Friday, October 4, 2013

Abdul Haji:Mkenya aliyekuwa tayari kuuawa

Wakati vyombo vya usalama vya Kenya vikitangaza kulidhibiti jengo lote la Westgate lililovamiwa na magaidi wanaodaiwa kuwa wa kundi la Al-Shabaab, baadhi ya watu waliojitoa muhanga na kufanikiwa kuokoa maisha ya wengine, wanaendelea kuibuka.
 
Hivi karibuni gazeti hili lilichapisha habari juu ya askari wa Kikosi Maalumu cha Anga (SAS) cha Uingereza, aliyeweza kuokoa zaidi ya watu 100 ndani ya jengo hilo.
Hivi karibu, baadhi ya vyombo vya habari vya Kenya vimemnukuu pia  Abdul Haji (38) ambaye ni raia wa kawaida aliyeweza kufika ndani ya jingo hilo na kuokoa watu waliokuwa wametekwa na wanamgambo hao wanaodaiwa kuwa wa Al Shabaab.
Gazeti la Daily Nation, limemnukuu kijana huyo akisema alipata ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (SMS) kutoka kwa kaka yake ukisomeka kuwa “Nimekwamba Westgate, nadhani kuna magaidi wamevamia hapa, niombee”.
Kijana huyo ambaye asili yake ni Msomali, alisema alipata sana hofu kutokana na ujumbe huo wa kaka yake kwani ilikuwa ni wiki mbili tu tangu televisheni moja ya nchi hiyo kumtaja kaka yake huyo kama mmoja wa watu anaowasaidia magaidi hao wa Al Shabaab.
Kijana huyo ambaye ni mtoto wa Seneta, Yusuf Haji alisema hali hiyo ilimpa wasiwasi zaidi kwani tayari walishaanza kupata vitisho kutoka kwa baadhi ya watu wakiamini kuwa kweli familia yake wanawasaidia Al Shabaab.
Anasema baada ya ujumbe huo alikimbia mara moja na kwenda katika jengo hilo la Westgate, na muda mfupi tu tangu magaidi hao kuingia ndani ya jengo hilo na kuanza kuwafetulia watu risasi alikuwa ameshawasili eneo hilo.
Haji ambaye ni mfanyabishara na baba wa watoto wane wa kike, alisema aliamini kuwa magaidi hao walikuja kumfuata kaka yake na baadaye familia nzima hivyo aliamua kujitoa muhanga ili kumuokoa kaka yake na familia yake yote.
Mtoto huyo ambaye baba yake ni Seneta wa Garissa na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ulinzi wan chi hiyo, alisema aliingia kwenye jengo hilo akiwa na bastola ambayo anaimiliki kwa kufuata sheria zote za Kenya.
Anasema kuwa, alipofika ndani ya jengo hilo aliona watu wengi wakiwa wameuwawa wakiwa wamelala chini na wengine wakiwa bado wapo hai huku milio ya risasi ikiendelea kulia kila kona.
Aliungana na watu wengine kama 10 waliokuwa ndani ya jengo hilo ambao pia walikuwa na silaha ili waone namna  ya kusaidia baadhi ya watu.
 “Nimewahi kuona miili ya watu waliokufa lakini sijawahi kuiona mingi kama ile ikiwamo ya watoto na kinamama wasiojiweza,” anasema Haji
chanzo-The citizen

No comments:

Post a Comment