Wednesday, January 16, 2013

Edward ngoyai lowasa na URAISI 2015-Fuatana na kamanda Jasiri Samweli Shami katibu Bavicha -Kahama

JE LOWASA NI MTU SAHIHI?
Ni mzee nguli katika siasa za fitina
Tanzania na afrika mashariki huku
akisifika kwa maamuzi magumu
anayoimba kila siku ilihali sijawahi
kuona maamuzi aliyowahi kuyatoa ilhali amekalia ofisi za uma kwa zaidi ya
nusu ya umri wake.
Aidha nijaribu kuainisha baadhi ya
matendo yake yenye utata ili
watanzania wanaorubunika kirahisi
wapate kuelewa aidha wakihamua wabaki na ushabiki ama wapone;-
1.Edward anatuhumiwa kwa kuchukua
maji kwa ubavu kutoka Arumeru na
kuyapeleka kusikojulikana [mito ya
maji 3 kwa kuyafukia kwenye
makalvat kina kirefu, pia yamewekewa patrol ya polisi ] ilihali akitoa tone na
kuyaelekeza kwenye kambi ya jeshi
monduli ili atumie fursa hiyo wanajeshi
wayalinde kwamba ni yao kumbe ni
kwa maslahi binafsi. Hapa tujiulize swali
inakuweje jeshi linalotumia kodi za watanzania lilinde maji ya lowasa?
Inakuweje askari polisi walinde maji
kwa maslahi siyo ya kitaifa ama jamii
bali ni uwekezaji wa lowasa? TAYARI
TULIMUAGIZA JOSH. NASSARI MB.
ALIFUATILIE LAKINI BADO HAJATOA JIBU.
2.RICHMOND – huu ulibainika ulikuwa
mradi wake akishirikiana na swahiba
wake kikwete ` `IF U HANDLE A
TERRORIST U ARE A TERRORIST TOO `` NI
KAULI YA WAMAREKANI. Tuhuma hii inamuangukia kutokana na kwamba
ndiye aliyekuwa na dhamana ya
shughuli za serikali na kushindwa
kuwawajibisha wahusika aidha kwa
kuwalinda wahuni hao pia naye uhuni
unakuwa sehemu ya maisha yake ama ndiye mwenye mradi moja kwa moja
maana hadi sasa RICHMOND ni
sintofahamu. YOTE KWA YOTE
ANAUTAKA URAISI WA TANZANIA
ANAYOTUHUMIWA KUIFILISI.
3.UJANGILI –edward anahusishwa na vitendo vya ujangili mkoani arusha na
manyara kupitia kivuli cha kampuni
yake LEOPARD TOURS YENYE MAGARI YA
CREAM Maana kuna LEOPARD TOURS
yenye magari meupe inamilikiwa na
tajiri wa kwanza nchini india mwenye hisa nyingi kwenye fast jet anaishi
JIJINI HYDRA MT. MUMBAMBEY- india. Hii
ni hatari kwa afya ya taifa letu endapo
tutamkubali mtu hatari namna hii
aitawale nchi yetu.
NYERERE ALISEMA `EDD IKIWA NIMEKUPA WIZARA YA MIFUGO
UMENIJENGEA MAGOROFA NA UKWASI
HUU JE NIKIKUPA NCHI ITAKUWEJE?
Watanzania wenzangu nachelea
kusema ikiwa kafanya haya akiwa
chini ya mtu je siku akiwa kileleni itakuweje?
4.GAMBA- Lowasa ,change na rostam
waliitwa magamba / wezi wa rasilimali
zetu siyo na shami bali na mkuu wan
chi,tena walitajwa na pius msekwa na
wakapewa siku tisini waachie ngazi jambo ambalo lisingetosha maana
ikiwa jinai imefanyika muhamuzi ni
mahakama, aghalabu hata hako
kaadhabu ka ubabaishaji
alikokabidhiwa nape kameishia mitini
amemalizia kwa kusema `JK HATUKUKUTANA BARABARANI`` Hivyo
ikadhihirisha kwamba madili wanapiga
wote kwa yamini. Bado huyu mtu
aliyetajwa kwamba ni mchafu leo hii
anaitia watu nyama wanajisahau na
kuanza kumuita jembe `POLE SANA MMA SHELUKINDO` KWA KUJITOA
FAHAMU……..
KWA HIYO MNATAKA KUSEMA GAMBA/
MWIZI APEWE NCHI AIONGOZE?
Watanzania mkiamua kufanya kinyesi
kwamba ni chakula sawa lakini hata mungu ataumia sana endapo mtajaribu
hili.
5.uadilifu, mzee huyu kwa orodha hii
chache suala la uadilifu ni sifuri ,ikiwa
anadiriki kutumia ofisi ya umma kwa
maslahi binafsi kama anavyotumia jeshi na polisi huko arumeru.
6. NGURDOTO MOTEL -kuna sintofahamu
kubwa juu ya umiliki wa hii hoteli
yenye kubeba maraisi 30 ndani ya
ikulu imara isiyoingiza bomu wala risasi
ambapo nimeifuatilia kwa uendeshaji wake inadaiwa kukwepa mapato na
shuru mbalimbali jambo ambalo
lilikuwa kwenye ilani yangu wakati
nilipokuwa natafuta kiti cha arumeru
mashariki.
Hili ni jambo hatari sana kwa ustawi wa taifa letu kwa kiongozi wa juu mwenye
ushawishi kufanya jambo kama hili nab
ado anahitaji uraisi. 7. PIA ANAHUSISHWA NA UMILIKI WA
ANAPA [ MOMELA NATIONAL PARK ]
inayomuingizia ukwasi bila kulipa kodi
kinyume na katiba ya nchi. IKIWA MNAHISI NIMEMUONEA
NIMETUMIA UHURU WANGU WA
KUHOJI ,KUDADISI NA NI JUKUMU LA
SERIKALI KUHAKIKISHA NAPATA HIZI
TAARIFA KWA WAKATI NA SIYO
KUNIPIGIA CM ZA VITISHO.LIWALO NA LIWE LAKINI HAKI YA WATANZANIA
ISIPOTEE.
`` KATIKA SUALA LA UKOMBOZI NI
LAZIMA WENGINE WAKUBALI KUWA
MBEGU`` WENU KAMANDA JASIRI
SAMWEL SHAMI KATIBU BAVICHA –
KAHAMA.

No comments:

Post a Comment