Saturday, November 1, 2014

WAZIRI WA FEDHA WA MAREKANI AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WATU MBALIMBALI DAR


Waziri wa fedha wa Marekani, Jacob J. Lew, akiwa katika picha ya pamoja na askari waliotekeleza ulinzi wakati wa ziara yake hapa nchini. Hapa ilikuwa muda mfupi baada ya kabla ya kuondoka jijini Jumanne jioni kwenye hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro Hotel, jijini Dar es Salaam.
Lew akiwa katika picha ya pamoja na madereva
Lew akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa ubalozi wa Marekani hapa nchini kutoka kitengo cha habari na mahusiano ya umma
Lew akiwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi (CP), Suleiman Kova, kwenye hoteli ya Hyatt Regency, saa chache kabla ya ,kuondoka jijini Dar esw Salaam, mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku moja iliyuojadili pamoja na mambo mengine, mahusiano ya kiuchumi baina ya Marekani na Tanzania pamoja na mradi wa Rais Barack Obama wa Power AfricaPicha kwa hiosani ya K-VIS

Jen.Traore ajitangaza rais Burkina Faso


Jenerali Honore Traore mkuu wa jeshi la Burkina Faso aliyejitangaza rais mpya wa nchi hiyo
Mkuu wa Jeshi la Burkina Faso Jenerali Honore Traore sasa amejitangaza kuwa rais baada ya aliyekuwa rais wa Burkina Faso Blaise Compaore kutangaza kujiuzulu.
Jenerali Traore ameshinikizwa na waandamanaji ambao walikuwa wanamtaka kuchukua usukani baada ya kuondoka kwa Bwana Compaore.
Bwana Compaore amesema kuwa amekubali kuondoka madarakani ili kutii matakwa ya waandamanaji ambao hawamtaki kuendelea kuongoza taifa hilo hata baada ya kutawala kwa miaka 27.
Bwana Compaore sasa ametaka uchaguzi mpya wa urais ufanyike baada ya siku 90.
Awali msemaji wa jeshi alikuwa amewaambia waandamanaji kuwa bwana Compaore hayuko tena madarakani huko Ouagadougou.
Maelfu ya waandamanji walikuwa wamerejea mabarabarani kwa siku ya pili
Hata hivyo hakubaini ikiwa afisa huyo wa kijeshi alikuwa akizungumza kwa niaba ya jeshi lote.
Jeshi lilisema kuwa litafanya mkutano na waandishi habari.
Siku ya Alhamisi waandamanaji waliokuwa wamekasirishwa na jitihada za rais za kuongeza muda wa uongozi wake baada ya kutawala kwa miaka 27 waliteketeza jengo la bunge na kuvamia kituo cha televisheni ya taifa.
Bwana Compaore alitupilia mbali jitihada za kubadilisha katiba ambayo ingemruhusu kuwania tena muhula mwingine kama rais lakini akasema kuwa angebaki madarakani kwa mwaka moja zaidi.
Chanzo bbc.

Boko Haram lawaoza wasichana wa Chibok



Wasichana wa Chibok waliodaiwa kuozwa na Boko Haram.kundi hilo limekana kuafikiana na serikali ya Nigeria
Kundi la wanamgambo wa Boko Haram nchini Nigeria limekana madai kutoka kwa serikali ya Nigeria kuwa wameafikia makubaliano.
Akizungumza kwa njia ya kanda ya video, kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau alisema kuwa zaidi ya wasichana 200 waliotekwa nyara kutoka eneo la Chibok kaskazini mwa Nigeria wamebadili dina na kuwa waislamu na kwamba wameolewa.
Abubakr Shekau
Shekau amasema kuwa hakujakuwa na majadiliano yoyote na serikali ya Nigeria.
Kiongozi huyo wa Boko Haram pia alitumia ujumbe huo kuthibitisha kuwa wanamshikilia raia mmoja mjerumani ambaye anakisiwa kuwa mwalimu aliyetekwa nyara mwezi Julai.
Serikali ya Nigeria inasema kuwa mazungumo na kundi Hilo yanaendelea kwenye nchi jirani ya Chad.

