Thursday, September 6, 2012

HII NDIO MECHI YA KWANZA ATAKAYOCHEZA MWANARIADHA MJAMAICA USAIN BOLT KAMA MCHEZAJI WA MAN U.



.
Mtu wangu, kama damu yako ya ushabiki inamilikiwa na Manchester United basi hii inakuhusu, unakumbuka mwanariadha alievunja rekodi kibao za dunia Mjamaica Usain Bolt alimiliki headlines siku kadhaa zilizopita baada ya kutangazwa kujiunga na club ya Manchester United kwa ajili ya kucheza soka?
Stori mpya ni kwamba kocha wa Man U Sir Alex Ferguson amekiri kupitia gazeti la Mirror UK kwamba Usain Bolt ambae ni shabiki mkubwa wa Manchester united atapata nafasi ya kuichezea Man U kama mchezaji kwenye mechi ya kirafiki na Real Madrid siku zijazo.
Tayari mpaka sasa Bolt ameshatembelea uwanja wa mazoezi wa Man United na kukutana na wachezaji wa club hiyo, na sasa imethibitika kwamba jamaa atapewa namba kwenye mechi ya Man U na Real Madrid ili kuangaliwa uwezo wake.

No comments:

Post a Comment