Wednesday, October 16, 2013

Zitto avitikisa vyama vya siasa ni kwa kuagiza ruzuku isitishwe.

Nape alifafanua kwamba hesabu za 2011/2012 bado ziko kwa wakaguzi wa nje, wakishakamilisha nazo zitawasilishwa kwenye vikao vya chama na hatimaye kwa CAG.
“Hesabu hizi zikikaguliwa kwa mujibu wa utaratibu, anapelekewa CAG ambaye ndiye anazipeleka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na sio vinginevyo,” alisema.
Alidai kuwa Zitto anapaswa kuanza kutoa ‘boriti kwenye jicho lake ndipo aone kibanzi kwenye jicho la mwenzake’ kwa sababu chama chake ndicho kimekuwa na matumizi mabaya ya ruzuku. Alisema Zitto kama Naibu Katibu Mkuu wa Chadema ni vyema akawajibika ndani ya chama chake ili kuonyesha mfano kwa wengine.
“Wote tunakumbuka kelele zilizopo mtaani kuhusu matumizi mabaya ya ruzuku zinazoelekezwa na Chadema na viongozi wake kutoka kwa wanachama wao, hivyo si ajabu wakawa wanakiuka sheria hii na ndiyo chanzo cha kelele hizo za wanachama wao,”alisema.
Vyama vingine
Kwa upande wake, Chadema kilieleza kwamba hakijapata barua inayowaarifu kuhusu kutaka kufungiwa ruzuku kutokana na kutowasilisha taarifa ya ukaguzi.
Ofisa Habari Mwandamizi wa Chadema, Tumaini Makene ilisema hata barua ya kuitwa kwenye Kamati ya PAC, iliwafikia kwa kuchelewa. “Tunasubiri barua rasmi ya suala hili ndio mamlaka zinazohusika na masuala ya fedha ndani ya chama, hususan, Baraza la Wadhamini wa Chama kuweza kutafakari hatua,” alisema Makene.
Hata hivyo, alisema angependa umma utambue kwamba “Chadema ndicho kilichokuwa mstari wa mbele tangu kabla na baada ya mwaka 2009 kutaka ukaguzi na wazi katika mapato na matumizi ya vyama vya siasa.”
Alifafanua kuwa msimamo wa Chadema kwenye mkakakati huo ulikuwa ni kuibana CCM kutokana na madai ya baadhi ya vigogo wake “kukwapua fedha Benki Kuu ( Akaunti ya Madeni ya Nje – EPA) na kuzitumia kwenye uchaguzi wa mwaka 2005.”
Alijigamba kuwa hesabu za chama chake zimekuwa zikikaguliwa kila mwaka na kwamba wanasubiri maelezo ya barua kuhusu kile kinacholalamikiwa.
Kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF) kimesema hesabu zake ziko safi, ila imeshindikana kukaguliwa kwa vile Serikali haijatoa fedha za kugharimia ukaguzi huo.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Tanzania Bara, Julius Mtatiro alisema hesabu zao zimekwishakaguliwa na wakaguzi wa ndani.

Tuesday, October 15, 2013

Mawaidha ya Shk. Bombo katika Ibada ya Idi iliyoadhimiwa leo na Answar Sunna

 Picture
Kutoka kwenye blogu ya Mwanafasihi Mahiri, Mkwinda — Waumini wa dini ya Kiislamu mkoani Mbeya wameungana na Waislamu wenzao duniani katika kusherehekea ibada ya Eid na kutoa ujumbe wa kuzitaka nchi za Magharibi ziache uvamizi katika nchi za Kiislamu ambazo zina maslahi ya kiuchumi.

Akizungumza katika Ibada ya Swala ya Eid katika viwanja vya Kiwanja Ngoma, Sokomatola Jijini Mbeya, kiongozi wa Ibada hiyo ambaye ni Imamu katika msikiti wa Baraa Bin Azb Isanga, Shekhe Ibrahim Bombo alisema kuwa uvamizi unaofanywa na nchi za Magharibi umelenga kupora mali za wananchi wa nchi hizo.

Shekhe Bombo alisema kuwa limekuwa ni jambo la kawaida kwa nchi za Magharibi kudondoka mate kwa mali zilizopo katika
nchi za Kiislamu, hivyo njia pekee inayofanywa na nchi hizo ni kuzichonganisha ili machafuko yaibuke na wao kutumia fursa hiyo kuhujuma mali zilizopo katika nchi hizo.

Alisema kuwa ipo mifano mingi katika nchi zenye utajiri mkubwa duniani ambazo zimevamiwa na mali zake kuporwa na wageni kutoka nchi za Magharibi. Alizitaja nchi hizo kuwa ni pamoja na Libya, Afghanistan, Misri, Syria, Yemen, Iran na Pakistan ambako kumekuwa kukiibuka mapigano ya mara kwa mara huku wageni wakiingia katika nchi hizo wakijifanya wanasuluhisha migogoro ilhali wakiingilia utawala wa ndani na kujinufaisha kwa mali zilizomo: ''Tunalaani vitendo vya nchi za Magharibi kufanya uchonganishi kwa nchi zenye utajiri wa mafuta, itafika mahala dunia nzima haitakubali kwa dhuluma hii, tunaungana na wenzetu duniani kulaani dhuluma hii.''alisema Shekhe Bombo.

