SUALA la Bunge kuandaa kanuni za maadili ili kuwadhibiti wabunge
 ambao wanatumia mianya ya kanuni zilizopo kufanya makosa mbalimbali 
ikiwamo kujihusisha na vitendo vya rushwa,limechukua sura mpya baada ya 
wabunge kueleza kuwa haziwezi kusaidia kuwabadilisha tabia wabunge.
Wiki iliyopita, Mwananchi ilibaini kuwapo kwa 
mpango wa kuandaliwa kwa kanuni za maadili ili kuwadhibiti wabunge ambao
 wanatumia mianya ya kanuni zilizopo kufanya makosa mbalimbali ikiwamo 
kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na 
Mkurugenzi wa Idara ya Shughuli za Bunge, John Joel zinaeleza kuwa hatua
 hiyo ya Bunge inatokana na wabunge kutuhumiwa kwa makosa mbalimbali 
wanayoyafanya wakiwa nje ya ndani ya Bunge ikiwamo rushwa.
Joel alisema masharti hayo mpaka sasa yapo katika hatua ya kuchapwa na kwamba muda si mrefu kanuni itatoka.
Joel alisema masharti hayo mpaka sasa yapo katika hatua ya kuchapwa na kwamba muda si mrefu kanuni itatoka.
Alisema wamegundua kuwa baadhi ya wabunge watumia 
Kanuni za Bunge zilizopo kuzikwepa na kufanya mambo yasiyofaa ambayo 
yanashusha hadhi ya Bunge.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofuati katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, wabunge hao wameshauri wabunge wenyewe kujitambua kuwa wao ni kioo cha jamii.
Mbunge wa Mbeya mjini, Chadema, Joseph Mbilinyi alisema kanuni za maadili kwa ajili ya wabunge ambazo zinaandaliwa haziwezi kuwabadilisha tabia wabunge.
Alisema sheria na kanuni za kumzuia mbunge kufanya mambo yasiyofaa zipo, lakini bado wanaendelea kuvivunja na baadhi hawachukuliwi hatua.
Mbilinyi alisema wananchi wanataka kuona watu wanaotuhumiwa kwa rushwa wakiwamo wabunge wanachukuliwa hatua kwa kutumia sheria zilizopo.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofuati katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, wabunge hao wameshauri wabunge wenyewe kujitambua kuwa wao ni kioo cha jamii.
Mbunge wa Mbeya mjini, Chadema, Joseph Mbilinyi alisema kanuni za maadili kwa ajili ya wabunge ambazo zinaandaliwa haziwezi kuwabadilisha tabia wabunge.
Alisema sheria na kanuni za kumzuia mbunge kufanya mambo yasiyofaa zipo, lakini bado wanaendelea kuvivunja na baadhi hawachukuliwi hatua.
Mbilinyi alisema wananchi wanataka kuona watu wanaotuhumiwa kwa rushwa wakiwamo wabunge wanachukuliwa hatua kwa kutumia sheria zilizopo.
Mbunge wa Nkasi Kaskazini, CCM, Ali Kessy alisema 
kuwa kanuni hizo haziwezi kusaidia badala yake vyombo vya dola ikiwamo 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), zifanye kazi yake 
bila ya upendeleo.
Alishauri wabunge wabadilishe tabia zao kwa kuacha
 kujiingiza katika vitendo vya kuvunja sheria kwani wao wajitambue kuwa 
ni vioo cha jamii.
Kwa upande wake, Mbunge wa Mkanyageni, CUF, 
Mohammed Mnyaa alisema kutungwa kwa kanuni za maadili kwa wabunge 
kutasaidia kuwadhibiti wabunge ambao wanafanya mambo yanayoshusha 
heshima ya wabunge.
Alisema kanuni hizo zitasaidia kuleta ustarabu 
miongoni mwa wabunge, kwani kila wanapotaka kufanya mambo yasiyofaa 
watakumbuka adhabu ambayo wataipata kutokana na kitendo hicho.
“Kuwapo kwa kanuni za maadili kutasaidia wabunge 
kujiheshimu. Kwa mfano Wabunge kuonekana baa wakifanya mambo yasiyofaa 
sasa kutapungua,” alisema.
Mbunge wa Iringa mjini, Chadema,  Peter Msigwa 
alisema tatizo la kuvunja sheria ikiwamo kupokea au kutoa rushwa sio la 
wabunge pekee nchi hii.
Alisema sheria zilizopo zinatosheleza sana kudhibiti watu kufanya mambo yasiyofaa ikiwamo rushwa, lakini viongozi wameshindwa kuzissimamia.Mbunge huyo alisema kuwa na sheria nyingi sio kumaliza tatizo, bali kinachotakiwa ni kuhakikisha watuhumiwa wanachukuliwa hatua zinazostahili.
Alisema sheria zilizopo zinatosheleza sana kudhibiti watu kufanya mambo yasiyofaa ikiwamo rushwa, lakini viongozi wameshindwa kuzissimamia.Mbunge huyo alisema kuwa na sheria nyingi sio kumaliza tatizo, bali kinachotakiwa ni kuhakikisha watuhumiwa wanachukuliwa hatua zinazostahili.
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment