Friday, September 21, 2012

Waisilamu waandamana kote duniani na zaidi ya watu 20 wanaripotiwa kufariki katika maandamano hayo

                                               Maandamano Pakistan
Mapambano yametokea baina ya polisi na waanda-manaji nchini Pakistan kabla ya sala ya Ijumaa, kulalamika juu ya filamu inayokejeli Uislamu iliyotengenzwa Marekani.
Shirika moja la habari la Pakistan limesema kuwa mfanyakazi wake mmoja ameuwawa mjini Peshawar wakati polisi walipofyatua risasi kutawanya makundi ya watu wenye hasira, waliojaribu kuchoma moto jengo la sinema.
Ulinzi ulidhibitiwa katika nchi nyingi za kiisilamu kama Misri, Libya, Tunisia Morocco na kwingineko huku zikijiandaa kwa maandamano makubwa baada ya maombi ya Ijumaa.
Maandamano hayo yalipinga filamu iliyotengezwa nchini Marekani kumkejeli Mtume Muhammad na dini ya kiisilamu.
Nchini Pakistan, serikali ilitenga siku maalum kwa jina "special day of love" kwa miniajili ya kumsifu na kumuenzi Mtume Muhammad.
Marekani imelipia matangazo ya kibiashara nchini Pakistan, rais Obama akionekana kukashifu vikali filamu hiyo
Maandamano makubwa kupinga filamu hiyo tayari yamesababisha vifo sehemu mbali mbali duniani.
Ingawa Marekani ndiyo imeathirika zaidi kutokana na mandamano hayo, uchochezi umeoneka kuongezeka kutoka barani Ulaya baada ya jarida moja nchini Ufaransa kuchapisha picha za kumfanyia mzaha Mtume na waisilamu waliopinga vikali filamu hiyo.
Vyama vyote rasmi vya kisiasa pamoja na mashirika ya kidini wametangaza maandmano kwa ushirikiano na makundi ya kibiashara huku maandamano hayo yakitarajiwa kuwa makubwa sana.
Waziri wa mambo ya nje nchini humo, Hina Rabbani Khar, ameambia shirika la habari la AP kwamba siku hiyo maalum inanuiwa kushinikiza maandamano ya amani na kuzuia watu wenye msimamo mkali kusababisha ghasia kutokana na hasira yao dhidi ya Marekani.
Duru zinasema kuwa vituo vya mafuta, maduka na masoko yatafungwa leo na huenda usafiri ukasitishwa .

No comments:

Post a Comment