Sunday, June 8, 2014

KAMA HAUKUPATA NAFASI YA KUTAZAMA PICHA ZOTE ZA HARUSI YA MH JOSHUA NASARI ILIVYOFANA..HIZI HAPA


Msafara wa gari chache majira ya saa 2:30 ulianza safari katika viwanja vya Usa-River ambako gari za maharusi zilikuwa zikipambwa mdogo mdogo zikapanda Kilima zikiwa na maharusi Joshua Nassari na Anande Nnko safari ilikuwa ni kanisa la Kipentekoste la Kilinga,Meru tayari kwa ajili ya Ndoa.
Hatimaye Bw Harusi Joshua Nassari anateremka katika usafiri wake aina ya Range Rover muda mfupi baada ya kufika katika viwanja vya kanisala la Kilinga maarufu kama kwa Mchungaji Babu.

waheshimiwa kibao walikwepo.


Photo: And more

Hawa walikwepo ili kunogesha wa kwanza kulia ni Jessica Paul na marafiki zake

Wageni mbalimbali walihudhuria ibada hiyo ya ndoa mmoja wapo ni huyu ,Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai(katikati)
Bibi Harusi Anande Nnko alikuwa ni mwenye furaha kila wakati ,"Full Tabasamu."
Wenyeji katika shughuli hiyo akiwemo mzee Samweli Nassari ,baba mzazi wa Jishu walikuwa wamevalia mavazi nadhifu aina ya suti wakingojea ugeni uliokuwa ukiwasili katika kanisa la Kilinga.
Hataimaye Bw Harusi Joshua Nassari akaingia kanisani yeye na wapambe wake na hapa anaye ngojewa ni Bibi Harusi Anande Nko.
Bi Harusi Anande Nko akashuka katika gari alilokuja nalo aina ya Land Cruser VX.
Bwaa Harusi Joshua Nassari akamvisha pete mkewe Anande Nnko.
Bibi Harusi Anande Nnko akamvisha pete mumewe Joshua Nassari
Kisha Maharusi wakapongezana.
Maharusi wa wakawekewa mikono na Maskofu wakiongozwa na Askofu mkuu wa kanisa la Pentekoste Tanzania (PCT) David Batenzi.
Maharusi wakiwasalimia waumini waliohudhuria ibada hiyo (hawapo pichani)
Maharusi wakionesha pete zao za ndoa muda mfupi baada ya kuvishana.
Uthibitsho wa ndoa ni vyeti vya ndoa ,na hapa maharusi wakitia saini katika vyeti vyao.
Wagebi mbalimbali walihudhuria ibada hiyo ,na hapa ni mbunge wa Viti maalum Lucy Owenya (wa kwanza)
"Mmetuona "ni kama ndio maneno yaliyokuwa vichwani mwao maharusi ,Joshua Nassari na Anande Nnko wakionesa vyeti vyao vya ndoa.
Gavana wa kwanza wa Tanzania Mzee Edwin Mtei na Mama Mtei pia walikuwa katika inada hiyo.
Wazazi wa Maharusi ,Joshua Nassari na Bi Anande Nnko.
Bw na Bi Joshua Nassari na wakiweka Sadaka zao katika kapu la sadaka.
Maharusi ,wakapata nafasi ya kusalimiana na Mzee Edwin Mtei.
Ibada ya ndoa ikawa imefika tamati na maharusi wakatoka kanisani tayari kwa msafara wa magari kuelekea uwanjani

