Monday, September 10, 2012

NAPE KUTINGA KORTINI MUDA WOWOTE KUANZIA LEO.

 Nape kortini
Mbowe alisema watamburuza mahakamani Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kutokana na kauli yake kuwa CHADEMA kinapewa mabilioni ya fedha na wafadhili nje ya nchi.
Alisema watampeleka Nape mahakamani ili aende kuithibitisha kauli hiyo na ukweli uweze kubainika.
“Ukifumbia macho hoja hii inaweza kuonekana kuwa ni ya kweli, sasa atakwenda kuithibitisha mahakamani, mahakama ikitenda haki ukweli utajulikana. Wanasheria wetu wanalifanyia kazi suala hili,” alisema.
Kwa muda sasa Nape amekaririwa akisema kuwa chama hicho kimekuwa kikipewa mabilioni ya fedha na wafadhili nje ya nchi na kuwahadaa Watanzania kupitia harambee mbalimbali.
CHADEMA kilimpa siku saba Nape kuthibitisha madai hayo, lakini hakufanya hivyo na kusema kuwa ana ushahidi kuhusu kauli yake dhidi ya chama hicho.
Dk. Slaa afafanua SMS
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa inawezekana IGP, Said Mwema na Waziri wa Mambo ya Ndani, Nchimbi ni mbumbumbu wa sheria kutokana na kudai ujumbe wake mfupi wa maandishi (SMS) ni wa kichochezi.
Alisema kama si mambumbumbu wa sheria, basi hawajui maana ya neno uchochezi na kuhoji kama ujumbe huo ni wa uchochezi kwa nini mpaka sasa hawajamkamata.
“Nilimtumia ujumbe ule IGP, lakini aliupeleka kwa Waziri Nchimbi maana yake anaomba ushauri ambao pia waziri ameshindwa kumpa mpaka mauaji yametokea.
“Nchimbi ameshindwa kutimiza wajibu wake, hivyo anatakiwa kujiuzulu kwa kushindwa kuufanyia kazi ujumbe wa thadhari,” alisema.

No comments:

Post a Comment