HATIMA ya rufaa ya kesi ya aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini
kupitia Chadema, Godbless Lema, itajulikana leo wakati Mahakama ya
Rufani, itakapotoa uamuzi kuhusu pingamizi lililowekwa na upande wa
wajibu rufaa dhidi ya rufaa hiyo.
Lema alivuliwa wadhifa huo na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha April 4 mwaka huu, kufuatia kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM, wakipinga ushindi wake katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.
Wanachama hao ni Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel.
Hata hivyo , kupitia kwa Wakili wake Method Kimomogoro, Lema alikata rufaa kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, huku akiorodhesha hoja 18 za kuipinga.
Siku ambayo rufaa hiyo ilipangwa kusikilizwa na jopo la Majaji watatu Mahakama ya Rufani wakili wa wajibu rufaa, Alute Mughwai, aliweka pingamizi la awali.
Jopo linalosikiliza kesi hiyo linawajumuisha Jaji Salum Massati, Jaji Natalia Kimaro na Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande.
Katika pingamizi hilo, Wakili Mghwai aliiomba mahakama, iitupile mbali rufaa hiyo, akidai kuwa ina kasoro za kisheria na za kikanuni, jambo ambalo liliibua mvutano wa hoja za kisheria baina ya pande zote.
Habari zilizolifikia Mwananchi kutoka mahakamani na kuthibitishwa na Afisa Habari wa Mahakama, Mary Gwao, kwa niaba Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma zilisema uamuzi wa pingamizi hilo utatolewa leo asubuhi.
Awali uamuzi wa pingamizi hilo ulipangwa kutolewa Novemba 29 mwaka huu, lakini baadaye rufaa hiyo ikaondolewa katika orodha ya kesi ambazo zilipangwa kusikilizwa na kutolewa uamuzi katika vikao vya Mahakama ya Rufani vya Novemba.
Maruma alisema kuwa uamuzi wa pingamizi hilo uliondolewa kwenye orodha ya kesi ambazo zilipangwa tarehe hiyo kwa kuwa ungeweza kukamilika wakati wowote hata kabla ya siku hiyo.
Lema alivuliwa wadhifa huo na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha April 4 mwaka huu, kufuatia kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa CCM, wakipinga ushindi wake katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.
Godbless Lema, |
Wanachama hao ni Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel.
Hata hivyo , kupitia kwa Wakili wake Method Kimomogoro, Lema alikata rufaa kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, huku akiorodhesha hoja 18 za kuipinga.
Siku ambayo rufaa hiyo ilipangwa kusikilizwa na jopo la Majaji watatu Mahakama ya Rufani wakili wa wajibu rufaa, Alute Mughwai, aliweka pingamizi la awali.
Jopo linalosikiliza kesi hiyo linawajumuisha Jaji Salum Massati, Jaji Natalia Kimaro na Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande.
Katika pingamizi hilo, Wakili Mghwai aliiomba mahakama, iitupile mbali rufaa hiyo, akidai kuwa ina kasoro za kisheria na za kikanuni, jambo ambalo liliibua mvutano wa hoja za kisheria baina ya pande zote.
Habari zilizolifikia Mwananchi kutoka mahakamani na kuthibitishwa na Afisa Habari wa Mahakama, Mary Gwao, kwa niaba Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma zilisema uamuzi wa pingamizi hilo utatolewa leo asubuhi.
Awali uamuzi wa pingamizi hilo ulipangwa kutolewa Novemba 29 mwaka huu, lakini baadaye rufaa hiyo ikaondolewa katika orodha ya kesi ambazo zilipangwa kusikilizwa na kutolewa uamuzi katika vikao vya Mahakama ya Rufani vya Novemba.
Maruma alisema kuwa uamuzi wa pingamizi hilo uliondolewa kwenye orodha ya kesi ambazo zilipangwa tarehe hiyo kwa kuwa ungeweza kukamilika wakati wowote hata kabla ya siku hiyo.
Habari zilizopatikana kutoka duru za Kimahakama na
kuthibitishwa na Wakili wa Mrufani, Method Kimomogoro, zimeeleza kuwa
uamuzi huo utatolewa Jijini Dar es Salaam baada ya jopo la majaji watatu
waliosikiliza pingimizi hizo kukamilisha kupitia hoja za mawakili.
Pingamizi hizo zilisikilizwa Jijini Arusha wakati
wa kikao cha Mahakama ya Rufaa kilichofanyika jijni Arusha mwanzoni mwa
Oktoba mwaka huu.
Akizungumza kwa njia ya simu, Wakili Method
Kimomogoro anayemwakilisha Lema katika rufaa hiyo akishirikiana na
Mwenzake Tindu Lissu alithibitisha kupokea hati ya kuitwa mahakamani
kusikiliza uamuzi huo leo Alhamisi.“Ni kweli nimetoka kuchukua
wito wa kufika mahakamani sasa hivi inayotuagiza kufika mbele ya
Mahakama ya Rufaa Alhamisi kusikiliza uamuzi wa pingamizi za rufaa ya
mteja wetu Novemba 8, mwaka huu,”alisema Kimomogoro.
No comments:
Post a Comment