Wednesday, October 9, 2013

Kuna Kelele nyingi sana juu ya viongozi kusafiri nje ya nchi.Kuna baadhi ya wana-CCM wanajaribu kutumia Safari ya Dr.Slaa nje ya nchi kuhalalisha safari za Kikwete alizofanya nje ya nchi.


Rais Kikwete amesafiri mara 357 tangu aingie Madarakani kwa kipindi cha miaka 7 na miezi kadhaa akitumia Kodi za watanzania ambao wanaambiwa kwamba ni lazima wachangie kodi ya laini za simu hata kama wapo kijijini na kutumia laini hizo kuwabip watoto wao walioko mjini bila kazi maalumu.Kodi hizo ni sehemu ya kugharamia safari hizi za Rais kama nitakavyoonyesha pichani hapo chini.Katika siku 357 alizosafiri, zimepungua siku 8 tu akamilishe mwaka wenye siku 365. Hapa tumeongelea safari ya siku moja tu,kuna nyingine amekaa nje zaidi ya wiki na nyingine wiki 2 kama hii aliyoifanya juzi.Safari nyingine sio Muhimu hata kidogo.Kuna nyingine zinamhusu waziri wa Mambo ya Nje,nyingine zinawahusu Mawaziri wa Utalii na hata Wakurugenzi wa Idara.Delegation of power(Kukasimisha madaraka) haipo katika Utendaji wake.Hata kama Rais hana Management skills,washauri wake walitakiwa kumshauri na kumwambia ukweli kuhusu hili.

Sasa hivi dunia ni kama kijiji,ni lazima tutumie fursa ya teknolojia.Sio Lazima kwa Rais kusafiri na kuwepo kwenye mkutano physically.Baadhi ya Mikutano hufanyika kupitia Mitandao.Balozi zetu nje zinaweza kuwa empowered na kuiwakilisha serikali kwenye mikutano mingine ya uwekezaji.Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe mara kadhaa amekua akiongea kama vile ni mtu anayeelewa sana dhana ya Economic Diplomacy.Sijui ni kwanini hataki kumshauri Rais Kikwete ambaye nina uhakika hana taaluma ya Diplomasia na Uhusiano wa kimataifa au hata taaluma yenye uhusiano na fani hiyo ingawa alijitutumua kisiasa alipokua waziri wa Mambo ya nje.Pamoja na kuwa na shahada ya Uchumi ya miaka hiyo ya 1970,sidhani kama Rais wetu( kama ilivyo kawaida ya Waafrika wengi) alifanya jitihada za kuendelea kujisomea nadharia nyingine au kujiendeleza kitaaluma(hata kwa kozi fupi) kulingana na mabadiliko ya Dunia ukizingatia kuwa alijiandaa kwa Miaka 10 kuwa Rais wa nchi(Kama alivyokiri mwenyewe).Diplomasia ya Uchumi alitakiwa aielewe.Sio busara kujiandaa kwa kujikusanyia mashabiki bila wewe kujiandaa kitaaluma kulingana na mahitaji ya muda.Ni uzembe na usalaiti.

Rais wa Zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo ndiye Mtawala aliyeweka Rekodi ya kusafiri mara nyingi zaidi.Viongozi wa Afrika wakisafiri mara nyingi hutumia gharama kubwa na misafara mikubwa.Matumizi mabaya ya fedha. Tanzania sasa inabidi kuwe na tume ya kudhibiti Ziara za Rais maana kama ndani ya Miaka Saba na miezi kadhaa Rais Kikwete amekaa nchini kwa miaka 6 tu sasa tunaelekea wapi?

Rais amesafiri nje ya nchi kwa wastani wa safari 45 kwa mwaka 1.Ni wastani wa safari 4 kwa Mwezi 1.Ni wastani wa safari 1 Kila wiki. Katika siku 5 za kufanya kazi kiofisi(Sheria zetu za kazi ziangaliwe upya),Rais anasafiri nje ya nchi siku 1.Yaani kuanzia Jumatatu hadi ijumaa,siku 1 Rais yupo safarini nje ya nchi kwa siku moja.Hapa hatujajumuisha idadi ya siku anazokaa humo

Waziri wa Mambo ya nje angesafiri hivyo tungemuelewa lakini kwa sababu za msingi.Aliyekua waziri wa Mambo ya nje wa Marekani(Taifa lenye Nguvu duniani za kiuchumi na Kijeshi) Bi.Hillary Rodham Clinton alikua muumini wa Falsafa ya Msanii wa Brooklyn,Woody Allen kuwa asilimia 80 ya mafanikio ya makubaliano au kikao chochote muhimu ni Uwepo wako. She reinforced the power of being there -- in a place, in a context, in a moment. Hillary aliweka rekodi ya kusafiri masaa 2,084.21 sawa na wastani wa siku 86.83 na jumla alisafiri siku 401.Huyo ni mtu aliyekua waziri wa mambo ya nje wa Taifa lenye ushawishi duniani kwa maslahi ya Taifa lake huku Rais akisafiri mara Chache.Alipokuja Tanzania Rais aliacha kazi zote na kuvuruga itifaki,alienda Kumpokea badala ya Waziri wa mambo ya nje kuchukua nafasi yake.Delegation of power hapa sijui ilikua in a reverse order ama ni nini?!

Mwalimu Nyerere katika Miaka 24 ya utawala wake alisafiri mara 60+ lakini JK kwa mika isiyofika 8 amesafiri karibia mara 360. Tunaambiwa(Kwa kufuata utamaduni wake ule wa kuambiwa) kuwa safari moja ni zaidi ya Sh.300,000,000(milioni 300) na pia tukifanya kuwa kila safari moja kwa kiwango cha chini anakaa siku 3 maana yake ni (357 X 3) sawa na siku 1071 ambayo ni sawasawa na miaka 2 na miezi 9 ,wiki 3,siku 4, masaa 4 na dakika 3, na sekunde 30 nukta 3.Huyu ndiyo Rais wa nchi ambayo ni miongoni mwa nchi Maskini duniani ambaye zaidi ya asilimia 50 ya Raia wake wanaishi chini ya dola moja ya Marekani kwa siku yaani zaidi ya nusu ya watanzania milioni 45 ambayo ni sawa na watu milioni 22.5(22,500,000) hawawezi kumudu matumizi ya Shilingi 16,00/ kuanzia saa 12 alfajiri hadi saa 12 alfajiri ya siku inayofuata.Rais

Hajui ni kwani hali hii imekua hivi,hata yeye anashangaa.Hata hivyo ili kufidia nakisi ya bajeti(deficit) ya shilingi bilioni 264,inabidi Raia hawa hawa watozwe kodi ya laini za Simu kwa mwezi.Safari za Rais hadi muda huu kwa wastani niliotaja umegharimu sh.107100000000(Zaidi ya Bilioni 107) ambazo ni karibia Nusu ya kodi ya laini itakayotozwa Tanzania nzima kutoka kwa wamiliki milioni 22 wa laini za simu ambao takwimu zinaonyesha milioni 8 kati yao hawana uwezo wa kutumia shilingi 1000 kwenye simu zao kwa siku.Wanatumia kwa Sms na kubip tu.Maskini wanagharamia safari hizi ambazo mara nyingi Rais amekua akijitetea za kutafuta wawekezaji zinaishia kuvuta hata wawekezaji ambao takwimu zinaonyesha kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Interfaith Standing Committee on Economic Justice and the Integrity of Creation mwaka jana uligundua kuwa kwa wastani Tanzania hupoteza dollar billion moja (takriban shs trilioni 1. kila mwaka kutokana na ukwepaji kodi, uhamishaji harama wa fedha na misamaha ya kodi.

Je ziara zote za Rais Kikwete zina manufaa na tija kwa taifa letu?Katibu Mkuu wa CHADEMA na aliyekua mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2010 kwa tiketi ya CHADEMA Dr.Wilbroad Slaa yupo nje ya nchi.Amesafiri mara chache na kwa kazi maalumu za kiofisi.

No comments:

Post a Comment