwa siku ya Jumapili.
Simba na Yanga zitashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam keshokutwa kukabiliana katika pambano la Ligi Kuu Bara mzunguko wa kwanza.
Mwananchi lilifanya uchunguzi wake unaoonyesha kuwa kuanzia mwaka 2000 mpaka mwaka huu Simba ina rekodi nzuri zaidi ya kushinda siku ya Jumapili kuliko wapinzani wao, Yanga.
Rekodi hizo zinaonyesha kuwa katika kipindi hicho Simba na Yanga zilikutana mara 20, ambapo kati ya hizo Simba iliibuka na ushindi mara saba, wakati Yanga ilishinda mara mbili, huku mara 11 zikitoka sare.
Mechi zilizochezwa Jumapili baina ya Simba na Yanga Juni 25, 2000 (Simba 2-1 Yanga), Agost i 18, 2002 (Simba 1-1 Yanga), Novemba 10 (Simba 1-0  Yanga),  Novemba  12, 2000 (Simba 0-0 Yanga), Septemba 28, 2003 (Simba 0-0 Yanga), Novemba  2, 2003(Simba 4-1 Yanga).
Machi  31, 2002 (Yanga 3-0 Simba), Aprili 20, 2003 (Simba 1-1 Yanga), Aprili  17, 2005 (Simba 2-1 Yanga), Machi  26,
2006 (Simba 0-0 Yanga), Oktoba 29, 2006 (Simba 0-0 Yanga), Julai  8, 2007 (Simba1-1 Yanga), Aprili  27, 2008 (Simba 0-0 Yanga).
Oktoba  26, 2008 (Yanga 1-0 Simba), Aprili  19, 2009 (Simba 2-2 Yanga), Aprili  18, 2010 (Simba 4-3 Yanga).
(Julai  27, 2008) Yanga haikutokea uwanjani, Simba ikapewa ushindi wa chee. Rekodi hizi zinajumuisha mechi za mashindano mbalimbali  ikiwemo Ligi Kuu Bara, Kombe la Mapinduzi, Tusker Cup, lililokuwa Kombe la Chama cha Soka Tanzania (FAT) na Kombe la Kagame.
Hata hivyo, ukiondoa michezo baina ya timu hizo iliyofanyika Jumapili, Yanga inaendelea kushikilia rekodi ya jumla baada ya kuibuka na ushindi mara 38, Simba 32, huku mara 32 zilitoka sare.
Katika hatua nyingine, Kocha wa Yanga, Ernest Brandts alisema, matokeo ya ushindi wa mabao 2-1 iliyopata kikosi chake katika pambano la kirafiki dhidi ya Chipukizi ya Pemba yamekoleza morali ya wachezaji wake kuhakikisha wanaibwaga  Simba keshokutwa.

Thursday, October 17, 2013

Wachezaji wa Zambia kukamatwa ni waliogoma kwenda kucheza na Brazil

Zambia ndio mabingwa wa kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2012
Zambia imetoa vibali vya kukamatwa kwa wachezaji wake watatu waliokosa mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil mjini Beijing China. Hata hivyo Zambia ilishindwa na Brazil mabao mawili kwa nunge.
Klabu ya DRC TP Mazembe ilisisitiza kuwa wachezaji hao Rainford Kalaba, Stoppila Sunzu na Nathan Sinkala walijeruhiwa na kusababisha mgogoro kati ya shirikisho la soka la Zambia na serikali ya Zambia.
Baada ya wachezaji hao kufanyiwa ukaguzi mjini Lusaka, shirikisho la soka la Zambia likasisitiza kuwa bado wanaweza kusafiri kwenda China kwa mchuano huo,lakini klabu ya Mazembe ambako wachezaji hao hucheza soka ya kulipwa ikawataka kurejea.
Hatua hiyo ilisababisha serikali ya Zambia kuingilia kati kwa kuwapokonya wachezaji hao pasi zao za usafiri ili kuwazuia kwenda kuchezea klabu yao mjini Lubumbashi.
Hata hivyo, wachezaji walifanikiwa kuvuka mpaka na wanaaminika kuwa nchini DR Congo.
Shirikisho la soka la Zambia limeandikia barua shirikisho la soka duniani Fifa, na kulalamika kuwa klabu ya Mazembe haikuwaruhusu wachezaji hao kushirki majukumu yao ya kimataifa.
Zambia ilishindwa kwenye mechi hiyo ya kimataifa mjini Beijing
Zambia ambao ni mabingwa wa kombe la taifa bingwa Afrika walikuwa wanashirki mechi yao ya kwanza wakiongozwa na kocha wao mpya Patrice Beaumelle, ambaye alichukua usukani siku nane zilizopita baada ya Herve Renard kucha kazi.

