Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu
---
Sehemu ya 11 ya Kanuni ya Bunge, Ibara ya 121 inaeleza kuwa mbunge
yeyote anaweza kuwasilisha kwa Spika taarifa ya hoja ya kumshtaki Rais
kwa madhumuni ya kumuondoa Rais madarakani kupitia azimio la Bunge kwa
mujibu wa Ibara ya 46 A ya Katiba ikiwa inadaiwa kwamba Rais; ametenda
vitendo ambavyo kwa ujumla vinavunja katiba au sheria ya maadili ya
viongozi wa umma.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge jana, Lissu alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona Bunge limeikalia ripoti ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyomhoji kuhusu kauli yake ya kuwatuhumu majaji kuwa baadhi yao hawana sifa.
SIKU moja baada ya Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni,
Tundu Lissu kusema atawasilisha hoja ya kumshtaki Rais Jakaya Kikwete
iwapo atashindwa kuwaondoa kazini majaji wasio na sifa aliowateua,
Ikulu imemwambia aendelee na mchakato wake.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema jana
kuwa hakuna anayemzuia Lissu kushtaki kama anaona kuna sababu za
kufanya hivyo.“Lissu ni Mbunge na ana haki zake za msingi na kama
amefikia hatua hiyo anaweza kufanya hivyo... hakuna mtu ambaye anaweza
kumkataza. Nani mwenye uwezo wa kuingilia uhuru wa mtu?”
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge jana, Lissu alisema amechukua uamuzi huo baada ya kuona Bunge limeikalia ripoti ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyomhoji kuhusu kauli yake ya kuwatuhumu majaji kuwa baadhi yao hawana sifa.
Alisema ameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuona Rais Kikwete ambaye
ana mamlaka ya kuteua majaji, ameshindwa kuwaondoa kazini majaji hao
wasiokuwa na sifa
No comments:
Post a Comment