Wednesday, August 29, 2012

POLISI WASEMA ALIYEKUFA KWENYE MAANDAMANO MORO HAKUPIGWA RISASI

POLISI WASEMA ALIYEKUFA KWENYE MAANDAMANO MORO HAKUPIGWA RISASI

Sarah Mgaji, Morogoro  Yetu
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro limesema kuwa marehemu  Ally Singano aliyeuawa wakati wa vurugu zailizotokea mkoani humo juzi hakupigwa risasi bali alikufa kutokana na kurushiwa kitu chenya ncha kali kilichosababishamajeraha na kupoteza maisha.
Ally Singano aliuawa katika vurugu zilizotokea baada ya Polisi kuzuia maandamano yaliyokuwa yakifanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema ) mjini Morogoro.
Akitoa taarifa ya uchunguzi wa mwili wa marehemu uliofanyika chini ya madaktari wawili Kamanda wa Polisi Mkoani humo Faustine Shilogile amesema kuwa uchunguzi uliofanyika umebaini kuwa marehemu Ally Singano alikuwa na majeraha kichwani ambayo yalisababishwa na kurushiwa kitu kilichomgonga kichwani  na kumsababishia majeraha hayo makubwa hadi kufikwa na mauti.
Kamanda Shilogile amesema taarifa za kutumika risasi za moto na kusababisha kifo cha kijana huyo sio sahihi na kwamba ni mabomu ya machozi ndiyo yaliyotumika kutawanya maandamano hayo.
Aidha kamanda Shilogile amesema uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini ni kitu gani kilichotumika kumpiga mtu huyo na nani aliyehusika na kumpiga ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani wale wote walioandaa maandamano hayo.
Hata hivyo hadi sasa hakuna mtu anayeshikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya kijana hao.
Jana jioni Polisi walisafirisha miwili wa marehemu kwenda mkoani Tanga ambako ndiyo mazishi yatafanyika.

No comments:

Post a Comment