Saturday, June 7, 2014

Panone FC na safari ya mafanikio ya soka

TIMU ya soka ya Panone FC ‘Matajiri wa Moshi’, ndio mabingwa wa Mkoa wa Kilimanjaro msimu wa 2013/2014, wakipokea kijiti kutoka kwa Machava FC.
Tangu Panone wajitwalie taji Machi 30 kwa kuwafunga Machava bao 1-0 katika mechi ya aina yake iliyochezwa Uwanja wa Ushirika, wamekuwa gumzo kubwa kwa wapenzi na mashabiki wa soka.
Lakini, wengi wamekuwa wakijiuliza timu hii imetokea wapi. Ni timu iliyoanzishwa mwaka 2011, ikiundwa na mafundi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha mafuta cha Kampuni ya Panone Co. Ltd, kilichopo Weruweru, wilayani Hai.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Simon Kajaus, ilianzishwa na mafundi wajenzi yeye akiwa ndiye fundi mkuu kwa wakati huo, kwa lengo la kujiepusha kufanya mambo yasiyofaa baada ya saa za kazi.
“Klabu hii ilianza kama utani tu mwaka 2011, tulikuwa ni mafundi katika kituo cha mafuta pale Weruweru, mimi na wasaidizi wangu tuliona badala ya kutumia muda mwingi kufanya mambo yasiyofaa baada ya kazi, ni bora tufanye mazoezi,” anasema Kajaus.
Anasema wakati huo wakiwa wachache, waliamua kutumia boya la tenki ya maji kama mpira ambapo baada ya wiki moja, wakaamua kuchangishana na kununua mpira wa miguu wa watoto.
“Tulianza kwa kutumia boya kama mpira, baada ya wiki moja lile boya lilipasuka, ndipo tukaamua kuchangishana shilingi elfu moja kila mmoja kupata fedha ya kununulia mpira, tulinunua mpira wa watoto,” anasema.
Kuhama uwanja/kupata uongozi
Kajaus anasema baada ya timu kukua waliamua kuchangishana na kupata kiasi cha shilingi 35,000 za kununua mpira wa wakubwa pamoja na kuhamia uwanja mkubwa wa Kimashuku Mnadani, kutokana na wingi wa wachezaji na ubovu wa eneo la awali.
“Baadae timu ilianza kukua kutokana na kuongezeka kwa wachezaji kwani hata vijana wa mitaani, waliamua kujiunga nasi,” anasema.
Baada ya kuhama, wakapata wazo la kuweka uongozi wa muda ambapo Kajaus akateuliwa kuwa mwenyekiti, kocha wa timu akawa Ayubu Joel chini ya unahodha wa Bahati Naligiga akisaidiwa na Michael Stewart.
Mechi ya kwanza
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Panone, Augustino Hess, ambaye pia ni mmoja wa wachezaji waanzilishi, baada ya kuona kikosi kimekamilika, waliamua kutafuta mechi ya kwanza ya majaribio kujua uwezo wao halisi dimbani.
Anakumbuka kuwa mechi yao ya kwanza ilikuwa dhidi ya Kimashuko FC ya kijijini hapo na kufungwa 7-3.
Anakiri kuwa pamoja na kipigio hicho, hawakuweza kukata tamaa ya kusonga mbele katika kupigania mafanikio wakitambua mwanzo ni mgumu.
“Kipigo hicho hakitukatisha tamaa, tulicheza mechi nyingine ambayo tulishinda 4-0, baadae tukapata moyo wa kuendelea mbele kwa kuomba kucheza na timu zenye uwezo zaidi ikiwemo dhidi ya Lambo FC, bingwa wa Wilaya ya Hai wakati huo, lakini tulifungwa, tulifungwa 6-4,” anasema Hess.
Walianza kufanya usajili kuimarisha kikosi baada ya kipigo hicho wakichukua vijana mitaani na kuwapa ajira, na katika usajili huo waliwanasa nyota kama Elia Massawe, Ali Muya na Omari Miraji.
“Desemba 2011 tulifanya usajili na tukaomba mechi na Deca Flower na tukashinda 3-1, yakifungwa na Simon Kajaus na Elia Massawe aliyefunga mawili,” anasema Hess na kuongeza: “Tukaomba mechi dhidi ya Machame United ambayo tulichezea eneo la Mkomwasi, tukashinda 4-2.”
Baada ya hapo, Panone ilicheza mechi nyingine za kirafiki ndani na nje ya Mkoa wa Kilimanjaro chini ya kocha mpya Vitalis Shamuhelo kutoka Lambo FC.
Hess anakumbuka mechi ya kwanza kwao wakiwa katika jezi rasmi za kuuzia mafuta, ilikuwa dhidi ya Selian FC ya Arusha walipofungwa mabao 3-2.
Safari ya ubingwa
Meneja wa Kanda wa Kampuni ya Panome, Gido Marando, anasema baada ya uongozi wa kampuni kupata taarifa za timu hiyo, Mkurugenzi wake Patrick Ngiloi, aliongeza nguvu kwa kumwajiri kocha Atuga Manyundo akitokea AFC ya Arusha akisaidiwa na Shamuhelo.
Marando anasema waliweka timu kambini pamoja na kuendesha mchakato wa kupata uongozi mpya kwa lengo la kusuka kikosi hicho tayari kwa Ligi Daraja la Nne msimu wa 2012/2013.
Katika  uchaguzi huo, Kajaus aliendekea kuwa mwenyekiti wa klabu hiyo hadi sasa huku makamu wake akiwa Habibu Ali, Katibu Mkuu Hess, Katibu Msaidizi ni Ramadhani Hussein na Mhazini ni Carolyn James.
“Baada ya mafanikio kuwafikia mabosi wetu, Mkurugenzi na Meneja wa Kanda, walifurahia na kuanza kutusapoti ambapo mwanzoni mwa mwaka 2013, Mkurugenzi alimuajiri Kocha Atuga Manyundo kutoka AFC ya Arusha akisaidiwa na Vitalis Shamuhelo,” anasema Hess.
Walipoingia Ligi Daraja la Nne Wilaya ya Hai, wakajitwalia tiketi ya kucheza Ligi Daraja la Tatu ngazi ya mkoa, lakini wakitolewa katika hatua ya awali baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye kundi lao; nyuma ya Polisi Kilimanjaro na Kitayosce SC.
Mwaka huo walishiriki mashindano mengine kadhaa ikiwemo Bonanza ya Elimu ya Watu Wazima mkoani Arusha na kutwaa ubingwa kabla ya kumaliza nafasi ya tatu kati ya timu 20 katika michuano ya UVCCM.
Ubingwa wa Mkoa
Msimu huu ndipo wamefanya makubwa katika historia yao wakifanikiwa kutwaa ubingwa wa mkoa dhidi ya Machava FC.
Katika mechi ya kwanza, Panone walifungwa 2-1, lakini kwa kanuni za usajili za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Panone walimkatia rufaa mchezaji Tony Kingunda wa Machava FC na kufanikiwa kupewa ushindi wa pointi tatu na mabao mawili.
Katika mechi ya pili, walikutana na Lang’ata bora, mechi iliyopigwa katika uwanja wa Cleopa Msuya, Mwanga, wakatoka sare ya bao 1-1 kabla ya kuibamiza Kilototoni FC 5-1; wakimalizia safari hiyo kwa sare ya bila kufungana dhidi ya Kitayosce SC.
Katika raundi ya timu 10 za mwisho, Panone FC ilipangwa katika kundi la kifo dhidi ya Machava FC, Kilimanjaro FC, New Generation na Forest FC ya Siha.
Kwenye mechi ya kwanza, walicheza na New Generation na kushinda 1-0 kabla ya kuichakaza Kilimanjaro FC 4-0.
Mchezo wa tatu katika hatua hiyo, Panone ilicheza na Machava na kushinda 1-0 kabla ya kumalizia hasira zao kwa Forest kwa kuichakaza 3-0 na kufanikiwa kuongoza kundi wakiwa na pointi 9.
Panone ilianza mzunguko wa kwanza wa hatua ya lala salama hatua ya sita bora ilikokuwa na timu za Machava, New Generation, Afro Boys, Agip Kahe, Polisi Kilimanjaro kwa kishindo, baada ya kuitandika Agip Kahe bao 1-0.
Mechi ya pili, Panone ilikutana na Afro Boys ikashinda 3-0 kabla ya kutoka sare ya bila kufungana na Polisi Kilimanjaro na baadae kutoa kipigo cha bao 1-0 kwa New Generation; mechi ambayo ilivunjika kutokana na vurugu, hivyo wao kuzawadiwa ushindi.
Katika mechi ya mwisho mzunguko wa kwanza, Panone FC iliwafunga Machava FC 1-0 katika dimba la Ushirika, hivyo kumaliza na pointi 13.
Kwenye raundi ya pili ya hatua hiyo, Panone FC ilikutana na Agip Kahe wakishinda 2-0 na kutoka sare ya 2-2 dhidi ya Afro Boys kabla ya kuvunja rekodi ya mkoa kwa kubeba ubingwa wakiwa na pointi 20, baada ya kuifunga Polisi Kilimanjaro bao 1-0.
Mechi mbili zilizofuata, Panone ilipoteza kwa kipigo cha 1-0 dhidi ya New Generation na kushinda nyingine dhidi ya Machava ambapo ilishinda 1-0 katika mechi kali iliyochezwa Uwanja wa Ushirika

Silinde apigania Tunduma kuwa na mamlaka kamili

MBUNGE wa Mbozi Magharibi, David Silinde (CHADEMA), ameitaka serikali ieleze ni lini mji mdogo wa Tunduma utakuwa na mamlaka kamili kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Silinde alisema kuwa mwaka 2011 serikali ilikubali kuwepo kwa kata 14 katika mji ndogo na kwa sasa kuna Mkurugenzi, lakini bado haijawa na mamlaka kamili.
“Naomba serikali ieleze ni lini mji wa Tunduma utakuwa na Mamlaka kamili kwa kuwa tayari zimeishatengwa kata 14 na kuna Mkurugenzi,” alihoji Silinde.
Katika swali la msingi, mbunge wa Karagwe, Gosbert Blandes (CCM), alitaka kujua ni lini kata za Kiruruma na Nyakahanga zitagawanywa kwa kuwa ni kubwa ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa sera ya serikali ya kupunguza ukubwa wa kata na vijiji, ili kurahisisha maendeleo.
Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na  Serikali za Mitaa (Tamisemi), Kasim Majaliwa, alisema ili mji huo uwe na mamlaka kamili ni lazima kuwepo na madiwani katika kata zote 14 tofauti na sasa ambapo yupo diwani mmoja.
Akizungumzia kuhusu kugawa kata na vijiji katika wilaya ya Karagwe ambavyo ni Karuruma na Nyakahanga, alisema vijiji hivyo vinatakiwa kugawiwa kwa mujibu wa sheria husika.
Alisema kata ya Nyakahanga ina wakazi 20,284 na Kata ya Kiruruma inakadiliwa kuwa na wakazi 34,945 kwa mujibu wa sensa na makazi ya mwaka 2012.
Majaliwa alisema kuhusu kugawa kata hizo, Waziri mwenye dhamana na serikali za Mitaa atazigawa kata hizo sambamba na maombi kutoka katika halmashauri nyingine kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa kufanyika.

DCI amkwepa Kibanda

MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Isaya MunguluMKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Isaya Mungulu, amekwepa kuzungumzia sakata la kutekwa, kuteswa, kutobolewa jicho na kukatwa kidole kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini, Absalom Kibanda.
Hali hiyo ilitokea jana, wakati Mungulu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo mwandishi wa gazeti hili alimtaka aeleze uchunguzi wa sakata la Kibanda umefikia wapi hadi sasa.
Tangu Kibanda atendewe unyama huo, Machi mwaka jana, hakuna mtuhumiwa aliyekamatwa, na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu na Makao Makuu wamekuwa na majibu ya kukinzana.
Huku akijibu kwa kubabaika na akitaja sakata jingine la Dk. Stephen Ulimboka aliyetendewa unyama kama huo Juni mwaka 2012, Mungulu alisema: “Suala la Kibanda ni suala la ghafla, siwezi kulisemea kwa sasa.”
Vile vile Mungulu alikwepa kujibu swali jingine kuhusu malalamiko ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, aliyedai kuna askari walioshirikiana na wezi bandarini kuiba shaba kwa kutumia kichwa cha treni ya Tazara.
“Kwa suala la askari waliotuhumiwa kuiba naomba aulizwe Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ndiye mwenye askari hao,” alisema Mungulu.
Tanzania Daima lilimtafuta Kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova, ambaye alisema bado halifahamu, na kwamba itabidi asubiri kuona taarifa hiyo iliyoripotiwa ili aweze kuita mkutano na waandishi kulifafanua.
Awali Mungulu alizungumzia operesheni ya wakati mmoja kwa nchi za Afrika Mashariki, na nchi za Kanda ya Kusini mwa Afrika, iliyofanya Mei 29 na 30 mwaka huu.
Alisema operesheni hiyo imetokana na maamuzi yaliyofikiwa kwenye mkutano wa wakuu wa majeshi ya polisi wa kanda zote mbili ulioandaa kikao kilichowakutanisha wakuu wa upelelezi wa nchi hizo.
Katika kikao hicho kilichofanyika Machi 13 -14 nchini Namibia, suala la usafirishaji wa binadamu na wahamiaji haramu, dawa za kulevya, wizi wa magari, makosa ya wanyama pori, silaha haramu, usafirishaji wa madini na wizi wa nyaya za shamba ndiyo yalipewa kipaumbele.
Alisema kuwa kwa upande wa Tanzania baada ya operesheni hiyo, usafirishaji haramu wa binadamu ulipata wahamiaji 84, ambapo 77 waliotoka Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo 7.
“Polisi wa Tanzania walikamata heroine gramu 5, bangi gramu 8 na misokoto 195, huku mirungi ikipatikana ya kilogram 200

Friday, February 21, 2014

Facebook buys WhatsApp in $16bn deal to target teens and boost messaging service Read more: http://www.dailymail.co.uk/sciencetech/article-2563379/Facebook-buys-WhatsApp-16bn-deal-attract-teens-boost-messaging-service.html#ixzz2txH1gNbf Follow us: @MailOnline on Twitter | DailyMail on Facebook


  • Social network will pay $12 billion in Facebook stock and $4 billion in cash
  • App's founders and employees will be granted $3 billion in Facebook stock
  • App and brand will continue in same way as Instagram

  • Facebook is buying mobile messaging service WhatsApp for up to $19 billion in cash and stock in the firms biggest ever acquisition.

