Monday, February 4, 2013

PICHA NA TAARIFA KUHUSU JENGO LA PPF TOWER DSM KUUNGUA

PPF Tower
Maelezo yaliyotolewa na James Samwel wa kikosi cha zimamoto Ultimate Security ni kwamba wao walipata alarm ya moto na walikwenda eneo la tukio na kukuta moshi unatoka mkubwa sana kwenye gorofa ya 19, kulikua na watu wanne gorofa ya 19 na wawili gorofa ya 16 ambao hao waliokolewa mwanzoni, moto ulipozidi uliongeza moshi zaidi hivyo kazi ya kuwaokoa wanne walioko juu ilikua ngumu lakini baadae waliokolewa.
Bado haijajulikana ni kiasi gani cha mali kilichoharibika lakini James anasema hakuna uharibifu mkubwa sana, ni baadhi ya vitu tu vimeharibika ambapo chanzo cha moto ni hitilafu ya umeme uliokua ukikatika na kurudi, hakuna yeyote aliyejeruhiwa ambapo watu sita waliokuwemo eneo la tukio wote waliokolewa salama.
James ameiambia millardayo.com kwamba hizo floor mbili zilizoungua kwa ndani moja wapo inahusika na kampuni ya mtandao ya Vodacom na floor nyingine hajajua ni ofisi ya kampuni gani lakini millardayo.com inaendelea kufatilia.

.
.
.
.
.
.
.chanzo-millardayo.com

No comments:

Post a Comment