Maelezo ya Dogo Janja 
yanaamplfy kwamba juzi (September 2) walivyokua Club Maisha aliperform 
akiwa na furaha kutokana na mashabiki zake waliojitokeza na alipomaliza 
kuperform alishuka kwenye stage akiwa na furaha baada ya kufanya vizuri 
lakini hiyo furaha ilikatishwa baada ya kwenda juu sehemu ya V.I.P
Janja anasema alipopanda V.I.P 
kumsalimia Producer Maneck alimjibu kwa dharau na kumwambia haongei na 
Masnich hivyo Dogo Janja akaondoka lakini muda mfupi baadae alirudi na 
kukuta Tunda Man yuko karibu na alipokaa Maneck, Janja pamoja na Tunda 
walimsogelea producer huyo ambae alianza kumtukana matusi mazito Dogo 
Janja.
Baada ya hapo ilibidi Dogo 
Janja kushuka chini na kwenda kumchukua Ustaz Juma ambae ndio boss wa 
kundi alilopo sasa Dogo Janja la Watanashati, walipofika alipo Maneck.. 
alianza kuiponda single mpya ya Dogo Janja aliyorekodi na producer Marco
 Chali kwa kusema wimbo huo ambao mwanzo ulikua urekodiwe kwa Maneck ni 
wa kawaida sana.
Kwenye line nyingine namkariri 
Dogo Janja akisema “nikawa nimepanic sana sasa leo nakuja kupokea simu 
eti Tunda man nae anasema nifute chorus ya ‘Anajua’ kwenye wimbo wangu, 
Bro ule wimbo nimeurekodi nikiwa Tip Top na nimeifanyia show nyingi sana
 Tanzania ambazo zimewaingizia hela nyingi sana, hawana ubinadamu yani 
wanaponiambia mimi nifute chorus, Tunda kawafanyia watoto wangapi 
chorus? Shetta, Pasha lakini mbona hamwaambii Pasha afute au labda 
sababu mi mdogo, hili swala nawaachia watanzania kwa sababu ile ni haki 
yangu, nilimshirikisha Tunda.. ule wimbo sio wa Tunda siwezi kufuta 
chorus”
Baada ya hayo maelezo ya Dogo 
Janja, Producer Maneck amezungumza exclusive na millardayo.com na 
namkariri akisema “Dogo Janja alikuja akanisalimia nikamwambia ebwana 
eeeh kaa mbali na mimi sihitaji kuongea na wewe kwa sababu unatabia za 
kisnich sana, kuna vitu flani alivifanya siku kadhaa zimepita na 
sikupendezwa navyo.. tuliandaa show ya Tunda Man pale Maisha Club  
tukamwambia na akakubali kufanya na tukatangaza kwamba atakuepo sasa 
mwisho wa siku akabroadcast msg kwenye BBM alafu sisi hakututumia ile 
msg ila akabroadcast kwa watu kwamba hao ni matapeli, hapohapo nachat 
nae namuuliza mbona umezingua anasema mi naona aibu sijui hata sura 
yangu sijui nitaiweka wapi kwa bwana Captain, huku anasema hivi huku 
anafanya hivi”
Tunda Man nae ametoa sababu za 
kumwambia Dogo Janja afute sauti yake kwenye kolabo waliyofanya ya 
‘Anajua’ na nina mkariri akisema ” sikuzungumza kwa ubaya, nimezungumza 
kwa nia nzuri tu.. kwenye chorus inasema niko na Captain Tunda man alafu
 mimi siko pale mashabiki wanakua kama hawakuelewi vizuri, kuna mistari 
mingine inasema narun city nikiwa na JCB, narun Dar City nikiwa na T.I.P
 sasa ujue kwenye show kuimba vitu kama hivyo wakati hayupo na Tip Top 
vinakua havileti maana, ni kama maoni tu nimemuomba aimbie beat  kwa 
sababu anaweza kurekebisha ile mistari, mfano kusema narun city nikiwa 
na Watanashati, kwenye show ndio abadilishe lakini kwenye audio ni sawa 
ikibaki na vionjo vya mwanzo”
chANzo Millardayo.com 



No comments:
Post a Comment