    The world's biggest social networking company said that it is paying $12 billion in Facebook stock and $4 billion in cash for WhatsApp.
    In addition, the app's founders and employees will be granted $3 billion in restricted stock that will vest over four years after the deal closes.
    Boom: The free instant messaging service created in 2009 has grown faster than Facebook in its five years, and now has more than 450million monthly users around the world
    Boom: The free instant messaging service created in 2009 has grown faster than Facebook in its five years, and now has more than 450million monthly users around the world

    WHATSAPP IN NUMBERS

    Over 450 million people using the service each month
    Firm has 50 employees
    70% of those people active on a given day;
    Messaging volume approaching the entire global telecom SMS volume
    Service adds more than 1 million new registered users per day
    600m photos uploaded each day
    200m voice messages sent each day
    Facebook says it is keeping WhatsApp as a separate service, just as it did with Instagram, which it bought for about $715.3 million.
    'The acquisition supports Facebook and WhatsApp's shared mission to bring more connectivity and utility to the world by delivering core internet services efficiently and affordably,' the social network said.
    WhatsApp has more than 450 million monthly active users. In comparison, Twitter had 241 million users at the end of 2014.
    Facebook CEO Mark Zuckerberg says WhatsApp is on path to reach a billion users.
    'The combination of WhatsApp and Facebook will allow us to connect many more people round the world,' Zuckerberg said.
    'We want to develop more mobile experiences like Instagram and Messenger.
    'WhatApp fits this vision perfectly, it has incredibly strong engagement and growth.'
    'It's the only app we've ever seen that has grown more quickly than Facebook itself.'
    'Their product roadmap is very exciting and won't change.
     
    'Overall, I'm very excited about this deal.
    'WhatsApp had every option in the world, so I'm thrilled they chose us.'
    As part of the deal, WhatsApp co-founder and Chief Executive Jan Koum will join Facebook's board, and the social network will grant an additional $3 billion worth of restricted stock units to WhatsApp's founders, including Koum.
    Boost: WhatsApp is still growing and is predicted to have a billion users soon
    Boost: WhatsApp is still growing and is predicted to have a billion users soon

    THE WHATSAPP FOUNDERS WHO WERE REJECTED FOR JOBS AT FACEBOOK

    Brian Acton

    The sale of WhatsApp to Facebook for $19 billion has made its founders Jan Koum and Brian Acton billionaires overnight. 
    But they are not your typical Silicon Valley entrepreneurs. Success came to them late. The pair were well over 30 when they launched their messaging app in 2009.
    The duo stand out in Silicon Valley for their unusual approach. They both hate advertising and have paid for almost no marketing to make the five-year-old app a success.
    This may be because 37-year-old Koum and 42-year-old Acton had unusual backgrounds. Koum was born and raised in a small village outside of Kiev, Ukraine.
    Growing up, his home had no electricity or hot water. His parents, a housewife and a construction manager, avoided talking on the phone in case it was tapped by the state.
    Jan Koum

    Koum and his mother immigrated to Mountain View when he was 16. By 18, Koum had taught himself computer networking by buying manuals from a used book store and returning them when he’d finished.
    In 1997, Koum took a job at Yahoo sitting across a desk from Acton. They hit it off, because they enjoyed each others straight-down-the-line style. 
    Twitter

    Michigan-born Acton studied engineering at the University of Central Florida and graduated in 1988. In May, 1992 he got a job at Rockwell International as systems administrator.
    Acton became Yahoo employee 44 in 1996, worked as software engineer, then senior software engineer, principal software engineer and director of engineering.
    The pair stayed with Yahoo for over a decade building their bond through games of ultimate frisbee.  In September 2007 Koum and Acton finally left Yahoo.
    They both applied to Facebook and were rejected. Instead they decided to set up their own venture, Whatsapp, now sold to Facebook for billions.
    According to reports, the success of Whatsapp hasn’t changed Koum or Acton. When a journalist visited the company's headquarters in July 2012, the Koum was barefoot and Acton was sporting flip-flops.

    'This is an incredible moment for me,' Mr Koum said.
    'Every day over 19bn messages are sent, with over 1m new users every day.
    'We wanted it to be simple, and a better service than SMS.'
    'We're excited and honoured to partner with Mark and Facebook as we continue to bring our product to more people around the world,'
    'WhatsApp's extremely high user engagement and rapid growth are driven by the simple, powerful and instantaneous messaging capabilities we provide.'
    The deal instantly makes WhatsApp cofounders Jan Koum and Brian Acton billionaires.
    Forbes estimates that Koum held about a 45% stake in the company, while Acton’s stake was over 20%.
    Proud moment: Jan Koum, pictured at a digital conference in January, described the deal as 'incredible'
    Proud moment: Jan Koum, pictured at a digital conference in January, described the deal as 'incredible'

    Facebook promised to keep the WhatsApp brand and service, and pledged a $1 billion cash break-up fee were the deal to fall through.
    WhatsApp will remain based in Mountain View, Calif., and Facebook said its own messenger app and WhatsApp's core messaging product will continue to operate as separate applications
    Shares in Facebook slid 5 percent to $64.70 after hours, from a close of $68.06 on the Nasdaq.
    Facebook was advised by Allen & Co, while WhatApp has enlisted Morgan Stanley for the deal.
    The deal is the latest aquisition for Facebook, which last year bought Instagram.
    It also reportedly offered to pay close to $3 billion or more to acquire messaging service Snapchat, though that offer was spurned by the site's founders.
    WhatsApp in numbers
    WhatsApp in numbers

    Zuckerberg said WhatsApp would operate in the same way as Instagram, as a separate firm.
    'It would be pretty stupid of us to interfere,' he said.
    He also said he was not planning to put ads on the service.
    'Our strategy is to grow and connect people.
    'Once we get to 2-3 billion people there are ways we can monetise.
    'Now we want to focus on growing users. I don't think ads are the right way here.'
    Koum also pledged not to add ads to WhatsApp, which makes money from a subscription model.
    'We think advertising is not the way to go - we create a direct relationship with customers,' said Koum.
    'We want to make the product better, faster and more efficient.'
    Experts say the deal could help Facebook attract teens.
    Professor Will Stewart from the Institution of Engineering and Technology (IET) said: 'Obviously WhatsApp adds instant messaging to Facebook which must strengthen their position for the moment.
    'Equally, all app types rise and fade, so established social media formats like Facebook will be overtaken by something new, and picking up candidates that might have ultimately replaced them may be a good survival strategy for a while.
    'This does show the growing significance of mobile, though of course Facebook is on mobile anyway.
    'But, Facebook has been around a while now so the real question is what comes next?'

    Read more: http://www.dailymail.co.uk/sciencetech/article-2563379/Facebook-buys-WhatsApp-16bn-deal-attract-teens-boost-messaging-service.html#ixzz2txGuR2Fn
    Follow us: @MailOnline on Twitter | DailyMail on Facebook

    Katiba mpya mbadala yaandikwa mafichoni-


    Mwandishi WetuToleo la 337
    5 Feb 2014

    Maprofesa, majaji wachambua taarifa nyeti za Warioba
    CCM sasa kuingia Bunge la Katiba na rasimu mbadala
    WIKI takriban mbili kabla ya kuanza kwa Bunge la Katiba, mjadala wa muundo wa serikali tatu uliopendekezwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba mpya umeendelea kupasua vyama vya siasa, Raia Mwema ikielezwa kwamba Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeandaa rasimu mbadala ndani ya Bunge hilo la Katiba.

    Kwa mujibu wa habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili, CCM ni kama vile imetengeneza tume yake ya Katiba mpya inayoshikirisha jopo la maprofesa, majaji na baadhi ya wanasiasa.

    Kati ya taarifa wanazotumia kutengeneza rasimu hiyo mbadala ya Katiba ni viambatanisho vya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba, viambatanisho ambayo pia walikabidhiwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein.

    Mbali na hao wengine waliokabidhiwa viambatanisho hivyo sambamba na Rasimu ya Pili ya Katiba mpya ni viongozi wengine mbalimbali wa kitaifa, akiwamo Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro.

    Ndani ya ‘tume’ hiyo ya CCM aliyepata kuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG) Andrew Chenge, anatajwa kuwamo na inaelezwa kwamba, ‘tume’ hiyo inalenga kuibua mawazo mbadala na yale ya Tume ya Warioba, hususan muundo wa serikali tatu ndani ya Muungano.

    Tayari, Rais Jakaya Kikwete, katika hotuba yake wakati wa maadhimisho ya miaka 37 ya CCM mkoani Mbeya Jumapili iliyopita alisema msimamo wa CCM ni serikali mbili na anayewapinga anapaswa kuibua hoja mbadala zenye ushawishi na si kutumia mabavu, akisisitiza hoja hazifutwi kwa “kupigwa rungu” bali hufutwa kwa kutumia hoja mbadala zenye mantiki.

    “Kinachofanywa na CCM ni kutengeneza mawazo au mapendekezo mbadala yenye mantiki zaidi. CCM haing’ang’anii mwonekano wa sasa wa serikali mbili. Ndani ya mwonekano wa sasa kuna imani kwamba yapo mabadiliko yanayoweza kufanywa ambayo pia yanaweza kuungwa mkono na wapinzani, lakini ni mabadiliko ambayo si ya moja kwa moja kwenda kwenye serikali tatu kama ilivyopendekeza Tume ya Warioba,” kilieleza chanzo chetu cha habari.

    Inaelezwa kwamba huenda CCM ikaibua mawazo mbadala wa muundo wa serikali ambayo chanzo chetu cha habari kimeelezea mawazo hayo mbadala kuwa ni “mawazo ya kati, yasiyo na msimamo mkali kuhusu muundo wa Muungano.”

    Lakini wakati CCM ikiwa katika juhudi za kuingiza rasimu mbadala kwenye Bunge la Katiba, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinashikilia msimamo wa serikali tatu uliopendekezwa na Tume ya Jaji Warioba.

    Katika msimamo wake, CHADEMA hakina mapendekezo mbadala kuhusu serikali tatu, bali kinaungana na yale ya Tume ya Warioba, kama ilivyo kwa vyama vingine vya upinzani, hususan vyenye wabunge bungeni.

    Hali hiyo inajitokeza katika wakati ambao vyama hivyo vya siasa chini ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vikitaraji kukutana Februari kesho, kujadili nafasi yao katika Bunge la Katiba.

    Kwa mujibu wa taarifa ya Msajili wa Vyama, Jaji Francis Mutungi, vyama hivyo vitakutana kupitia chombo chao maalumu, kinachoitwa Baraza la Vyama vya Siasa, kikiwa ni chombo cha kisheria ambacho wajumbe wake ni viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa kutoka Tanzania Bara na Zanzibar walioteuliwa kuwakilisha vyama vyao.

    Katika hatua nyingine, duru za kisiasa kutoka Zanzibar zinaarifu kwamba tafsiri ya mambo kuhusu serikali tatu au serikali mbili imebadilika, baada ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa uwakilishi katika Jimbo la Kiembesamaki, ambako Mahmoud Thabit Kombo wa CCM ameshinda baada ya jimbo hilo kuachwa wazi kutokana na kufukuzwa kwa mwakilishi wa awali, Mansoor Himid.

    Vyanzo kadhaa vya habari vinabainisha kwamba uchaguzi huo ulibeba tafsiri kubwa kuhusu mijadala mizito ya kisiasa Zanzibar.

    Wengi wanasema ushindi wa Kombo ambao msingi wake ni wapiga kura wa ngazi ya chini na si safu ya viongozi wa juu pekee, tafsiri yake ni ushindi wa serikali mbili, ikielezwa kwamba Kombo ni muumini wa serikali mbili na alihojiwa na kuthibitisha hivyo katika Kamati Kuu ya CCM iliyoketi Zanzibar mwezi uliopita kwa ajili ya uteuzi wa mgombea wa jimbo hilo.

    Mansoor Himid aliyefukuzwa, aliweka wazi msimamo wake kwamba si tu serikali tatu, bali Zanzibar kuwa na mamlaka yake kamili, akitajwa kuungwa mkono na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

    “Matokeo ya uchaguzi huo mdogo maana yake ni kwamba watu wa chini hawana tatizo na hoja za aina ya serikali, bali hizi ni hoja za viongozi wa kitaifa tu. Uchaguzi huu ulikuwa na kambi mbili tofauti na ulikuwa kipimo mbele ya wananchi kwamba kambi ipi inakubalika.

    “Kambi ya kwanza ni ile iliyokuwa ya Mansoor. Na unapomwona Mansoor ni dhahiri Karume yupo. Lakini kambi ya pili ni Dk. Shein (Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein) na CCM kwa ujumla, ambamo wamo watu kama kina Seif Khatib na wengineo. Kambi hizi zilikuwa zikipimwa kwa hoja ya serikali tatu, ndani yake madai ya mamlaka kamili ya Zanzibar na nyingine ni hoja ya serikali mbili. Ushindi umekwenda kwa kambi ya CCM,” kilieleza chanzo chetu cha habari.

    - See more at: http://www.raiamwema.co.tz/katiba-mpya-mbadala-yaandikwa-mafichoni#sthash.aOGnCHBH.dpuf