ALIYEKUWA Waziri Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Nne, Edward Lowassa yupo nchini Ujerumani kwa matibabu na uchunguzi wa kiafya.Lowassa
ambaye pia ni Mbunge wa Monduli jana hakuwapo katika uzinduzi wa mradi
wa Barabara ya Minjingu hadi Arusha na shule jimboni kwake, uliofanywa
na Rais Jakaya Kikwete aliye ziarani mkoani Arusha.Kwa mujibu wa
taarifa iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Jowika
Kasunga na baadaye kusambazwa kwa waandishi wa habari, Lowassa alieleza
kusikitishwa kutokuwapo jimboni kwake wakati huo ambao Rais Kikwete
anatembelea jimbo lake.
Lowassa alisema kuwa, hali hiyo imetokana
na kuwa safarini kwa ajili matibabu lakini akasema anaamini mambo
yataenda vizuri si kwa ziara hiyo ya Rais Kikwete bali hata vikao vya
juu vya CCM vinavyotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
taarifa hiyo, alimsifu Rais Kikwete kuwa, kutokana na kutekeleza vizuri
na kwa uadilifu Ilani za uchaguzi za CCM, wiki mbili zijazo wanaCCM
watakwenda Dodoma kuidhihirishia dunia na Watanzania wenye shaka kwamba
wanamwamini na kuuthamini uongozi wake.Katika maelezo hayo, Lowassa alieleza tatizo linalomsumbua kuwa ni macho, lakini pia atatumia nafasi hiyo kuchunguza afya yake.
Aidha,
alimshukuru Rais Kikwete kwa kuzindua miradi hiyo akisema inadhihirisha
mambo mawili makubwa aliyoyafanya kwa kiwango cha juu chini ya uongozi
wake akiwa Rais wa Tanzania.“Mosi, chini ya uongozi wako shule
nyingi zaidi zimejengwa kuliko awamu zote zilizotangulia. Pili, kilomita
za barabara za lami zilizoongezeka wakati wa awamu yako ni ndefu kuliko
wakati mwingine wowote,” alisema Lowassa na kuongeza:
“Kwa
hakika umetekeleza vizuri, kikamilifu na kwa uadilifu Ilani za uchaguzi
za CCM, mwaka 2005 na 2010. Sisi wanachama wa CCM na wananchi wa Monduli
ni mashahidi wa jambo hili. Tunaamini ndivyo ilivyo kwa nchi nzima.”
Mwishoni
mwa wiki ijayo CCM itafanya uchaguzi mkuu wa uchaguzi ngazi ya taifa
kuanzia mwenyekiti wa chama na viongozi wengine, ili kukamilisha kupanga
safu mpya ya uongozi kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa 2015.CCM
ipo katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho ambapo tayari jumuiya zake
za Wazazi, Vijana na Wanawake zimekamilisha chaguzi hizo, huku kambi ya
Lowassa ikitajwa kuibuka kidedea kwa kunyakua nafasi mbalimbali
zilizowaniwa, kuanzia ngazi za wilaya hadi jumuiya za chama kitaifa.
Katika
uchaguzi wa UWT, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Taifa, Sophia Simba ambaye
alitetea nafasi yake na Makamu wake, Asha Bakari Makame wanatajwa kuwa
wafuasi wa Lowassa, huku wajumbe sita kati ya wanane waliochaguliwa
kuwakilisha jumuiya hiyo katika Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama
hicho, wakiwa waumini wa kambi hiyo.
Wajumbe sita kati ya wanane
walioshinda nafasi za ujumbe wa NEC kupitia jumuiya hiyo wanatajwa
kuwa wafuasi wa Lowassa, huku mmoja akitajwa kuwa hana kundi lolote
huku mwingine akitajwa kumuunga mkono aliyekuwa mgombea wa uenyekiti wa
UWT na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Killango Malecela.Kwa
upande wa UVCCM, Mbunge wa Donge, Sadifa Juma Khamisi ambaye
alichaguliwa kuwa Mwenyekiti kwa kura 483 na makamu wake, Mboni Muhita
pia wanatajwa kuwa wafuasi wa kambi ya Lowassa.Waliotwaa ujumbe wa NEC na ujumbe wa Baraza Kuu la Umoja huo, pia wanatajwa kuwa waumini wa kambi hiyo.Hata
hivyo, katika uchaguzi wa Jumuiya ya Wazazi uliokuwa wa funga dimba la
mfululizo wa chaguzi za chama hicho tawala kuanzia ngazi za shina tangu
Aprili, waliokuwa wagombea wa nafasi ya uenyekiti, John Barongo na
Abdallah Bulembo kwa nyakati tofauti walikanusha kuwa na masilahi na
makundi huku Martha Mlata akikataa kuzungumzia uchaguzi huo.
chanzo mwananchi jumapili
No comments:
Post a Comment