Ni baada ya kulipukiwa na bomu la kutupwa kwa 
mkono wakati walipokuwa wakichezea Bomu hilo lililookotwa kwenye vyuma 
chakavu na kudhani kuwa ni mpira.
                     Tukio hilo lilitokea Jumatano majira
 ya asubuhi huko Wilayani Karagwe mkoani Kagera Magharibi mwa Tanzania 
wakati watoto  walipokuwa wakichezea kitu mfano wa mpira mdogo ,ambacho 
baadaye kilikuja kutambulika kuwa lilikuwa Bomu la kurushwa kwa mkono.
                     Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC mjini Dar es 
Salama, Eric David Nampesya , mkuu wa Wilaya wa Karagwe Bi Darli 
Rwegasira amesema kuwa watoto hao walilipukiwa na Bomu hilo ambapo 
watatu kati yao walikufa papo hapo huku wawili wakifia hospitalini. 
                     Kwa Mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya, awali mzazi 
wa watoto hao amekiri kuwa aliliona bomu nyumbani kwake hapo juzi ambapo
 watoto wake walikuja nalo baada ya kuliokota huku wakidhani kuwa ni 
mpira.
                     Naye Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Philipo 
Kalangi alisema kuwa utafiti waliofanya umeonyesha kuwa Bomu hilo 
lililookotwa na kijana mmoja ambaye alikuwa akikusanya vyuma chakavu kwa
 lengo la kuviuza hapo wilayani karagwe. 
                     Bomu hilo lilikuwa mojawapo katika vyuma 
alivyokuwa ameokota na baadaye watoto hao walienda kulichezea nyumbani 
kwao na hatimaye kusababisha maafa hayo.
                     Mkuu huyo wa Polisi mkoani Kagera alidokeza kuwa
 uchunguzi unaendelea ili kujua kwa undani Bomu hilo lilitokea wapi na 
iwapo kama kuna mabomu mengine yanayoweza kuwa yamebaki katika maeneo 
mbali mbali hapo Wilayani Karagwe.
                     Mkuu huyo wa Polisi hakuweza kukiri wala kukana 
moja kwa moja kuhusisha Bomu hilo Kama matokeo ya uwepo wa wakimbizi wa 
Rwanda waliowahi kuishi Wilayani hapo mwaka 1994 baada ya mauaji ya 
kimbari nchini Rwanda ambapo Wilaya ya Karagwe ni moja ya wilaya 
zilizopokea wakimbizi wengi kutoka nchini Rwanda.
                     Uchunguzi zaidi unaendelea huku ukiwahusisha wataalam wa milipuko kutoka Polisi na jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
source bbc.com 
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment