Sunday, January 13, 2013

Swansea yailaza Chelsea 2-0



Wachezaji wa Chelsea baada ya kulazwa magoli 2-0 na Swansea
Michael Laudrup amakiri kuwa ushindi wa Swansea wa magoli mawili kwa bila dhidi ya Chelsea katika raundi ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la ligi, ulikuwa wa kushangaza.
Makosa yaliyofanywa na mlinda lango wa Chelsea Branislav Ivanovic ilisababisha Michu na Danny Graham kuifungia Swansea magoli hayo katika mechi iliyochezwa katika uwanja wa Stampford Birdge.
Raundi ya pili cha mechi hiyo itachezwa tarehe 23 mwezi huu katika uwanja wa nyumbani wa Swansea.
Chelsea ilithibiti mpira kwa asilimia kubwa lakini makosa hayo yaliyofanywa na Ivanovic yalisababisha matumaini ya Chelsea ya kufuzu kwa fainali za kombe hilo kudidimia.

Goli la Chelsea lakataliwa


Demba Ba
Mlinda lango huyo wa timu ya taifa ya Serbia alipokonywa mpira katika kipindi cha kwanza na kuipa Swannsea bao lake la kwanza bao ambalo pia ni la 16 kwa Michu msimu huu.
Katika dakika za mwisho za mechi hiyo Ivanovic vile vile akafanya kosa lingine la kupeana pasi, bila kumtizama mlinda lango mwenzake, na kuumpa nafasi Graham ya kufunga bao la pili.
Goli lililofungwa na mshambulizi wa Chelsea Demba Ba dakika ya tisini ilikataliwa na msaidizi wa refa ambaye alisema kuwa, Ba alikuwa ameotea.
Laudrup aliwapongeza wachezaji wake kwa kutumia fursa walizopata wakati wa mechi hiyo.
Mshindi kati ya Chelsea na Swansea atacheza na mshindi kati ya Aston Villa na Bradford City.

No comments:

Post a Comment