Wednesday, September 5, 2012

MSG ILIYOTUMWA NA DR SLAA KWA MKUU WA POLISI TANZANIA KABLA YA KIFO CHA MWANDISHI IRINGA.

Dr Slaa kwenye maziko ya mwandishi Daudi Mwangosi.
Ikiwa ni siku ya pili toka mwandishi wa habari wa Channel Ten Daudi Mwangosi kuuwawa kwa bomu akiwa kwenye mikono ya polisi Iringa, Waziri wa mambo ya ndani Dr Emmanuel Nchimbi ameunda tume huru ya watu watano kwa ajili ya kuchunguza chanzo cha kifo hicho.
Hiyo tume inaongozwa na jaji mstaafu Stephen Kihema na itafanya kazi yake kwa siku 30 ambapo pamoja na mambo mengine, inapaswa kuainisha ukubwa wa nguvu iliyotumika kumuua mwandishi huyo, ichunguze kama upo uhasama kati ya Polisi na waandishi wa habari mkoani Iringa, pia iangaliwe kama kweli ipo orodha ya waandishi wa habari watatu waliopangwa kushughulikiwa na jeshi hilo.
Waziri Nchimbi ameahidi hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakaebainika kuhusika na kifo hicho bila kujali nafasi aliyonayo.
Kwenye line nyingine, namkariri Nchimbi akisema “kuna maswali kama sita ambayo mimi sina majibu yake na ningependa sana nipate majibu yake, nini chanzo cha kifo cha mwandishi wa habari wa Iringa Daudi Mwangosi? nikiwa Waziri mwenye dhamana ya usalama wa raia kwa sababu hiyo basi naunda kamati ya uchunguzi ya watu watano”
Kuhusu msg iliyotumwa na Dr Slaa kwa Mkuu wa jeshi la Polisi IGP Said Mwema kabla ya mwandishi kuuwawa, naendelea kumkariri Waziri Nchimbi akisema “IGP Mwema alitutumia hiyo msg viongozi wenzake, Dr Slaaa alimuandikia kwamba IGP nasubiri simu yako wajulishe polisi wako waandae risasi za kutosha kutakua na karamu ya mauaji na kisha kusherehekea mjiandae kwenda Mahakamani The Hague”
Marehemu Daudi.
Kwenye nukuu nyingine Waziri Nchimbi amesmea “nikiona mtu katuma msg ya namna hii kwa IGP alafu bado yuko barabarani anaendelea kutembea, hajahojiwa, hajapelekwa Mahakamani kwa kuandaa vurugu, ni jambo nalishangaa sana… kwa kweli ujumbe wangu ni kwa watu wawili.. IGP namshangaa kwamba aliemtumia msg hiyo yuko barabarani anatembea akiwa huru, pili namshangaa alietuma ujumbe huo ambae ameona vifo vimetokea baada ya ujumbe wake bado hajajisalimisha polisi”

No comments:

Post a Comment