Tuesday, October 15, 2013

Nigeria kifua mbele kwelekea Brazil

Nigeria Super Eagles

Nigeria Super Eagles
Ushindi wa Super Eagles ya Nigeria ugenini dhidi ya Ethiopia umeipa matumaini ya kushiriki kombe lijalo la dunia.
Ethiopia ilipata goli la kuongoza kunako dakika ya 56 kupitia mchezaji Asefa.
Bao hilo halikukaa kwa muda mrefu.kunako dakika ya 67 mkwaju uliopigwa na Emanuel Emenike uliishia langoni na kuwa 1-1.
Ethiopia watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kutumia nafasi kadhaa walizopata na pengine waliponea chupuchupu kunako dakika 77 ambapo mkwaju wa Nigeria ulirudishwa na mlingoti wa lango.
Goli la ushindi la Nigeria limepatikana kwenye dakika ya mwisho kwa njia ya penalty iliyofungwa kimiani na Emmanuel Emenike na kupalilia njia kwa bingwa hao wa Afrika ya kwenda Brazil.

No comments:

Post a Comment