Friday, September 14, 2012

Njama ya mashambulizi ya kigaidi yatibuliwa Kenya

Magwanda ya mabomu ya kujilipua


Polisi nchini Kenya wamenasa magwanda yenye mabomu ya kujilipua pamoja na zana zengine ambazo zilikuwa zitumike kwa mashambulizi ya kigaidi mjini Nairobi.
Washukiwa wawili wamekamatwa katika msako huo uliofanywa asubihi ya leo katika mtaa wa Eastleigh mjini Nairobi.
"tunaamini kuwa silaha hizi zilinuiwa kutumika kufanya mashambulizi ya kigaidi mjini Nairobi'' alisema bwana Kiraithe.
Silaha hizo zinasemekana kufanana na zile zilizotumika katika mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika nchini Uganda dhidi ya watu waliokuwa wanatazama fainali ya kombe la dunia mwaka 2010, ambapo watu 76 waliuawa

No comments:

Post a Comment