Thursday, January 31, 2013

HAPA NDIPO ANAPOISHI MCHEZAJI MKENYA AMBAE MAN U INA MPANGO WA KUMSAJILI.


Victor Wanyama ni mchezaji wa Harambee Stars ambae pia anaichezea Celtic ya Scotland, hapa ndipo nyumbani anapoishi ndani ya mji wa Glasgow.
Mtandao wa Ghafla umeripoti kwamba mchezaji huyu amefanya kitendo cha kijasiri cha kukubali kuonyesha nyumba yake kupitia vyombo vya habari kitu ambacho mastaa wengi wa Kenya ni waoga kukifanya, yani huwa hawakubali kuonyesha wanapoishi.
Taarifa zilizosambaa kwa sasa na hata kuripotiwa na Supersport Blitz ni kwamba Club ya soka ya Manchester United inampango wa kumsajili staa huyu Mkenya.

No comments:

Post a Comment