MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania
(TIC), Balozi Elly Mtango ametoa somo kwa wafanyabiashara wajasirimali
nchini na kuwaeleza kuwa siri ya mafanikio katika biashara yoyote ni
uwezo, juhudi na mtazamo.
Alisema hayo alipozungumza katika sherehe
fupi za kutoa vyeti kwa wajasiriamali walioshinda mpango wa kuandaa
miradi inayohusiana na biashara za nishati zilizoandaliwa na taasisi
inayotoa huduma za maendeleo ya ujasiriamali na biashara ya SEED.
Balozi
Mtango alisema kanuni za mafanikio yoyote ni juhudi za mhusika na
akawataka wajasiriamali kutumia mbinu tofauti zitakazoziwezesha
biasharaa zao kufanikiwa na kuifanya miradi yao iwe endelevu.
“Zaidi
ya uwezo na jitihada ni muhimu pia kuwa na mtazamo, kadiri mtu
anavyozidisha mtazamo chanya na ari ya kutenda jambo, ndivyo hivyo
maisha yake yanavyokuwa na ufanisi zaidi,” alisema Balozi Mtango.
Alisema
watu wengi wanazo ndoto za kufanya mambo makubwa katika maisha yao,
lakini akasema ndoto zinaweza kutimia kwa kufanya kazi kwa bidiii na sio
kwa njia ya mkato.
“Bila jitihada, ndoto nzuri sana itabaki bila
kukamilishwa, katika safari ya maisha hakuna muujiza, tunapaswa kutembea
hatua moja kwa wakati, tunapaswa kuwa na subira, jitihada za kila siku
huleta ushindi,katika maisha na kwenye biashara yoyote, hatua moja kwa
wakati ndio njia pekee ya uhakika ya kubadili ndoto kuwa jambo la kweli”
alisema
Akizungumza katika sherehe hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa
SEED, Msafiri Chagama alisema taasisi yake imekuwa katika mpango wa
kuwajengea uwezo wafanyabiashara wajasiriali na kuchagua wale
wanaoshughulika na biashara za nishati.
Alisema jumla ya kampuni 73
za wajasiriamali zilijitokeza kushiriki katika shjindano hilo ambapo
baada ya mchuzo zilipatikana 53 zilizoshindanishwa kabla ya kupata
washindi 15 kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Alisema kati ya 15
waliopatikana, washindi wanne walipata zawadi ya kutembelea nchini
Uholanzi ambapo watapata fursa ya kujifunza zaidi kuhusu shughuli
mbalimbali zinazoohusu biashara pamoja na kupata uzoefu kutoka kwa
wenzao wanaofanya biashara kama zao nchini humo.
Aliwataja washindi
hao ambao watakaa Uholanzi kwa wiki nzima kuwa ni Godfrey Mosha,
Lawrence Makenya, Cuthbert Kajuna na Mshindwa Edith Banzi.
Alisema
washindi hao vile vile watapata fursa ya kushiriki katika maonyesho na
kuonyesha kile wanachokifanya katika biashara za nishati.
Alisema wale washiriki wengine ambao hawakupata fursa ya kwenda uholanzi watasaidiwa ushauri na jinsi ya kuboresha biashara zao.
No comments:
Post a Comment