Wednesday, October 16, 2013

Utafiti: Wasio na elimu waongoza kumpenda Rais Jakaya Kikwete

Dar es Salaam. Ripoti mpya ya utafiti imebaini kuwa asilimia kubwa ya Watanzania wenye elimu ya darasa la saba na wale wasiosoma, ndiyo wanaokubaliana na utendaji kazi wa Rais Jakaya Kikwete.
Ripoti ya utafiti huo iliyopewa jina la ‘Namna Watanzania wanavyouangalia utendaji kazi wa Bunge na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania’ ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Asasi ya Afrobarometer, inaonyesha kuwa asilimia 77 ya waliokosa elimu ndiyo wanamuunga mkono Rais Kikwete.
Afrobarometa ni Asasi ya Kimataifa inayojumuisha taasisi tatu za Institute for Democracy ya Afrika Kusini, Ghana Centre for Democratic Development ya Ghana na Political Science Department ya Chuo Kikuu cha Michigan cha Marekani.
Mtafiti Msaidizi wa Afrobarometer, Stephen Mwombela akisoma ripoti hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alisema asilimia 72 ya wale walioishia darasa la saba ndiyo wanamuunga mkono Rais.
Wakati asilimia 23 ya watu wasiosoma ndiyo hawamkubali Rais na asilimia 28 ya wale walioishia darasa la saba, pia hawaridhishwi na utendaji wa kiongozi huyo.
Mwombela, hata hivyo, alisema utafiti huo uliohusisha watu 2,400 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaonyesha kuwa idadi kubwa ya wasomi wa kiwango cha sekondari na kuendelea wanaunga pia mkono utendaji wa Rais, lakini siyo kwa kiwango cha juu kama wale ambao hawajasoma.
“Asilimia 60 ya waliosoma elimu ya sekondari na kuendelea wanaunga mkono utendaji wa Rais, lakini 40 hawakubaliani na utendaji wake,” ilisema taarifa ya matokeo ya utafiti huo uliofanyika kati ya Mei hadi Juni mwaka jana.
Matokeo ya utafiti huo yanatofautiana na yale ya mwaka 2008, ambayo yalionyesha kuwa wasomi walikuwa wanamuunga mkono Rais kwa asilimia 92.
Pia katika matokeo ya utafiti huo wa mwaka 2008, ulionyesha kuwa wasiosoma walimuunga mkono kiongozi huyo kwa asilimia 92.

Imani ya wananchi kwa Rais
Ripoti hiyo ilisema pia imani ya wananchi kwa utendaji wa Rais imeshuka hadi kufikia asilimia 74 kwa mwaka jana, tofauti na asilimia 94 ya mwaka 2005 wakati aliposhika wadhifa huo.

