Friday, November 29, 2013

Rais Kabila azuru mashariki mwa Congo

Rais Joseph Kabila wa DR Congo
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo,Joseph Kabila, anatembelea eneo la mashariki mwa Congo ambalo awali lilidhibitiwa na kikundi cha waasi wa M23, ambacho kilishindwa katika mapigano dhidi ya majeshi ya Congo yakisaidiwa na yale ya Umoja wa Mataifa, mwezi mmoja uliopita.
Anatarajiwa kuwasili eneo la Rutshuru -- eneo ambalo lilikuwa ngome kuu ya waasi karibu na mpaka wa Uganda.
Bwana Kabila amefanya safari ya urefu wa kilomita mia tisa kwa njia ya gari mashariki mwa Congo kuonyesha imani yake kuhusu kuimarika kwa usalama katika eneo hilo.
Amevitaka vikundi vingine vyenye silaha nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kujisalimisha, la sivyo vitashughulikiwa kama ilivyotokea kwa kikundi cha M23.
Eneo la Rutshuru lilikuwa chini ya udhibiti wa M23 kwa zaidi ya mwaka mmoja na wakaazi wa eneo hilo wameiambia BBC kuwa waasi hao waliwaua na kuwateka watu wengi.

No comments:

Post a Comment