Thursday, January 31, 2013

SIKUJUA KAMA MIALIKO YA HIZI TIMU KUCHEZA NA TAIFA STARS ILITOSWA NDIO IKACHAGULIWA CAMEROON.

.
January 30 2013 ndio nimefahamu kwamba kumbe timu za taifa za Congo Brazzaville, Equatorial Guinea, Rwanda na Swaziland ziliomba mechi ya kirefiki na timu ya taifa Taifa stars lakini zikatoswa.
Baada ya hizo timu za taifa kutoswa, iliyochaguliwa kucheza na Stars ni Cameroon katika mechi ambayo iko kwenye kalenda ya (FIFA) ya mechi za kirafiki zitakazochezwa kote duniani Februari 6 mwaka huu.
.
Hizo timu zote zilizotoswa kasoro Swaziland, zilikua zinataka hiyo mechi na Taifa stars ichezwe kwenye viwanja vya nyumbani kwao na sio hapa bongo lakini hii mechi ya Tanzania na Cameroon itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni.
Kikosi cha Cameroon kilichokamilishwa na wachezaji wengi wa kulipwa wanaocheza katika nchi mbalimbali duniani kitaanza kuwasili bongo Februari 3 mwaka huu ambapo pia TFF imesema Kocha wa Stars Kim Poulsen mwenyewe ndio alichagua stars ichezwe na Cameroon ambayocaptain wake ni staa Samuel Etoo.

No comments:

Post a Comment