Pia utafiti huo uliodhaminiwa na Taasisi ya Utafiti kuhusu Kuondoa Umaskini (Repoa) umebainisha kuwa imani ya wananchi kwa Rais imeshuka kutoka asilimia 88 mwaka 2008 hadi asilimia 74, huku idadi ya watu wasiokubaliana kabisa na Rais ikiongezeka kutoka asilimia 11 mwaka 2008 hadi asilimia 26 mwaka 2012.
Imani kwa Bunge
Wananchi wengi pia wameonyesha kutokuwa na imani na mwenendo wa Bunge, kwa kulipa asilimia 76 mwaka 2012, idadi yao ikishuka kutoka asilimia 83 ya mwaka 2008.
Imani ya wananchi kwa Bunge imeshuka katika kipindi hiki ambalo liko chini ya Spika Anne Makinda, ambaye alichukua uongozi mwaka 2010 wakati mwaka ule wa 2008 lilikuwa chini ya Samuel Sitta imani ilikuwa juu. Taarifa hiyo pia inaeleza kuwa watu wanaoishi vijijini ndiyo wanaoridhishwa zaidi na Bunge kwa kupata asilimia 63, ikilinganishwa na wakazi wa mijini ambao ni asilimia 60.
Pia imebainika kuwa wananchi wa Zanzibar wanaridhishwa zaidi na utendaji wa Bunge kwa asilimia 64, tofauti na wananchi wa Tanzania Bara ambao wanaridhishwa kwa asilimia 61.
“Watu waliokuwa wanakubaliana na utendaji wa Bunge mwaka 2003 walikuwa asilimia 31, lakini mwaka 2012 idadi iliongezeka hadi asilimia 61,” alisema Mwombela wakati akiwasilisha matokeo ya utafiti huo unaofanyika kwa mara ya tano nchini Tanzania.
Hata hivyo, Mwombela alisema kuwa wananchi wengi bado wanafurahishwa na utendaji wa Mahakama, lakini idadi yao imepanda kutoka asilimia 73 kwa mwaka 2008 na kuwa asilimia 74 mwaka 2012.
Akichangia baada ya ripoti hiyo kuwasilishwa, Dk Abel Kinyondo, alisema kuwa matokeo ya utafiti huo hayajaonyesha kuporomoka kwa imani kwa Rais badala yake yameonyesha uhalisia.
“Inawezekana imani kwa Rais haijashuka, badala yake imekaa katika hali yake, kwa sababu kitu gani alikifanya 2008 watu wakampenda sana, ambacho leo hii hajakifanya hadi wasimpende?” alihoji Kinyondo. Kinyondo alionekana kushangazwa na namna Rais alivyoweza kupata asilimia 71 wakati nchi inapita katika kipindi kigumu cha rushwa na ufisadi.
Mwakilishi kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Victor Kimesera alisema utafiti huo una kasoro kadhaa ikiwa ni pamoja na kumtaja Rais kuwa ndiye mwakilishi pekee wa Serikali wakati kuna viongozi wengine wengi. “Kwa upande wa Rais walitakiwa kuhoji viongozi wengi zaidi kwa sababu Rais siyo kiongozi pekee yake katika Serikali,” alisema.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Dk Jonas Kipokola alisema kama utafiti huo ungefanyika Mei hadi Juni mwaka huu, huenda matokeo yangekuwa tofauti. “Siwezi kusema yangekuwaje, lakini yasingekuwa hivyo yalivyo,” alisema Kipokola.

Misri na Kichapo ilichopata toka kwa Ghana

Ghana iko katika nafasi nzuri sasa ya kwenda Brazil
Ghana ilipiga hatua kubwa katika kufikia kinyang'anyiro cha kombe la dunia baada ya kuicharaza Misri mabao 6-1 katika mkondo wa mwisho wa mechi za kufunzu kwa kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil.
Asamoah Gyan aliingiza bao la kwanza ambalo lilifuatiwa na lengine la mchezaji wa Misri Wael Gomaa katika lango la Ghana.
Mchezaji wa Misri, Mohamed Aboutrika aliingiza bao la penalti lakini Gyan akaingiza bao lengine na kuyafanya matatu dhidi ya moja kabla ya kipindi cha mapumziko.
Bao lengine la penalti liliingizwa na Sulley Muntari na kuyafanya manne.
Christian Atsu naye alipata fursa na kuopnyesha nyota yake kwa kuingiza bao lengine huku akiiweka Ghana kifua mbele na kudhibiti mechi.
Mechi hiyo, ilikuwa imesemekana kuwa ngumu kwani timu hizo mbili zina wachezaji wazuri sana
Lakini kwa sasa ni kama wazi kuwa Black Stars wa Ghana wataabiri ndege ya kwenda Brazil baada ya ushindi wao mkubwa mjini Kumasi.
Hali ya wasiwasi ilijitokeza kabla ya mechi huku Ghana ikilalamikia FIFA kuwa inahofia kucheza mechi hiyo mjini Cairo kutokana na hali ya kisiasa ilivyo nchini Misri.
Huku ikiwa bado haijulikani mechi ya marudio itakochezwa, nia ya Ghana ilikuwa kupata alama nzuri zaidi ya Misri, nyumbani na hivyo ndivyo ilivyofanyika.

