Saturday, September 15, 2012

MECHI YA 700 YA Paul Scholes NA GOLI LAKE KUONESHA MASHABIKI KWAMBA BADO YUPO FITI 100%

Man U 4-0 Wigan

Paul Scholes afunga bao la kwanza
Licha ya umri wake ,Paul Scholes alionyesha umahiri wa soka baada ya kuifungia Manchester United bao la kwanza walipocheza na Wigan katika uwanja wa Old Trafford siku ya Jumamosi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 alifunga bao hilo dakika sita tu baada ya timu hizo mbili kutoka mapumzikoni.
Hii ilikuwa ni mechi ya 700 kwa Scholes kuichezea Man U .
Mchezaji Javier Hernandez ambaye mkwaju wake wa penalti uliokolewa na Kipa wa Wigan Ali Al Habsi hapo awali, alifunga katika dakika ya 63 kabla ya Alex Buttner na Nick Powell kufunga katika dakika ya 66 na 83 hivyo mpira ukimalizika kwa mabao 4-0
Japo Man U walifunga lakini hawakuonyesha mchezo mzuri ila tu walitumia nafasi chache walizozipata na kufunga mabao ya haraka haraka.
Sasa vijana wa Sir Alex Ferguson wako katika nafasi ya pili, pointi moja tu nyuma ya vinara Chalsea ambao walitoka sare na timu ya Queen Park Rangers siku hiyo hiyo ya jumamosi.

No comments:

Post a Comment