Shekhe Bombo alidai kuwa katika uvamizi huo yanafanyika mauaji ya kikatili kwa raia wasio na hatia ilhali akina mama na watoto wakidhalilishwa na kubakwa jambo ambalo halipaswi kuvumilika na kwamba itafika wakati Waislamu wote wataungana kupinga ukatili huo.

Aidha aliwataka waumini wa dini ya Kiislamu kutokubali kutenganishwa kwa imani zao moja na kwamba Waislamu wote wanaongozwa na Kitabu kimoja na Mtume mmoja na kwamba miongozo ya Uislamu inafuata taratibu za kitabu cha Koran na Hadith za Mtume Muhammad (SAW): ''Sisi sote ni Waislamu! inakuwaje  tukubali kutofautiana na wenzetu walioko Mecca Saudi Arabia ambao wanatekeleza ibada hii ya Hijja leo nasi tukiadhimisha kwa kufanya ibada ya Swala ya Eid el Haj?" alihoji Shekhe Bombo.

Wakati Waislamu wengine wameswali leo, kesho Waislamu wengine wanatarajia kuswali swala ya Eid kutokana na matangazo yatakayotolewa na viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Commonwealth Scholarships for developing Commonwealth country citizens, 2014

Commonwealth Scholarships for students from developing Commonwealth countries are offered for Master’s, PhD, and split-site (PhD) study in the UK. These scholarships are funded by the UK Department for International Development (DFID).

NominationsThere is a nominating agency for Commonwealth Scholarships in each Commonwealth country. In addition, universities and university bodies in a number of developing Commonwealth countries are invited to nominate candidates to the CSC.


Each year, the CSC invites each nominating agency/university/university body to forward a specific number of nominations. Each nominating agency/university/university body is responsible for its own selection process, and in most cases they will set their own closing date, which will be before the CSC’s deadline for nominations (17 December 2013).

Approximately 300 of these scholarships are awarded each year. The CSC invites around three times more nominations than scholarships available – therefore, nominated candidates are not guaranteed to get a scholarship. There are no quotas for scholarships for any individual country. Candidates nominated by national nominating agencies are in competition with those nominated by universities/university bodies, and the same standards will be applied to applications made through either channel.

Other scholarships offered by the CSC

Terms and conditions and eligibility Applications are considered according to the following selection criteria:

  • Academic merit of the candidate
  • Quality of the proposal
  • Likely impact of the work on the development of the candidate’s home country

See Selection criteria – 2014 Commonwealth Scholarships for developing Commonwealth country citizens for further details.

Please note that the CSC does not impose any age limit on applicants for its awards, but national nominating agencies may do so in line with their own priorities.

Candidates may also find the Feedback for unsuccessful candidates in 2013 useful.

Levels of studyYou can apply for a Commonwealth Scholarship for the following levels of study:
  • Master’s (one-year courses only)
  • PhD
  • Split-site, where the CSC supports one year’s study at a UK university as part of a PhD being undertaken in your home country
All subject areas are eligible, although the CSC’s selection criteria give priority to applications that demonstrate strong relevance to development.

You are requested to apply for a course of study at a UK university with which the CSC has a part funding agreement.
How to apply

All applications must be made through your nominating agency (or university/university body, if applicable) in your home country. You must check with them in the first instance for specific advice on how to make an application and for their own closing date. The CSC cannot accept any applications direct from candidates.

The CSC expects all Commonwealth Scholarship candidates to be nominated by an approved nominating agency/university/university body, and to have completed an application form using our Electronic Application System (EAS).

Full help on how to apply using the EAS is provided in our guides, which should be read in full before making any attempt to use the EAS.

The EAS will close to applicants on 3 December 2013 and no further applications can be made after that date. The CSC will not accept any applications which are not submitted via the EAS to the nominating agency/university/university body in the candidate’s home country.

How to access the EAS

Please note that all enquiries about these scholarships should be directed to the nominating agency/university/university body in your home country.


Source: http://cscuk.dfid.gov.uk/apply/scholarships-developing-cw/

Ivory Coast yapiga hatua kwenda Brazil


Didier Drogba
Ushindi wa Ivory Coast dhidi ya Senegal umekuwa hatua muhimu ya kuelekea katika fainali za kombe la dunia.
Didier Drogba Mabao 3 yaliyofungwa na washambuliaji Didier Drogba, Gervinho na Salomon Kalou yametosha kuiongezea matumaini Ivory Coast ya kushiriki fanali za kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil.
Goli la kufutia machozi upande wa Senegal lilifungwa kimiani na mshambuliaji wa NewCastle Papiss Demba Cisse.
Mechi ya mkondo wa pili itachezwa mwezi ujao nchini Morocco kwa sababu Senegal inatumikia adhabu ya kutochezea kwenye uwanja wa nyumbani.

