Thursday, November 8, 2012

Wenger amsifu Theo Walcott,

Theo Walcott
Meneja Arsene Wenger amemsifu Walcott kwa mchezo wa kuvutia
Meneja wa klabu ya soka ya Arsenal ya Uingereza, Arsene Wenger, amemsifu sana Theo Walcott, kwa kuichezea vizuri sana timu hiyo usiku wa Jumanne, katika mechi ambayo timu hiyo ilitoka sare ya 2-2 katika mechi ya ugenini dhidi ya Schalke ya Ujerumani.
Walcott, ambaye mashauri ya kuongezewa mkataba yalivunjika mwezi Agosti, alianza vyema katika mechi hiyo, kwa kuifungia Arsenal bao la kwanza, na ikiwa ni mara ya nne msimu huu anapoingia katika mechi tangu mwanzo.

Lakini ilikuwa ni mara ya kwanza kucheza tangu mwanzo katika mechi ya Ulaya tangu mwezi Machi.

"Alicheza vizuri sana," alisema Wenger. "Alikuwa ni kati ya wachezaji wetu waliocheza vizuri sana."

Kulikuwa na wasiwasi kama Walcott angelicheza katika mechi ya jana, baada ya kuugua kwa muda, lakini kwa kutokuwepo Aaron Ramsey, ilibidia aingie uwanjani.

Lakini mechi ikielekea kumalizika, katika muda wa majeraha, Walcott alikosa nafasi nzuri ya kuiwezesha Arsenal kuzoa pointi zote tatu.

Kabla ya mechi hiyo, mara zote 12 ambazo ameshirikishwa katika mechi, mara tisa aliingia kama mchezaji wa zamu.

Hata hivyo hayo hayakumzuia kuandikisha magoli saba.

No comments:

Post a Comment