Thursday, November 8, 2012

Watawa zaidi wajiteketeza kupinga China

                                      Mtawa aliyejiteketeza kuonyesha kero na China
Wanaharakati nchini China wanasema kuwa vijana watatu watawa wa Tibet pamoja na mama mmoja walijiteketeza mkesha wa kongamano la chama cha tawala cha kikomunisti nchini China.
Shrika la Free Tibet linasema kuwa mmoja wa watawa hao alifariki katika kile inachosema ni idadi kubwa ya watu kujiteketeza kama njia ya kuonyesha kukerwa na utawala wa china.
Matukio ya hivi karibuni ya watu kujiteketeza moto katika maeneo ya china yaliyo na watu wa Tibet yamefikisha idadi ya watu hao wanaojiteketeza kuwa zaidi ya watu sitini tangu mwaka jana.
Wengi wao wamefariki. Na huenda kuna umuhimu katika wakati ambapo visa hivi vimetokea.
Kuimarishwa kwa usalama kote China kwa kongamano la chama tawala cha kikomyunisti nchini, hakujazuia malalamiko ya raia wa Tibet dhidi ya utawala wa China. Badala yake yameongezeka.
Wanaharakati wanasema idadi ya watu kujiteketeza kwa muda wa siku moja, hii leo, haikutarajiwa.
Tangu mwaka jana zaidi ya raia sitini wa Tibet wameamua kutumia njia kubwa kabisa ya kuonyesha kuvunjwa moyo, kwa kile wanachosema ni ukandamizaji wa China kwa tamaduni zao.
Raia wa Tibet wanaopinga China
Maafisa wa serikali wa China wametoa fedha katika maeneo yaliyo na raia wa Tibet na wameendelea kukana tuhuma hizo za ukandamizaji.
Mkurugenzi wa kundi linalotetea kuachiwa huru maeneo ya Tibet, amesema malalamiko ya hivi karibuni yananuiwa kutoa ishara kwa kizazi kipya cha uongozi China, kitakachoidhinishwa katika kongamano linaloendelea Beijing, kuwa raia wa Tibet wataendelea kupigania uhuru wao.
Baadhi ya raia wa Tibet walio uhamishoni, wanatumai kuwa mwanamume anayedokezwa kuwa kiongozi mpya, Xi Jinping, huenda akawapatia nafasi ya kufanyika mabadiliko.
chanzo-bbc.com

No comments:

Post a Comment