Wednesday, November 27, 2013

Kikosi cha Manchester United chaponea chupuchupu na ajali ya ndege nchini Ujerumani

Kikosi cha Manchester United jana kiliingiwa na wasiwasi mkubwa baada ya ndege iliyokuwa imeibeba timu kulazimika kusitisha kutua uwanjani, mita 400 tu kutoka njia ya kutulia kwenye uwanja wa ndege wa mjini Cologne, Ujerumani uitwao Konrad Adenauer.
Rubani wa ndege alilazimika kuirudisha tena angani ndege ya hiyo, Monarch Airlines A321 baada ya ndege nyingine kuwa mbele yake kwenye runway. Ndege hiyo iliuzunguka uwanja na kutua tena dakika 10 baadaye.
Baada ya tukio hilo, Rio Ferdinand aliandika’Landed in Germany….just….I’ve only just recovered after that choppy landing!

No comments:

Post a Comment