Hayo yalibainika mwishoni mwa wiki baada ya Mkuu
wa Mkoa wa Kagera Fabian Massawe kulicharukia Baraza la Madiwani wa
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba na watumishi,kufuatia taarifa ya Mkaguzi
na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali kubainisha hujuma ya miradi ya
maendeleo.
Huku akisoma sehemu ya barua aliyodai imetoka
katika Ofisi ya Waziri Mkuu,alisema hayuko tayari kuwajibishwa kutokana
na uzembe wa watumishi na madiwani ambao wanashindwa kutekeleza wajibu
wao wa kuisimamia halmashauri.
“Utawajibika kwa taarifa zenye kasoro katika mkoa
wako"alinukuu sehemu ya barua hiyo na kusema hayuko tayari kuwajibika
kwa sababu ya uzembe wa madiwani na watumishi na kudai wakati mwingine
madiwani huyafumbia macho madudu yanayofanyika ndani ya halmashauri kwa
sababu pia wao ni sehemu ya watuhumiwa.
Mkuu wa Mkoa alitumia nafasi hiyo kuishutumu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru),kwa kukaa kimya
dhidi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba waliotajwa na
Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali kuhusika na hujuma ya
miradi ya maendeleo.
Akisoma matokeo ya ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi
Mkuu mbele ya Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo,Massawe alisema
kuwa Takukuru haifanyi kazi kwani ilitakiwa kuwa imewachukulia hatua
baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo.
Miongoni mwa mambo yaliyomstaajabisha Massawe ni
watumishi kufanya biashara ya kuiuzia halmashauri yao mafuta,vifaa vya
ofisi na kukodisha magari hali aliyosema inaleta mgongano wa maslahi na
kuitaka Takukuru kuwahoji watuhumiwa.
“Takukuru hamfanyi kazi mnaacha watuhumiwa
wanaendelea kuwa huru,nataka kupata matokeo ,manunuzi yanafanyika bila
uwazi wa ushindani, miradi inatekelezwa chini ya kiwango, na hata baba,
mama na watoto wanapewa tenda,”alisema Massawe.
Aidha alisema ukaguzi ulibaini kuwa halmashauri
hiyo iko taabani huku akiwataka madiwani kuacha woga na kuwataja
aliowaita mafisadi wanaotafuna fedha za halmashauri hiyo kupitia
utekelezaji duni wa miradi ya maendeleo.
Pia alilitaka Baraza hilo kuwawajibisha haraka
baadhi ya watumishi ambao katika ukaguzi maalumu uliofanywa na Tamisemi
kwa kushirikiana na ofisi yake walibainika kuhujumu miradi ya maji, afya
na elimu.
Awali, Mwenyeki wa Halmashauri hiyo, George Katomero alisema kuwa mtiririko wa mapato sio mzuri na kuwa hawana takwimu sahihi zinazowasaidia kupima kiwango wanachostahili kukusanya kila mwezi kutoka kila chanzo cha mapato.
Awali, Mwenyeki wa Halmashauri hiyo, George Katomero alisema kuwa mtiririko wa mapato sio mzuri na kuwa hawana takwimu sahihi zinazowasaidia kupima kiwango wanachostahili kukusanya kila mwezi kutoka kila chanzo cha mapato.
No comments:
Post a Comment