Friday, October 18, 2013

Simba noma Jumapili pale Taifa

Yanga inaendelea kushikilia rekodi ya jumla baada ya ushindi mara 38, Simba 32, huku mara 32 zilitoka sare
 
Dar es Salaam.  Huku zikiwa zimesalia siku mbili, rekodi za miaka 13 iliyopita, zinaonyesha Simba imeibuka na ushindi mara nyingi zaidi ya Yanga katika mapambano baina ya timu hizo iliyopigwa siku ya Jumapili.
Simba na Yanga zitashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam keshokutwa kukabiliana katika pambano la Ligi Kuu Bara mzunguko wa kwanza.
Mwananchi lilifanya uchunguzi wake unaoonyesha kuwa kuanzia mwaka 2000 mpaka mwaka huu Simba ina rekodi nzuri zaidi ya kushinda siku ya Jumapili kuliko wapinzani wao, Yanga.
Rekodi hizo zinaonyesha kuwa katika kipindi hicho Simba na Yanga zilikutana mara 20, ambapo kati ya hizo Simba iliibuka na ushindi mara saba, wakati Yanga ilishinda mara mbili, huku mara 11 zikitoka sare.
Mechi zilizochezwa Jumapili baina ya Simba na Yanga Juni 25, 2000 (Simba 2-1 Yanga), Agost i 18, 2002 (Simba 1-1 Yanga), Novemba 10 (Simba 1-0  Yanga),  Novemba  12, 2000 (Simba 0-0 Yanga), Septemba 28, 2003 (Simba 0-0 Yanga), Novemba  2, 2003(Simba 4-1 Yanga).
Machi  31, 2002 (Yanga 3-0 Simba), Aprili 20, 2003 (Simba 1-1 Yanga), Aprili  17, 2005 (Simba 2-1 Yanga), Machi  26,
2006 (Simba 0-0 Yanga), Oktoba 29, 2006 (Simba 0-0 Yanga), Julai  8, 2007 (Simba1-1 Yanga), Aprili  27, 2008 (Simba 0-0 Yanga).
Oktoba  26, 2008 (Yanga 1-0 Simba), Aprili  19, 2009 (Simba 2-2 Yanga), Aprili  18, 2010 (Simba 4-3 Yanga).
(Julai  27, 2008) Yanga haikutokea uwanjani, Simba ikapewa ushindi wa chee. Rekodi hizi zinajumuisha mechi za mashindano mbalimbali  ikiwemo Ligi Kuu Bara, Kombe la Mapinduzi, Tusker Cup, lililokuwa Kombe la Chama cha Soka Tanzania (FAT) na Kombe la Kagame.
Hata hivyo, ukiondoa michezo baina ya timu hizo iliyofanyika Jumapili, Yanga inaendelea kushikilia rekodi ya jumla baada ya kuibuka na ushindi mara 38, Simba 32, huku mara 32 zilitoka sare.
Katika hatua nyingine, Kocha wa Yanga, Ernest Brandts alisema, matokeo ya ushindi wa mabao 2-1 iliyopata kikosi chake katika pambano la kirafiki dhidi ya Chipukizi ya Pemba yamekoleza morali ya wachezaji wake kuhakikisha wanaibwaga  Simba keshokutwa.

No comments:

Post a Comment