Friday, December 27, 2013

Bayern yazidi kujitwalia makombe 2013,yachapa Raja Casablanca


Bayern Munich inafunga mwaka wa 2013 kwa kutwaa Kombe la Klabu Bingwa duniani baada ya kupata ushindi dhidi ya mabingwa wa Morocco, Raja Casablanca katika mchezo uliochezwa mjini Marrakech, Morocco.
Mabingwa hao wa Ujerumani wameongeza kombe lingine katika mkusanyiko wa makombe waliyoyatwaa likiwemo la klabu bingwa ya ligi ya Bundesliga,Ujerumani na kombe la Uefa katika mwaka huu wa mafanikio.
Raja ilukuwa na matumaini ya kuwa klabu ya kwanza kutoka Afrika kutwaa kombe hilo, lakini matumaini hayo yakayeyuka baada ya kukubali kipigo kutoka kikosi cha timu Pep Guardiola.
Dante na Thiago Alcantara walifunga mabao hayo mawili na kuandikisha ushindi kwa timu ya Bayern.

Bayern Munich mabingwa wa dunia

Pep Guardiola kocha wa Bayern, amefanikiwa kulitwaa kombe hilo mara tatu akiwa na timu mbili tofauti. Mhispania huyo alishinda akiwa na Barcelona mwaka 2009 na 2011.
Bayern walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kutwaa kombe hilo kwa kuwachapa Raja ambao matarajio yao yalizidi hatua ya kufikia fainali katika mchezo uliochezwa nchini mwao Morocco.
Timu hiyo ya Morocco ambayo ilishangiliwa na umati mkubwa wa watu waliojitokeza katika uwanja wa nyumbani wa Marrakach, walichukuliwa kuwa timu dhaifu kuliko zote katika michuano hiyo ya kuwania ubingwa wa dunia kwa vilabu. Lakini waliwatoa Auckland City, Monterrey na timu ya Ronaldinho, Atletico Mineiro.
Kwa upande wao timu ya Bayern iliicharaza Guangzhou Evergrande mabingwa wa bara la Asia, huku mabingwa hao wa Ulaya wakiingia hatua ya nusu fainali. Waliwatandika Guangzhou 3-0 huku wakipata urahisi wa kuwacharaza Raja mabao 2-0 katika muda wa robo saa ya mchezo.

No comments:

Post a Comment