Maafisa wa serikali ya Japan,
wamesema kuwa wamewasilisha rasmi malalamiko yao, kwa balozi wa
Marekani, Mjini Tokyo, baada ya mwanajeshi mmoja wa Marekani kutuhumiwa
kumjeruhi kijana mmoja raia wa nchi hiyo.
Ripoti zinasema, mwanajeshi huyo aliiingia
katika chumba kimoja katika kisiwa cha Okinawa, ambako alimpiga mvulana
mmoja mwenye umri wa miaka 13.Mvulana huyo alianguka kutoka dirishani na alikimbizwa hospitalini.
Uhalifu unaohusishwa na wanajeshi wa Marekani, katika kisiwa hicho cha Okinawa, umekuwa chanzo cha mzozo wa kibalozi kati ya nchi hizo mbili.
Wanajeshi wote wa Marekani nchini Japan sasa wamepigwa marufu, ya kutembea nyakati za usiku, kufuatia tuhuma za ubakaji katika kisiwa hicho wiki mbili zilizopi.
No comments:
Post a Comment