Wednesday, November 7, 2012

Alichosema mh. John Mnyika Juu ya uhaba wa mafuta nchini



Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Mbunge wa Ubungo (Chadema)John Mnyika akihoji Kiti cha Spika juu ya serikali kushindwa kuleta bungeni kauli ya serikali juu ya mkakati wa kukabiliana na uhaba wa mafuta nchini Tanzania.

Uhaba wa mafuta jana umewakimbiza kwenye kikao cha Bunge mjini Dodoma asubuhi, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na naibu mawaziri wake George Simbachawene na Steven Masele.

Waziri huyo na naibu mawaziri wake hawakuwepo bungeni leo wakati Mbunge wa Ubungo (Chadema) John Mnyika akiitaka serikali itoe sababu ya kutokuja bungeni leo kutoa tamko la serikali jinsi inavyoshughulikia suala la uhaba wa mafuta nchini.

Spika wa Bunge Anne Makinda alimlazimisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kusimama na kujibu hoja ya Mnyika aliyemtaka Spika kulazimisha serikali ijibu hoja yake pamoja na mkakati wa serikali wa kutatua uhaba wa mafuta nchini.Waziri Mkuu Mizengo Pinda alilazimika kunyanyuka na kusema kwa ufupi kuwa serikali ilikuwa ikijiandaa na kuja na hoja nzito ya kueleza umma mikakati kabambe ya kutatua uhaba wa mafuta nchini.

No comments:

Post a Comment