Afueni ya muda kwa serikali ya Obama,Yanusurika kuondolewa madarakani

                               Wabunge wa bunge la waakilishi
Baraza la Congress nchini Marekani, limepitisha mswaada utakaowezesha serikali kuendelea ma majukumu yake ya kifedha na kuongeza muda wake wa kulipa madeni yanayoikabili.
Hatua hii imekuja masaa kadhaa kabla ya serikali kutumbukia kwenye mkwamo wa kifedha.
Baraza la senate lenye waakilishi wengi wa Democtrats lilishinda kura ya mswaada huo kwa kura 81 dhidi ya 18
Mswaada ulipitishwa kwa kura 285 dhidi ya 144 katika bunge la waakilishi ambapo wabunge wa Republican waliunga mkono mswaada huo shingo upande.
Afueni hii kwa serikali ya Rais Barack Obama imekuja masaa kadhaa kabla ya makataa ya kuongeza kiwango cha deni la serikali hadi dola trilioni 16.7.
Mswaada huo sasa utawezesha serikali kuendelea na majukumu yake ya kifedha na hata kuomba pesa zaidi kutoka katika hazina ya serikali hadi Februari tarehe saba.
Pia itawezesha serikali kupata pesa hadi Januari kumi na tano na kufungua mashirika ya kifedha katika majimbo na kuwaresha kazini maelfu ya wafanyakazi wa serikali.
Ikulu ya White house sasa imewataka wafanyakazi wa umma kurejea kazini leo.
Mswaada huo hata hivyo ni afueni ya muda na sio suluhu kwa matatizo ya bajeti ya serikali ambayo yaliwagawanya wanasiasa wa Republican na Democrats.
Baada ya mswaada kupitishwa, Rais Barack Obama aliwaambia waandishi wa habari kuwa atasaini mswaada huo na kuufanya sheria.