Burkinafaso 3 Algeria 2

Penalti ya dakika za mwisho iliyopewa Burkinafaso katika mazingira ya kutatanisha iliiwezesha timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Algeria.
Hadi dakika ya 85 matokeo yalikuwa magoli 2-2 kabla ya Burkinafaso kupata penalti iliyowawezesha kuondoka na ushindi mdogo.

Tuzo ya Mo Ibrahim yakosa mshindi tena

Mo
Wakfu wa Mo Ibrahim ambao humzawidi Rais mstaafu aliyeonyesha uongozi mzuri umesema hakuna kiongozi wa Afrika aliyetosha kutuzwa mwaka huu.
Hata hivyo utafiti wa wakfu wa Mo umeonyesha kuwa Afrika imepiga hatua pakubwa tangu mwanzoni mwa karne hii katika maswala ya uongozi.
Tuzo hiyo haijapata mshindi kwa miaka minne mfululizo tangu kuzinduliwa kwake miaka saba iliyopita.
Katika mkutano na waandishi wa habari mjini London, wakfu wa Mo umesema kuwa baada ya ukaguzi kufanyika hakuna hata kiongozi mmoja alistahili kutuzwa.
Tuzo hiyo ambayo hutolewa na mfanyabiashara bilionea mzaliwa wa Sudan na raia wa Uingereza, Mo Ibrahim hutoa dola milioni 5 kwa kipindi cha miaka kumi na dola laki mbili kila mwaka hadi kiongozi huyo atakapofariki. Na pia dola laki zingine mbili hutolewa kwa mradi wowote unaoungwa mkono na mshindi wa tuzo hiyo kwa kipindi cha miaka kumi.
Hata hivyo, kwa mujibu wa takwimu za wakfu huo, kuna baadhi ya sehemu ambapo hali bado ni mbaya ikiwemo kutii sheria.
Wakfu huo wake Mo Ibrahim tajiri mkubwa sana mwenye uraia wa Sudan ulianza kutoa takwimu zake kuhusu utawala barani Afrika mwaka 2007.
Katika mwaka ambapo Afrika ilisherehekea miaka hamsini tangu kuzinduliwa kwa muungano wa nchi za Afrika, AU. Kwa mujibu wa utafiti wa wakfu wa Mo Ibrahim, mustakabali wa Afrika sio mbaya.

Washindi wa tuzo ya Mo

2005 Joaquim Chissano: Msumbiji
2008 Festus Mogae : Botswana
2011 Pedro Pires : Cape Verde
Asilimia tisini na nne ya waafrika sasa wanaishi katika nchi ambayo angalau imeonyesha uongozi umeimarika tangu mwaka 2000.
Nchi 18 kati ya hamsini na mbili, zilionekana kupata alama nzuri tangu mwaka 2007.
Utafiti huu unaanganzia mambo kadha kwa kadha kama vigezo vya utawala mzuri ikiwemo, ukuwaji wa uchumi , afya na sheria.
Taifa lililopata alam,a nzuri kuliko zote ni Mauritius,ikifuatiwa na Botswana na Cape Verde.
Mataifa yaliyoshika mkia ni pamoja na Eritrea, DRC na Somalia. Nchi zenye uchumi mkubwa barani Afrika,ikiwemo Afrika Kusini na Nigeria zilishika nambariya sita na 45 mtawalia.
Ripoti ya Mo inaonyesha kuwa mizozo sasa imepungua barani humo kuliko ilivyokuwa mwongo mmoja uliopita.
Hata hivyo, bado kuna tatizo la pengo kubwa kati ya masikini na matajiri na ripoti hiuyo inaonya kuwa ikiwa tatizo hili litapuuzwa huenda mizozo zaidi ikaibuka.

Nigeria kifua mbele kwelekea Brazil

Nigeria Super Eagles

Nigeria Super Eagles
Ushindi wa Super Eagles ya Nigeria ugenini dhidi ya Ethiopia umeipa matumaini ya kushiriki kombe lijalo la dunia.
Ethiopia ilipata goli la kuongoza kunako dakika ya 56 kupitia mchezaji Asefa.
Bao hilo halikukaa kwa muda mrefu.kunako dakika ya 67 mkwaju uliopigwa na Emanuel Emenike uliishia langoni na kuwa 1-1.
Ethiopia watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kutumia nafasi kadhaa walizopata na pengine waliponea chupuchupu kunako dakika 77 ambapo mkwaju wa Nigeria ulirudishwa na mlingoti wa lango.
Goli la ushindi la Nigeria limepatikana kwenye dakika ya mwisho kwa njia ya penalty iliyofungwa kimiani na Emmanuel Emenike na kupalilia njia kwa bingwa hao wa Afrika ya kwenda Brazil.

DO THIS BEFORE YOU HIT 25yrs of age.

1. Begin to put money in the bank and learn to
leave it there.
2. Date the right person.
3. Get your own place, stop having room-mates.
4. Get out of debt.
5. Get that body you always dreamed of and
maintain it.
6. Surround yourself with people that will take
you a step ahead. 

7. Start to accumulate a fortune and wealth. 

8. Learn to dress well not sexy.
9. Accept that you are an adult and stop your
kiddish behaviors.
10. Let go of the past and look forward to the
future