Thursday, January 31, 2013

Kufanya majukumu yako kunadumisha ndoa



Wanaume hata hivyo wanoonywa wasitumie utafiti huu kama kigezo cha kutowasaidia wanawake
Wanaume utafiti uliofanywa kwa watu waliooana nchini Marekani umebaini kuwa pale mme na mke wanapozingatia majukumu yao ya kitamaduni ndani ya nyumba huwa na maisha mazuri ya ndoa.
Utafiti huo ulihusisha wanandoa elfu nne na mia tano.
Ulibaini kuwa wakati wanawake wanapofanya kazi za kike pekee kama vile kupika na usafi na wanaume kufanya kazi za kiume kama vile kutengeneza gari na kupanga vitu kabatini hushiriki tendo la ndoa mara 1 nukta sita kwa mwezi zaidi ya wanaume wanaofanya kazi za kike.
Hata hivyo watafiti wamewaonya wanaume dhidi ya kutumia matokeo ya utafiti huu kama sababu ya kutowasaidia wanawake.
Wanasema hii inaweza kusababishha mzozo na pengine kupungua kwa muda wa kujamiiana.

No comments:

Post a Comment