Mfumo wa kupanga alama kidato cha 4 na 6 kubadilishwa

Ikiwa yamebaki majuma machache wanafunzi wa kidato cha nne waanze mtihani wa wa taifa, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iko kwenye mchakato wa kubadilisha mfumo wa upangaji za mitihani ya sekondari na matumizi wa alama za maendeleo ya mwanafunzi (Continuous Assessment (CA).
Mfumo huo ambao unatarajiwa kuanza kutumika kwenye Mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka huu, unakuja ikiwa ni miezi michache tangu Tume ya Waziri Mkuu iliyoundwa kuchunguza chanzo cha kufeli kwa maelfu ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012.
Akizungumzia mchakato huo, Kamishna wa Elimu Profesa Eustella Bhalalusesa alisema kwamba hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni sehemu ya kuboresha elimu na kuwa haina uhusiano na taarifa ya tume iliyoundwa na Waziri Mkuu ambayo mpaka sasa haijawekwa hadharani.
“Mambo yanakwenda yanabadilika hata binadamu yeyote anabadilika kila siku, mfumo unaotumika sasa hivi ni wa siku nyingi,” alisema.
Alisema kuwa, ili kuweza kuboresha vyema mfumo huo wameshirikisha wadau mbalimbali zikiwamo shule za sekondari.
“Kama unataka kuboresha lazima upate maoni, lengo letu ni kushirikisha shule zote za sekondari za Tanzania, ila siwezi kukuhakikishia kama zote zitashiriki kwa kuwa tunawatumia zaidi maofisa elimu mkoa na wilaya. Tumeweka pia dodoso kwenye mdandao ili watu zaidi washiriki.
Kuhusu tume ya Pinda hapa haihusiki kabisa, ile ilikuwa na mambo yake, hata bila ile tume sisi hii tungefanya tu,” alisema Profesa Bhalalusesa.
Alisema kuwa, mpaka sasa wameshapokea zaidi ya asilimia 60 ya maoni hayo kutokana na lengo walilo jiwekea.
Dodoso hilo ambalo pia Mwananchi imefanikiwa kuliona, linasema kuwa serikali inakusanya maoni ya wadau wa elimu kuhusu Upangaji wa Viwango vya Alama (Grade Ranges) katika mitihani ya kuhitimu kidato cha nne na cha sita pamoja na matumizi ya ‘Alama Endelevu ya Mwanafunzi [Continuous Assessment (CA)].
“Serikali imeamua kukusanya maoni haya kwa sababu kwa muda mrefu sasa upangaji wa viwango vya alama vinavyotumika katika mitihani ya kuhitimu kidato cha nne na kidato cha sita havifanani pamoja na kwamba mitihani hiyo yote ni ya elimu ya sekondari.
Pia mfumo wa elimu ya sekondari umekuwa na miundo tofauti ikiwemo ule unaotumika shuleni na ule wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta),” sehemu ya dodoso inasema.
Dodoso hilo linafafanua kuwa, muundo wa kwanza ni ule wa shule ambao alama mgando (Fixed Grade Ranges) ambao alama zinazotumika kupanga madaraja: A = 81 – 100; B = 61 – 80; C = 41 – 60; D = 21 – 40 na F = 0 – 20.

Muundo wa pili ulioidhinishwa kutumiwa na Necta kuanzia mwaka 2012 ni Upangaji wa Alama Mgando usiobadilika (Fixed Grade Range).
Kwa kidato cha nne alama zilizotumika ni A = 80 – 100, B = 65 – 79, C = 50 – 64, D = 35 – 49 na F = 0 – 34.
Kwa upande wa kidato cha sita alama zilizotumika ni A = 80 – 100; B = 75 - 79; C = 65 – 74; D = 55 – 64; E = 45 – 54; S = 40 – 44 na F = 0 – 39.
Kwa mujibu wa dodoso hilo, alama zinazopendekezwa ni A = 81 – 100, B = 61 – 80, C = 41 – 60, D = 21 – 40 naF = 0 - 20.
Utaratibu mwingine ambao washiriki wanapaswa kuchagua ni A = 80 – 100, B = 65 – 79, C = 50 – 64, D = 35 – 49 na F = 0 – 34 huku utaratibu wa tatu ukiwa A+ = 91 – 100, A = 81 – 90, B+ = 71 - 80, B = 61 - 70, C+ = 51 – 60, C = 41 – 50, D+= 31 – 40, D = 21 – 30, E = 11 – 20 na U = 0 – 10.
Akisoma Kauli ya Serikali Bungeni kuhusu Taarifa ya Awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wiliam Lukuvi alisema kuwa matokeo yaliyotangazwa awali na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi yafutwe na yapangwe tena kwa kutumia mfumo uliobadilika mwaka 2011 kama ilivyopendekeza tume ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Hata hivyo, baada ya kufutwa kwa matokeo hayo na kupangwa upya, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa utaratibu uliotumika kupanga matokeo hayo mapya ni uleule uliotumika kuandaa matokeo yaliyofutwa wa Fixed Grade Ranges.
“Kuanzia sasa matokeo ya mtihani ya kidato cha nne na sita yatachakatwa kwa kutumia Fixed Grade Ranges na Standardization (alama zisizobadilika na kuuwisha alama za mitihani),” alisema Kawambwa.